Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
Wakati anakaribia kugombea urais wa Tanzania, Jakaya Kikwete, alihutubia mkutano wa hadhara pale Bagamoyo, Pwani na kulisifia sana Kanisa Katoliki nchini, akisema wao ndio waliompa elimu na kwamba kama si wao, basi yeye angekuwa kituo cha mabasi Chalinze akiuza biashara ndogondogo. Baadhi ya Waislamu hawakuipenda kauli hiyo......
Source: Rai, Alhamisi, Julai 23 - 29, 2009, uk. 17.
***********************
My Take:
Hapa alikuwa anawapumbaza Wakristo ili wasishtukie mpango wake wa Mahakama ya Kadhi? Au alisema kweli yaliyotoka moyoni?
===========
UPDATE:
Januari 23, 2014:
Mhadhiri (Dr. Kasoga wa University of Bagamoyo) abainisha Rais Kikwete alisoma Seminari akiwa anajulikana kama "Samwel Luhanga"
Source: Rai, Alhamisi, Julai 23 - 29, 2009, uk. 17.
***********************
My Take:
Hapa alikuwa anawapumbaza Wakristo ili wasishtukie mpango wake wa Mahakama ya Kadhi? Au alisema kweli yaliyotoka moyoni?
===========
UPDATE:
Januari 23, 2014:
Mhadhiri (Dr. Kasoga wa University of Bagamoyo) abainisha Rais Kikwete alisoma Seminari akiwa anajulikana kama "Samwel Luhanga"
Kwa mujibu wa Dr. Kasoga, mhadhiri wa chuo kikuu cha Bagamoyo aliyealikwa katika kipindi cha malumbano ya hoja. Anasema alisomea shule za seminari na kutumia jina la Samwel Luhanga na baadaye ndipo akatumia jina la Jakaya Mrisho Kikwete. Tuna mengi ya kujifunza.
Hongera Samwel Jakaya Kikwete
Chanzo: ITV malumbano ya hoja
Nimetazama kipindi hicho pia, kimemalizika muda wa dakika kadhaa zilizopita. Mimi pia nimeshangazwa na taarifa hiyo. Lakini kama ni ya kweli, inamuongezea credit Mwalimu Nyerere kwa uamuzi wake wa kutaifisha shule za misheni, kwamba baada ya utaifisho huo waislamu walikuwa na uhuru kamili wa kusoma katika shule hizo bila kulazimika kutumia majina ya kikiristo au kuigiza ukiristo.
Majuzi nimemaliza kusoma kitabu cha historia ya shule ya Ilboru kilichoandikwa mwaka 1969. Ilboru ilikuwa shule ya kiluteri na ilianza miaka ya mwanzoni ya 1940's. Katika sehemu fulani kitabuni mle, kuna ripoti ya mkutano mmojawapo wa bodi ambako walilalamikia suala la kulazimishwa na serikali (baada ya uhuru) kuanza kudahili wanafunzi wa imani nyingine. Bila msukumo na shinikizo la serikali ya Nyerere, baadhi ya shule za madhehebu ya dini kamwe zisingekubali kusomesha watoto wa dini tofauti na ya wenye shule.
Ndio maana naungana na wote wanaomsifu Mwalimu Nyerere kwa jitihada zake za kuondoa matabaka Tanzania, na mfano wa leo wa Mh Samuel Luhanga ni kumbukumbu nyingine nzuri sana to Nyerere's credit.