Elections 2010 Kikwete: Sijawahi kunyonga

Hajawahi kunyonga...........kwa hiyo? Haoni sababu basi ya kufutilia mbali adhabu ya kifo? Au anatumia kama mtaji wa kisiasa
 
Unapokuwa na mkulu anaropoka kwa kufurahisha umati hii ni hatari sana. Huyu jamaa akiri zake ni za-kimbayuwawayu hivi. Muuaji ni muuaji tu. Tumeshuhudia mauaji ya kinyama kwa watanzania wengi wasio na hatia kwa rangi zote bila kubagua kuwa huyu ni albino.

Mbona hajawahi kuwanyonga?? Au anatafuta kura kupitia Albino. Ni kweli kila mtanzania aliguswa sana na mauaji ya wenzetu albino. Lakini yeye kama Rais haitaji kusema maneno hayo hadharani.

Kama anachukia watu wanaoua wanadamu wenzao basi aidhinishe wanyongwe wote bila ubaguzi.
 
Unajua, kuua siyo mpaka utumie silaha au unyonge kwa mikono. Kuua kunaweza kuwa kwa ulimi kupitia matamshi, kwa kupuuza hali duni ya mtu hadi anakufa kwa njaa, kwa kuchafua mazingira, kwa kuwaachia huru mafisadi au kutowachukulia hatua baada ya kukwapua mabilioni ambayo yangetumika kununulia chakula wakati wa njaa au kununua madawa hospitalini.... je, hayo yote na mengineyo kama hayo hayamaanishi ''kuua''? Au mpaka ushike panga na kuidhinisha kwa kalamu? Tusichore graph kwa kutumia point moja.
 
RAIS Jakaya Kikwete amesema, tangu aingie madarakani Desemba 2005, hajawahi kuidhinisha kunyongwa kwa mtu yeyote.

Kikwete amesema, atatoa uamuzi wa kunyongwa au la kwa watu waliotiwa hatiani kwa kuua albino, suala hilo likifika mezani kwake.

Rais Kikwete alibainisha hayo juzi kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini hapa, wakati akihutubia maelfu ya wananchi katika mkutano wa kampeni kuomba achaguliwe tena kuongoza Tanzania.

"Tuliendesha kura za maoni hapa juu ya suala la watu wanaoua albino.Baada ya kura hizo, wengine wanachunguzwa hadi sasa, wengine wamefungwa na mahakama," alisema Rais Kikwete na kuongeza:

"Baada ya hukumu ya mahakama, baadhi ya viongozi wa albino wamenitumia ujumbe na kutaka wale waliohukumiwa kunyongwa, niwanyonge.

"Sijawahi kunyonga hata mtu mmoja tangu niingie madarakani, lakini nitaamua suala hilo likifika mezani kwangu."

Mahakama Kuu ya Tanzania katika mikoa ya Mwanza na Shinyanga, imetoa hukumu za kifo hadi kunyongwa mwaka jana kwa watu wapatao saba ambao iliwatia hatiani kwa mauaji ya albino.

Rais hataki ku uphold the law of the land, hataki kunyonga wauaji kibao waliohukumiwa na mahakama.

Lakini anataka kunyonga kwa kufuata process zinazoanza na extra judicial circuses za kura za maoni, kura ambazo zinaweza kuwa nothing but a witch hunt, literally. Mwinyi alishajiuzulu uwaziri wa mambo ya ndani kwa sababu vibibi vizee vyenye macho mekundu viliuawa Shinyanga, hii kura ya maoni ina tofauti gani na another witch hunt itakayoweza kusema "vibibi vyenye macho mekundu ndivyo vinavyoua ma albino"

Yeye mwenyewe kashasema watanzania 70% ni bendera kufuata upepo, sasa anataka kuua watu kwa sababu ya kura ya maoni ya watu ambao 70% ni bendera kufuata upepo na wanaweza kuwa manipulated na mtu yeyote tu kumpigia adui yake kura ya kuwa muuaji ?

Huyu Kikwete vipi ?
 
Back
Top Bottom