kichenchele
JF-Expert Member
- Jun 28, 2010
- 539
- 176
nimekuwa nikisikia ahadi nyingi sana zinazoendelea kutolewa na wagombea urais wa vyama mbalimbali vilivyosimamisha wagombea, hali hii inanifanya nijiulize hawa wagombea wamekuwa wakiishi nchi gani maana kama ni matatizo ya watanzania wameshayaona muda mwingi na si kusubiri mpaka kipindi hiki cha uchaguzi kifike, kilichonitia kichefuchefu ni ahadi iliyotolewa na mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Jakaya Mrisho Kikwete, ya kwamba kama atachaguliwa atajenga reli kutoka dar-es-salaam hadi mikoa yote ya kanda ya ziwa, mimi ningemuona mwenye hoja kama angesema atahakikisha reli yetu iliyopo inaboreshwa kwa kiwango cha juu, sasa hii iliyopo ni taabani unasema utajenga nyingine, huku ni kuwaongopea watanzania, toweni hoja zenye mantiki na si kutoa verse ambazo haziimbiki,
MUNGU IBARIKI,TANZANIA, MUNGU WABARIKI WATANZANIA, MUNGU IBARIKI AFRICA, MUNGU WABARIKI WAAFRIKA,
MUNGU IBARIKI,TANZANIA, MUNGU WABARIKI WATANZANIA, MUNGU IBARIKI AFRICA, MUNGU WABARIKI WAAFRIKA,