Watanzania wanalia, kina Mkapa wako wapi?
Baada ya kushindwa kutekeleza ahadi yake ya mwaka 2005 ya kuleta "Maisha Bora kwa kila Mtanzania" kupitia kauli mbiu yake ya Ari mpya, NGUvu mpya na KAsi mpya (ANGUKA), sasa CCM inakuja na Ari zaidi, Nguvu zaidi na Kasi zaidi (ANGUKA ZAIDI) kwenye uchaguzi wa 2010.
Laiti kama Rais Jakaya Kikwete angekuwa ni muungwana basi angeitendea haki Tanzania kwa kung'atuka madarakani baada ya kipindi chake cha kwanza kwa kushindwa kutekeleza ahadi yake kuu ya kuboresha maisha ya Watanzania. Kikwete angetoa fursa kwa kiongozi mwingine ajaribu kutekeleza ilani ya CCM baada ya yeye kushindwa. Badala yake, kachukua tena fomu za kugombea Urais kwa mbwembwe bila haya na anaelekea kuwa mgombea pekee. Viongozi wa CCM wamebaki kunong'oneka chini kwa chini kuhusu jinsi JK alivyoivuruga nchi na kukidhoofisha chama kwa kuachia genge la mafisadi wa RICHMONDULI likiteke chama. Hivi ni kweli hakuna hata mwanasiasa mmoja mwenye ujasiri ndani ya CCM wa kuchukua fomu kum-challenge Kikwete kwa kushindwa kutekeleza ilani ya chama na kukidhoofisha chama?
Wote tumeshuhudia jinsi ukali wa maisha ulivyozidi kukithiri tangu JK aingie madarakani na idadi ya Watanzania wanaoishi kwenye umasikini imeongezeka. Hii ni kwa mujibu wa takwimu za serikali yenyewe.
Serikali hii hii ya JK imedhihirisha kuwa wala haijui umasikini halisi wa wananchi wake baada ya majuzi tu kuweka viingilio vya kati ya shilingi elfu 30 na laki mbili kwenye mechi ya Taifa Stars na Brazil na kudhani kuwa eti Watanzania wanaweza kumudu gharama hizo. Matokeo yake ni kuwa nusu ya uwanja ulikuwa mtupu huku wananchi wengi wasio na kipato wakibaki kushangaa tu.
Sipendi kuamnini kuwa ndani ya CCM hakuna kiongozi mwenye ushupavu wa kusimama na kuchukua fomu kugombea Urais 2010 ili aiepushe Tanzania na zigo hili la Kikwete kwa miaka mitano zaidi.
Uku wapi Waziri Mkuu mstaafu Frederick Tluway Sumaye? Simama tukuone Katibu Mkuu wa zamani wa OAU Dk. Salim Ahmed Salim. Amka usingizini Prof. Mark Mwandosya.
Dk. Harison Mwakyembe je? Onyesha ushupavu wako Spika Samuel Sitta.
Na mwisho kabisa, ewe BENJAMIN WILLIAM MKAPA tuokoe Watanzania wenzako tunalia. Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alifariki dunia mwaka 1999 huku nchi ikiwa mikononi mwako. Yeye ndiye aliyekuamini wewe na kukukabidhi uongozi wa nchi.
Ni kweli MKAPA umetukabidhi Watanzania kwa Kikwete? Ni kweli unaachia nchi iendelee kuteketea kwenye dimbwi la umasikini na hopelessness kwa miaka 5 zaidi?
Ewe Mkapa, unalalaje usiku huku ukijua kuwa nchi imerudi miaka 10 nyuma kimaendeleo chini ya uongozi legevu wa JK ambao wewe ndiyo umeurithisha kutawala nchi hii?
Zinduka MKAPA, nchi inateketea!
Baada ya kushindwa kutekeleza ahadi yake ya mwaka 2005 ya kuleta "Maisha Bora kwa kila Mtanzania" kupitia kauli mbiu yake ya Ari mpya, NGUvu mpya na KAsi mpya (ANGUKA), sasa CCM inakuja na Ari zaidi, Nguvu zaidi na Kasi zaidi (ANGUKA ZAIDI) kwenye uchaguzi wa 2010.
Laiti kama Rais Jakaya Kikwete angekuwa ni muungwana basi angeitendea haki Tanzania kwa kung'atuka madarakani baada ya kipindi chake cha kwanza kwa kushindwa kutekeleza ahadi yake kuu ya kuboresha maisha ya Watanzania. Kikwete angetoa fursa kwa kiongozi mwingine ajaribu kutekeleza ilani ya CCM baada ya yeye kushindwa. Badala yake, kachukua tena fomu za kugombea Urais kwa mbwembwe bila haya na anaelekea kuwa mgombea pekee. Viongozi wa CCM wamebaki kunong'oneka chini kwa chini kuhusu jinsi JK alivyoivuruga nchi na kukidhoofisha chama kwa kuachia genge la mafisadi wa RICHMONDULI likiteke chama. Hivi ni kweli hakuna hata mwanasiasa mmoja mwenye ujasiri ndani ya CCM wa kuchukua fomu kum-challenge Kikwete kwa kushindwa kutekeleza ilani ya chama na kukidhoofisha chama?
Wote tumeshuhudia jinsi ukali wa maisha ulivyozidi kukithiri tangu JK aingie madarakani na idadi ya Watanzania wanaoishi kwenye umasikini imeongezeka. Hii ni kwa mujibu wa takwimu za serikali yenyewe.
Serikali hii hii ya JK imedhihirisha kuwa wala haijui umasikini halisi wa wananchi wake baada ya majuzi tu kuweka viingilio vya kati ya shilingi elfu 30 na laki mbili kwenye mechi ya Taifa Stars na Brazil na kudhani kuwa eti Watanzania wanaweza kumudu gharama hizo. Matokeo yake ni kuwa nusu ya uwanja ulikuwa mtupu huku wananchi wengi wasio na kipato wakibaki kushangaa tu.
Sipendi kuamnini kuwa ndani ya CCM hakuna kiongozi mwenye ushupavu wa kusimama na kuchukua fomu kugombea Urais 2010 ili aiepushe Tanzania na zigo hili la Kikwete kwa miaka mitano zaidi.
Uku wapi Waziri Mkuu mstaafu Frederick Tluway Sumaye? Simama tukuone Katibu Mkuu wa zamani wa OAU Dk. Salim Ahmed Salim. Amka usingizini Prof. Mark Mwandosya.
Dk. Harison Mwakyembe je? Onyesha ushupavu wako Spika Samuel Sitta.
Na mwisho kabisa, ewe BENJAMIN WILLIAM MKAPA tuokoe Watanzania wenzako tunalia. Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alifariki dunia mwaka 1999 huku nchi ikiwa mikononi mwako. Yeye ndiye aliyekuamini wewe na kukukabidhi uongozi wa nchi.
Ni kweli MKAPA umetukabidhi Watanzania kwa Kikwete? Ni kweli unaachia nchi iendelee kuteketea kwenye dimbwi la umasikini na hopelessness kwa miaka 5 zaidi?
Ewe Mkapa, unalalaje usiku huku ukijua kuwa nchi imerudi miaka 10 nyuma kimaendeleo chini ya uongozi legevu wa JK ambao wewe ndiyo umeurithisha kutawala nchi hii?
Zinduka MKAPA, nchi inateketea!