Salas
JF-Expert Member
- Feb 15, 2009
- 382
- 82
Watanzania tumegubikwa na tamaduni ya kukurupuka na kuendeshwa na matukio siku zote, rais ambaye ni mtulivu ambaye anajua kupanga ni kuchagua huwa asilani hana papara rais amekuwa akitumia muda mwingi kusafiri huku na huko kutafuta ni jinsi gani ataweza kusaidia changamoto zinazowakabili watu wake. Tusiwe tunafikiri kwa kutumia ubongo na sio ufahamu kama vile tunavyo wakshifu wengine kuwa wanatumia matumbo kufikiri tukiwa tuna maanisha wanafikiri kwa njaa.
Rais Kikwete ameonekana akiwa bega kwa bega na watu wake katika mambo mbalimbali yanayokabili hali ya maisha ya kila siku, alikuwepo mkapa shutuma nyingi zilielekezwa juu yake ni mbabe, sio msikivu, dictator nakadhalika lakini leo hii wale watu hao kwa fikra zilezile wanadiriki kumkashifu muheshimiwa rais kwa tuhuma nzito na kubwa kabisa lakini tunajua agenda zao, wanatumiwa na uma wa wezi na wenye uchu wa madaraka.
Tanzania ni kisiwa cha Amani na Utulivu, kama unabisha leo hii njoo burundi uone nini kinachoendelea, Asilani tutalinda amani na utulivu wa nchi hii kwa nguvu hata kwa tone la mwisho la damu kama itatupasa kufanya hivyo.
Tumekuwa wepesi wa kulaumu na kuendeshwa na matukio haya swala la UMEME, je unafikiri kama raisi akitatua tatizo la umeme matatizo mengine yatakuwa yameeisha kwa mfano, vifo vya kinamama na watoto, elimu, maji, masoko ya biashara kwa wakulima wetu, ajira kwa watu wetu tunakurupuka kwa mihemuko ya kisiasa.
Fikra sahihi huja pale mwanadamu, anapotumia na kufikiri nnje ya boksi kwa kuangalia na mbinu nyingine mbadala ambazo zinaweza zikasaidia kutatua matatizo.
Raisi hafurahi kuona kuwa nchi inakuwa gizani, huitaji kuwa na degree ya chuo kikuu kudadaviua hili, la hasha hali ya uchumi wetu ndio inayosababisha yote haya yanayojitokeza kwa sasa. Rais amekuwa akitumia muda mwingi kutumia Muda wake kuwaza kuhusu mtoto yule anayekufa kwa kansa tandahimba, mzee yule anayekosa chakula leo masieda mbulu, na mama yule aliyeko mwandiga kigoma, ambae anajifungua akiwa anamsubiri nesi ambaye yuko kwenye foleni nmb kupokea mshahara wake.
Rais nasema ndio anayefaa kuongoza nchi hii kwasababu anatumia uelewa wa wananchi wake kuzungumzia hali ya maisha, kwa mfano ni wangapi mlioku humu kwenye jamii forum mnao amini kukua kwa uchumi ni hata kuwa na gari, kwani uongo mwaka themanini ni wangapi wetu waliokuwa wanamiliki magari, leo hii ooh magari sio kukuwa kwa uchumi rais hafikirii angetatua tatizo la foleni, Je rais kama angeshauriana na Magufuli na kusema parking mjini kwa siku ni shilling elfu ishirini si mngeandamana uchi nyie mnaokuwa wepesi kulalamika??? Faini iliposomwa laki tatu badala ya hamsini mlipanua midomo mpaka kimeo kikaonekana.
Rais kikwete ndio anayeweza kuongoza nchi hii, kuna baadhi ya wananchi wanao ona umeme ni anasa NDIO pia sisi tunaongozwa na huyo huyo mnao muona hafai kwetu tatizo sio umeme, HATUNA MAJI je kila mtu akianza kumuambia rais arudi safarini alipoenda KUHEMEA kwa ajili ya watu wake je mambo mengine yatatatulika??? Kwani ni asilimia ngapi ya wananchi wenye access ya umeme???? Hapa watu wanatumia kila nafasi kupayuka hasa kwa miitikio ya kisiasa, Angekuwa Dr Slaa rais angefunga vinu vya nuclear vizalishe umeme au angeangalia juu mwenyezi Mungu alete mvua????
Kikwete wewe ndio unaofaaa sisi asilimia 80% tuishio vijijini wewe ndio rais wetu, tunakutambua na kukuunga mkono na yote ufanyayo ni kwa ajili yetu, rais haendi ulaya kufanya shopping ya chakula ndani, wala nguo za kuvaa anenda kwa lengo moja tu la kutafuta jinsi ya kutimiza AHADI ya maisha bora kwa kila Mtanzania.
Rais kikwete ndio anayefaa kuongoza Tanzania, Mungu mpe afya na hekima ya kuendelea kutatua matatizo ya watu wako, ningekuwa na namba ningekutumia sms ya kukupongeza.
MAISHA BORA HAYAJI KWA KULALA, MAJUNGU NA MAANDAMANO AMKA FANYA KAZI TANZANIA ITAJENGWA NA MWANANCHI MMOJA MMOJA:
Rais Kikwete ameonekana akiwa bega kwa bega na watu wake katika mambo mbalimbali yanayokabili hali ya maisha ya kila siku, alikuwepo mkapa shutuma nyingi zilielekezwa juu yake ni mbabe, sio msikivu, dictator nakadhalika lakini leo hii wale watu hao kwa fikra zilezile wanadiriki kumkashifu muheshimiwa rais kwa tuhuma nzito na kubwa kabisa lakini tunajua agenda zao, wanatumiwa na uma wa wezi na wenye uchu wa madaraka.
Tanzania ni kisiwa cha Amani na Utulivu, kama unabisha leo hii njoo burundi uone nini kinachoendelea, Asilani tutalinda amani na utulivu wa nchi hii kwa nguvu hata kwa tone la mwisho la damu kama itatupasa kufanya hivyo.
Tumekuwa wepesi wa kulaumu na kuendeshwa na matukio haya swala la UMEME, je unafikiri kama raisi akitatua tatizo la umeme matatizo mengine yatakuwa yameeisha kwa mfano, vifo vya kinamama na watoto, elimu, maji, masoko ya biashara kwa wakulima wetu, ajira kwa watu wetu tunakurupuka kwa mihemuko ya kisiasa.
Fikra sahihi huja pale mwanadamu, anapotumia na kufikiri nnje ya boksi kwa kuangalia na mbinu nyingine mbadala ambazo zinaweza zikasaidia kutatua matatizo.
Raisi hafurahi kuona kuwa nchi inakuwa gizani, huitaji kuwa na degree ya chuo kikuu kudadaviua hili, la hasha hali ya uchumi wetu ndio inayosababisha yote haya yanayojitokeza kwa sasa. Rais amekuwa akitumia muda mwingi kutumia Muda wake kuwaza kuhusu mtoto yule anayekufa kwa kansa tandahimba, mzee yule anayekosa chakula leo masieda mbulu, na mama yule aliyeko mwandiga kigoma, ambae anajifungua akiwa anamsubiri nesi ambaye yuko kwenye foleni nmb kupokea mshahara wake.
Rais nasema ndio anayefaa kuongoza nchi hii kwasababu anatumia uelewa wa wananchi wake kuzungumzia hali ya maisha, kwa mfano ni wangapi mlioku humu kwenye jamii forum mnao amini kukua kwa uchumi ni hata kuwa na gari, kwani uongo mwaka themanini ni wangapi wetu waliokuwa wanamiliki magari, leo hii ooh magari sio kukuwa kwa uchumi rais hafikirii angetatua tatizo la foleni, Je rais kama angeshauriana na Magufuli na kusema parking mjini kwa siku ni shilling elfu ishirini si mngeandamana uchi nyie mnaokuwa wepesi kulalamika??? Faini iliposomwa laki tatu badala ya hamsini mlipanua midomo mpaka kimeo kikaonekana.
Rais kikwete ndio anayeweza kuongoza nchi hii, kuna baadhi ya wananchi wanao ona umeme ni anasa NDIO pia sisi tunaongozwa na huyo huyo mnao muona hafai kwetu tatizo sio umeme, HATUNA MAJI je kila mtu akianza kumuambia rais arudi safarini alipoenda KUHEMEA kwa ajili ya watu wake je mambo mengine yatatatulika??? Kwani ni asilimia ngapi ya wananchi wenye access ya umeme???? Hapa watu wanatumia kila nafasi kupayuka hasa kwa miitikio ya kisiasa, Angekuwa Dr Slaa rais angefunga vinu vya nuclear vizalishe umeme au angeangalia juu mwenyezi Mungu alete mvua????
Kikwete wewe ndio unaofaaa sisi asilimia 80% tuishio vijijini wewe ndio rais wetu, tunakutambua na kukuunga mkono na yote ufanyayo ni kwa ajili yetu, rais haendi ulaya kufanya shopping ya chakula ndani, wala nguo za kuvaa anenda kwa lengo moja tu la kutafuta jinsi ya kutimiza AHADI ya maisha bora kwa kila Mtanzania.
Rais kikwete ndio anayefaa kuongoza Tanzania, Mungu mpe afya na hekima ya kuendelea kutatua matatizo ya watu wako, ningekuwa na namba ningekutumia sms ya kukupongeza.
MAISHA BORA HAYAJI KWA KULALA, MAJUNGU NA MAANDAMANO AMKA FANYA KAZI TANZANIA ITAJENGWA NA MWANANCHI MMOJA MMOJA: