Makala nzuri na imejaa kila aina ya ukweli lakini bado ina ile tabia maarufu ya kitanzania: Woga na Unafiki. Kwanini? Katika uma wa viongozi wenzake wa CCM (pamoja na mwandishi wa hii makala) hajapatikani hata mmoja mwenye ujasiri wa kumwambia ukweli? Mbona wananung'unikia uvunguni tu?
Hii inaonyesha hulka yetu waTZ, kunung'unika lakini tunashindwa kuweka jitihada za kutosha kubadili mfumo huu mbovu.
Nawalaumu sana wale wanaoshiriki vikao vya CC na NEC wakashiriki kutoa maamuzi mabovu kisha utawasikia wakilaumu kama vile hawamo; huu ni unafiki mkubwa![/QUOTE]
Wanafiki katika maisha ya ukombozi wa mwanadamu hawadum kabisa, utoweka kama upepo; yaani hawaishi kati ya watu mara wanaporejea kwa muumba wao. Wanachoacha nyuma yao ni jamii yenye majonzi, na isiyoelewa ni kwa nini walifanya waliyofanya