Kikwete ziarani Zanzibar: Ahadi, vijembe, na maagizo

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,006
Date::1/21/2009
Kikwete asimamisha ununuzi magari ya serikali
Na Mwandishi Maalum, Pemba
Mwananchi​

RAIS Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa serikali yake inatafakari kusimamisha ununuzi wa magari ya serikali kwa muda, ili fedha zitakazookolewa katika zoezi hilo zitumike kununua matreka kwa ajili ya kuinua kilimo nchini.

Akizungumza wakati wa kukagua ujenzi wa barabara ya lami kutoka Jondeni hadi kufikia Makombeni, Kisiwani Pemba, katika siku ya pili ya ziara yake ya siku sita Tanzania Visiwani, Rais Kikwete alisema kuwa mawazo ya kusimamisha ununuzi wa magari ya serikali ni jitihada za serikali yake kuinua hali ya kilimo nchini.

Rais Kikwete alianza ziara ya Tanzania Visiwani juzi, katika Mkoa wa Kaskazini Pemba na jana, alimaliza ziara ya kisiwa cha Pemba kwa kutembelea mkoa wa Kusini Pemba. Aliondoka kwenda Kisiwa cha Unguja kuendelea na ziara yake.

Rais Kikwete tayari ametoa maelekezo kuhusu suala hilo la kusimamisha ununuzi wa magari ili kupata fedha za kuwekeza katika sekta ya kilimo. Inakisiwa kuwa serikali inaweza kuokoa kiasi cha kikubwa na kuridhisha cha fedha kwa uamuzi wa kusimamisha ununuzi wa magari katika serikali.

Wakati anakutana na kufanya mazungumzo na uongozi wa wizara ya fedha na mipango ya uchumi kuhusu tathmini ya utendaji wa serikali yake katika miaka mitano iliyopita, Rais Kikwete aliuelekeza uongozi wa wizara hiyo Jumatatu wiki hii mjini Dar Es Salaam kuchukua hatua za kusimamisha ununuzi wa magari ya Serikali, ili kuokoa fedha za kuwekeza katika kilimo.

Rais Kikwete ametoa ufafanuzi huo kwa wananchi baada ya kuwa ameambiwa na wananchi katika eneo hilo kuwa walikuwa na mahitaji ya pembejeo ikiwa ni pamoja na tretka za kilimo. Wilaya ya Mkoani inahitaji kiasi cha trekta sita kwa ajili ya kilimo.

Kuhusu ziara za nje, Rais alisema kuwa hatua ya viongozi wa Tanzania kutembelea nchi za nje siyo kupoteza wakati wala fedha, bali ni jitihada za viongozi hao kujazia raslimali za maendeleo ya Tanzania.

Rais ametoa ufafanuzi huo wakati alipofungua mradi wa tanki la maji kwenye kijiji cha Kengeja, mradi ambao umegharimiwa na serikali ya Japan na utakaowanufaisha kiasi cha watu 19, 000 wa kijiji hicho na maeneo ya jirani.

Mradi huo uliogharimu jumla ya Sh milioni 138, ikiwa ni pamoja na Sh milioni 30 zilizotolewa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) na Sh milioni mbili za wananchi, ni mradi wa 10 wa maji kugharimiwa na Serikali ya Japan katika Tanzania Visiwani katika miaka saba iliyopita.

Alisema Rais: "Hivi bila kwenda kuzungumza na wenzetu wa Japan tungepata wapi miradi hii? Wajapan wangelijua vipi kijiji cha Kengeja? Kijiji cha Kengeja na watu wake wanawahusu nini Wajapan? Bila kuwatambulisha watu hawa wa Kengeja, Wajapan wangewajua wapi?"

Aliongeza: "Kunawatu wanatuambia tubakia hapa Kengeja na pale Moshi ama Arusha…Tusipotoka kwenda kuwaona watu hawa, watashughulika na wale ambao wamekwenda na wamewaona."

Alisema kuwa maendeleo ya Tanzania yana sura mbili ya vyanzo vya raslimali. "Moja ni nguvu zetu wenyewe, na sura ya pili ni nguvu za marafiki watu...Vyote hivi muhimu sana na hivyo tutaendelea kusaka raslimali za maendeleo popote tunapoweza na kwa kutumia kila aina ya mbinu."
 
Last edited by a moderator:
Kikwete awasuta wanaomshutumu kusafiri nje
Mgaya Kingoba, Pemba
Daily News; Wednesday,January 21, 2009 @20:21​

Rais Jakaya Kikwete amesema watu wanaodai anapoteza muda kwa ziara za nje ya nchi, hawana hoja kwa sababu ziara hizo zina manufaa makubwa na zinawahusu Watanzania kwa ajili ya maendeleo yao.

Amesema maendeleo ya Watanzania yana sura mbili; moja ni nguvu za wananchi na nyingine ni misaada kutoka kwa nchi wahisani au washirika wa maendeleo, ambao lazima kama kiongozi, akutane nao nje ya nchi.

"Wapo watu wanaosema kwenda nje tunapoteza muda, kwamba huko kwingine hakutuhusu…kunatuhusu sana. Maendeleo yana sura mbili, moja ni nguvu za wananchi na nyingine ni misaada ya kuchangia maendeleo yetu," alisema Rais.

"Sasa ili kupata misaada hiyo ya maendeleo ni lazima utoke na ukutane na wahisani hao sehemu mbalimbali," alisema Rais Kikwete jana wakati akizindua tangi la maji katika Shehia ya Kengeja katika Wilaya ya Mkoani katika Mkoa wa Kusini Pemba, ambalo limejengwa kwa ufadhili wa Serikali ya Japan.

"Japan hapa hajileti mwenyewe…Japan anawajua ninyi? Anawahusu nini? Japan anakuja hapa mpaka awepo mtu wa kuwatambulisha, ndio maana tumepata msaada huu. Ndiyo maana mwaka jana nilikwenda katika mkutano wa ushirikiano wa Japan na Afrika unaoitwa TICAD.


"TICAD wameahidi kutusaidia kwa maendeleo yetu watu wa Afrika. Sasa usipotoka ukaenda, watashughulika na waliokwenda," alisema Rais Kikwete akifafanua umuhimu wa safari za nje na misaada ya wahisani kwa maendeleo.

Alisema misaada hiyo ni muhimu kwa maendeleo, na akaishukuru Serikali ya Japan kwa msaada wake huo na mingine inayoitoa kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) na Serikali ya Jamhuri ya Muungano.

Kikwete, ambaye alikuwa katika ziara ya siku mbili katika mikoa ya kisiwani Pemba, aliwataka wananchi wa Shehia ya Kengeja pamoja na vijiji vya jirani kuhakikisha mradi huo unadumu kwa manufaa na maendeleo yao.

Awali, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Zanzibar, Hemed Salum Hemed alisema mradi huo ulianza Agosti mwaka 2007 na ulikamilika kufikia Agosti mwaka jana, na unatarajiwa kuwanufaisha wakazi 12,000 wa Kengeja na jirani zao Mwembe.

Alisema tangi hilo litakuwa na uwezo wa kuchukua lita za ujazo 200,000, wakati lile la awali lilikuwa na uwezo wa kuchukua lita 20,000. Alisema Serikali ya Japan imetoa Sh milioni 106.8 wakati SMZ imetoa Sh milioni 30 na nguvu za wananchi ni Sh milioni mbili. Alisema huo ni mojawapo ya miradi 10 iliyoanza kutekelezwa kuanzia mwaka 2000.
 
Hivi Japan walikuwa hawaijui Tanzania kabla ya Kikwete kuingia madarakani hivyo ikabidi aitambulishe tena wa Wajapan? Mbona Mwalimu alikuwa hasafiri sana nchi za nje lakini hilo halikuzuia kupata misaada toka nchi mbali mbali marafiki ikiwemo Japan!?
 
Pamoja na safari za nje basi tunamwomba azidi kubana mianya ya matumizi mabaya ya raslmali za taifa kwani tunaweza omba misaada sana lakini tusiposimaia matumizi ya misaada hiyo basi tutakuwa hatufanyi kitu ambacho kinasaaidia wananchi kwa ujumla.
 
Inaonekana kama yeye na Pinda wamezinduka na kuanza safari za visiwani.
 
Alisema tangi hilo litakuwa na uwezo wa kuchukua lita za ujazo 200,000, wakati lile la awali lilikuwa na uwezo wa kuchukua lita 20,000. Alisema Serikali ya Japan imetoa Sh milioni 106.8 wakati SMZ imetoa Sh milioni 30 na nguvu za wananchi ni Sh milioni mbili. Alisema huo ni mojawapo ya miradi 10 iliyoanza kutekelezwa kuanzia mwaka 2000.

"TICAD wameahidi kutusaidia kwa maendeleo yetu watu wa Afrika. Sasa usipotoka ukaenda, watashughulika na waliokwenda,"

The syndrome, the syndrome, the aid dependency syndrome!!! Paul Kagame might have some of the answers!!!

Tuliweza kuchanga millioni 300 kwa siku tu baada ya ushindi wa Taifa Stars... leo hii tunashindwa kuchangia 150mil. kwa ajili ya tangi la maji yetu safi..... The case of misguided priorities is vividly proved here, isn't it?!!!
 
Tuliweza kuchanga millioni 300 kwa siku tu baada ya ushindi wa Taifa Stars... leo hii tunashindwa kuchangia 150mil. kwa ajili ya tangi la maji yetu safi..... The case of misguided priorities is vividly proved here, isn't it?!!!

Serikali ya Japan imetoa Sh milioni 106.8 wakati SMZ imetoa Sh milioni 30 na nguvu za wananchi ni Sh milioni mbili. Alisema huo ni mojawapo ya miradi 10 iliyoanza kutekelezwa kuanzia mwaka 2000.

Miradi kama hii mara nyingi huwa aianzishwi na serikali kuu. Huwa inakuja kutokana na kuzidiwa kwa kero katika kitongoji ama kijiji husika. Sasa ni wao wenyewe kupitia kamati zao uangalia ni kwa namna gani wanaweza kuondoa kero hiyo.

Ndio maana utaona kuwa hata nguvu zao ingawa ni chache hutajwa katika mradi, ninachotaka kusema hapa ni kuwa aina hii ya miradi ni mizuri sana, kwani inatokana na kero wanazo ziona wananchi wenyewe na wala sio kwa utashi wa serikali ama mfadhili.
 
NAdhani Mheshimiwa Rais ameshaguswa na madai hayo ya utalii wa nje ya nchi kila wakati na anajibaraguza tu. Kama anaona safari za nje zina manufaa makubwa kwa wanachi atuambie tumefaidika kwa kiasi gani ukilinganisha na gharama za safari zake za ughaibuni, pia atuambie ziara hizo zimekuwa na manufaa zaid kuliko aliyemtangulia (Mkapa) ambaye hakuwahi kulalamikwa kwa ziara za ovyo-ovyo za nje?
 
Safari za kwa Rais sawa lakini safari nyingi ni kwa Waziri wa mambo ya nje na ziwe safari zenye tija si za kusaini mikataba hotelini kama alivyofanya Karamagi.
 
Huu ni usanii wa kujiandaa na uchaguzi wa 2010. Yale magari mapya pale ikulu (BMW) kulikuwa na haja gani ya kuyanunua wakati alikuta benzi bado nzuri na nzima?.

Bado kura yangu haijapatikana kwa upuuzi huu.
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete amewaambia wapinzani wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kuwa inaweza kuwachukua muda mrefu mno kupata nafasi ya kuunda Serikali, ama pengine wasiipate kabisa, na hivyo ni muhimu kwao kushirikiana na Serikali ya CCM katika kuwaletea wananchi wa Tanzania Visiwani maendeleo.
Rais pia amesema kuwa ni fitina za kisiasa kwa wapinzani wa Serikali ya SMZ kuibeza na kuikejeli Serikali hiyo kwa madai kuwa haijaleta maendeleo yoyote Tanzania Visiwani.
Aidha Rais amewaambia wananchi wa Pemba kuwa wanayo haki ya kuendelea kumchagua yoyote wanayemtaka ili awe mbunge ama mwakilishi, ili mradi tu waendelee kukabidhi dhamana ya kuendesha Serikali kwa Chama cha Mapinduzi.
Amesisitiza kuwa Serikali ya SMZ na ile ya Muungano zitaendelea kuwaletea maendeleo wananchi wa Visiwani bila upendeleo wala kubagua yoyote kwa sababu huo ndiyo mkataba kati ya Serikali na wananchi, na kwa sababu kuleta maendeleo ni dhamana ya Serikali iliyoko madarakani, na wala siyo wapinzani.
“Madai kuwa Serikali haijafanya lolote wala chcochote ni fitina tu za kisiasa. Unajua midomo kazi yao ni kusema. Unaweza kusema lolote hasa inapokuwa usemaji wenyewe ni wa kufitini, yaani kudanganya watu, ili wakuchague. Mafanikio yamepatikana mengi ndugu wananchi katika elimu, katika barabara. Na hizi barabara tutazijenga pote, hata pale Mtambwe,” alisema na kuongeza:
“Tutamwendeleza kila mtu kwa sababu dhamana ya maendeleo ni yetu katika Serikali. Hawa wengine hawana Serikali. Kazi yao, na wabunge wao, na wawakilishi wao, ni kufoka tu. Sisi ndio wenye dhamani ya Serikali na wala hatubagui.”
Rais aliyasema hayo wakati aliposalimiana na wananchi katika nyakati na matukio tofauti jana, Jumatano, Januari 21, 2009 kwenye siku yake ya pili na ya mwisho ya ziara yake katika Kisiwa cha Pemba ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku sita Tanzania Visiwani. Rais ameanza ziara ya siku nne katika Kisiwa cha Unguja leo, Alhamisi, Januari 22, 2009 baada ya kuwa amekamilisha ziara yenye mafanikio katika Pemba.
Akizungumza na wananchi baada ya kuwa amefungua mradi wa maji wa Kengeja, Mkoa wa Kusini Pemba, Rais alisema kuwa ni muhimu kwa wananchi wote, bila kujali itikadi zao za kisiasa, kushirikiana na Serikali iliyoko madarakani katika kusaka maendeleo.
Alisema kuwa ni kinyume cha taratibu za ushindani wa kidemokrasia kwa chama kimoja kusema kuwa hakiwezi kushirikiana na Serikali iliyoko madarakani kikidai kuwa kinasubiri mpaka kitakapoweza kuunda Serikali.
“Ni muhimu kwa watu kukubali kuwa ipo Serikali iliyoko madarakani hata kama wanakataa jinsi ilivyoingia madarakani. Ukweli ni kwamba ipo na ni muhimu kwa watu wote kushirikiana nayo katika kuleta maendeleo. Maana ukisubiri hiyo Serikali yako inaweza ikachelewa sana ama pengine isije kabisa katika uhai wako,” alisema na kuongeza:
Akizungumzia mabezo na kejeli za wapinzani wa CCM kuwa Serikali ya SMZ haijaleta maendeleo yoyote kwa wananchi, Rais Kikwete aliwaambia wananchi hao wa Kengeja: “Wananchi, hizi ni fitina tu. Unajua midomo kazi yake ni kusema. Unaweza kusema lolote hasa inapokuwa kwenye kufitini, kudanganya watu ili wakuchague.”
Aliongeza Rais Kikwete: “Ukweli ni kwamba mafanikio yamepatikana mengi…iwe kwenye elimu ama barabara. Nimesema kuwa tutatoa huduma za kijamii kwa wananch wote bila kubagua kati ya wale waliotupigia kuara ama wale waliokipigia kile chama kingine. Hata ile barabara ya Mtambwe tutaijenga tu.”
Rais Kikwete alisema kuwa ni muhimu kwa Serikali kuendelea kutoa huduma kwa wananchi bila kubagua kwa sababu Serikali ndiyo yenye dhamana ya kuleta maendeleo, akisisitiza: “Maana wao hawana Serikali, kazi yao na wabunge wao na wawakilishi wao ni kufoka tu. Sisi ndio wenye dhamana ya Serikali. Ujumbe wetu kwa wapinzani wetu ni rahisi kabisa kuwa nyie endeleeni kuwachagua mnaowataka, lakini sisi endeleeni kutukabidhi Serikali na dhamana ya kuleta maendeleo.”
Alisisitiza: “Wao wacha waendelee kutia fitina, kubeza maendeleo, lakini maji safi wanaendelea kunywa. Barabara wanaendelea kupita wakipepeza bendera zao kwa sababu zinateleza kama mgongo wa ngisi. Anapata taabu sana kuisifia Serikali ya CCM hadharani, lakini akikaa na mkewe chumbani anasema kuwa hawa CCM kiboko kwa maendeleo. Lakini akitoa hadharani anabeza akisema hawa CCM watu gani? Lakini maji anakunywa.”
Akizungumza baada ya kuwa amekagua ujenzi wa barabara ya lami kati ya Mkoani na Makombeni katika mkoa huo huo wa Kusini Pemba, Rais Kikwete aliendeleza somo lake kwa wapinzani akisema:
“Ndugu wananchi, msije kudanganywa. Kazi ya maendeleo haiku mikononi mwa mbunge ama mwakilishi. Hii ni kazi na dhamana ya Serikali…zote mbili ya SMZ na Muungano. Mbunge hawezi kujenga barabara ya lami. Sisi ndio wenye dhamani kwa waliotuchagua na hata wale ambao hawakutuchagua”
Alisema kuwa lazima Watanzania watofautishe vipindi vya uchaguzi na vipindi vya maendeleo. “Tutofautishe kipindi cha uchaguzi na kipindi cha maendeleo. Tutambue kuwa siasa za uchaguzi ni siasa za uchaguzi, baada ya hapo mleta maendeleo ni Serikali. Na hata baadhi ya watu wakinuna wakati tukipita, lakini ukweli ni kwamba Serikali tunayo sisi. Anayewaongopea vinginevyo, mwambie hivyo sivyo.”
“Wakati ya ushindani ni wakati wa uchaguzi. Yakitangazwa matokeo hata kama hukuridhika nayo ni lazima ukubali kushirikiana na washindi. Sasa utafanyaje hata kama huyo ndiye mwenye dhamani. Lakini huyo ndiye binadamu, akishakuwa ameshiba ugali na ngisi, basi maneno yanakuwa mengi.”
Akizungumza baada ya kuwa amefungua soko la Mvumoni na kutoa boti na nyavu za uvuvi kwa vikundi mbali mbali, Rais Kikwete amesema kuwa amefurahi kusikia kuwa vikundi vya kupata boti na nyavu havikuchaguliwa kwa ubaguzi wa vyama ana itikadi.
“Nafurahi kusikia kuwa tabia hii haiko kwenye mradi huu. Maana baada ya uchaguzi mtu wa CCM alikuwa akinyimwa huduma dukani ama kukataliwa kubebwa kwenye boti. Sasa sukari ina CCM na CUF? Ama kama kila mwanachama wa chama siasa akianzisha duka lake tutakuwa na maduka mangapi? Aliuliza Rais Kikwete na kusisitiza:
“Mwanademokrasia wa kweli, akimaliza uchaguzi hushirikiana na wenzake katika kuleta maendeleo. Hivi kama Serikali ingekuwa na fikra kama yule anayemkataza mwenzake kupanda boti yake kwa sababu ya itikadi, hivi Pemba ingekuwa maji, ama barabara nzuri, ama maji, ama skuli?”
Rais Kikwete alisema kuwa ni wajibu wa vyama vya siasa kujua kuwa kina mtu anatawala kwa zamu yake ya kutawala kama anachaguliwa na wananchi lakini muhimu ni kushirikiana. “Kila mtu kwa zamu yake. Lakini ushirikiano ni wakati wote. Hivi wewe hutaki kushiriki na Serikali iliyopo ukingojea Serikali yako. Hivi itakuja lini? Na kama haikuja je?”
Alisema kuwa mfano nzuri ni wa Marekani. “Pale Marekani alikuwa ni Rais Bush wa Chama cha Republican. Watu wamekikataa chama hicho zamu hii. Wamemchagua Barak Hussein Obama, Mswahili, tena baba yake Jaluo. Ameapa jana na vyama vyote viwili sasa vitashirikiana katika kuleta maendeleo. Midahalo yako itabakia Bungeni tu.”
“Kama nilivyosema kila mahali nilipopita. Tupambane wakati wa uchaguzi, baada ya hapo tujenge nchi yetu kwa pamoja. Hata kama hukuridhika na jinsi mwenzako alivyoshinda, yeye ndiye kashinda,yeye ndiye yuko madarakani. Muhimu kushirikiana naye.”
 
Kwa usemi mwingine ni kwamba hata kama wapinzani wataichagua CUF visiwani CCM itaendelea kutawala. Duh! njia kweli bado ni ndefu. Mimi nilidhani serikali inaundwa kutokana na utashi wa watu kumbe ni utashi wa CCM?
 
Kwa usemi mwingine ni kwamba hata kama wapinzani wataichagua CUF visiwani CCM itaendelea kutawala. Duh! njia kweli bado ni ndefu. Mimi nilidhani serikali inaundwa kutokana na utashi wa watu kumbe ni utashi wa CCM?

Wanajua kuwa upinzani ukiachia kutawala visiwani ....na bara nako sio muda mrefu itabidi hali ibadilike, kwa hiyo inafanywa juu chini kuhakikisha kuwa upinzani hauwezi kutawala visiwani.
 
Huyu jamaa anaanza kulewa madaraka kama hayo hapo yalioandikwa ni kweli basi basi tu dicteta on the progress. Sasa mbona hakulinganisha uchaguzi ,amerukia tu eti Bushi kamaliza Obama kashinda yaani ni aibu kwa alichokizungumza, halafu anaenda kuwazungumzia utumbo huo watu wa Pemba ,nafikiri anawasikia tu hawajui walivyo ,anataka kujivisha koti lililowashinda wenzake , Mheshimiwa kama hufahamu hizo barabara hazikujengwa na serikali yako ,hizo ni fedha za hao waPemba wachuma Karafuu mnazowaibia kwa kuwapa bei ndogo.

Mtamaliza njia zote lakini hao WaPemba hawataichagua serikali ya CCM na siyo mtachukua muda mrefu kujenga barabara na kugawa nyavu na madau bali milele hamtoshinda, na itawapata kazi ya kwenda mkiwaua kila unapofanyika Uchaguzi Mkuu na naona kama maneno hayo ni yako basi bila ya shaka yeyote ile mwaka ujao ni zamu yako kwenda kuwaua kwa kulazimisha matokeo.

Ila ndio hivyo Mkapa anapelekwa kwenye Mahakama ya Kimataifa na dai la serikali ya Pemba lipo palepale tena wameshasema lisihusishwe na Chama chochote si wabunge wala wawakilishi bali ni wao wote kama waPemba wamechoshwa kuishi ndani ya ukiritimba.
Eti bara bara ,juzi nilikuwepo huko ukiona hiyo bara bara utadhani plasta iliyotiwa kwenye kidonda,na itakudhihirikia wazi wazi kuwa kuna kitu kinakuja ndio ikatayarishwa,sherehe za Mapinduzi na ziara ya Mheshimiwa Jakaya,hakuna jingine na wala si maendelea kama anavyodai Mkuu wa Nchi,hebu atueleze barabara inayotokea wete kuelekea Konde,barabara ambayo ilikuwa swafi lakini leo mwendo wa robo saa unakuchukua masaa mawili, unajenga mpya wakati za zamani hazipitiki ,kama si kuwadanganya watu ni kitu gani na zaidi ni serikali kujidanganya wenyewe maana hivi sasa watu wameshaamka na kila kinachofanywa kinaonekana kama ni kwa ajili ya maendeleo au kigogo anakuja.

Sijui habari iliyoandikwa inatoka kwenye sosi gani ?
 
Kwahiyo Serikali "imeshindwa" kulipia gharama za kujenga tanki la maji kwa wananchi wake (kitu ambacho ni very cheap indeed) na mpaka yeye Kikwete et al waende uko Japani ndio hawa jamaa waje kutujengea hilo tanki? I think hapa ndugu Kikwete amechemsha.

Tanzania ni nchi tajiri in terms of Natural Resources. Ndugu Kikwete, kama ungeweka priority ya kuhakikisha maliasili zinawanufaisha wananchi na sio wateule wachache, I think tungekuona mtu wa maana sana. Kutetea safari zisizo na tija ni kuwaongezea umaskini watanzania.

Ndugu Kikwete, kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hata kama unatoa hutuba kwa watu wenye uelewa mdogo lakini kumbuka semi (hotuba) zako zinahifadhiwa for future references. Nafikiri hotuba hii ikitumiwa vyuoni ama mashuleni kufundishia wanafunzi itakuwa ni moja ya hotuba zenye ideology mbovu kihistoria.
 
Last edited:
Rais Jakaya Mrisho Kikwete amewaambia wapinzani wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kuwa inaweza kuwachukua muda mrefu mno kupata nafasi ya kuunda Serikali, ama pengine wasiipate kabisa, na hivyo ni muhimu kwao kushirikiana na Serikali ya CCM katika kuwaletea wananchi wa Tanzania Visiwani maendeleo.
Rais pia amesema kuwa ni fitina za kisiasa kwa wapinzani wa Serikali ya SMZ kuibeza na kuikejeli Serikali hiyo kwa madai kuwa haijaleta maendeleo yoyote Tanzania Visiwani.
Aidha Rais amewaambia wananchi wa Pemba kuwa wanayo haki ya kuendelea kumchagua yoyote wanayemtaka ili awe mbunge ama mwakilishi, ili mradi tu waendelee kukabidhi dhamana ya kuendesha Serikali kwa Chama cha Mapinduzi.
Amesisitiza kuwa Serikali ya SMZ na ile ya Muungano zitaendelea kuwaletea maendeleo wananchi wa Visiwani bila upendeleo wala kubagua yoyote kwa sababu huo ndiyo mkataba kati ya Serikali na wananchi, na kwa sababu kuleta maendeleo ni dhamana ya Serikali iliyoko madarakani, na wala siyo wapinzani.
“Madai kuwa Serikali haijafanya lolote wala chcochote ni fitina tu za kisiasa. Unajua midomo kazi yao ni kusema. Unaweza kusema lolote hasa inapokuwa usemaji wenyewe ni wa kufitini, yaani kudanganya watu, ili wakuchague. Mafanikio yamepatikana mengi ndugu wananchi katika elimu, katika barabara. Na hizi barabara tutazijenga pote, hata pale Mtambwe,” alisema na kuongeza:
“Tutamwendeleza kila mtu kwa sababu dhamana ya maendeleo ni yetu katika Serikali. Hawa wengine hawana Serikali. Kazi yao, na wabunge wao, na wawakilishi wao, ni kufoka tu. Sisi ndio wenye dhamani ya Serikali na wala hatubagui.”
Rais aliyasema hayo wakati aliposalimiana na wananchi katika nyakati na matukio tofauti jana, Jumatano, Januari 21, 2009 kwenye siku yake ya pili na ya mwisho ya ziara yake katika Kisiwa cha Pemba ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku sita Tanzania Visiwani. Rais ameanza ziara ya siku nne katika Kisiwa cha Unguja leo, Alhamisi, Januari 22, 2009 baada ya kuwa amekamilisha ziara yenye mafanikio katika Pemba.
Akizungumza na wananchi baada ya kuwa amefungua mradi wa maji wa Kengeja, Mkoa wa Kusini Pemba, Rais alisema kuwa ni muhimu kwa wananchi wote, bila kujali itikadi zao za kisiasa, kushirikiana na Serikali iliyoko madarakani katika kusaka maendeleo.
Alisema kuwa ni kinyume cha taratibu za ushindani wa kidemokrasia kwa chama kimoja kusema kuwa hakiwezi kushirikiana na Serikali iliyoko madarakani kikidai kuwa kinasubiri mpaka kitakapoweza kuunda Serikali.
“Ni muhimu kwa watu kukubali kuwa ipo Serikali iliyoko madarakani hata kama wanakataa jinsi ilivyoingia madarakani. Ukweli ni kwamba ipo na ni muhimu kwa watu wote kushirikiana nayo katika kuleta maendeleo. Maana ukisubiri hiyo Serikali yako inaweza ikachelewa sana ama pengine isije kabisa katika uhai wako,” alisema na kuongeza:
Akizungumzia mabezo na kejeli za wapinzani wa CCM kuwa Serikali ya SMZ haijaleta maendeleo yoyote kwa wananchi, Rais Kikwete aliwaambia wananchi hao wa Kengeja: “Wananchi, hizi ni fitina tu. Unajua midomo kazi yake ni kusema. Unaweza kusema lolote hasa inapokuwa kwenye kufitini, kudanganya watu ili wakuchague.”
Aliongeza Rais Kikwete: “Ukweli ni kwamba mafanikio yamepatikana mengi…iwe kwenye elimu ama barabara. Nimesema kuwa tutatoa huduma za kijamii kwa wananch wote bila kubagua kati ya wale waliotupigia kuara ama wale waliokipigia kile chama kingine. Hata ile barabara ya Mtambwe tutaijenga tu.”
Rais Kikwete alisema kuwa ni muhimu kwa Serikali kuendelea kutoa huduma kwa wananchi bila kubagua kwa sababu Serikali ndiyo yenye dhamana ya kuleta maendeleo, akisisitiza: “Maana wao hawana Serikali, kazi yao na wabunge wao na wawakilishi wao ni kufoka tu. Sisi ndio wenye dhamana ya Serikali. Ujumbe wetu kwa wapinzani wetu ni rahisi kabisa kuwa nyie endeleeni kuwachagua mnaowataka, lakini sisi endeleeni kutukabidhi Serikali na dhamana ya kuleta maendeleo.”
Alisisitiza: “Wao wacha waendelee kutia fitina, kubeza maendeleo, lakini maji safi wanaendelea kunywa. Barabara wanaendelea kupita wakipepeza bendera zao kwa sababu zinateleza kama mgongo wa ngisi. Anapata taabu sana kuisifia Serikali ya CCM hadharani, lakini akikaa na mkewe chumbani anasema kuwa hawa CCM kiboko kwa maendeleo. Lakini akitoa hadharani anabeza akisema hawa CCM watu gani? Lakini maji anakunywa.”
Akizungumza baada ya kuwa amekagua ujenzi wa barabara ya lami kati ya Mkoani na Makombeni katika mkoa huo huo wa Kusini Pemba, Rais Kikwete aliendeleza somo lake kwa wapinzani akisema:
“Ndugu wananchi, msije kudanganywa. Kazi ya maendeleo haiku mikononi mwa mbunge ama mwakilishi. Hii ni kazi na dhamana ya Serikali…zote mbili ya SMZ na Muungano. Mbunge hawezi kujenga barabara ya lami. Sisi ndio wenye dhamani kwa waliotuchagua na hata wale ambao hawakutuchagua”
Alisema kuwa lazima Watanzania watofautishe vipindi vya uchaguzi na vipindi vya maendeleo. “Tutofautishe kipindi cha uchaguzi na kipindi cha maendeleo. Tutambue kuwa siasa za uchaguzi ni siasa za uchaguzi, baada ya hapo mleta maendeleo ni Serikali. Na hata baadhi ya watu wakinuna wakati tukipita, lakini ukweli ni kwamba Serikali tunayo sisi. Anayewaongopea vinginevyo, mwambie hivyo sivyo.”
“Wakati ya ushindani ni wakati wa uchaguzi. Yakitangazwa matokeo hata kama hukuridhika nayo ni lazima ukubali kushirikiana na washindi. Sasa utafanyaje hata kama huyo ndiye mwenye dhamani. Lakini huyo ndiye binadamu, akishakuwa ameshiba ugali na ngisi, basi maneno yanakuwa mengi.”
Akizungumza baada ya kuwa amefungua soko la Mvumoni na kutoa boti na nyavu za uvuvi kwa vikundi mbali mbali, Rais Kikwete amesema kuwa amefurahi kusikia kuwa vikundi vya kupata boti na nyavu havikuchaguliwa kwa ubaguzi wa vyama ana itikadi.
“Nafurahi kusikia kuwa tabia hii haiko kwenye mradi huu. Maana baada ya uchaguzi mtu wa CCM alikuwa akinyimwa huduma dukani ama kukataliwa kubebwa kwenye boti. Sasa sukari ina CCM na CUF? Ama kama kila mwanachama wa chama siasa akianzisha duka lake tutakuwa na maduka mangapi? Aliuliza Rais Kikwete na kusisitiza:
“Mwanademokrasia wa kweli, akimaliza uchaguzi hushirikiana na wenzake katika kuleta maendeleo. Hivi kama Serikali ingekuwa na fikra kama yule anayemkataza mwenzake kupanda boti yake kwa sababu ya itikadi, hivi Pemba ingekuwa maji, ama barabara nzuri, ama maji, ama skuli?”
Rais Kikwete alisema kuwa ni wajibu wa vyama vya siasa kujua kuwa kina mtu anatawala kwa zamu yake ya kutawala kama anachaguliwa na wananchi lakini muhimu ni kushirikiana. “Kila mtu kwa zamu yake. Lakini ushirikiano ni wakati wote. Hivi wewe hutaki kushiriki na Serikali iliyopo ukingojea Serikali yako. Hivi itakuja lini? Na kama haikuja je?”
Alisema kuwa mfano nzuri ni wa Marekani. “Pale Marekani alikuwa ni Rais Bush wa Chama cha Republican. Watu wamekikataa chama hicho zamu hii. Wamemchagua Barak Hussein Obama, Mswahili, tena baba yake Jaluo. Ameapa jana na vyama vyote viwili sasa vitashirikiana katika kuleta maendeleo. Midahalo yako itabakia Bungeni tu.”
“Kama nilivyosema kila mahali nilipopita. Tupambane wakati wa uchaguzi, baada ya hapo tujenge nchi yetu kwa pamoja. Hata kama hukuridhika na jinsi mwenzako alivyoshinda, yeye ndiye kashinda,yeye ndiye yuko madarakani. Muhimu kushirikiana naye.”

sasa mafuta ni yapamoja na mainisha ni ya WATANZANIA shuhuli amekwisha ikamilisha Rais jakwaya kwa maelezo ya hapo juu hakuna tena mvutano
 
Back
Top Bottom