Elections 2010 Kikwete Umekosea Mno!

Wa Ndima

JF-Expert Member
Aug 13, 2010
1,526
323
Wote tumesikia au kusoma kuhusu tamko la Jeshi kuhusu Uchaguzi Mkuu wa 31 October, 2010.

JWTZ kutoa angalizo hili ni kujidhalilisha ingawa ninaamini kabisa kuwa amri hii imetoka kwa KIKWETE akiwa kama Amiri Jeshi Mkuu watoe tamko hilo. Kwa nini, na kwa wakati gani kama hatujafikia kipindi hicho cha vurugu kiasi kwamba Jeshi la Polisi Tanzania limeshindwa? Basi watwambie kama hakuna Jeshi la Polisi Tanzania kiasi cha wao kutoa angalizo hilo.

Huku ni kutisha wananchi katika haki yao ya msingi, ni kupumbaza watu na kuwafanya wajinga uendelee kutawala. Kikwete ukiwa kama amiri jeshi mkuu kwa wakati huu kabla ya Oktoba 31 umekosea sana na tumekutambua wewe ni mtu usiyekubali kushindwa, kwako ushindi ni lazima. Unadhani itakuwa rahisi kihivyo?

Watanzania wasiotaka mabadiliko na maendeleo kwa nchi yao wataichagua CCM, lakini ikumbukwe kuwa ni hiyohiyo CCM iliyotufikisha hapa kwenye umasikini huu mkubwa tulionao. Ni hawahawa walioshindwa kudhibiti mfumuko wa bei. Ndio hawahawa wanaotuletea uchungu na shida katika nchi yetu wenyewe. Wakoloni Weusi, ndugu zetu,jamaa na rafiki zetu wa tangu udogoni.Wananchitwendeni tukapige Kura kisha tuzilinde kura hizo dhidi ya madhalimu. Tusikae jirani ya vituo vya kupigia kura ila mbali na eneo la kupigia kura na kuchukua tahadhari kwa yeyote atakayekwenda eneo la kuhesabia kura baada ya muda wa mwisho wa kupiga kura hasa kipindi cha kuhesabu kura hizo. Najua Polisi watamwagwa kuhakikisha mmerudi majumbani nafasi ambayo wataitaka sana, jigaweni katika zamu zenu kulinda haki yenu mpaka kieleweke, msiamini mawakala pekee nao ni binadamu, kila mmoja awe mlinzi wa kura yake. Je wataweza kutuhonga sote?

Kama kuumia kwa miaka mingine mitano tutaumia sote na kizazi chetu. Tusifanye makosa tena

Sijapata kuona mwanasiasa mwerevu na mwenye hekima kama Dr. Slaa. Ni mtu anayeipenda Tanzania kwa moyo ndo maana hakupanga kugombea lakini alipoombwa alijitolea. Huyu ndiye Nyerere aliyemsema kwamba Ikulu haikimbiliwi ni mzigo. Lakini leo tunaona who is dying for IKULU. Nakuambia Dr. Slaa asingeombwa kugombea wala asingejitokeza kamwe ila kwa kuwa tumemtaka achukue hatamu za kutuvusha hapa tulipo kwenda kwenye Tanzania bora basi amekubali na anaifanya vyema kazi yake.

Sijapata kuona kwa mara ya kwanza vyombo vya dola vikifanya kazi kwa maslahi ya watawala kama sasa. Siamini kwamba TISS wametumwa mikoani kwa ajili ya maslahi ya CCM. inaonesha nani ananufaika na watawala wabovu. Sio viongozi peke yake bali kuna kundi kubwa nyuma yake ambalo ndo wanufaikaji wakubwa wa uongozi mbovu nchi hii. Kumbukeni Kagoda, Deep Green, Meremeta, Mwanancho Gold et all.
 
Kwani wewe ni mgeni wa huyu jamaa? Maana kila wakati yeye ni kukosea. Nadhani ni kutapatapa tu maana ameona watu wamekigeuka chama chake na hawana imani naye na serikali yake.
 
hivi , kuna wiki inapita bila jk kuongopewa au kuingizwa mkenge na washauri wake
 
Kwani wewe ni mgeni wa huyu jamaa? Maana kila wakati yeye ni kukosea. Nadhani ni kutapatapa tu maana ameona watu wamekigeuka chama chake na hawana imani naye na serikali yake.

Walidhani ujio wa Dr Slaa ni mbwembwe tu! wakachomeka upadri na kutumwa na kanisa, watanzania wakasema No,no! wakachomeka ndoa na maisha binafsi,Watanzania wanazidi kusema No,no, no! CCM wameangalia upepo na kutambua wazi kuwa ushindi 2010 ni mtihani. Ndio maana wamealika taasisi nyeti. Ni wiki moja tu iliyopita Mwenyekiti wa NEC amesifu kampeni kuwa za kistaarabu na zisizo na fujo, huyu ni Jaji Makame! Sasa Luteni Kanali Shimbo anaposema amani inavunjika atueleze wapi, vinginevyo katumwa na boss atishe watz.
GO WAPINZANI GO!
 
Walidhani ujio wa Dr Slaa ni mbwembwe tu! wakachomeka upadri na kutumwa na kanisa, watanzania wakasema No,no! wakachomeka ndoa na maisha binafsi,Watanzania wanazidi kusema No,no, no! CCM wameangalia upepo na kutambua wazi kuwa ushindi 2010 ni mtihani. Ndio maana wamealika taasisi nyeti. Ni wiki moja tu iliyopita Mwenyekiti wa NEC amesifu kampeni kuwa za kistaarabu na zisizo na fujo, huyu ni Jaji Makame! Sasa Luteni Kanali Shimbo anaposema amani inavunjika atueleze wapi, vinginevyo katumwa na boss atishe watz.
GO WAPINZANI GO!

Noted
 
Wote tumesikia au kusoma kuhusu tamko la Jeshi kuhusu Uchaguzi Mkuu wa 31 October, 2010.

JWTZ kutoa angalizo hili ni kujidhalilisha ingawa ninaamini kabisa kuwa amri hii imetoka kwa KIKWETE akiwa kama Amiri Jeshi Mkuu watoe tamko hilo. Kwa nini, na kwa wakati gani kama hatujafikia kipindi hicho cha vurugu kiasi kwamba Jeshi la Polisi Tanzania limeshindwa? Basi watwambie kama hakuna Jeshi la Polisi Tanzania kiasi cha wao kutoa angalizo hilo.

Huku ni kutisha wananchi katika haki yao ya msingi, ni kupumbaza watu na kuwafanya wajinga uendelee kutawala. Kikwete ukiwa kama amiri jeshi mkuu kwa wakati huu kabla ya Oktoba 31 umekosea sana na tumekutambua wewe ni mtu usiyekubali kushindwa, kwako ushindi ni lazima. Unadhani itakuwa rahisi kihivyo?

Watanzania wasiotaka mabadiliko na maendeleo kwa nchi yao wataichagua CCM, lakini ikumbukwe kuwa ni hiyohiyo CCM iliyotufikisha hapa kwenye umasikini huu mkubwa tulionao. Ni hawahawa walioshindwa kudhibiti mfumuko wa bei. Ndio hawahawa wanaotuletea uchungu na shida katika nchi yetu wenyewe. Wakoloni Weusi, ndugu zetu,jamaa na rafiki zetu wa tangu udogoni.Wananchitwendeni tukapige Kura kisha tuzilinde kura hizo dhidi ya madhalimu. Tusikae jirani ya vituo vya kupigia kura ila mbali na eneo la kupigia kura na kuchukua tahadhari kwa yeyote atakayekwenda eneo la kuhesabia kura baada ya muda wa mwisho wa kupiga kura hasa kipindi cha kuhesabu kura hizo. Najua Polisi watamwagwa kuhakikisha mmerudi majumbani nafasi ambayo wataitaka sana, jigaweni katika zamu zenu kulinda haki yenu mpaka kieleweke, msiamini mawakala pekee nao ni binadamu, kila mmoja awe mlinzi wa kura yake. Je wataweza kutuhonga sote?

Kama kuumia kwa miaka mingine mitano tutaumia sote na kizazi chetu. Tusifanye makosa tena
Mkuu umenena vyema kabisa. unisome kwenye bold yako.
Kama vyama vya upinzani vinasoma hapa, wajipange vyema na mawakala wao kwani inawezekana hizo kura zisiletwe bali zikawa zimeingizwa kituoni usiku wake au jana yake. Hivyo kabla ya kupigwa kura mawakala wakague vituo vya kura chini ya uangalizi wa polisi na waangalizi kuhakiki emptiness na uhakika wa masanduku yaliyopo. Mwaka huu kuna vioja vingi vitatokea. kuna watu wameapa kuwa hatoki mtu hata kama tukisema nooooooo!!!!
 
Mkuu umenena vyema kabisa. unisome kwenye bold yako.
Kama vyama vya upinzani vinasoma hapa, wajipange vyema na mawakala wao kwani inawezekana hizo kura zisiletwe bali zikawa zimeingizwa kituoni usiku wake au jana yake. Hivyo kabla ya kupigwa kura mawakala wakague vituo vya kura chini ya uangalizi wa polisi na waangalizi kuhakiki emptiness na uhakika wa masanduku yaliyopo. Mwaka huu kuna vioja vingi vitatokea. kuna watu wameapa kuwa hatoki mtu hata kama tukisema nooooooo!!!!

Nimekusoma sana
 
mwache ajidanganye kutegemea jeshi, lakini lazima ajifunze kwa kuangalia nchi nyingine nazo zilikuwa na majeshi kama yeye
 
Nguruvi3; Your amnalysis is very good.
Walidhani ujio wa Dr Slaa ni mbwembwe tu! wakachomeka upadri na kutumwa na kanisa, watanzania wakasema No,no! wakachomeka ndoa na maisha binafsi,Watanzania wanazidi kusema No,no, no! CCM wameangalia upepo na kutambua wazi kuwa ushindi 2010 ni mtihani. Ndio maana wamealika taasisi nyeti. Ni wiki moja tu iliyopita Mwenyekiti wa NEC amesifu kampeni kuwa za kistaarabu na zisizo na fujo, huyu ni Jaji Makame! Sasa Luteni Kanali Shimbo anaposema amani inavunjika atueleze wapi, vinginevyo katumwa na boss atishe watz.
GO WAPINZANI GO!

Keep it up
 
mwenye akili zake anajua nn cha kufanya, mm nitawashangaa wananchi ambao baada ya kupiga kura watabaki vtuoni iwe mbali au karibu kwa dai la kulinda kura

na ninawashangaa wenye kuwashawishi wananchi kubakia kwa dai hilo hilo

wanataka kuwaingiza wananchi kwenye matatizo na vyombo vya dola makusudi, wao watakuwa wametimiza matashi yao kisiasa na kuchafua jina la nchi yetu, ila wananchi watakuwa wameumizwa kwa kuhatarisha amani, na maisha yao yatakuwa hatarini

nakumbuka vyema CUF walipowatumia wananchi kuwa kama ngao yao ya kufanikisha ajenda yao, wananchi wengi walikufa, walikua vilema na kuhama nchi kwa matashi ya watu wachache

jee sasa malengo yao yamefanikiwa wamewakumbuka walioumia kwa matashi yao ?

nasisitiza hakuna haja ya kuhatarisha maisha ya wananchi huku sote tukijua kwamba:-

kila chama kimepewa nafasi ya kuwa na mawakala wa kutosha kwenye vituo vya kuhesabia kura(kitu ambacho kama kuna udanganyifu wataripoti kwa vyama vyao)

kutakuwa na wasimamizi wa ndani na wa nje kushuhudia jinsi gani uchaguzi unavyoendeshwa na mwisho watatoa ripoti zao ambazo kila mtu anaamini wataeleza mapungufu na matimilifu ya zoezi zima

wagombea watatakiwa kusaini matokeo katika vituo vyao kukubali kushinda au kushindwa na kama kweli kuna dhuluma wagombea watakataa kusaini

sheria zipo ambazo tumezitunga kwa kushirikiana ni nn cha kufanya baada ya matokeo kutangazwa na haujaridhika

sasa nani anaweza kutwambia kuna mchango gani wa hao wananchi watapokaa nje ya kituo iwe mbali au karibu na uhesabuji wa kura na kulinda kura?


tuwe pamoja kudumisha amani ya nchi yetu na tusiwe wapuuzi na wajinga au kubomoa nyumba yetu kwa kuchochewa na wageni au nyumba za jirani
 
Unajua JK anajua fika october 31 ataangukia pua so solution ni kuchakachua kura.
Sasa kamwomba Shimbo asaidie kupiga bit ila watu ata kama hawataridhika na matokeo wawe watulivu.
JK anashindwa soma alama za nyakati kuwa kuna watz wako tayari kufa kwa ajili ya kutetea haki yao.
Ni kujiandaa na chemli za kutosha ili wakikata umeme kwa ajili ya kuchakachua watu mwawasha chemli niko tayari ata kuweka silence gari yangu ili mwanga wa taa utumike kuhesbia kura.
TUMECHOKA KUONGOZWA NA WATU WASIOTUJARI
 
mwenye akili zake anajua nn cha kufanya, mm nitawashangaa wananchi ambao baada ya kupiga kura watabaki vtuoni iwe mbali au karibu kwa dai la kulinda kura

na ninawashangaa wenye kuwashawishi wananchi kubakia kwa dai hilo hilo

wanataka kuwaingiza wananchi kwenye matatizo na vyombo vya dola makusudi, wao watakuwa wametimiza matashi yao kisiasa na kuchafua jina la nchi yetu, ila wananchi watakuwa wameumizwa kwa kuhatarisha amani, na maisha yao yatakuwa hatarini

nakumbuka vyema CUF walipowatumia wananchi kuwa kama ngao yao ya kufanikisha ajenda yao, wananchi wengi walikufa, walikua vilema na kuhama nchi kwa matashi ya watu wachache

jee sasa malengo yao yamefanikiwa wamewakumbuka walioumia kwa matashi yao ?

nasisitiza hakuna haja ya kuhatarisha maisha ya wananchi huku sote tukijua kwamba:-

kila chama kimepewa nafasi ya kuwa na mawakala wa kutosha kwenye vituo vya kuhesabia kura(kitu ambacho kama kuna udanganyifu wataripoti kwa vyama vyao)

kutakuwa na wasimamizi wa ndani na wa nje kushuhudia jinsi gani uchaguzi unavyoendeshwa na mwisho watatoa ripoti zao ambazo kila mtu anaamini wataeleza mapungufu na matimilifu ya zoezi zima

wagombea watatakiwa kusaini matokeo katika vituo vyao kukubali kushinda au kushindwa na kama kweli kuna dhuluma wagombea watakataa kusaini

sheria zipo ambazo tumezitunga kwa kushirikiana ni nn cha kufanya baada ya matokeo kutangazwa na haujaridhika

sasa nani anaweza kutwambia kuna mchango gani wa hao wananchi watapokaa nje ya kituo iwe mbali au karibu na uhesabuji wa kura na kulinda kura?


tuwe pamoja kudumisha amani ya nchi yetu na tusiwe wapuuzi na wajinga au kubomoa nyumba yetu kwa kuchochewa na wageni au nyumba za jirani

Nimekusoma.! lakini naona nawe ni uko na hiyo system ya kutaka walio wengi waendelee kuumia na uongozi usio na manufaa kwao. Hongera kwa hilo mTu wa Pwani.
 
Nimekusoma.! lakini naona nawe ni uko na hiyo system ya kutaka walio wengi waendelee kuumia na uongozi usio na manufaa kwao. Hongera kwa hilo mTu wa Pwani.


wahtever the case it is, tufate taratibu ambazo ni kweli zitasaidia na sio kuleta upuuzi

kazi yetu kuu ni kuwahmiza wakapige kura, wasiuze shahada na wampigie wanaemuona anafaa na hapa si vibaya mkajinadi ati nyie hasa mnafaaa

baada ya kupiga kura muwashukuru na muwambie kazi yenu imeisha na sasa ni kazi yetu kulinda kura zenu na subirini mushangirie hilo ndio jukumu la chama chenye akili sio kuwaangamiza wanachama wake wakijua nn kitafuatia

mbona wao hawakai vituoni baada ya kupiga kura ?
 
wahtever the case it is, tufate taratibu ambazo ni kweli zitasaidia na sio kuleta upuuzi

kazi yetu kuu ni kuwahmiza wakapige kura, wasiuze shahada na wampigie wanaemuona anafaa na hapa si vibaya mkajinadi ati nyie hasa mnafaaa

baada ya kupiga kura muwashukuru na muwambie kazi yenu imeisha na sasa ni kazi yetu kulinda kura zenu na subirini mushangirie hilo ndio jukumu la chama chenye akili sio kuwaangamiza wanachama wake wakijua nn kitafuatia

mbona wao hawakai vituoni baada ya kupiga kura ?

Haina haja hiyo itakuwa ni sawa na kujidhulumu tu kama una wasi wasi hutatendewa haki inabidi ujilinde dhidi ya hiyo dhulma mimi sioni vibaya iwapo watu watakaa mbali na kituo kwa madhumuni hayo ya kuwa asiingie mtu au kikundi chochote baada ya muda wa mwisho wa kupiga kura na sio lazima kila mpiga kura akawepo inaweza kuwa hata watu wa2 au wa3 tu ili kuwahakikishia wengine imani zao, unajua jambo moja kuu ni kwamba watu wamekosa imani na uongozi wao hivyo wana shauku ya kutaka mabadiliko na wako tayari kubadilika hiyo ni vyema wakaamini kile wakitakacho kuwa kiwe na hata kama kisipokuwa basi kimefanyika kwa haki, lakini sio kuwaambia wamwage damu au walete vurugu Tanzania sio nchi ya mambo haya mabaya abadn.
 
Haina haja hiyo itakuwa ni sawa na kujidhulumu tu kama una wasi wasi hutatendewa haki inabidi ujilinde dhidi ya hiyo dhulma mimi sioni vibaya iwapo watu watakaa mbali na kituo kwa madhumuni hayo ya kuwa asiingie mtu au kikundi chochote baada ya muda wa mwisho wa kupiga kura na sio lazima kila mpiga kura akawepo inaweza kuwa hata watu wa2 au wa3 tu ili kuwahakikishia wengine imani zao, unajua jambo moja kuu ni kwamba watu wamekosa imani na uongozi wao hivyo wana shauku ya kutaka mabadiliko na wako tayari kubadilika hiyo ni vyema wakaamini kile wakitakacho kuwa kiwe na hata kama kisipokuwa basi kimefanyika kwa haki, lakini sio kuwaambia wamwage damu au walete vurugu Tanzania sio nchi ya mambo haya mabaya abadn.


bado sijakuelewa, wao wanasema wakae wote, halafu hao waili si weshakuwamo kwenye vituo kama mawakala na wanajuana itakuwaje aje wa nje wasimtambue. huyo wa nje atawezaje kutofautisha akija observer na wizi wa kura? sioni logic ni kuwasumbua tu na kama watu wawili watatu kuna haja gani ya chama kutangaza si wawateue siri na wafuatilie kisiri siri

huwaamini viongozi wepi ? wachama chako? maana wao ndio walioteuwa mawakala wenu, au tume ? kama tume kwa nn uliamua kuingia kwenye uchaguzi?

hawa wanatafuta visingizio vya kuleta vurugu na kwa hilo katu nchi haiwezi kuwavumilia
 
Back
Top Bottom