Yona F. Maro
R I P
- Nov 2, 2006
- 4,202
- 218
ni mstari gani vile unaosema usipojisaidia hatokusaidia? Nadhani shy hapa umetudanganya hakuna mahali katika biblia au quran ambapo mungu amesema tujisaidie na yeye atusaidie. Kama upo tunaomba mtuwekee hapa.
Watanzania wametimiza wajibu wao kwa kiasi kikubwa. Wamejenga shule ambazo serikali imeshindwa hata kupeleka walimu, wala vifaa vya maabara. Wamejenga zahanati kwa mikono yao, lakini serikali imeshindwa kupeleka madaktari. Unaposema watanzania wajisaidie, unamaanisha waanzishe vyuo vya ualimu na udaktari wenyewe? Hii ni mifano tu kwamba wananchi wametimiza wajibu wao lakini serikali imeshindwa kutimiza sehemu yake.
Si uungwana kabisa kufikiria kumpiga mawe jk, lakini ni busara kuangalia ni kwa kiasi gani amefanikia kutimiza ndoto za watanzania wengi kwa kutekeleza wajibu halali aliokabidhiwa kuutekeleza. Na tufanye maamuzi yetu kwenye sanduku la kura tar 31/10. Binafsi naona tofauti kubwa sana kati ya uongozi wa mkapa na kikwete katika suala la kujenga nchi. Tafakari.
ndugu yangu unafikiri kila mtu ni muisilamu au mkristo tu kuna dini nyingi duniani ona mbali sio lazima neno au msitari huo uwe ndani ya upeo wako