Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,756
Kikwete, uliwahi kutamka kuwa katika vita dhidi ya mafisadi huna rafiki wala ndugu, huo ulikuwa wakati sakata la Kagoda lilipopamba moto hadi kuihusisha Ikulu. Nakumbuka pesa za walipa kodi ilivyotumiwa na serikali eti katika kujaribu kufichua utata ulioigubika Kagoda hadi makachero wa Tanzania wakalazimika kusafiri hadi nchi za Ulaya na Asia kwa ajili ya kuchunguza baadhi ya kampuni zilizohusishwa na Kagoda.
Cha jabu ni kuwa hivi sasa kuna kesi kortini imefunguliwa dhidi ya Kagoda na mtu anayedai kuwa ndiye alieidhamini Kagoda kuchota fedha Benki Kuu. Si hilo tu mtu huyo anaenda mbali na kudai kuwa hata wakati utata wa Kagoda unatuumiza vichwa, mtu huyo huyo kwa mara nyingine aliweza kuikopesha Kagoda kiasi kikubwa cha fedha. Huyo mtu naambiwa si mwingine bali ni mshikaji wako Yusufu Manji.
Wananchi wengi wanajua kuwa hadi leo serikali inadai haiwajui wamiliki wa Kagoda na hivyo imeshindwa kuichukulia hatua zozote. Swali langu kwako ni je, mathalan mshiriki wa Kagoda sasa kajitokeza wazi bila kificho, serikali yako inasubiri nini kumkamata mara moja ili aweze kuhojiwa zaidi. Kama serikali itakaa kimya bila kuchukua hatua yoyote dhidi ya Manji, basi tutaamini zile tetesi kuwa Kagoda ndiyo CCM.
Kuchaguliwa kwa Kikwete kulileta faraja kubwa kwa mafisadi !
Cha jabu ni kuwa hivi sasa kuna kesi kortini imefunguliwa dhidi ya Kagoda na mtu anayedai kuwa ndiye alieidhamini Kagoda kuchota fedha Benki Kuu. Si hilo tu mtu huyo anaenda mbali na kudai kuwa hata wakati utata wa Kagoda unatuumiza vichwa, mtu huyo huyo kwa mara nyingine aliweza kuikopesha Kagoda kiasi kikubwa cha fedha. Huyo mtu naambiwa si mwingine bali ni mshikaji wako Yusufu Manji.
Wananchi wengi wanajua kuwa hadi leo serikali inadai haiwajui wamiliki wa Kagoda na hivyo imeshindwa kuichukulia hatua zozote. Swali langu kwako ni je, mathalan mshiriki wa Kagoda sasa kajitokeza wazi bila kificho, serikali yako inasubiri nini kumkamata mara moja ili aweze kuhojiwa zaidi. Kama serikali itakaa kimya bila kuchukua hatua yoyote dhidi ya Manji, basi tutaamini zile tetesi kuwa Kagoda ndiyo CCM.
Kuchaguliwa kwa Kikwete kulileta faraja kubwa kwa mafisadi !