Kikwete kuwa Gorbachev wetu?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
Mojawapo ya hofu nilizonazo ni kuwa Kikwete hatimaye anaweza kuwa Gorbachev wetu. Yawezekana akaja na mawazo ya Perestroika anapotaka kugombea mara ya pili na watu wakakubali na matokeo yake itakuwa ni kuvunjika kwa Muungano wetu.

Kama Gorbachev sidhani kama atakuwa na ujasiri wa kutumia nguvu kuzuia kumeguka kwa muungano au kama ana ujuzi wa kisiasa kuimarisha Muungano. Hadi hivi sasa ni wazi kuwa suala al Muungano analiona ni gumu mno kiasi cha kushindwa hata kujaribu kulirekebisha na matokeo yake yeye na CCM wanaamua kutafuta "the path of least resistance" a.k.a referendum.

Kuna watu hata hivyo wanamuona Gorbachev shujaa na wanamshukuru kwa maamuzi yake; na kuna watu (kama kina Putin) ambao wamesimama na kurudisha ukutufu wa yule "Dubu" wa Ulaya Mashariki.

Hili swali bado natafuta jibu lake kwani pande zote mbili naweza kuziona kinadharia.
 
Mojawapo ya hofu nilizonazo ni kuwa Kikwete hatimaye anaweza kuwa Gorbachev wetu. Yawezekana akaja na mawazo ya Perestroika anapotaka kugombea mara ya pili na watu wakakubali na matokeo yake itakuwa ni kuvunjika kwa Muungano wetu.

Kama Gorbachev sidhani kama atakuwa na ujasiri wa kutumia nguvu kuzuia kumeguka kwa muungano au kama ana ujuzi wa kisiasa kuimarisha Muungano. Hadi hivi sasa ni wazi kuwa suala al Muungano analiona ni gumu mno kiasi cha kushindwa hata kujaribu kulirekebisha na matokeo yake yeye na CCM wanaamua kutafuta "the path of least resistance" a.k.a referendum.

Kuna watu hata hivyo wanamuona Gorbachev shujaa na wanamshukuru kwa maamuzi yake; na kuna watu (kama kina Putin) ambao wamesimama na kurudisha ukutufu wa yule "Dubu" wa Ulaya Mashariki.

Hili swali bado natafuta jibu lake kwani pande zote mbili naweza kuziona kinadharia.

Muungano haulazimishwi na JK pekee, na si jambo la kumuangalia mtu moja moja na kutoa hukumu..muungano ni majumuisho ya historia, faida/hasara, wananchi, na wakati wake

Kama muungano utavujika ni wakati wake umefika wala halitakuwa kosa la gorbachov wala JK, wanaolilia muungano watuambie kinagaubaga wanataka muungano kwasababu zipi? na wanapata faida zipi kwa kuangalia historia yake nk. please "msilete habari za alinacha eti nyerere kasema" this is an old crying song hatutaki kusikia..tuambiwe sasa hivi (wakati huu) muungano unatusaidia nini? na uwe muungano wa aina gani? kwa manufaa zaidi?

Wanaokataa muugano vilevile watuambia hawataki kwasababu gani wanapata hasara gani na wanataka muugano wa aina gani?

Hoja ziwekwe wazi..hii mambo imefichwa sana utafikiri karume na nyerere walikuwa malaika ni ujinga kwa nchi yenye wasomi kama nchi yangu
 
Kuna watu hata hivyo wanamuona Gorbachev shujaa na wanamshukuru kwa maamuzi yake; na kuna watu (kama kina Putin) ambao wamesimama na kurudisha ukutufu wa yule "Dubu" wa Ulaya Mashariki.

Hili swali bado natafuta jibu lake kwani pande zote mbili naweza kuziona kinadharia.

Kikwete atakuwa shujaa wangu pale atakaporuhusu huu muungano kuvunjika.

Muunguja anaweza kuweka bayana faida anazozipata kutokana na muungano huu. Zipi faida za muungano kwa mtanganyika wa Mtwara. Kama bahari Mtwara ipo, tena bahari ya Hindi. Kama ni reserves za mafuta, hata mtwara zipo, kama ni marine parks, hata Mtwara zipo, kama ni natural gas, hata Mtwara ipo. Kama ni watalii hata Arusha wapo. Kama ni ardhi, huku Tanganyika ndio usiseme, kama ni ng'ombe wa nyama, mbuzi, kuku wa kienyeji, ndizi, nyanya, vitunguu, matunda, mazao ya nafaka na ya jamii ya kunde tunayo.

Je tunataka muungano ili tufaidike na karafuu?

Hata mapacha inafika wakati kila mtu anachukua time na kuendelea na maisha, ije kuwa muungano wa kuchanganya kias kidogo cha mchanga! Huo mchanga uliochanganywa ulichukuliwa kila mkoa wa Tanganyika na Unguja?
 
Muungano huu ulilazimishwa. Pamoja na mawazo mazuri ya Karume Senior na Nyerere wakati huo, tukiri kwamba wakati huu ni mwingine. Bila shaka, Karume Senior na Nyerere wangekuwa serious tangu wakati huo, wangeruhusu mchanganyiko halisi wa wazanzibari na wabara. Hili halikufanyika. Muungano feki sana ulikuwa, na Kikwete hana namna ya kuuokoa
 
hali zenu, wajukuu wangu,

kwanza kabisa tutulie ikiwa sehemu ya kumuombea mjukuu wangu, wa jina la kipenzi changu chief swetu.swetu fundikira mwanangu nenda kapumzike kwa amani ....................maana ukifungua masikia ni mengi yanasemwa haswa juu ya chanzo cha kifo chako.mungu wa baba yao ramadhani na babu yako swetu ndio wanaojua.buriani mwanangu.

pili, nimeguswa kuchangia mjadala aliuanzisha mjukuu wangu, mwanakijiji hapo juu.

kwanza , ieleweke huo ni mtazamo wake na kwa kiswahili kifupi hayo ni maneno yake. nisingefikiri kama mwana kijiji anaweza kutofautiaa na yule wa juzi ambaye wakati wote akili yake imejaa kuamsha hisia ambazo yeye anafikiri zimefichwa.naomba niruhusu nikutoe wasiwasi.

ni ukweli usiofichika kuwa mabadiliko yoyote yale uja na wakati. ninapozungumzia sababu nazungumzia pia viambata vyake.vitu kama uongozi uliopo na maafisa waandamizi wa uongozi huo ni sehemu pia ya mabadiliko hayo.

lakini pamoja na yote. mabadiliko si jambo ambalo mtu mmoja anawerza sema fanya ikawa siku ya pili. ni jambo ambalo watu wote katika utawala wa muda ule ukubaliana na wakafanya. hapa nazungumzia uwepo wa vyombo vya kiusalama na wananchi kwa jumla yao.

sasa sioni kama kuwa raisi kunakufanya wewe uwe chachu ya kuleta mabadiliko yote hayo peke yako isipokuwa kama mfumo mzima unaoishi utakubaliana na haya.

kwa tanzania silioni hilo.mambo mengi sana yanafanyika na sidhani kwa mtu kama wewe ambaye unaangalia mambo kwa juujuuu tu unaweza yaona. angalia kati ya mistari.

hivi unafikiri, inawezekana
......karume kuongezewa muda kwa kuwa wazanzibar wanataka.
.....muungano wetu kuondoka sababu ya kitu kinaitwa referendum
.....kuwa na chama kinaitwa CCJ bila ya serikali kujua nani wamo ndani
.....kufanya vita na serikali wakati maisha yako yanaangaliwa na hao.
.....kufanya watu millioni 40 wahangaike na tabu kwa sababu ya watu wawili
....kuwa mnatuma sms huku big brother anakuangalia tu

Mjukuu wangu, kama unaweza pata majibu ya haya maswali machache basi pia unaweza jua nini ninachokizungumzia.

Mabadiliko ni jinsi mfumo unavyotaka. wakati tulionao ni wakati wa mpito na maisha yanaendelea.

Toa wasiwasi , mchi haiwezi kufikia huko na hata huyo bwana Jakaya hawezi kuwa hicho unachofikiria wewe ndicho.

HABARI ZA ASUBUHI.
 
JK wetu asipoisimamia na kuilinda KATIBA yetu ya JMT atakuwa Gorbachev wetu. Zanzibar sasa hivi wanatoa matamshi yao kama vile katiba hii haipo, haiwahusu. JK amewekwa pale kwa mujibu wa katiba hii lakini anakuwa kama anaionea haya vile!
 
Ni wazi kwamba muungano una matatizo makubwa, wote yanatuhtusu haya,nadhani ni vema tushauri namna ya kuuboresha au kuuvunja kwa heri, binafsi naamini Zenj itaendelea vizuri sana ikiwa nchi huru..
 
Muungano haulazimishwi na JK pekee, na si jambo la kumuangalia mtu moja moja na kutoa hukumu..muungano ni majumuisho ya historia, faida/hasara, wananchi, na wakati wake

Kama muungano utavujika ni wakati wake umefika wala halitakuwa kosa la gorbachov wala JK, wanaolilia muungano watuambie kinagaubaga wanataka muungano kwasababu zipi? na wanapata faida zipi kwa kuangalia historia yake nk. please "msilete habari za alinacha eti nyerere kasema" this is an old crying song hatutaki kusikia..tuambiwe sasa hivi (wakati huu) muungano unatusaidia nini? na uwe muungano wa aina gani? kwa manufaa zaidi?

Wanaokataa muugano vilevile watuambia hawataki kwasababu gani wanapata hasara gani na wanataka muugano wa aina gani?

Hoja ziwekwe wazi..hii mambo imefichwa sana utafikiri karume na nyerere walikuwa malaika ni ujinga kwa nchi yenye wasomi kama nchi yangu

Mkuu Tumain,

I second you on this...
Its time hawa viongozi wetu waweke haya mambo wazi... We all know more problems huu muungano uko nayo, dawa si kuyakimbia but rather tudiscuss tukiangalia yapi yalikuwa makosa yapi ni mazuri, ili wote (bara/visiwani) tufaidike nao.

Kweli imauma sana kuona nchi kama hii yenye wasomi na watu wenye upeo tunakalia ubabaishaji na kudhani waasisi walikuwa miungu!!!

Amandla.
 
wajukuu zangu, mie naungana na nyie juu ya ulinzi wa katiba yetu na wazo la kuwa makini juu ya utawala wa kikatiba maana huu ndiyo msingi wa muungano wa nchi hizi mbili.

manufaa ya muungano, hauwezi yagusa kwa mkono hasa ukiangalia juu ya nini ambacho wewe kama mtanzania unapata haswa kwa upande wa hewa au mambo yanavyokwenda. hapa nanzungumzia mwananchi anayeishi chunya au kule kibondo upande wa kigoma.

lakini yapo mengine ambayo yataharibika baada ya muungano huu kuvunjika.ni dhahiri kwamba hali ya amani na utulivu iliyopo na tafsiri ya mshikamo iliyopo baina ya mataifa yetu ,kwa upande wa biasharana hata mahusiano binafsi yanatia moyo.kuvunjika kwa hili kutaathiri sana haya.

lakini pamoja na haya yapo mambo mengine mengi ambayo kwa kweli tutayapoteza kama hali hii itatoweka.

suala la kulinda muungano ni letu wote na nisingependa tulipuuze. watu wa kwanza kuchukiwa ni wale wanaopinga muungano huu.
 
JK wetu asipoisimamia na kuilinda KATIBA yetu ya JMT atakuwa Gorbachev wetu. Zanzibar sasa hivi wanatoa matamshi yao kama vile katiba hii haipo, haiwahusu. JK amewekwa pale kwa mujibu wa katiba hii lakini anakuwa kama anaionea haya vile!

Pamoja na kwamba ni muhimu kuilinda katiba na ni wajibu wa raisi na raiya wake, elewa kuwa katiba sio msaafu au bible. Kama ikidhihirika kwamba haikidhi mahitaji ya wananchi kwa wakati uliopo ni muhimu kuibadili kwa utaratibu unaofaa. Katiba tulio nayo ya JMT ina upungufu mkubwa sana hasa kwenye masuala ya muungano. Hivyo JK anatakiwa afungue macho aone hata kama itabidi awe Gorbachev kwa maslahi ya utaifa ni bora zaidi.
 
Muungano haulazimishwi na JK pekee, na si jambo la kumuangalia mtu moja moja na kutoa hukumu..muungano ni majumuisho ya historia, faida/hasara, wananchi, na wakati wake

Kama muungano utavujika ni wakati wake umefika wala halitakuwa kosa la gorbachov wala JK, wanaolilia muungano watuambie kinagaubaga wanataka muungano kwasababu zipi? na wanapata faida zipi kwa kuangalia historia yake nk. please "msilete habari za alinacha eti nyerere kasema" this is an old crying song hatutaki kusikia..tuambiwe sasa hivi (wakati huu) muungano unatusaidia nini? na uwe muungano wa aina gani? kwa manufaa zaidi?

Wanaokataa muugano vilevile watuambia hawataki kwasababu gani wanapata hasara gani na wanataka muugano wa aina gani?

Hoja ziwekwe wazi..hii mambo imefichwa sana utafikiri karume na nyerere walikuwa malaika ni ujinga kwa nchi yenye wasomi kama nchi yangu


Natumai na wewe ni msomi mbona hueleweki where did u stand on? and why? TOA MTIZAMO WAKO.:mad::mad:
 
Muungano haulazimishwi na JK pekee, na si jambo la kumuangalia mtu moja moja na kutoa hukumu...
Lakini, Ikulu au rais (kama taasisi) nimoja ya mihimili muhimu ya Muungano. Mtu anayeongoza taasisihiyo anapaswa kutoa uongozi utakaotyoa mwelekeo wa mambo muhimu kama nchi na kwa sisi, Muungano ni moja ya mambo muhimu kabisa. Kwa hiyo, JK hatoweza kukwepa lawama au sifa iwapo lolote litatokea kuuhusu Muungano wakati wa kipindi cha yeye kuongoza taasisi hiyo
 
Natumai na wewe ni msomi mbona hueleweki where did u stand on? and why? TOA MTIZAMO WAKO.:mad::mad:

Mkuu,

Msimamo wangu ni kwamba mambo ya siri za muungano ni ujima na ujinga

Muungano ujadiliwe upya prons and cons uwekwe nje utolewa sirini mpaka hadharini (public)

Pakubaliwe kama muungano uwepo au usiwepo! (referendum) na wa namna gani kwa faida ya watu walioungana!

Kuogopa mizimu ya kina nyerere na karume ni dalili ya shirk yaani tunaamini wafu utafikiri hatuna elimu...bana!

Wanachofanya wazanzibar nakiunga mkono kwakuwa watanganyika ni kanyaboya, hawajui kwanini wako kwenye muungano na faida zake.
 
Lakini, Ikulu au rais (kama taasisi) nimoja ya mihimili muhimu ya Muungano. Mtu anayeongoza taasisihiyo anapaswa kutoa uongozi utakaotyoa mwelekeo wa mambo muhimu kama nchi na kwa sisi, Muungano ni moja ya mambo muhimu kabisa. Kwa hiyo, JK hatoweza kukwepa lawama au sifa iwapo lolote litatokea kuuhusu Muungano wakati wa kipindi cha yeye kuongoza taasisi hiyo
Umuhimu wa muungano ni nini?

Muungano ni muhimu kupita maji na umeme shinyanga?

Muungano ni muhimu kupita kuondoa mafisadi serikalini?

Muungano ni muhimu kupita kujadili tume huru, katiba mpya? kidding!
 
Kusigina katiba kuanzia kwenye SMZ kutaka Bendera yao, then Ukaja kupigwa kwa wimbo wao wa taifa kwenye baraza la wawakilishi, ikaja kodi , mafuta na hivi karibuni wabara wataambiwa kuanza kutumia pasi za kusafiria kuingia huko visiwani. Hadithi ya Mwarabu na Ngamia inakaribia kutimia. Nadharia yangu ni kwamba ata kama URT itavunjika then kuna hatari ya kuwa na serikali ya Pemba na Zanzibar { Makubaliano ya Maalimu na Karume nyuma ya Pazia}. Kikwete inaonekana ameridhia kufa kwa URT.
 
Muungano ulipigiwa kura na Bunge la Tanganyika na Baraza la Wawakilishi wa Zanzibar. Pande zote mbili zilijadili (najua wengi hawajui historia hiyo). Nyerere alileta hoja Bungeni na kuwaelewa wabunge wetu kwanini mataifa mawili haya yataungana. Wabunge wakaridhia na ni baada ya hapo ndio Muungano ukafanyika.

Hivyo ni Muungano halali na ni jukumu la kila Mtanzania kuulinda. Katika kuulinda huko ni jukumu letu kuwapinga pasipo kuwapepesea macho wale wote wanaotaka Muungano uvunjike kwa sababu hawataki kufanya maamuzi magumu au kuzungumzia mambo yanayoleta utata katika Muungano. Wapo watu wa bara ambao kwa kawaida hatupendi sana migongano, tunapenda vitu lelemama kiasi kwamba tumekuwa kama tumedekezwa hivi!

Serikali ikisema "hawa wanaleta mgawanyiko katika jamii" basi kama watoto tunakubali na kuwakimbia wenzetu kwa sababu "serikali imesema"; Serikali ikija na kusema wapinzani wanataka kuligawa taifa basi tunakimbia kama watoto huku tumenyanyua mikono tubebwe huku tunaonesha vidole "yule anataka kuligawa taifa mama!".

Hatutaki kugonganisha mawazo na matokeo yake hata kwenye vikao vya kazi tumekuwa hivi hivi tu. Mtu anayebisha sana anaonekana "mbishi tu"; mtu anayetaka maelezo zaidi anaonekana kama anataka kujipendekeza. Tunataka mambo ya upole upole na taratibu.

Ndio maana utaona watu wengi wa bara wanaotaka Muungano uvunjike wanafanya hivyo kwa sababu utaondoa "migongano" na kubishana bishana. Tunataka "utulivu, amani, na mshikamano" wa uongo. Ndio maana watu wa bara wanaona kama Zanzibar ni wakorofi kweli kumbe kule Zanzibar wao wameshazoea zile siasa za kujibizana, kubishana na serikali, na kutunishiana misuli.

Ninaamini athari kubwa sana ya ukoloni katika psyche ya watu wa bara ni unchecked docility ya ajabu sana. Na watawala wetu wanatumia sana hii kuwatuliza watu wa bara.

Muungano tutaulinda na tutaudumisha na kuuboresha. Tutawapinga watu wa bara wanaotaka kuuvunja kwa sababu hawataki kubishana na kulumbana na kugongana kifikra na tutawapinga watu wa visiwani wanaotaka kuuvunja kwa sababu wanaogopa kukubali ukweli wa umuhimu wa muungano.

Tutawaunga mkono wale wote majasiri ambao watasimama na kutoa hoja za jinsi ya kuudumisha, watakaokuwa tayari kutoa mapendekezo ya jinsi ya kuuboresha na wale watakaonesha uongozi wa kuboresha muungano wetu kwa uwazi na ukweli na ujasiri usio kikomo.

Natumaini hatutawafumbia macho wala kuwaonea haya kuwashughulikia pasipo kuwabembeleza watu wanaofanya njama za kuuvunja muungano wetu.

Muungano daima!
 
Kusigina katiba kuanzia kwenye SMZ kutaka Bendera yao, then Ukaja kupigwa kwa wimbo wao wa taifa kwenye baraza la wawakilishi, ikaja kodi , mafuta na hivi karibuni wabara wataambiwa kuanza kutumia pasi za kusafiria kuingia huko visiwani. Hadithi ya Mwarabu na Ngamia inakaribia kutimia. Nadharia yangu ni kwamba ata kama URT itavunjika then kuna hatari ya kuwa na serikali ya Pemba na Zanzibar { Makubaliano ya Maalimu na Karume nyuma ya Pazia}. Kikwete inaonekana ameridhia kufa kwa URT.

Hiyo siyo nadharia yako ila mwl nyerere..alisema hayo kwenye maongezi yake...kama amekuwa yahaya na yeye sijui!

Hata ikiwa hivyo wewe mtanganyika inakuhusu nini? ombeni na nyinyi kusitokee mwanza zone and kilimanjaro zone damn!
 
Muungano ulipigiwa kura na Bunge la Tanganyika na Baraza la Wawakilishi wa Zanzibar. Pande zote mbili zilijadili (najua wengi hawajui historia hiyo). Nyerere alileta hoja Bungeni na kuwaelewa wabunge wetu kwanini mataifa mawili haya yataungana. Wabunge wakaridhia na ni baada ya hapo ndio Muungano ukafanyika.

Hivyo ni Muungano halali na ni jukumu la kila Mtanzania kuulinda. Katika kuulinda huko ni jukumu letu kuwapinga pasipo kuwapepesea macho wale wote wanaotaka Muungano uvunjike kwa sababu hawataki kufanya maamuzi magumu au kuzungumzia mambo yanayoleta utata katika Muungano. Wapo watu wa bara ambao kwa kawaida hatupendi sana migongano, tunapenda vitu lelemama kiasi kwamba tumekuwa kama tumedekezwa hivi!

Serikali ikisema "hawa wanaleta mgawanyiko katika jamii" basi kama watoto tunakubali na kuwakimbia wenzetu kwa sababu "serikali imesema"; Serikali ikija na kusema wapinzani wanataka kuligawa taifa basi tunakimbia kama watoto huku tumenyanyua mikono tubebwe huku tunaonesha vidole "yule anataka kuligawa taifa mama!".

Hatutaki kugonganisha mawazo na matokeo yake hata kwenye vikao vya kazi tumekuwa hivi hivi tu. Mtu anayebisha sana anaonekana "mbishi tu"; mtu anayetaka maelezo zaidi anaonekana kama anataka kujipendekeza. Tunataka mambo ya upole upole na taratibu.

Ndio maana utaona watu wengi wa bara wanaotaka Muungano uvunjike wanafanya hivyo kwa sababu utaondoa "migongano" na kubishana bishana. Tunataka "utulivu, amani, na mshikamano" wa uongo. Ndio maana watu wa bara wanaona kama Zanzibar ni wakorofi kweli kumbe kule Zanzibar wao wameshazoea zile siasa za kujibizana, kubishana na serikali, na kutunishiana misuli.

Ninaamini athari kubwa sana ya ukoloni katika psyche ya watu wa bara ni unchecked docility ya ajabu sana. Na watawala wetu wanatumia sana hii kuwatuliza watu wa bara.

Muungano tutaulinda na tutaudumisha na kuuboresha. Tutawapinga watu wa bara wanaotaka kuuvunja kwa sababu hawataki kubishana na kulumbana na kugongana kifikra na tutawapinga watu wa visiwani wanaotaka kuuvunja kwa sababu wanaogopa kukubali ukweli wa umuhimu wa muungano.

Tutawaunga mkono wale wote majasiri ambao watasimama na kutoa hoja za jinsi ya kuudumisha, watakaokuwa tayari kutoa mapendekezo ya jinsi ya kuuboresha na wale watakaonesha uongozi wa kuboresha muungano wetu kwa uwazi na ukweli na ujasiri usio kikomo.

Natumaini hatutawafumbia macho wala kuwaonea haya kuwashughulikia pasipo kuwabembeleza watu wanaofanya njama za kuuvunja muungano wetu.

Muungano daima!

Acha kupotosha watu...

Muungano ulikuwa wa nyerere na karume

Unataka tuulinde kwasababu zipi? tuambie faida zake

Ni wakati muafaka muungano utoke sirini uje hadharani upigie kura
 
Sasaunategemea nini kama 'Gobachev' wetu yuko kiguu na njia angani kwenye Uswiss et al? Lini anakaa na kusoma au kujisomea taarifa mbali mbali za kuhusu matatizo ya URT hasa hasa huu mwiba ulipo kwenye Muungano? Matokeo yake unakuta rais anategemea wasaidizi wake asilimia 100 ambayo ni hatari kwa usalama wa Taifa. Anaweza akawa analishwa 'kasa' kila siku. Rejea kituko cha wasaidizi wake kwenye kutoa msaada wa magari ya wagonjwa na sakata la kuwepo kwa MD wa wilaya ya ngorongor. Kaazi kweli kweli.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom