eliakeem
JF-Expert Member
- May 29, 2009
- 15,631
- 13,764
Wanajamii kama mlimsikia jana Waziri Mkuu Pinda kwenye taarifa ya habari jana saa mbili usiku kwenye ITV, alieleza kuwa, kuna viongozi wastaafu, ambao wengine walikuwa marais, mawaziri wakuu, n.k. wana uzoefu mzuri na mkubwa tu wa chama na serikali. Sasa hawa watu wakiwa na dukuduku au jambo fulani wanaweza kumuona rais na kumshauri juu ya jambo hilo
. Na baada ya kujadiliana na rais nadhani watafikia muafaka
. Lakini sasa wanavyotumia majukwaa ya vyombo vya habari kueleza mambo yao yanayo wakera haioneshi kuwa wana dhamira njema. Kufanya hivyo ni kana kwamba wamepeleka maoni yao kwa rais na yamekataliwa. Kitu ambacho si kweli, wangeenda kwanza kwa rais, ikitokea wamekataliwa basi wanaweza Kwenda kwenye media.
Namnukuu:
Kama malalamiko yako uliyatolea katika vikao halali na ukakataliwa kusikilizwa na hivyo ukaamua kutoka na kuyasema nje, hilo halina tatizo. Na hasa viongozi wastaafu. Hawa wana fursa ya ziada, wana uhuru hata wa kumwona Rais na kusema naye, wakitumia uzoefu walionao kumsaidia hata yeye, alisema Pinda.
My Take:
Hayo maelekezo ambayo ameyatoa kwa viongozi wastaafu mbona hawakuyatumia wakati wanampinga Dr. Magufuli waziri wa ujenzi kwenye zoezi lake la bomoa bomoa? Je yeye [Dr. Magufuli] walimwita na kushauriana naye juu ya bomoa bomoa na akakaidi na hivyo kuamua kumchonganisha na wananchi majukwaani? Au maelekezo kama hayo [ya kujadiliana kwenye vikao stahili (hapa tunaongea baraza la mawaziri)] hayatumiwi kwa watu walio chini yao? Na kama Dr. Magufuli alikana kuachana na mpango wake huo wa bomoa bomoa kwenye kikao, kwa nini wasinge mshauri ili ajiondoe/kumuondoa, wa sababu hakuafikiana na matakwa ya baraza la mawaziri na aliyemteua, maana hilo ni nafuu kuliko kuchonganishwa na wananchi?
Hapa inaonesha kwamba mkubwa akiumbuliwa majukwaani/kwenye vyombo vya habari, waliomuumbua [wanaambiwa eti] hawaja fuata utaratibu na ni wabaya. LAKINI wadogo wakiumbuliwa na wakubwa majukwaani/vyombo vya habari, hilo halina neo. TAFAKARI.
Source: HabariLeo | Pinda awashangaa Sumaye, Lowassa
Namnukuu:
Kama malalamiko yako uliyatolea katika vikao halali na ukakataliwa kusikilizwa na hivyo ukaamua kutoka na kuyasema nje, hilo halina tatizo. Na hasa viongozi wastaafu. Hawa wana fursa ya ziada, wana uhuru hata wa kumwona Rais na kusema naye, wakitumia uzoefu walionao kumsaidia hata yeye, alisema Pinda.
My Take:
Hayo maelekezo ambayo ameyatoa kwa viongozi wastaafu mbona hawakuyatumia wakati wanampinga Dr. Magufuli waziri wa ujenzi kwenye zoezi lake la bomoa bomoa? Je yeye [Dr. Magufuli] walimwita na kushauriana naye juu ya bomoa bomoa na akakaidi na hivyo kuamua kumchonganisha na wananchi majukwaani? Au maelekezo kama hayo [ya kujadiliana kwenye vikao stahili (hapa tunaongea baraza la mawaziri)] hayatumiwi kwa watu walio chini yao? Na kama Dr. Magufuli alikana kuachana na mpango wake huo wa bomoa bomoa kwenye kikao, kwa nini wasinge mshauri ili ajiondoe/kumuondoa, wa sababu hakuafikiana na matakwa ya baraza la mawaziri na aliyemteua, maana hilo ni nafuu kuliko kuchonganishwa na wananchi?
Hapa inaonesha kwamba mkubwa akiumbuliwa majukwaani/kwenye vyombo vya habari, waliomuumbua [wanaambiwa eti] hawaja fuata utaratibu na ni wabaya. LAKINI wadogo wakiumbuliwa na wakubwa majukwaani/vyombo vya habari, hilo halina neo. TAFAKARI.
Source: HabariLeo | Pinda awashangaa Sumaye, Lowassa