Kikwete na taswira ya Shehu Shagari Tanzania?

Shadow

JF-Expert Member
May 19, 2008
2,897
671
Wasalaam wana JF,

Na kwa Mh. J.K, mosi, kheri ya miaka 20 ya ndoa japo watoto wamepita miaka hiyo 20 ; Pili, nawatakia kheri katika kuijongelea jubilee ya Silver ya ndoa yenu! Mungu na awajalie afya njema na maisha marefu na yenye upendo wa kweli na kuvumiliana.


Samahani kwa kuchepuka, ilibidi nimpe kwanza ongera mkulu, sasa turudi kwenye mada nilioitaja hapo kwenye kichwa cha habari;


Je wajua kwamba:


1. Alikuwa na aiba ya kupendwa kutokana na ucheshi na uvaaji wake.

2. Alikuwa na sifa ya kupenda kusafiri na hasa kutembelea nje ya bara la Africa.

3. Shehu Shagari alishinda uchaguzi wa mwaka 1979 kwa msaada wa rafiki na mshirika wa matajiri Umaru Dikko ambaye alikuwa na ajenda ya kulinda maslahi ya ‘wanene'.

4. Mafisadi waliompelekea madarakani mwaka 1979, Kupinduka na kuzama kwa maadili ya kazi kwa mawaziri wake huku utawala wake ukifunikwa na wingu zito la rushwa.

5. Kuanguka kwa uchumi wa Nigeria huku akitizama.

6. Viongozi walioshindwa kutaja mali zao aliwalinda.

7. Hakuweza kufuatilia nini chanzo cha rushwa nchini mwake bali alikaa na kuangalia achezeje kete zake kulinda public image yake.

Waenga wamenena kwamba ni kheri yule mtawala anayewatumikia wananchi wake, pia mtu utamjua tabia yake vizuri kupitia au kwa kuangalia kundi linalomzunguka .
Je, hii inajenga taswira gani kwenye utawala wa Mh. JK na Serikali yake kwa ujumla?

For info about Sheu Shagari: click: [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Shehu_Shagari"]Shehu Shagari - Wikipedia, the free encyclopedia[/ame]
 
obvious there is no doubt. Mkulu is the same. maneno mengi vitendo kidogo and very extremely slow!!!!!! sijui hana maamuzi as an excutive or washauri wanamchanganya I do'nt know. some times kila kitu kiko wazi still utaona anasuasua kwa kisingizio vyombo vya sheria ili hali anajua hivyo vyombo vyake vimeoza ama havijui what to do!! kashafa kibao na cmplains za wananchi anazikwepa! Anaendesha nchi kirafikirafiki!!! NO ACCOUNTABILITY NO RSSPONSIBILITY.
 
Back
Top Bottom