Vin Diesel
JF-Expert Member
- Mar 1, 2011
- 9,088
- 6,368
Siku hizi imekuwa kama desturi, kila kukicha utasikia kuwa Waziri Mkuu 'aliyejiuzuru' kasema hili mara kafanya lile na yote ayafanyayo au kuyasema hayana tija kwa mustakabali wa nchi yetu.
Hapa namzungumzia Waziri Mkuu aliyejiuzuru terehe 7 mwezi Februari mwaka 2008 mbele ya Wabunge wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kwa KASHFA ya RICHMOND. Vyombo vya habari vimeandika sana na watu mbali mbali wamesema na kuchambua kwa kina juu ya KASHFA hii ya RICHMOND. Sihitaji kurudia kuandika juu ya sakata hili.
Kinachotokea kwa Kiongozi huyu si ajali, bali ni mavuno ya mbegu alizopanda. Watanzania wanakumbuka wazi kuwa mwaka 1995 Kiongozi huyu alitupa karata yake ya kuomba kuliongoza Taifa hili ktk nafasi ya juu kabisa ya Urais kupitia Chama chake, lakini kwa msaada mkubwa wa Mwenyezi Mungu kupitia Hayati Baba wa Taifa Mwenyeheri Mwalimu, Julius Kambarage Nyerere, jaribio hilo lilizimwa. Mwenyeheri Mwl.
Nyerere alisema wazi kuwa Bwana Huyu HAFAI KUWA KIONGOZI WA NCHI kwani ni mtu mwenye TAMAA kubwa sana ya MALI na MADARAKA.
Lakini kwa kutumia nguvu ya fedha alizoziiba alipokuwa Serikalini, na ujanja mwingine 'Waziri Mkuu' huyu mwenye weledi wa sanaa akafanikiwa kurudi madarakani na kupanda ngazi za uongozi na hamadi akaukwaa u waziri mkuu.
Waswahili wanasema jasiri haachi asili kwani ndani ya muda mfupi akapiga dili ya mamilioni ya shilingi, akakwama kwenye dili ya umeme ya RICHMOND hadi akalazimika kuachia ngazi.
Leo hii 'MSTAAFU' huyu anafanya kila jitihada kujisafisha ili aingie patakatifu mwaka 2015, japo haoni kwamba kwa jaribio la yeye kuingia Ikulu ni sawa na ngamia kupita kwenye tundu la sindano.
Baadhi ya washirika wake muhimu ktk kambi yake wameona ugumu huo, na sasa wameamua kutafuta njia mbadala ya kuwasogeza mahala patakatifu.
Jitihada anazozifanya za kujisafisha ili afikiriwe kuliongoza Taifa hili zinamgharimu kiasi kikubwa sana cha fedha, na mbinu anazozitumia zina hatari kubwa kwa usalama wan chi yetu.
Pamoja na mambo mengine, amekuwa akitumia baadhi ya vyombo vya habari kumsafisha, lakini baya zaidi, ni pale anapomchafua Rais Kikwete na familia yake.
Ameleta mfarakano mkubwa ndani ya Chama chake, na sasa tunashuhudia, baadhi ya wenyeviti wa Chama chake wanapita sehemu mbali mbali kuhubiri uasi dhidi ya maazimio yaliyofikiwa hivi karibuni ktk vikao halali mkoani Dodoma.
Hakika, kwa haya anayoyafanya mstaafu huyu yasingeweza kuvumilika kwa ma-Rais waliopita, kwani ana kila hatia ya kujibu.
Rais Kikwete anatakiwa kujua kuwa yeye ni Rais wa wengi, na hivyo anatakiwa kusikiliza na kutekeleza ya wengi, hata Ponsio Pirato lilipomshinda kwa Nabii Issa (Yesu Kristo) alisema VOX POPULI, VOX DEYI, maana yake SAUTI YA WENGI, SAUTI YA MUNGU.
Nchi hii ni masikini saaana, umasikini huu unatokana na kuwa na viongozi wasiokuwa na mipango mizuri ya kututoa ktk dimbwi hili la umasikini. Maendeleo ktk nchi yeyote duniani huhitaji vitu vifuatavyo: ARDHI, WATU, SIASA SAFI NA UONGOZI BORA.
Mheshimiwa Kikwete, nakushauri uchukue hatua madhubuti sasa, kwani si muda mrefu watanzania wataanza kuhoji ufanisi wako kwa kigezo cha marafiki zako wanaonuka machoni pa wananchi.
Ponsio Pilato alimtoa Yesu kwa wayahudi ili asulubiwe japo yeye hakuona kosa lolote juu yake na sie twamtaka 'mstaafu' huyu ahukumiwe na kama ni msafi basi damu yake na iwe juu yangu na kizazi changu chote.
Inasikitisha sana kuona wezi wa kuku wamefungwa jela wakati wezi wa mabilioni wanatanua na Rais anapata wasaa wa kuonana nao, kama anaonekana msafi basi namuomba umlete Kariakoo aone wenye nchi yao watakavyo mlaki kwa hoi hoi, nderemo na vifijo.
MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI AFRIKA .
Hapa namzungumzia Waziri Mkuu aliyejiuzuru terehe 7 mwezi Februari mwaka 2008 mbele ya Wabunge wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kwa KASHFA ya RICHMOND. Vyombo vya habari vimeandika sana na watu mbali mbali wamesema na kuchambua kwa kina juu ya KASHFA hii ya RICHMOND. Sihitaji kurudia kuandika juu ya sakata hili.
Kinachotokea kwa Kiongozi huyu si ajali, bali ni mavuno ya mbegu alizopanda. Watanzania wanakumbuka wazi kuwa mwaka 1995 Kiongozi huyu alitupa karata yake ya kuomba kuliongoza Taifa hili ktk nafasi ya juu kabisa ya Urais kupitia Chama chake, lakini kwa msaada mkubwa wa Mwenyezi Mungu kupitia Hayati Baba wa Taifa Mwenyeheri Mwalimu, Julius Kambarage Nyerere, jaribio hilo lilizimwa. Mwenyeheri Mwl.
Nyerere alisema wazi kuwa Bwana Huyu HAFAI KUWA KIONGOZI WA NCHI kwani ni mtu mwenye TAMAA kubwa sana ya MALI na MADARAKA.
Lakini kwa kutumia nguvu ya fedha alizoziiba alipokuwa Serikalini, na ujanja mwingine 'Waziri Mkuu' huyu mwenye weledi wa sanaa akafanikiwa kurudi madarakani na kupanda ngazi za uongozi na hamadi akaukwaa u waziri mkuu.
Waswahili wanasema jasiri haachi asili kwani ndani ya muda mfupi akapiga dili ya mamilioni ya shilingi, akakwama kwenye dili ya umeme ya RICHMOND hadi akalazimika kuachia ngazi.
Leo hii 'MSTAAFU' huyu anafanya kila jitihada kujisafisha ili aingie patakatifu mwaka 2015, japo haoni kwamba kwa jaribio la yeye kuingia Ikulu ni sawa na ngamia kupita kwenye tundu la sindano.
Baadhi ya washirika wake muhimu ktk kambi yake wameona ugumu huo, na sasa wameamua kutafuta njia mbadala ya kuwasogeza mahala patakatifu.
Jitihada anazozifanya za kujisafisha ili afikiriwe kuliongoza Taifa hili zinamgharimu kiasi kikubwa sana cha fedha, na mbinu anazozitumia zina hatari kubwa kwa usalama wan chi yetu.
Pamoja na mambo mengine, amekuwa akitumia baadhi ya vyombo vya habari kumsafisha, lakini baya zaidi, ni pale anapomchafua Rais Kikwete na familia yake.
Ameleta mfarakano mkubwa ndani ya Chama chake, na sasa tunashuhudia, baadhi ya wenyeviti wa Chama chake wanapita sehemu mbali mbali kuhubiri uasi dhidi ya maazimio yaliyofikiwa hivi karibuni ktk vikao halali mkoani Dodoma.
Hakika, kwa haya anayoyafanya mstaafu huyu yasingeweza kuvumilika kwa ma-Rais waliopita, kwani ana kila hatia ya kujibu.
Rais Kikwete anatakiwa kujua kuwa yeye ni Rais wa wengi, na hivyo anatakiwa kusikiliza na kutekeleza ya wengi, hata Ponsio Pirato lilipomshinda kwa Nabii Issa (Yesu Kristo) alisema VOX POPULI, VOX DEYI, maana yake SAUTI YA WENGI, SAUTI YA MUNGU.
Nchi hii ni masikini saaana, umasikini huu unatokana na kuwa na viongozi wasiokuwa na mipango mizuri ya kututoa ktk dimbwi hili la umasikini. Maendeleo ktk nchi yeyote duniani huhitaji vitu vifuatavyo: ARDHI, WATU, SIASA SAFI NA UONGOZI BORA.
Mheshimiwa Kikwete, nakushauri uchukue hatua madhubuti sasa, kwani si muda mrefu watanzania wataanza kuhoji ufanisi wako kwa kigezo cha marafiki zako wanaonuka machoni pa wananchi.
Ponsio Pilato alimtoa Yesu kwa wayahudi ili asulubiwe japo yeye hakuona kosa lolote juu yake na sie twamtaka 'mstaafu' huyu ahukumiwe na kama ni msafi basi damu yake na iwe juu yangu na kizazi changu chote.
Inasikitisha sana kuona wezi wa kuku wamefungwa jela wakati wezi wa mabilioni wanatanua na Rais anapata wasaa wa kuonana nao, kama anaonekana msafi basi namuomba umlete Kariakoo aone wenye nchi yao watakavyo mlaki kwa hoi hoi, nderemo na vifijo.
MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI AFRIKA .