Kwa sababu lugha yetu tunayoitumia ni Kiswahili, hakuna haja ya kujilazimisha kuongea Kiingereza wakati lugha hii ni tatizo kwako. Watu wengi hudhani kuongea kiingereza ni kielelezo cha ustaarabu (civilisation) na usomi - hii si kweli. Wazungu wakija hapa kwetu wanalazimika kuongea Kiswahili, japo wanachapia lakini hawana budi kukiongea sababu ndiyo lugha ya mawasiliano hapa kwetu. Sasa wewe mtanzania kwa nini ung'ang'anie kuongea Kiingereza broken hapa kwetu uswahilini?Ongea Kiingereza unapolazimika tu na katika mazingira yanayokihitaji, vinginevyo kama unalazimisha kuongea wakati hujui na hakuna ulazima lazima tukwambie tu kwamba unaongea broken English!
Lakini hata watu ambao wana matumizi ya Kiingereza sawa na sis mf. India, Pakistan na Nigeria huwa wanakosea sana, na wanajivunia namna wanavyozungumza.
Sisi ni mabingwa wa kufoji matamshi, huwezi kujua kama hiki ndio Kiingereza cha Tanganyika.
baada ya miaka kama 50 hivi lugaha nyingi za makabila ya hapa tz zitakuwa zimepoteza mwelekeo kutokana na kiswahaili kuzimeza. baada ya miaka kama 100 hivi dunia itazidi kuwa kama kijiji na hivi ni lugha chache tu zitatumika kuwasliana. baadhi ya lugha zitapoteza umaarufu. sijui kiswahili kitakuwa na nafasi gani. kuna lugha amabazo zinajinyumbua na kushindana kuwa lugha ya dunia na kiingereza ni moja ya lugha hizo.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.