Lukolo
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 5,143
- 3,196
Hayo maghala yalikuwepo toka enzi ya Nyerere miaka ya sabini.Je mwaka 1978 Prof.Tibaijuka alikuwa mkuu wa UN Habitat.?
Pili je ni makambi ya jeshi yalijengwa karibu na makazi ya watu au watu walijenga karibu na makambi ya jeshi?
Naomba majibu halafu utajua validity ya thread yako
Je umoja wa mataifa unaruhusiwa kuingilia shughuli za kila siku za serikali za nchi?
Kwenye hoja ya kwamba watu ndo walijenga karibu na kambi za jeshi, napata kigugumizi kuikubali. Maana kwa kusema hivyo, ni sawa na kusema Dar haikupaswa kuwa na wakazi. Maana pande zote za Dar es salaam zimezungukwa na kambi za jeshi zenye silaha. Tuanzie Mbagala, Kigamboni, Mgulani, Tabata (makuburi), uwanja wa ndege, gongo la mboto, upanga, changanyikeni, kunduchi, Lugalo etc. Hadi hapo unaweza kuona kwamba mahali salama kwa maisha ya binadamu kwa Dar es salaam Nzima ni magomeni na manzese tu. Sasa watu milioni nne wote waliopo Dar es salaam wangetosha kuishi Magomeni na Manzese?