Kikwete na Pinda wameona ukweli au usanii?

mpayukaji

JF-Expert Member
Oct 31, 2010
940
349
Waziri mkuu Mizengwe Pinda ndiye aliyeanza kuwaaasa watanzania kutochagua watu wanaotafuta uongozi kwa kumwaga pesa. Aliyasema haya akiwa kwa wanyalukolo. JK naye baada ya kutua Mwanza kuadhimisha miaka 35 ya ukandamizaji alirejea usemi huo huo. Je wameambizana au wameamua kuendeleza sanaa? Kwanini kuliona hili baada ya wenye pesa kupeta na kuukwaa ulaji akiwamo Njaa Kaya mwenyewe?
 
Waziri mkuu Mizengwe Pinda ndiye aliyeanza kuwaaasa watanzania kutochagua watu wanaotafuta uongozi kwa kumwaga pesa. Aliyasema haya akiwa kwa wanyalukolo. JK naye baada ya kutua Mwanza kuadhimisha miaka 35 ya ukandamizaji alirejea usemi huo huo. Je wameambizana au wameamua kuendeleza sanaa? Kwanini kuliona hili baada ya wenye pesa kupeta na kuukwaa ulaji akiwamo Njaa Kaya mwenyewe?

Hivi wewe ni mtanzania gani unayedanganya watu na kauli zako za hovyo hovyo?
Nina mashaka na uelewa wako na elimu yako kwa ujumla...wewe ni mtu gani unayeshindwa
hata kuelewa tu maana ya neno ukandamizaji?
 
VGL una maana gani unaposema una wasi wasi na elimu yangu? Sitaki nikueleze nimesoma nini na kiasi gani bali nakushauri ugoogle jina langu Mpayukaji utajua mimi ni nani katika hayo unayotaka. Tujadili hoja badala ya kutafuta upenyo kwenye kujadili watu. Kama ni kusoma nimesoma tena nje ya nchi mnakoabudia na ndani ya nchi kwenye fani tatu vilivyo. Hivyo VGL tafuta mashiko ya hoja zako badala ya kuumka bila sababu.
 
[h=3]Kujivua gamba CCM tushike la nani au ndiyo mwanzo wa mwisho?

chanzo: www.mpayukaji.blogspot.com[/h]


"Haiwezekanitukaendelea kuwa na watu wa hovyo, lazima chama kijipange na kujiweka sawa ilikisipoteze sifa kwa jamii," Jakaya Kikwete akiwa Mwanza jana. Anaongeza, "Hivi karibuni nikiwana NEC hapo Dodoma, nilitumia kauli ‘Nyoka Kujivua Gamba'. Usemi huo ulienezwatofauti kabisa. Kimsingi tulipitisha maazimio mengi, lakini wenzetu wameonaazimio moja tu la kujivua gamba."


"Hatuwezi kuwa nachama imara kama hatukuondoa magamba, mwenyekiti wetu wa chama taifa lazimatuyaondoe magamba yanayokipaka chama matope." Fredrick Sumaye akiwa Pangani mkoani Jana.


"Hata Waingerezawanatabia moja. Wakiona jambo linawasumbua, wanaunda Royal Commission, jambo hilolitachunguzwa kwa muda mrefu. Wakimaliza, watu wameshasahau," Wilson Mukama katika mahojiano maalum na gazeti la Mwananchi wiki jana.
Kwa kauli hizo hapo juu tutegemee nini?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom