Kikwete na semina elekezi kwa Mawaziri - Dodoma 2011

kama ni hizo hela za semina wanahitaji wangesainishana cheque tu kikaisha.. suala la kwenda kukaa dodoma sidhani kama lina maana yeyote
 
Kama matamko yote yaliyokwisha kutolewa na JK yangekuwa yanatimizwa mbona tungekuwa mbali!

Hivi ni akili za JK na Mawaziri wake wote kwenda mpaka Dodoma kuwakumbusha wajibu wao?Hivi ni kwa nini mnateketeza hizi pesa zetu(Watanzania)tukiona jamani?

Hivi Jk hao mawaziri wako uliowachagua ni kweli hawayajui majukumu Yao? Raisi 0 Wabunge 0 Baraza la mawaziri 0 wote zero mnaudhi sana.
 
safi sana Presidaa! lazima mawaziri wasimame kifua mbele kuelezea mafanikio ya serikali kamayanavyoonekana katika picha
 

Attachments

  • MAISHA BORA.jpg
    MAISHA BORA.jpg
    24.4 KB · Views: 32
  • kasi mpya 3.jpg
    kasi mpya 3.jpg
    8.8 KB · Views: 33
  • wodini.jpg
    wodini.jpg
    255.8 KB · Views: 31
  • kasi mpya 4.jpg
    kasi mpya 4.jpg
    12.3 KB · Views: 32
kama ni hizo hela za semina wanahitaji wangesainishana cheque tu kikaisha.. suala la kwenda kukaa dodoma sidhani kama lina maana yeyote

Au angesema hivi angeonekana shujaa
Natoa siku 30 kila waziri awe amehamia Domoma. Vitengo vingine vya wizara vitafuata taratibu. Nataka kuona mawaziri na manaibu waziri mnakuwa dodoma kama eneo la kazi. Nasema ndani ya siku 30............ makofiiiiii
 
Vile vile niliagiza yafanyike maonesho maalum katika Uwanja wa Maonyesho wa Julius Nyerere hapa Dar es Salaam na kote mikoani kwenye viwanja vya maonesho, kuelezea mafanikio yaliyopatikana katika nyanja mbalimbali katika miaka 50 tangu Uhuru wa Tanzania Bara. Kwa kuwa tunakaribia nusu ya mwaka huu, ni vema sasa kukumbushana kuendelea na maandalizi ya sherehe hizo. Ni matumaini yangu kwamba kila Wizara inakaribia kukamilisha tathmini hiyo. Walio nyuma sana waongeze kasi. Tuliazimia pia kuwa tuanzishe mchakato wa kuipitia Katiba yetu.

Tumeanza, lakini kuna upotoshaji mkubwa, lakini wajibu wetu sote tuliopo hapa kukabili hila na njama hizo chafu. Naamini tutafika salama. Kinachotakiwa ni mshikamano na umoja miongini mwetu.

Hivi mpaka leo hawajaacha kumuongopea tu jamani mbona mnamtia aibu huyu Raisi wetu?

Sasa HAPA NI DAR AU DOM?
 
Hotuba imetulia kweli na inatoa maelekezo ya kutosha kwa hao wakuu wa nchi. Muhimu ni wao kuyafanyia kazi ili matokeo yaonekane
 
Pamoja na nyongeza hiyo bado tunao uwezo wa kuongeza zaidi. Kuna watu wengi ambao bado hawajafikiwa na wigo wa kodi. Laiti wangefikiwa mapato ya Serikali yangekuwa makubwa zaidi ya ilivyo sasa. Tutafanyaje tufanikishe hilo ni changamoto yetu sote Serikalini. Tufanye nini ili tuzibe mianya inayovujisha mapato ya Serikali ni swali ambalo sote katika Serikali hatuna budi kutoa jibu muafaka. Kwa upande wa tozo mbalimbali karibu kila Wizara inazo tozo za namna hiyo. Wengi wenu hamjafikia hata theluthi moja ya malengo. Tutafanyaje ili tufikie malengo na kuyavuka ni swali ambalo kila mmoja wetu anatakiwa kujiuliza na kutoa majibu sahihi.

Ndugu Mawaziri na Ndugu Makatibu Wakuu;
Sote tunajua kuwa licha ya tozo na kodi, chanzo kingine cha mapato ya Serikali ni mikopo na misaada kutoka Mabenki, Mataifa Rafiki, na Mashirika ya Fedha ya Kimataifa. Tumepata misaada na mikopo mingi ya kutoka nje katika kipindi kilichopita na muelekeo ni kuwa tutaendelea kupata zaidi katika miaka mitano ijayo. Tunatambua haja na hoja ya kupunguza utegemezi wa misaada na mikopo kutoka nje kwa kuongeza mapato yetu ya ndani. Katika miaka mitano hii tumeendelea kupunguza utegemezi lakini nia yetu sote iwe kupunguza zaidi. Naamini tutafika kwenye shabaha hiyo iwapo tutaongeza mapato ya ndani. Naomba tuzungumzie namna ya kufikia shabaha hiyo.

Ndugu Mawaziri na Ndugu Makatibu Wakuu;
Usimamizi wa matumizi ya fedha tunazokusanya kama mapato ni jukumu jingine kubwa kwetu sote. Tuna wajibu wa kuhakikisha kuwa fedha za walipa kodi zinatumika ipasavyo kuwaletea maendeleo wananchi. Katika kudhibiti matumizi ni muhimu kuelewa na kusimamia sheria, taratibu na kanuni za fedha na manunuzi ya umma kwa ufanisi wa hali ya juu. Taarifa za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali zinaonyesha kuongezeka kwa ubora lakini bado tunayo kazi ya kufanya kufikia kiwango cha kusema sasa tunapumua. Bado kuna makosa mengi katika kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za mapato na matumizi ya fedha za umma. Nataka tuzungumze kwa dhati tutafikaje kwenye ufanisi wa hali ya juu kwenye eneo hilo. Hali hii hatuwezi kuiacha iendelee kuboreka kwa kasi ndogo iliyopo sasa.

Viongozi na watendaji wakuu wa Serikali, mnatakiwa kuwa mfano kwa wafanyakazi mnaowaongoza kwa kuzingatia nidhamu ya matumizi ya fedha za umma.

Hakikisheni bajeti hazikiukwi, fedha zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa na sheria na kanuni za fedha zinaheshimiwa. Niliagiza Kamati za Fedha ziundwe katika kila Wizara na Idara za Serikali zinayojitegemea. Je zimeundwa? Je zinafanya kazi? Hakikisheni zipo hai na zinatimiza wajibu wake. Zitasaidia sana kwa upande wa kuongeza mapato na kudhibiti matumizi katika Wizara.
Hii kipande kimenibore kabisa anasema matatizo bila majibu na mahala penyewe ni kwenye semina Raisi wetu anamatatizo kabisa
 
Kama matamko yote yaliyokwisha kutolewa na Jk yangekuwa yanatimizwa mbona tungekuwa mbali!!.
Hivi ni akili za Jk na Mawaziri wake wote kwenda mpaka Dodoma kuwakumbusha wajibu wao?Hivi ni kwa nini mnateketeza hizi pesa zetu(Watanzania)tukiona jamani?
Hivi Jk hao mawaziri wako uliowachagua ni kweli hawayajui majukumu Yao?Raisi 0 Wabunge 0 Baraza la mawaziri 0 wote zero mnaudhi sn.

Ukifuatilia inawezekana hii semina ni donor funded Project na njia pekee ya kuhakikisha pesa inatumika yote ni kwenda mbali na kituo cha kazi
 
Hotuba imetulia kweli na inatoa maelekezo ya kutosha kwa hao wakuu wa nchi. Muhimu ni wao kuyafanyia kazi ili matokeo yaonekane


Kaka mbona Comment yako inapingana na SLOGAN YAKO ya "Effective leadership is not about making speeches or being liked; leadership is defined by results not attributes" Peter Drucker
 
Bajeti ya kuwapeleka Dodoma wangepewa mikopo wajasiriamali wangapi? asilimia 95 yao wote wametoka Dar, Capital ihamie Dar tusidanganyane
 
Ifikapo mwaka 2025 mtanzania awe na kipato cha dola 3000 kwa mwaka? angalia leo Gabon wana 15,000 dola, Angola 10,000 na Ushelisheli tuliowakomboa wenyewe kwa jeshi la nyerere wanapata dola 20,000 kwa mwaka leo hii, sisi baada ya miaka 25 ndio tupate dola 3000? hatufiki
 
Bravo JK kwa kuchukua hatua wakati muafaka!!!n:israel:
Mkuu!

Amiri jeshi hatakiwi kutoa hotuba ya namna hiyo kwa watendaji wake ambao keshafanya nao kazi kwa takribani miezi sita! Alitakiwa ayaseme hayo kabla hajawaapisha. isitoshe hayo yooooote ni matakwa ya utumishi wa umma hivyo hakuwa na sababu ya kuwasomea bali kuwawajibisha!!!

Kwa Maoni yangu:- Hizo bado ni bla bla ambazo hazina mwisho unaohitajika na watanzania maskini!
 
Wakuu mi naomba niulize swali:
Hivi hawa watu si alishaonana nao wakati anatembelea wizara mwezi jana. Kila wizara ilitoa hotuba yake na yeye akatoa maelezo yake kwa wizara hizo. Sasa kama kila mwezi unakutana nao kuwaelekeza mambo hayo hayo kuna haja gani ya kuwa na hao watu, si bora kazi zao azifanye yeye? Au jamaa hana "To do list" so ikifika asubuhi gari litakapoelekea basi ndo huko huko. Haya ni matumizi mabaya sana ya kodi zetu.
 
mlizani cdm mtasema nn kwa kikwete zaidi yakukosoa ata marekan mpo,obama kazaliwa kenya, katoa cheti et alikuwa hana akili darasan hakustail kusoma havad chochote cha kikwete kwenu kibaya tu kama si wachawi nn
 
Mambo yote anayoyaorodhesha leo ndio standard operation manual ya serikali.

Kuna matatizo mawili makubwa yanayomkabili Kikwete na serikali yake:

Kwanza, haya hayatekelezwi na pili, ambalo ndilo kubwa zaidi, hakuna hatua yoyote inayochukuliwa kutokana na kutotekelezwa haya zaidi ya maneno zaidi kama anavyofanya kupitia hiyo semina elekezi.

Kwa hali jinsi ilivyo hakutakiwa kuwe na semina elekezi tena. Huu ulikuwa ni wakati wa vichwa kuviringika, si kukumbushana wajibu kwa sababu kila mmoja serikalini anajua wajibu wake... kama kuna ambaye hajui, hakustahili kuwepo humo

...You can say that again!
 
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Hii JF nayo inaboa pale ambapo jitihada zinafanyika ambazo zinaleta matumanini ya maendeleo lakini watu wengine bado wanaponda. Yani ni kama biashara kichaa vile. Watanzania wenyewe ndio sisi, kama PUNDA, mpaka tusukumwe, iwe kazini iwe wapi. Rais ni binadamu tuu, na japokuwa kiboko anacho punda nao mbishi ati. Kubalini mtu akifanya positive step. JF move away from promoting sewage talk and towards more constructive criticism. The majority of political views in this forum, which I dare say are not too divergent, seem to be unable to produce objective and constructive critiques of the government or the ruling party. Perhaps it is true that there is little to be lauded in their actions but being unable to demonstrate objectivity is definitely a sign that when such an entity comes into power, they themselves will be unable to withstand political dissidence. If you cant be objective in your thinking, then you most certainly will not in your actions.

On this seminar, congratulations JK, and I hope these public servants of yours will heed the words.
 
Back
Top Bottom