TandaleOne
JF-Expert Member
- Sep 4, 2010
- 1,644
- 709
Thursday, 09 September 2010
Waandishi Wetu
MGOMBEA urais kupitia CCM, Jakaya Kikwete ameviponda vyama vya upinzani akisema kuwa huibuka wakati wa uchaguzi tu, ukimalizika vinayeyuka. Kauli hiyo aliitoa jana katika mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika majira ya jioni katika uwanja wa Azimio mjini Handeni, Tanga na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa watu waliokuja kumsikiliza.
"Chagueni kwa mafiga matatu, rais, mbunge na diwani wote wa CCM. Sisi ndiyo wenye uwezo mkubwa wa kuwaletea maendeleo ukilinganisha na wa vyama vya upinzani ambao huibuka wakati wa uchaguzi mkuu pekee, wakishindwa wanapotea," alisema Kikwete na kuongeza.
"Wao wanategemea kupata nguvu kutoka kwa wanachama wa CCM ambao walikigombea katika kura za maoni wakishindwa wanachukia na hukimbilia kwao," alisema. Kikwete aliwaomba wananchi nchini kote kuwachagua wagombea wa CCM katika ngazi zote kwa kuwapigia kura ili waweze kipindi kuingine cha miaka mitano ijayo. Akizungumzia mafanikio ya serikali yake wilayani Handeni katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, Kikwete alisema ni kuongezeka kwa shule za sekondari.
Kikwete alisema wakati anaingia madarakani mwaka 2005, wilaya hiyo ilikuwa na sekondari 11 sasa zimefikia 30 na kwamba idadi ya wanafunzi walioandikishwa kuanza darasa la kwanza kwa sasa wamevuka lengo na kwa zaidi ya asilimia mia moja.
"Awali ilikuwa wakati wa matokeo ya mtihani wa darasa la saba ilikuwa ni kilio kwa kila kaya kutokana na wanafunzi wengi kufanya vibaya, lakini sasa wakati wa matokeo hayo kila nyumba sasa ni kicheko kutokana na watoto wengi kufaulu mitihani yao," alisema Kikwete.
Rais Kikwete alisimama na msafara wake kwenye vijiji vya Kimbe, Viadigwa, Masagala na kufanya mkutano mkubwa Songe katika jimbo la Kilindi, mkoani Tanga ambapo aliahidi kuwaboreshea zaidi sekta za afya, elimu, kilimo, maji na mawasiliano. Akiwa Songe alizungumza na maafisa wafugaji na kuwaambia kuwa ataboresha pia malisho ya mifugo ili kupunguza wafugaji kuhama hama hovyo kwasababu ya kusaka malisho hatua ambayo wakati mwingine husababisha mapigano kati yao na wakulima.
SAU, DP waungana kufungua kesi
Wakati huo huo, vyama hivyo vya Sauti ya Umma (Sau) na Democratic ( DP), vinatarajia kufungua kesi hiyo ya kikatiba Mahakama Kuu leo kuiomba mahakama isimamishe uchaguzi huo Chama cha SAU kinachoongozwa na Paul Kyara na DP, Mchungaji Christopher Mtikila, vimeungana kesi hiyo baada ya kuenguliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) kuwania nafasi ya urais.
Kesi inayopangwa kusimamiwa na wakili Israel Mgusi, ilitarajiwa kufunguliwa jana mchana, lakini ilishindikana kutokana na taratibu kadhaa kutokamilika. Katibu Mwenezi wa Sau, Johnson Mwangosi aliliambia Mwananchi kuwa watafungua kesi hiyo leo asubuhi chini ya kiapo cha dharura.
Alisema katika kesi hiyo inayopinga hatua za Nec kuwaondoa katika kinyang'anyiro cha urais na kwamba wameandaa hoja 19 kutetea ombi lao la kuitaka Nec isitishe mchakato huo. SAU na DP vimeondolewa kwenye kinyang'anyiro hicho baada ya kudaiwa kushindwa kutimiza sharti la kuwa na wanachama 200 kutoka kila mkoa kwa mikoa kumi nchini.
Alisema moja ya maombi yao ni kuitaka mahakama hiyo isitishe kwanza kampeni za urais zinazoendelea hadi kesi hiyo itakapomalizika na wao kuruhusiwa kushiriki. "Sisi ni washiriki halali katika uchaguzi huu, lakini kwa kuwa Makame (Lewis Mwenyekiti wa Nec ) ametuengua bila sababu za msingi, sasa tutaiomba mahakama itamke kuwa sisi ni wagombea halali katika uchaguzi huu; "Tutafungua kesi hii chini ya hati ya dharura na baada ya kuwasilisha hati ya madai yetu tutaiomba mahaka isimamishe kwanza uchaguzi hadi tutakapotendewa haki," alisisitiza Mwangosi.
Mgombea wa urais wa Sau, Kyara alienguliwa na Nec katika kinyang'anyiro hicho Agosti 19 mwaka huu kwa madai ya kushindwa kutimiza sharti la kuwa na wadhamini 200 kwa kila mkoa katika mikoa 10 nchini. Kwa upande wake Mchungaji Mtikila ambaye pia alikuwa ni mgombea wa urais kupitia chama chake cha DP, alienguliwa na Nec katika mchakato huo kwa madai kushindwa kutimiza sharti hilo la wadhamini kutoka mikoa 10.
CUF wamkataa msimamizi wa uchaguzi
Wakati huo huo, CUF kimemkataa Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Sengerema na Buchosa, Erika Msika na wakidai kuwa hawama imani naye kwa sababu ameshindwa kutimiza wajibu amekuwa akitumiwa na wagombea wa CCM.
Akizungumza jana na waandishi wa habari jijini Mwanza kuelezea ziara yake ya kampeni katika mikoa ya Kanda ya ziwa, Mgombea mwenza wa CUF, Juma Haji Duni alisema chama chake kimeamua kumwandikia Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi kutokana na kutoridhika na jinsi alivyolishughulikia pingamizi alilowekewa mgombea wao wa ubunge, Mbaraka Saidi Chiru na mgombea udiwani wa kata ya Katunguru, Pelece Essau Balalukuliliza.
Duni alieleza kuwa makosa ambayo yametumika kuwaengua wagombea wa CUF hayana nguvu, lakini pia msimamizi huyo amekuwa akiwashauri wagombea kujitoa (wa CUF) na kuwaacha wa CCM kuendelea na uchaguzi. "Kwa niaba ya chama change ninatoa tamko rasmi kuwa hatuna imani naye msimamizi huyo wa uchaguzi, kwa vile ametumika na CCM bila ya kuzingatia wajibu wake na kuwaengua wagombea watu" alieleza.
Awali akitoa ufafanuzi wa rufaa hizo jinsi zilivyoshughulikiwa na maimamizi huyo, mkurugenzi wa siasa taifa wa CUF, Mbaraka Maharagande alidai kuwa katika pingamizi la mgombea ubunge, aliyetumika kumuwekea ni Msimamizi Msaidizi wa uchaguzi, Roida Makopora.
Lipumba amtibulia Mkuchika
Naye mgombea wa urais kupitia Chama cha Wananchi, CUF Profesa Ibrahim Lipumba jana aliingia kwa kishindo wilayani Newala na kumponda Waziri wa Habari na Utamaduni, George Mkuchika akidai kuwa ameshindwa kutekeleza ahadi zake hasa kumaliza kero ya maji kwa wapiga kura wake.
"Mkuchika ameshindwa kumaliza tatizo la maji, akidai kuwa eti Newala imeinuka kama meza hivyo maji hayawezi kupanda. Mbona mkoa wa Kilimanjaro una milima, lakini maji yanapanda? Bonde la Mto Niger linafafanana kabisa na Bonde la Mto Ruvuma, lakini wenzetu Niger hawana shida ya maji," alisema Lipumba.
Aliongeza: "Ukitazama Dar es Salaam kuna chuo kikuu, Morogoro kuna chuo kikuu, Dodoma kuna chuo kikuu, Kilimanjaro, Arusha, Mwanza kote kuna nvyuo vikuu, lakini mikoa ya kusini, anzia Pwani, Lindi na Mtwara hakuna vyuo vikuu. Mikoa ya kusini imetengwa. Mkiichagua CUF nitaweka mtu maalumu wa kushughulikia kero za mikoa ya kusini".
Imeandaliwa na James Magai,Dar; Edwin Mjwahuzi, Kilindi; Frederick Katulanda, Mwanza; Hussein Semdoe-Handeni na Elias Msuya, Newala.
Source: Mwananchi
Waandishi Wetu
MGOMBEA urais kupitia CCM, Jakaya Kikwete ameviponda vyama vya upinzani akisema kuwa huibuka wakati wa uchaguzi tu, ukimalizika vinayeyuka. Kauli hiyo aliitoa jana katika mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika majira ya jioni katika uwanja wa Azimio mjini Handeni, Tanga na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa watu waliokuja kumsikiliza.
"Chagueni kwa mafiga matatu, rais, mbunge na diwani wote wa CCM. Sisi ndiyo wenye uwezo mkubwa wa kuwaletea maendeleo ukilinganisha na wa vyama vya upinzani ambao huibuka wakati wa uchaguzi mkuu pekee, wakishindwa wanapotea," alisema Kikwete na kuongeza.
"Wao wanategemea kupata nguvu kutoka kwa wanachama wa CCM ambao walikigombea katika kura za maoni wakishindwa wanachukia na hukimbilia kwao," alisema. Kikwete aliwaomba wananchi nchini kote kuwachagua wagombea wa CCM katika ngazi zote kwa kuwapigia kura ili waweze kipindi kuingine cha miaka mitano ijayo. Akizungumzia mafanikio ya serikali yake wilayani Handeni katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, Kikwete alisema ni kuongezeka kwa shule za sekondari.
Kikwete alisema wakati anaingia madarakani mwaka 2005, wilaya hiyo ilikuwa na sekondari 11 sasa zimefikia 30 na kwamba idadi ya wanafunzi walioandikishwa kuanza darasa la kwanza kwa sasa wamevuka lengo na kwa zaidi ya asilimia mia moja.
"Awali ilikuwa wakati wa matokeo ya mtihani wa darasa la saba ilikuwa ni kilio kwa kila kaya kutokana na wanafunzi wengi kufanya vibaya, lakini sasa wakati wa matokeo hayo kila nyumba sasa ni kicheko kutokana na watoto wengi kufaulu mitihani yao," alisema Kikwete.
Rais Kikwete alisimama na msafara wake kwenye vijiji vya Kimbe, Viadigwa, Masagala na kufanya mkutano mkubwa Songe katika jimbo la Kilindi, mkoani Tanga ambapo aliahidi kuwaboreshea zaidi sekta za afya, elimu, kilimo, maji na mawasiliano. Akiwa Songe alizungumza na maafisa wafugaji na kuwaambia kuwa ataboresha pia malisho ya mifugo ili kupunguza wafugaji kuhama hama hovyo kwasababu ya kusaka malisho hatua ambayo wakati mwingine husababisha mapigano kati yao na wakulima.
SAU, DP waungana kufungua kesi
Wakati huo huo, vyama hivyo vya Sauti ya Umma (Sau) na Democratic ( DP), vinatarajia kufungua kesi hiyo ya kikatiba Mahakama Kuu leo kuiomba mahakama isimamishe uchaguzi huo Chama cha SAU kinachoongozwa na Paul Kyara na DP, Mchungaji Christopher Mtikila, vimeungana kesi hiyo baada ya kuenguliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) kuwania nafasi ya urais.
Kesi inayopangwa kusimamiwa na wakili Israel Mgusi, ilitarajiwa kufunguliwa jana mchana, lakini ilishindikana kutokana na taratibu kadhaa kutokamilika. Katibu Mwenezi wa Sau, Johnson Mwangosi aliliambia Mwananchi kuwa watafungua kesi hiyo leo asubuhi chini ya kiapo cha dharura.
Alisema katika kesi hiyo inayopinga hatua za Nec kuwaondoa katika kinyang'anyiro cha urais na kwamba wameandaa hoja 19 kutetea ombi lao la kuitaka Nec isitishe mchakato huo. SAU na DP vimeondolewa kwenye kinyang'anyiro hicho baada ya kudaiwa kushindwa kutimiza sharti la kuwa na wanachama 200 kutoka kila mkoa kwa mikoa kumi nchini.
Alisema moja ya maombi yao ni kuitaka mahakama hiyo isitishe kwanza kampeni za urais zinazoendelea hadi kesi hiyo itakapomalizika na wao kuruhusiwa kushiriki. "Sisi ni washiriki halali katika uchaguzi huu, lakini kwa kuwa Makame (Lewis Mwenyekiti wa Nec ) ametuengua bila sababu za msingi, sasa tutaiomba mahakama itamke kuwa sisi ni wagombea halali katika uchaguzi huu; "Tutafungua kesi hii chini ya hati ya dharura na baada ya kuwasilisha hati ya madai yetu tutaiomba mahaka isimamishe kwanza uchaguzi hadi tutakapotendewa haki," alisisitiza Mwangosi.
Mgombea wa urais wa Sau, Kyara alienguliwa na Nec katika kinyang'anyiro hicho Agosti 19 mwaka huu kwa madai ya kushindwa kutimiza sharti la kuwa na wadhamini 200 kwa kila mkoa katika mikoa 10 nchini. Kwa upande wake Mchungaji Mtikila ambaye pia alikuwa ni mgombea wa urais kupitia chama chake cha DP, alienguliwa na Nec katika mchakato huo kwa madai kushindwa kutimiza sharti hilo la wadhamini kutoka mikoa 10.
CUF wamkataa msimamizi wa uchaguzi
Wakati huo huo, CUF kimemkataa Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Sengerema na Buchosa, Erika Msika na wakidai kuwa hawama imani naye kwa sababu ameshindwa kutimiza wajibu amekuwa akitumiwa na wagombea wa CCM.
Akizungumza jana na waandishi wa habari jijini Mwanza kuelezea ziara yake ya kampeni katika mikoa ya Kanda ya ziwa, Mgombea mwenza wa CUF, Juma Haji Duni alisema chama chake kimeamua kumwandikia Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi kutokana na kutoridhika na jinsi alivyolishughulikia pingamizi alilowekewa mgombea wao wa ubunge, Mbaraka Saidi Chiru na mgombea udiwani wa kata ya Katunguru, Pelece Essau Balalukuliliza.
Duni alieleza kuwa makosa ambayo yametumika kuwaengua wagombea wa CUF hayana nguvu, lakini pia msimamizi huyo amekuwa akiwashauri wagombea kujitoa (wa CUF) na kuwaacha wa CCM kuendelea na uchaguzi. "Kwa niaba ya chama change ninatoa tamko rasmi kuwa hatuna imani naye msimamizi huyo wa uchaguzi, kwa vile ametumika na CCM bila ya kuzingatia wajibu wake na kuwaengua wagombea watu" alieleza.
Awali akitoa ufafanuzi wa rufaa hizo jinsi zilivyoshughulikiwa na maimamizi huyo, mkurugenzi wa siasa taifa wa CUF, Mbaraka Maharagande alidai kuwa katika pingamizi la mgombea ubunge, aliyetumika kumuwekea ni Msimamizi Msaidizi wa uchaguzi, Roida Makopora.
Lipumba amtibulia Mkuchika
Naye mgombea wa urais kupitia Chama cha Wananchi, CUF Profesa Ibrahim Lipumba jana aliingia kwa kishindo wilayani Newala na kumponda Waziri wa Habari na Utamaduni, George Mkuchika akidai kuwa ameshindwa kutekeleza ahadi zake hasa kumaliza kero ya maji kwa wapiga kura wake.
"Mkuchika ameshindwa kumaliza tatizo la maji, akidai kuwa eti Newala imeinuka kama meza hivyo maji hayawezi kupanda. Mbona mkoa wa Kilimanjaro una milima, lakini maji yanapanda? Bonde la Mto Niger linafafanana kabisa na Bonde la Mto Ruvuma, lakini wenzetu Niger hawana shida ya maji," alisema Lipumba.
Aliongeza: "Ukitazama Dar es Salaam kuna chuo kikuu, Morogoro kuna chuo kikuu, Dodoma kuna chuo kikuu, Kilimanjaro, Arusha, Mwanza kote kuna nvyuo vikuu, lakini mikoa ya kusini, anzia Pwani, Lindi na Mtwara hakuna vyuo vikuu. Mikoa ya kusini imetengwa. Mkiichagua CUF nitaweka mtu maalumu wa kushughulikia kero za mikoa ya kusini".
Imeandaliwa na James Magai,Dar; Edwin Mjwahuzi, Kilindi; Frederick Katulanda, Mwanza; Hussein Semdoe-Handeni na Elias Msuya, Newala.
Source: Mwananchi