Wa Ndima
JF-Expert Member
- Aug 13, 2010
- 1,526
- 323
Wote tumesikia au kusoma kuhusu tamko la Jeshi kuhusu Uchaguzi Mkuu wa 31 October, 2010.
JWTZ kutoa angalizo hili ni kujidhalilisha ingawa ninaamini kabisa kuwa amri hii imetoka kwa KIKWETE akiwa kama Amiri Jeshi Mkuu watoe tamko hilo. Kwa nini, na kwa wakati gani kama hatujafikia kipindi hicho cha vurugu kiasi kwamba Jeshi la Polisi Tanzania limeshindwa? Basi watwambie kama hakuna Jeshi la Polisi Tanzania kiasi cha wao kutoa angalizo hilo.
Huku ni kutisha wananchi katika haki yao ya msingi, ni kupumbaza watu na kuwafanya wajinga uendelee kutawala. Kikwete ukiwa kama amiri jeshi mkuu kwa wakati huu kabla ya Oktoba 31 umekosea sana na tumekutambua wewe ni mtu usiyekubali kushindwa, kwako ushindi ni lazima. Unadhani itakuwa rahisi kihivyo?
Watanzania wasiotaka mabadiliko na maendeleo kwa nchi yao wataichagua CCM, lakini ikumbukwe kuwa ni hiyohiyo CCM iliyotufikisha hapa kwenye umasikini huu mkubwa tulionao. Ni hawahawa walioshindwa kudhibiti mfumuko wa bei. Ndio hawahawa wanaotuletea uchungu na shida katika nchi yetu wenyewe. Wakoloni Weusi, ndugu zetu,jamaa na rafiki zetu wa tangu udogoni.Wananchitwendeni tukapige Kura kisha tuzilinde kura hizo dhidi ya madhalimu. Tusikae jirani ya vituo vya kupigia kura ila mbali na eneo la kupigia kura na kuchukua tahadhari kwa yeyote atakayekwenda eneo la kuhesabia kura baada ya muda wa mwisho wa kupiga kura hasa kipindi cha kuhesabu kura hizo. Najua Polisi watamwagwa kuhakikisha mmerudi majumbani nafasi ambayo wataitaka sana, jigaweni katika zamu zenu kulinda haki yenu mpaka kieleweke, msiamini mawakala pekee nao ni binadamu, kila mmoja awe mlinzi wa kura yake. Je wataweza kutuhonga sote?
Kama kuumia kwa miaka mingine mitano tutaumia sote na kizazi chetu. Tusifanye makosa tena
JWTZ kutoa angalizo hili ni kujidhalilisha ingawa ninaamini kabisa kuwa amri hii imetoka kwa KIKWETE akiwa kama Amiri Jeshi Mkuu watoe tamko hilo. Kwa nini, na kwa wakati gani kama hatujafikia kipindi hicho cha vurugu kiasi kwamba Jeshi la Polisi Tanzania limeshindwa? Basi watwambie kama hakuna Jeshi la Polisi Tanzania kiasi cha wao kutoa angalizo hilo.
Huku ni kutisha wananchi katika haki yao ya msingi, ni kupumbaza watu na kuwafanya wajinga uendelee kutawala. Kikwete ukiwa kama amiri jeshi mkuu kwa wakati huu kabla ya Oktoba 31 umekosea sana na tumekutambua wewe ni mtu usiyekubali kushindwa, kwako ushindi ni lazima. Unadhani itakuwa rahisi kihivyo?
Watanzania wasiotaka mabadiliko na maendeleo kwa nchi yao wataichagua CCM, lakini ikumbukwe kuwa ni hiyohiyo CCM iliyotufikisha hapa kwenye umasikini huu mkubwa tulionao. Ni hawahawa walioshindwa kudhibiti mfumuko wa bei. Ndio hawahawa wanaotuletea uchungu na shida katika nchi yetu wenyewe. Wakoloni Weusi, ndugu zetu,jamaa na rafiki zetu wa tangu udogoni.Wananchitwendeni tukapige Kura kisha tuzilinde kura hizo dhidi ya madhalimu. Tusikae jirani ya vituo vya kupigia kura ila mbali na eneo la kupigia kura na kuchukua tahadhari kwa yeyote atakayekwenda eneo la kuhesabia kura baada ya muda wa mwisho wa kupiga kura hasa kipindi cha kuhesabu kura hizo. Najua Polisi watamwagwa kuhakikisha mmerudi majumbani nafasi ambayo wataitaka sana, jigaweni katika zamu zenu kulinda haki yenu mpaka kieleweke, msiamini mawakala pekee nao ni binadamu, kila mmoja awe mlinzi wa kura yake. Je wataweza kutuhonga sote?
Kama kuumia kwa miaka mingine mitano tutaumia sote na kizazi chetu. Tusifanye makosa tena
Sijapata kuona mwanasiasa mwerevu na mwenye hekima kama Dr. Slaa. Ni mtu anayeipenda Tanzania kwa moyo ndo maana hakupanga kugombea lakini alipoombwa alijitolea. Huyu ndiye Nyerere aliyemsema kwamba Ikulu haikimbiliwi ni mzigo. Lakini leo tunaona who is dying for IKULU. Nakuambia Dr. Slaa asingeombwa kugombea wala asingejitokeza kamwe ila kwa kuwa tumemtaka achukue hatamu za kutuvusha hapa tulipo kwenda kwenye Tanzania bora basi amekubali na anaifanya vyema kazi yake.
Sijapata kuona kwa mara ya kwanza vyombo vya dola vikifanya kazi kwa maslahi ya watawala kama sasa. Siamini kwamba TISS wametumwa mikoani kwa ajili ya maslahi ya CCM. inaonesha nani ananufaika na watawala wabovu. Sio viongozi peke yake bali kuna kundi kubwa nyuma yake ambalo ndo wanufaikaji wakubwa wa uongozi mbovu nchi hii. Kumbukeni Kagoda, Deep Green, Meremeta, Mwanancho Gold et all.