Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Nimesikitishwa na kitendo cha Rais Kikwete ambaye kwa maneno yake alidai kuwa ana uwezo wa kulipia fomu za kugombea lakini alikubali kuchukua tufedha tudogo kwa maskini wa Tanzania ambayo yeye aliamini wamefanya hivyo kwa sababu ya mapenzi yao kwake. Maskini hawa ambao kwa mifano yake Rais kwenye mkutano mkuu walimchangia kuanzia shilingi 200 na fedha nyingine.
- Vijana waliouza maandazi kumchangia shilingi elfu thelathini
- Mama aliyetoa shilingi 200
- Mtoto wa shule aliyetoa fedha za shule kumpa JK
- na wengine wengi..
Mimi ninaombi kabisa.. kama kuna fedha zozote alizochukua kutoka kwa maskini wa Tanzania kuchangia kuchukua fomu na kama ana mpango wa kuchukua tena fedha kwa maskini kama alivyoahidi (kwenye fomu za serikali) naomba chonde.. tafadhali warudishie.
Jilipie mwenyewe kwani tayari una fedha za kutosha. Huna sababu ya kuchangiwa hata senti moja na maskini wa Tanzania.
Ni ombi tu na ni ushauri lenye kufanana na lazima ya aina fulani; usiwafanye maskini wakamlilia Mungu mbinguni.
- Vijana waliouza maandazi kumchangia shilingi elfu thelathini
- Mama aliyetoa shilingi 200
- Mtoto wa shule aliyetoa fedha za shule kumpa JK
- na wengine wengi..
Mimi ninaombi kabisa.. kama kuna fedha zozote alizochukua kutoka kwa maskini wa Tanzania kuchangia kuchukua fomu na kama ana mpango wa kuchukua tena fedha kwa maskini kama alivyoahidi (kwenye fomu za serikali) naomba chonde.. tafadhali warudishie.
Jilipie mwenyewe kwani tayari una fedha za kutosha. Huna sababu ya kuchangiwa hata senti moja na maskini wa Tanzania.
Ni ombi tu na ni ushauri lenye kufanana na lazima ya aina fulani; usiwafanye maskini wakamlilia Mungu mbinguni.