AmaniKatoshi
Senior Member
- Mar 31, 2009
- 158
- 14
Inatia shaka, labda alikuwa anatania tuu, kwani Salva Rweyemanu yuko wapi akanushe?
Kweli JK hapa ka-bore kwa jinsi alivyotumia lugha kutoa ujumbe lakini ule ujumbe wenyewe wa kwamba kupata UKIMWI kupitia ngono baada ya maridhiano ya watu wawili mwanaume na mwanamke ni wa kujitakia. Tatizo hapo JK ametumia lugha isiyofaa kwa kundi la watu wale wenye uelewa mdogo na elimu ya chini au kutokuwa na elimu kabisa ya msingi na kwenye masuala ya ukimwi. Na tafiti zinaonesha ngono ndio njia ambayo inaongoza kwa kusambaza VVU. Yeye angeweza tu kuwaambia namna ambavyo angewasaidia na janga hili kama vile kupunguza kabisa umaskini wao ambao unachochea pia maambukizi kitu ambacho ni ndoto! Pia ameshindwa kufahamu kuwa 'sex' ni moja ya 'basic needs'!
JK na kunyanyapaaa! Jisomee gazeti la mwananchi, 29/09/2010
Akizungumza katika mkutano wake wa awali uliofanyika Kijiji cha Lalago, Kikwete aliunyamazisha umati huo baada ya kuanza kuelezea maambukizi ya Ukimwi yalivyoshamiri kijijini hapo na wilaya nzima ya Maswa.
"Ndugu zangu maambuziki ya ukimwi hapa yako juu sana. Maambukizi hapa Lalago ni asilimia saba, nikiwa na maana kuwa kati ya watu 100, saba wanaugua ukimwi. Maswa ina wagonjwa 3,000 wanaohudumiwa na serikali," alisema Kikwete.
"Sasa, naomba akina mama wanapokwenda kliniki, muombe kupima ukimwi. Ukipata Ukimwi unajitakia kwa hiari yako; unaweza kujikinga kwa kuwa kupata Ukimwi si bahati mbaya; ni bahati mbaya ni kwa mtu aliyebakwa au aliyeongezewa damu isiyo salama."
Kikwete aliongeza kusema: "Lakini wengine ni kwa viherehere; wanapanga kupata kwa kuwa mnapanga siku; saa; na mahala pa kukutania. Sasa basi, mkipanga mkubaliane, nani alete kinga, wewe
au yeye... ndugu zangu tufuate mafundisho ya viongozi wa dini kuwa msivunje amri ya sita.
"Wale ambao bado wasubiri wakati wao na wale ambao wako kwenye ndoa zao wadumishe uaminifu... hapa uaminifu ni mgogoro."
JK na kunyanyapaaa! Jisomee gazeti la mwananchi, 29/09/2010
Akizungumza katika mkutano wake wa awali uliofanyika Kijiji cha Lalago, Kikwete aliunyamazisha umati huo baada ya kuanza kuelezea maambukizi ya Ukimwi yalivyoshamiri kijijini hapo na wilaya nzima ya Maswa.
"Ndugu zangu maambuziki ya ukimwi hapa yako juu sana. Maambukizi hapa Lalago ni asilimia saba, nikiwa na maana kuwa kati ya watu 100, saba wanaugua ukimwi. Maswa ina wagonjwa 3,000 wanaohudumiwa na serikali," alisema Kikwete.
"Sasa, naomba akina mama wanapokwenda kliniki, muombe kupima ukimwi. Ukipata Ukimwi unajitakia kwa hiari yako; unaweza kujikinga kwa kuwa kupata Ukimwi si bahati mbaya; ni bahati mbaya ni kwa mtu aliyebakwa au aliyeongezewa damu isiyo salama."
Kikwete aliongeza kusema: "Lakini wengine ni kwa viherehere; wanapanga kupata kwa kuwa mnapanga siku; saa; na mahala pa kukutania. Sasa basi, mkipanga mkubaliane, nani alete kinga, wewe
au yeye... ndugu zangu tufuate mafundisho ya viongozi wa dini kuwa msivunje amri ya sita.
"Wale ambao bado wasubiri wakati wao na wale ambao wako kwenye ndoa zao wadumishe uaminifu... hapa uaminifu ni mgogoro."
Ni aibu kuwa na rais asiyejua njia ambazo ukimwi unaambukizwa.