Kikwete kumalizia kumsafisha Lowassa

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Kabla ya kuletwa tena na serikali ripoti ya utekelezaji wa maamuzi ya bunge juu ya richmond Lowassa atakuwa amesafishwa rasmi-siyo na bunge, siyo na magazeti bali na rafiki wa siku nyingi na mshirika wake katika safari ya siasa. Si kwamba JK ana uchaguzi katika hilo; hana. Na wana CCM wote (hamaanisha wote) watasema "amina". Na bomu la wapiganaji ccm litakuwa limeteguliwa kitaalam. EL ametambua kuwa : mlete rafiki yako karibu lakini adui yako karibu zaidi.
 
Last edited:
usishange hata lowasa nae akijiunga na wapinga mafisadi-tunapigwa changa la macho
 
Tusubiri tuone itakuwaje. kama kweli itakuwa ndivyo hivyo lazima tukubali kuwa sisi ni wajinga. Yaani ndivyo tulivyo. Lowassa hasafishiki, kama mtu amewahi kulidanganya bunge lenye maprofesa kuwa uchumi unapaa wakati hata Rostowian theory hajui, amejaribu kuwaghilibu watanzania kwa mvua za bandia ambazo hatuzihitaji, na Richmond and so on then tutakuwa wajinga....tusubiri. lakini sitaki kuamini kama bunge litarui kulekule kuwa mhuri.
 
Ukiona mtu amechafuka na tope na maji yanayomzunguka ni ya matope ujue kwamba yeyote atakayejaribu kumsafisha kwa maji hayo naye atajikuta amechafuka na tope.
 
Ukiona mtu amechafuka na tope na maji yanayomzunguka ni ya matope ujue kwamba yeyote atakayejaribu kumsafisha kwa maji hayo naye atajikuta amechafuka na tope.

Weli at the end wote watachafuka. Swala la msingi ni jee mmoja au wote wakichafuka SISI tunafanya nini? Baada ya kuona uchafu no one cares. By the way ni lini huyu msafishaji aliwahi kuwa Msafi ndo sasa tuseme atachafuka??
 
Umenena kweli. Huyu mtu laona anuanuka uvundo wa chuma, ili atakate labda akaoge oil ya gear box au Acid, vinginevyo hatakati kabisa
 
Kabla ya kuletwa tena na serikali ripoti ya utekelezaji wa maamuzi ya bunge juu ya richmond Lowassa atakuwa amesafishwa rasmi-siyo na bunge, siyo na magazeti bali na rafiki wa siku nyingi na mshirika wake katika safari ya siasa. Si kwamba JK ana uchaguzi katika hilo; hana. Na wana CCM wote (hamaanisha wote) watasema "amina". Na bomu la wapiganaji ccm litakuwa limeteguliwa kitaalam. EL ametambua kuwa : mlete rafiki yako karibu lakini adui yako karibu zaidi.

Mkuu Mwanakijiji,

Na inasemekana ktk mkutano wa bunge ujao mwezi Novemba, wabunge wote wa CCM watakaa kama kamat ya chama na kukubaliana kuanza upya na kusahau yaliyopita na hapo watatangaza rasmi kuwa hoja ya ufisadi imefungwa ndani ya chama na yaliyobaki yashughulikiwe na vyombo vya dola.

Baada ya hapo itafuata ripoti ya utekelezaji ya masuala ya richmond (iliyofanyiwa marekebisho na mkulu) na hapo itatamkwa wazi kwamba EL hakuwa na kosa kisheria bali alishauriwa vibaya na wataalamu ambao wamekwisha onywa.

Serikali kupitia waziri mkuu itatoa taarifa ya kuufunga mjadala wa richmond ndani ya chama na nje ya chama. Huu ndio utakuwa mwisho wa kikundi cha akina Mwakyembe na EL atakuwa huru rasmi baada ya kikao hicho cha bunge.
 
Ukiona mtu amechafuka na tope na maji yanayomzunguka ni ya matope ujue kwamba yeyote atakayejaribu kumsafisha kwa maji hayo naye atajikuta amechafuka na tope.

Tena atachafuka kuliko yeye, kwani msafishwa atatakata na msafisha atachafuka.
Ni sawa na kusafisha samaki unabaki na shombo
 
Juzi hapa kasema wametoka mbali na Mkuu wa Kaya hawajakutana barabarani na hata hawatatenganishwa barabarani na watu wanao mchafua mlitegemea nini hapo ndicho tunacho kisubili sasa kama maamuzi ya Bunge kuhusu swala la Richomnduli kuna kauvivu flani kushughulikia basi tutarajie kusafishwa rasmi EL na tutegemee atachukua nchi 2015 Uswahiba unaendelea.
 
Njaa bwana, ninaamini kama vya vya upinzani vingejiunga pamoja kama walivyo fanya Kenya CCM ingetoka, shida wataanza kugombania madaraka.
 
Katika hindu mythology kuna kitu kinaitwa 'Karma',msingi mkuu wa dhana ya Karma ni kama ule wa Murphy's law kwamba 'la kuwa litakuwa tu',tuko pamoja Wakuu wa jamvi?
 
No walikuwa na uwezo wa kuchukua nchi 2015, 2020 kama strategy zao zingekuwa makini zaidi.

Japo umesema kwa ku-conclude,still I hope wanachance kubwa ya kushika nchi, if and only if they will face reality na kupata wapiga kura

Maana kazi si kutetea maamuzi yao, kazi ni kwa jinsi gani kila wanachofanya wanaathiri wapiga kura.

siasa is a game though,

Vyama vya upinzani visahau kuchukua nchi kwa njia ya kura unless mambo yafuatayo yafanyike kwanza.

1. Waongeze nguvu zao katika kudai mabadiliko ya Katiba ili kuwe na Tume huru ya uchaguzi itakayodhibiti mbinu zote chafu za wizi wa kura na kumanipulate final tallies of election results- Kwa hili sisiM imejipanga vilivyo kulizima.

2. Wakiisha pata Tume huru ya Uchaguzi, wagombee ubunge kwanza si Mbowe, Lipumba et al ili kulichukua bunge yaani wawe na filibuster majority ya kupitisha agenda za mageuzi, hili nalo kwa sisiM ni bora punda afe mzigo ufike wapo tayari kwa lolote.

3. Kukiisha kuwa mazingira ya usawa na haki na uhuru katika chaguzi, na baada ya kuwaonesha wananchi kuwa wapinzani wanaweza tena zaidi ya sisiM hapo tunaweza pata rais wa kwanza wa kidemokrasia halisi katika historia ya nchi.

Vinginevyo haya yoote tunayoongea ni kelele za mlango, sisiM wanajua wanachokifanya kwani style yao ni kuwa, Jeshi la wananchi, UWT, Polisi na kila chombo kilicho katika serikali ni lazima kijue kuwa masilahi yao ni masilahi ya CCM, kushindwa kwa CCM ni kupoteza kwaoa maslahi hayo. Hivyo wamekula viapo vya mioyoni kuwa watailinda CCM mpaka tone la mwisho.

Ukweli ni kwamba Tanzania ilitakiwa ifikirie kuingia kwenye siasa za vyama vingi labla mwaka 2080. VINGINEVYO KUWE NA WA KUFANYIWA KAFARA KWA AJILI YA UKOMBOZI WA KWELI WA KULETA DEMOKRASIA- Un-option which is not recommended by any one unless you feel useless and stranded for you life is no difference to death because of "POVERTY"
 
wajinga ndio waliwao, huyu EL kama tayari amesharudi kwa hii serikali ya jk
 
Ukiona mtu amechafuka na tope na maji yanayomzunguka ni ya matope ujue kwamba yeyote atakayejaribu kumsafisha kwa maji hayo naye atajikuta amechafuka na tope.

- Mkuu Jasusi, maneno mazito sana haya, sio siri kwamba the mafisadi's plan ni Lowassa kurudishwa next cabinet, katika capacity ya foreign au defense, ili aweze kuwa na nafasi nzuri ya urais 2015, lakini tatizo la hii theory ni wapiganaji na Membe, ambaye sasa hivi sio siri ndiye namba two,

- Kwa maoni yangu ni kwamba Lowassa hatakuja kuwa anything tena zaidi tu ya alipofikia sasa, kosa kubwa sana alilolifanya kisiasa ni kukosa umakamu wa CCM kwa sababu tu ya tamaa zake za fisi, mbio zake zote huko pembeni ni bure tu na wala sio siri kwamba anatumia hela nyingi sana za kifisadi kujitengeneza njia ya kurudi, lakini CCM as a chama hawawezi ku-afford maana ni kuwapa Chadema risasi za bure.

- CCM haiwezi kupambana na Chadema majukwaani bila ya kuwa ya wabunge wake wapiganaji 11, majuzi wamejaribu maji kule NEC, wameona response ya media na wananchi na hata baadhi ya viongozi mbali mbali kuanzia wa dini mpaka wa upinzani, tatizo la Lowassa ni hawa wapiganaji 11 ambao hana dawa ya kuwamaliza au kuwatoa kwenye picha, kwa hiyo he is stuck and done, ingawa hatakwenda hivi hivi.

Respect.

FMEs!
 
Vyama vya upinzani visahau kuchukua nchi kwa njia ya kura unless mambo yafuatayo yafanyike kwanza.

1. Waongeze nguvu zao katika kudai mabadiliko ya Katiba ili kuwe na Tume huru ya uchaguzi itakayodhibiti mbinu zote chafu za wizi wa kura na kumanipulate final tallies of election results- Kwa hili sisiM imejipanga vilivyo kulizima.

2. Wakiisha pata Tume huru ya Uchaguzi, wagombee ubunge kwanza si Mbowe, Lipumba et al ili kulichukua bunge yaani wawe na filibuster majority ya kupitisha agenda za mageuzi, hili nalo kwa sisiM ni bora punda afe mzigo ufike wapo tayari kwa lolote.

3. Kukiisha kuwa mazingira ya usawa na haki na uhuru katika chaguzi, na baada ya kuwaonesha wananchi kuwa wapinzani wanaweza tena zaidi ya sisiM hapo tunaweza pata rais wa kwanza wa kidemokrasia halisi katika historia ya nchi.

Vinginevyo haya yoote tunayoongea ni kelele za mlango, sisiM wanajua wanachokifanya kwani style yao ni kuwa, Jeshi la wananchi, UWT, Polisi na kila chombo kilicho katika serikali ni lazima kijue kuwa masilahi yao ni masilahi ya CCM, kushindwa kwa CCM ni kupoteza kwaoa maslahi hayo. Hivyo wamekula viapo vya mioyoni kuwa watailinda CCM mpaka tone la mwisho.

Ukweli ni kwamba Tanzania ilitakiwa ifikirie kuingia kwenye siasa za vyama vingi labla mwaka 2080. VINGINEVYO KUWE NA WA KUFANYIWA KAFARA KWA AJILI YA UKOMBOZI WA KWELI WA KULETA DEMOKRASIA- Un-option which is not recommended by any one unless you feel useless and stranded for you life is no difference to death because of "POVERTY"

I support your point, ni kweli tutapiga kelele bila tume huru na kuondoa mbinu chafu za CCM hamna kitu ushindi na kuiondoa madarakani
 
Kabla ya kuletwa tena na serikali ripoti ya utekelezaji wa maamuzi ya bunge juu ya richmond Lowassa atakuwa amesafishwa rasmi-siyo na bunge, siyo na magazeti bali na rafiki wa siku nyingi na mshirika wake katika safari ya siasa. Si kwamba JK ana uchaguzi katika hilo; hana. Na wana CCM wote (hamaanisha wote) watasema "amina". Na bomu la wapiganaji ccm litakuwa limeteguliwa kitaalam. EL ametambua kuwa : mlete rafiki yako karibu lakini adui yako karibu zaidi.

sentensi nzito sana hiyo. Kuna hidden message hapo. Nadhani wanaJF tungependa ufafanuzi zaidi...
 
Mkuu Mwanakijiji,

Na inasemekana ktk mkutano wa bunge ujao mwezi Novemba, wabunge wote wa CCM watakaa kama kamat ya chama na kukubaliana kuanza upya na kusahau yaliyopita na hapo watatangaza rasmi kuwa hoja ya ufisadi imefungwa ndani ya chama na yaliyobaki yashughulikiwe na vyombo vya dola.

Baada ya hapo itafuata ripoti ya utekelezaji ya masuala ya richmond (iliyofanyiwa marekebisho na mkulu) na hapo itatamkwa wazi kwamba EL hakuwa na kosa kisheria bali alishauriwa vibaya na wataalamu ambao wamekwisha onywa.

Serikali kupitia waziri mkuu itatoa taarifa ya kuufunga mjadala wa richmond ndani ya chama na nje ya chama. Huu ndio utakuwa mwisho wa kikundi cha akina Mwakyembe na EL atakuwa huru rasmi baada ya kikao hicho cha bunge.
Hasa ukizingatia kuwa Six naye alishapigwa bit la nguvu
 
Back
Top Bottom