Kikwete kainua uchumi wa Tanzania

Kwanini unogopa kukubali kuwa GDP ya TANZANIA IMEKUA? N a kama huamini takwimu za CIA, basi tupe kile chanzo unachokiamini. Kwa sababu hatuwezi kuishi bila takwimu kama tupo makini. Ni lazima tujue juzi tulikuwa wapi, jana, leo na ndipo tutaweza kupanga mipango ya kesho. Sasa tuambie mwenzetu unapotaka kujua uchumi wa nchi kama unapanda au kushuka unaangalia wapi?

HIV/AIDS inakula sana uchumi wa Taifa kuliko hilo punguo la watu.
1) Mgonjwa ambaye huugua zaidi ya miaka mitano anakosa nguvu na morali ya kufanya kazi.
2. Ndugu na jamaa huacha kazi kwa ajili ya kumuuguza mgonjwa.
3. Gharama kubwa kwa serikali katika kutoa elimu, matangazo, madawa na wataalam.

Kupungua kwa Annual growth rate kumetokana na azma ya Kikwete kushirikisha wananchi wa kawaida katika uchumi. Kitu ambacho mimi ninamuunga mkono, kwani Mkapa hakukifanya na hata kudharau kabisa kile tuitacho uti wa mgongo wa Uchumi "Kilimo". Kumbuka: Muundo wowote wa uchumi usiowashirikisha wananchi, utafeli.

Hatuwezi kujenga uchumi kama India. India ni moja kati ya nchi ambazo zinatafsiriwa kama Tajiri na masikini kwa wakati mmoja. Kwa sababu uchumi wa nchi umeshikwa na 20% ya wananchi, na wengine wamesahauliwa kabisa. Ninaposema kusahauliwa, ninamaanisha kuwa hawapo kabisa katika program ya taifa hata kwa siku zijazo. Hivyo japo India inaviwanda vikubwa (TATA, Vifaru, computa, matrekta n.k) lakini huwezi kuamini kuwa 60% ya wananchi wake wanaishi kwa kipato cha chini ya $1 kwa siku. China na India zina idadi ya watu karibu sawa, lakini tofauti ya nchi hizo ni mipango kwa wananchi wao. Wakati China ina mpango kwa wanachi wake (Elimu, afya, kilimo, malazi n.k), India haiwekezi hata senti tano kwenye hayo maeneo.

Ukifanya hivyo kama India, annual growth rate itakua. Mahesabu hapo ni madogo, chukulia unafamilia ya watoto 5 sawa na kaka yako. Wote mnafanya biashara ya Duka,, itoayo faida ya milioni 2 kwa mwezi. Watoto wako wakifika darasa la saba ndio mwisho, hakuna sekondari. Aidha waolewe au waoe na kujiendeshea maisha yao wenyewe. Na kaka yako akaamua kuwaendeleza na kulipa takriban 1milioni kwa mwaka kwa kila mtoto. Kimahesabu kaka yako yuko chini kwa 5milion (-5milion), kwa mwaka, nawe utakuwa na +5milion. Kama unadhani nchi iendeshwe hivyo kama mdogo wako +5M)basi Msifu Mkapa, Vinginevyo (-5M) msifu Kikwete.

Ni Zimbabe tu ndio iliyoshuka GDP yake, nyingine zote zimepanda lakini si kama Tanzania.

Kifupi unanikumbusha msemo niliousoma humu humu JF, Mwana JF aliandika " If you think that education is expensive, try ignorance"


[/QUkwani Mkapa hakukifanya na hata kudharau kabisa kile tuitacho uti wa mgongo wa Uchumi "Kilimo". Kumbuka: Muundo wowote wa uchumi usiowashirikisha wananchi, utafeli.
Hicho kisehemu kwamba kama wananchi hawatashirikishwa katka mambo ya uchumi wao na state security basi malengo yataanguka. Hii inafanana na hoja moja walioibuka nayo tribal leaders in Afghanistan na kuwaambia waandishi wa habari ; America will fail war in Afghanistan if will not involve tribes and communities in the removal of Taliban regime. Power and task force needed to be coordinated through particiaption na pia to maintain strong network.
sawa
 
Ahsante JMK, toka umeingia madarakani, takwimu zote zinaonyesha ukuaji, mashule ya sekondari zaidi ya asilimia 100 juu, vyuo vikuu zaidi ya asili mia 100, mazahanati zaidi ya asilimia 100, kazi mpya zaidi ya asilimia mia moja, uchumi ndio kama hiyo report hapo juu inavyojieleza, kesi zinazosikilizwa na kumalizwa mahakamani zaidi ya asilimia 200, na, na, na, Yote hiyo kwa muda mchache wa kuanzia 2005.

Ni Rais gani mwingine wa Tanzania aliyeweka rekodi inayokaribia hii? = HAKUNA!

Mkuu kama kweli hiki ndio unachokiona pole sana. Una aamini kweli waalimu ni asilimia 100? madai yao wameshughulikiwa, ajira mpya? pole sana mkuu. Naona bado Mkapa was far better than JK. Miaka 5 ya kwanza ya Ben tuliona mengi tangible lakini sasa ya JK wewe ndio unayaona.
 
Why don't you go and get direct figures www.cia.gov; these are correct figures just released: Create Date: Sep-17-2009 08:51
GDP (Purchasing Parirt); there are no current estimates for 2009

GDP (purchasing power parity):
$54.25 billion (2008 est.)
country comparison to the world: 88 $50.65 billion (2007 est.)
$47.27 billion (2006 est.)
note: data are in 2008 US dollars
GDP (official exchange rate):
$20.72 billion (2008 est.)
GDP - real growth rate:
7.1% (2008 est.)
country comparison to the world: 36 7.1% (2007 est.)
6.7% (2006 est.)
GDP - per capita (PPP):
$1,300 (2008 est.)
country comparison to the world: 204 $1,300 (2007 est.)
$1,200 (2006 est.)
note: data are in 2008 US dollars
GDP - composition by sector:
agriculture: 27.1%
industry: 22.5%
services: 50.4% (2008 est.)
Angalia hapo nilipoweka wino mwekundu ktk quate. Utagundua kwamba hata hizo takwimu ulizotoa zinakubaliana na kichwa cha habari. Yaani GDP ni $1300, ukilinganisha na ile niliyoiandika $1400. Tofauti sio kubwa na katika takwimu, hiyo hukubalika na ndio maana ameadika EST( kadirio). Hivyo uchumi umepanda na unaendelea kupanda kama takwimu zako zinavyoonyesha. Na hilo ndilo la msingi.

Ukweli ni kwamba kila utapojaribu kwenda kutafuta vyanzo vingine, ni moja utakutana nalo, hili la kupanda kwa uchumi. Jamani tumpe sifa zake huyu raisi kijana, angalau katika hili. Ndio, kama binaadam ana udhaifu wake lakini hapa kaonyesha ujasiri. Kikwete anaweza!!!!
 
Mkuu kama kweli hiki ndio unachokiona pole sana. Una aamini kweli waalimu ni asilimia 100? madai yao wameshughulikiwa, ajira mpya? pole sana mkuu. Naona bado Mkapa was far better than JK. Miaka 5 ya kwanza ya Ben tuliona mengi tangible lakini sasa ya JK wewe ndio unayaona.
Unajua, ndugu Bongo lander nikwambie kitu kimoja ambacho bado hujakifahamu. Ikitokea vita, utafunzwa kuendesha gari masaa 5, na kukabidhiwa Scania kupeleka chakula kwenye uwanja wa mapambano. Askari atafundishwa silaha na ujanja wa porini kwa siku 5, na kukabidhiwa bnduki na kwenda mapambanoni. Hivyo ndivyo ilivyo popote duniani.

Sasa kitu usichokifahamu ni kuwa Tanzania tupo katika VITA. Vita ya kumuondoa adui ujinga. Hii ni vita kubwa kuliko ya kumtoa Idd Amin. Maana si vita utayoimaliza kwa mwaka au miaka10, bali ni vita endelevu. Tunawasiliana mimi na wewe kwa sabau tulikwenda shule. Lakini kwa mtindo ule, kati ya wanafunzi darasa la saba 100 eti wanafaulu 2 tu, ni aibu kubwa sana. Katika hilo hakukua na jinsi ila kutangaza vita.

Ikiwa vijana hawajui kusoma na kuandika, hata kama ukaweka matangazo ya kukomesha ukimwi lakini vijana hawajui kusoma unapoteza pesa yako tu. Lakini kwa sasa hivi, angalia hata magazeti wanunuaji ni walala hoi ambao zamani walikuwa hawajui kusoma. Hii itaturahisishia hata katika ukuaji wa Demokrasia nchini. Hivyo tuunge mkono hali iliyopo, angalau moja tumetatua, hili la madarasa. Kuwa hatutaonyeshwa tena kwenye CNN vijana wetu wkisomea kwenye miti. Sasa tuje kwenye hili la walimu. Ninahakika kabisa kuwa linawezekana. Tumuunge mkono Rais wetu Kikwete.
 
Hapana :

www.aneki.com siyo website ya CIA. CIA kama chombo cha serikali ya Marekani, website yao lazima iwe na extension ya .gov.

CIA wanatumia secire servers kwa computer zao zote na website ya CIA https://www.cia.gov. Mara ya mwisho nilipofika kwenye ofisi zao na laptop yangu, nilishangaa kutambua kuwa walikuwa wanajua kila kitu kilichoko kwenye hard disk yangu. Kwa bahati nzuri nilikuwa na mambo ya uhandisi tu, kwa hiyo sikupata kashkash yoyotte.

Webpage ya CIA kuhusu Tanzania ni hii hapa.

Wao wenyewe wamasema hivi kuhusu uchumi wa Tanzania. Napenda uangalie hiyo sentensi ya kwanza kwa vile inazima yote yanayofuatia.
Kwanini usituandikie GDP ya Tanzaini toka cia.gov? Ukazunguka maneno Mengi! Unajua kwanini! Gues! Kwa sababu unajua kuwa haitofautiani sana na hiyo niliyoiandika.

Hata hivyo, ndugu Interested Observer #8 ametusaidia. ANGALIA MAANDIKO YALIYO KATIKA wino mwekundu. Hata huko mambo si mabaya kwa Kikwete. Kama macho yangu hayanidanganyi, inasoma GDP $1300. Si tofauti kubwa ($1400], inakubalika katika takwimu. KWA HIYO UCHUMI UNAPANDA. tUMSIFU HUYU RAIS KIJANA.

"Why don't you go and get direct figures www.cia.gov; these are correct figures just released: Create Date: Sep-17-2009 08:51
GDP (Purchasing Parirt); there are no current estimates for 2009

GDP (purchasing power parity):
$54.25 billion (2008 est.)
country comparison to the world: 88 $50.65 billion (2007 est.)
$47.27 billion (2006 est.)
note: data are in 2008 US dollars
GDP (official exchange rate):
$20.72 billion (2008 est.)
GDP - real growth rate:
7.1% (2008 est.)
country comparison to the world: 36 7.1% (2007 est.)
6.7% (2006 est.)
GDP - per capita (PPP):
$1,300 (2008 est.)
country comparison to the world: 204 $1,300 (2007 est.)
$1,200 (2006 est.)
note: data are in 2008 US dollars
GDP - composition by sector:
agriculture: 27.1%
industry: 22.5%
services: 50.4% (2008 est.)"
 
Haba tukubalitu tu yaishe!!!

Uchumi umependa, full stop, whether aliyepandisha ni Kikwete, au Mkapa au mimi na wewe? We don't care... Ukweli Uchumi umependa.
 
Hatuwezi kujenga uchumi kama India. India ni moja kati ya nchi ambazo zinatafsiriwa kama Tajiri na masikini kwa wakati mmoja. Kwa sababu uchumi wa nchi umeshikwa na 20% ya wananchi, na wengine wamesahauliwa kabisa. Ninaposema kusahauliwa, ninamaanisha kuwa hawapo kabisa katika program ya taifa hata kwa siku zijazo. Hivyo japo India inaviwanda vikubwa (TATA, Vifaru, computa, matrekta n.k) lakini huwezi kuamini kuwa 60% ya wananchi wake wanaishi kwa kipato cha chini ya $1 kwa siku. China na India zina idadi ya watu karibu sawa, lakini tofauti ya nchi hizo ni mipango kwa wananchi wao. Wakati China ina mpango kwa wanachi wake (Elimu, afya, kilimo, malazi n.k), India haiwekezi hata senti tano kwenye hayo maeneo.

Ukifanya hivyo kama India, annual growth rate itakua.

Umeshawahi kufika china weye au unaandika tu kwa sababu unaweza kufanya hivyo?!muwe mnaandika vitu mlivyo na uhakika navyo..,hakuna program ya afya,elimu,malazi, kama unavyoongea wewe kutoka kwa serikali ya china kwenda kwa wananchi wake..,iwe masikini au matajiri..,

information mnazoweka hapa ni elimu kwa baadhi ya watu..,go a little further to verify them kabla ya kuziweka hapa..,ni hayo tu.

FYI:much of what you read on the internet is incorrect..,usitegemee sana Google.:)
 
Umeshawahi kufika china weye au unaandika tu kwa sababu unaweza kufanya hivyo?!muwe mnaandika vitu mlivyo na uhakika navyo..,hakuna program ya afya,elimu,malazi, kama unavyoongea wewe kutoka kwa serikali ya china kwenda kwa wananchi wake..,iwe masikini au matajiri..,

information mnazoweka hapa ni elimu kwa baadhi ya watu..,go a little further to verify them kabla ya kuziweka hapa..,ni hayo tu.

FYI:much of what you read on the internet is incorrect..,usitegemee sana Google.:)
Tena tunapenda sana watu kama nyie, Sasa tupe uhondo wa hayo ya China, maana mwenzetu umesoma na kuishi huko. Wana JF wanakusubiri, mbona una kanusha tu bila kutoa takwimu zako zitazoonyesha tusemayo si kweli.

Vibaya hivyo, si unajua hapa ni pahala pa kuelimishana. Tupe elimu na ulinganishe kati ya India na China. Kwa muono wangu huwezi kulinganisha China na India katika hilo.
 
Ninafura kusema kuwa kumbe wote ukweli tunaujua kuwa Serikali ya Kikwete imefanya kazi kubwa sana ya kuinua uchumi wa Taifa. Kwa sababu hakuna hata mmoja aliyekuja na Data tofauti, ama aliyekataa moja kwa moja kuwa uchumi haukui.

Na tunajua kuwa uchumi hauwezi kukua wenyewe tu, au sijui ushuke toka Mbinguni. Kwa hilo ninafuraha sana, na nitazidi kuleta mafanikio ya awamu ya 4. Kwa vile kilio cha wengi huko nyuma kilikuwa : Hivi huyu Kikwete kafanya nini cha maana? Kuna wengi wameingia mtini baada ya kupata hoja dhahir. Ukibisha. lete takwimu na chanzo. Hii ndio kanuni ya mchezo huu.

Huu ni uwanj wa mafanikio, wa kufeli utakuja baadaye.
 
Tabasam la Kikwete lina bahati, ngekewa na linazivuta nchi zote duniani kuiona Tanzania kama Tumaini la uwekezaji.

Ee bana kweli kabisa Zawadi Ngoda! Kikwete haitaji kufanya lolote zaidi ya kutabasamu tu, na Voila! Uchumi wa nchi "unapaa" wenyewe kwa miujiza.

Kulingana na takwimu za CIA, uchumi wa Tanzania unakadiriwa kupaa kwa asilimia 0.00000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000001
kila Kiwete anapotabasamu!
 
Na idadi ya waalimu Over 100%
na vyuo vya waalimu Over 100%
na mishahara ya waalimu imepanda sijui kwa asili mia ngapi?
na madai ya waalimu yanashughulikiwa kwa kasi kuliko kipindi chochote kile.
na karibuni tutaanza kuona matunda ya kuipa nchi elimu.

Kutokuwa na waalimu bora (wasio na taaluma) ni uozo alioukuta JMK na ndio anaushughulikia ipasavyo! Upo hapo ulipo?

Jee kama hukuanza sasa kujenga mashule na kutumia hao waalimu uozo uliowakuta hao bora utawatoa wapi ghafla ghafla? Kwanza jenga madarasa, pili nyumba za waalimu, tatu tafuta waalimu bora, hata ikibidi kuwaleta kutoka nje ya nchi. Kama huna madarasa, nyumba za kuishi hao waalimu hata ukiwaajiri leo watasomesha wapi? chini ya muembe kama wakati wa awamu zilizopita? hebu fanya fikra japo kidogo tu!

Ee bana Dar es Salaam sawa kabisa! Imebaki Kikwete kujenga misikiti ya Ijumaa kila mkoa Tanzania. Nadhani akifanya hivi, uchumi utakuwa 100%! Kipato kitapanda 100% kwa kudra ya Allah na tabasamu ngekewa ya Kikwete! Watu tutakuwa tunaishi mbinguni!
 
DAR-ES SALAAM KASEMA
Ahsante JMK, toka umeingia madarakani, takwimu zote zinaonyesha ukuaji, mashule ya sekondari zaidi ya asilimia 100 juu, vyuo vikuu zaidi ya asili mia 100, mazahanati zaidi ya asilimia 100, kazi mpya zaidi ya asilimia mia moja, uchumi ndio kama hiyo report hapo juu inavyojieleza, kesi zinazosikilizwa na kumalizwa mahakamani zaidi ya asilimia 200, na, na, na, Yote hiyo kwa muda mchache wa kuanzia 2005.

Ni Rais gani mwingine wa Tanzania aliyeweka rekodi inayokaribia hii? = HAKUNA!

JE NI SHULE GANI MPYA YENYE HADHI YA ILBORU AU MZUMBE!SHULE SI IDADI BALI KIWANGO. ni bora ujenge shule tatu kama Ilboru ya Arusha kuliko kujenga shule 20 zenye hadhi ya chini na hazina walimu. Kwanini wasikuze shule zilizopo!
 
no social mobility

poor programmes to reach the poor

no encouragement to grow internal bussinessess

no self help programmes to increase the government income

still looking for doners on his budget

begging investors to rob us (by the way this is where the GDP inakuongopea)

lastly poor kilimo, kilimo strategy looh! ebu nendeni mka waulize wa-russia, romania etc kilimo kiliwapeleka wapi zaidi ya kuishia kuwacha vyakula vinaoza kwenye ma-warehouse. You need all you can get to advance. Na si kuangalia projection or facts ambazo zina base na government income through foreign investment.

$1,300 GDP hiyo ni kusema bongo over 1.5mil (lowest estimate) bongo shillings, monthly ni karibu laki 140,000 uoni hadithi tupu on what transactions tumetengeneza hiyo GDP. It does not reflect the income of 36million people nor the government revenue for that period year so how did you come up with those figure pleeease.

Na education in terms of literacy nyerere katuacha na almost ninety percent the decline ni walio fuatia hana shughuli JK.

Even the society ina msuta with the amount of poverty watu walionayo. Aende badilisha sheria na kujipunguzia madaraka kwanza kama kweli ana nia na maendeleo.

Na si kuja kuwacha watu waendelee na ignorance sijui za kuja na project nini wala nini ambazo ni malumbano yasiokuwa na muelekeo ni yeye kipenzi chako ndio anaweza kuleta mabadiliko. Kwa kuanza na kuimarisha sheria zifanye kazi yake na kuangalia uchumi ulivyo vinginevyo mta corrupt jamii nzima iseme miafrica ndivyo ilivyo.

na watu wengine waje hapa kutuhamasisha na project zao zisizo kua na vichwa wala miguu sijui project Y sijui nini pumba tupu. wengine atuko intrest na politics but social mobility na kuweza kuleta changamoto nyumbani na sheria za Tanzania zina kwamisha na ufisadi wa chini pia unakwamisha sort that mess.

na wenye personal vendetta na serikali sijui baadhi ya watu serikalini waendelee but sort the mess and open the economy channels sisi wengine ndio tunachokitaka.
 
Last edited by a moderator:
Zawadi,

Kwa nini Deni la Taifa limeongezeka marudufu?

Ikiwa Deni hili ni 33% ya GDP kwa mwaka wa pesa 2008, si kweli kuwa true GDP basi si $1300 bali ni $910?

Je kwa nini Matumizi ya Serikali kuu yameongezeka na ile Surplus aliyotuachia MKapa imepotea kabisa?

Je kukua huku kwa uchumi kuna factor rushwa katika Baeti ya nchi ambapo kwa kauli yake mwenyeke Kikwete ni kuwa mwaka jana wa fedha, rushwa, ubadhirifu, hujuma na matumizi mabaya ya fedha kwenye bajeti ilikuwa ni 30% ya Bajeti ya 2008 ikiwa ni ongezeko la 10% kutoka kiwando cha rushwa cha 20% kwenye bajeti ya 2007?

Je ikiwa kila sarafu ya Dunia ilipata nguvu dhidi ya Dola ya Marekani kutokana na Uchumi wa Marekani kuporomoka, ni kwa nini sisi bado tunachechemea na hatukuona ahueni?
 
kwa ukweli mtu anayehitaji hongera ni mkapa. Mkapa kafanya kazi kubwa sana kwenye uchumi lakini anamapungufu yake ya kuwaachia mafisadi na kusaini mikataba mibaya. Mkapa pamoja na kuchukiwa alikuwa na mipango mizuri zaidi kwa wawekezaji hata kwenye sera ya afya kuliko kikwete. Kikwete amekuwa raisi kwa muda mfupi sana na ni wawekezaji wachache wapya wamekuja wakati wa kikwete. Kikwete lakini atasaidiwa na pinda wawekezaji wameshajua pinga ni mtu anayejua mambo na mfuatiliaji kuliko kikwete sana wanamtumia pinda, kenya wamemtumia pinda na alikuwa huko majuzi na sasa hawalalamiki tena, south korea wametumia pinda. Pinda ndiye mtu atakaye msaidia kikwete kwani anaonekani ni mtu serious na muda unavyoenda watu wanamuona pinda atakuwa kama putin wa russia.

ni kweli mkapa anahitaji hongera ya kuuwa na kuiba mali ya umma
 
Ee bana Dar es Salaam sawa kabisa! Imebaki Kikwete kujenga misikiti ya Ijumaa kila mkoa Tanzania. Nadhani akifanya hivi, uchumi utakuwa 100%! Kipato kitapanda 100% kwa kudra ya Allah na tabasamu ngekewa ya Kikwete! Watu tutakuwa tunaishi mbinguni!


Mkapa si alijenga makanisa kila kipembe kule Zanzibar , mpaka kwenye vile visiwa vidogodogo ambako hakuna mkristo hata mmoja kumejengwa makanisa . Aliuwa Watanzania na kuhujumu uchumi na kuuza nchi . uchumi ulikuwa kwa 100000%
 
Ukiziamini takwimu za CIA kupitia website yao(www.aneki.com), basi hutakuwa na ubavu wa kukipinga kichwa cha habari hapo juu. CIA ni shirika lnaloaminika sana duniani, na lipo up to date katika takwimu zao.

Miaka miwili iliyopita nilitembelea mtandao wao na nikapata aibu, pale nilipoiona Tanzania katika bora 10 masikini duniani. Kwa wasomaji wazuri wa mtandao wa wakati ule T/Daima wanaweza kukumbuka jinsi nilivyokuwa naleta takwimu hizi kwa masikitiko. Mara leo hii upepo umegeuka na naweza kuandika kwa majigambo jinsi uchumi ulivyopanda kama ndege, mig 21. Leo hii Tanzania ipo nafasi ya 28, ikipanda toka nafasi ya 8 mwaka 2007. Ifuatayo ni orodha ya nchi 33, ikianzia Zimbawe msikini sana ikiwa na GDP $200, na ya 33 ni Chad ikiwa na GDP $1600
Top 100 countries with the lowest GDP per capita
Samahani; nilijaribu kuziweka hapa hizo nchi lakini hazijatokea. Hivyo tembelea www.aneki.com. Na angalia katika Top 100 countries.........kama hapo juu.


Mwaka 2007 Tanzania ilikuwa na GDP kama Somalia leo hii, $600 (sh 780000) na tulishika nafasi ya 8. Ninafura kusema kuwa leo hii tuna GDP ya $1400 ( sh 1820000). na kuzibwaga nchi kadhaa na kushika nafasi ya 28. Kiwango hicho cha pesa kinafanya tofauti ya sh 1040000 kwa kipindi cha miaka miwili. Kwa hesabu rahisi ukuaji wa GDP kwa kipindi cha miaka miwili ni wastani wa sh 520000 kwa mwaka.

Ikiwa kama Kikwete atachaguliwa tena, katika uchaguzi wa 2010 na kuwa madarakani mpaka 2015, na kwa mwendo kasi huu ina maanisha kuwa GDP ya Tanzania mwaka 2015 itakuwa sh 1820000 +(520000*6)= 4940000 = $3800. Hii inamaanisha kwamba kama ilivyo leo hii, basi Tanzania itakuwa katika nafasi ya 67, sawa na Djibouti yenye kiwango hicho leo hii.

Watanzania tutakuwa wendawazimu kama hatutaridhika na kufurahia maendeleo hayo kiuchumi. Kwa maendeleo hayo, tunaweza vile vile tukasema bye bye misaada, sasa wenyewe tutajiendesha, kama vile warusi walivyofanya mwaka 2004 kwa IMF na World Bank. Na hii ndio ndoto yangu kubwa na nafikiri ndio ndoto ya Serikali na watanzania wote kwa jumla.

Tabasam la Kikwete lina bahati, ngekewa na linazivuta nchi zote duniani kuiona Tanzania kama Tumaini la uwekezaji. Kusema kuwa Kikwete anaweza, sio tu propaganda bali Takwimu zinajionyesha. Pamoja tutashinda, safari ni ndefu na uvumilivu ndio dawa.

Watanzania haifai tuwe kama mbwa koko, amezoea kulala njaa basi akiona vimifupa ana kenua hadi jino la mwisho…tunatakiwa kuona mbali mkuu Zawadi, nchi hii imejaa minofu kila upande…hivi Tanzania ni nchi ya kuwa na GDP ya dola1300 kweli? kwa nini tuwe na GDP ya 1300?? Kwa nini tufurahi na kujivunia kuulinganisha uchumi wetu wa miaka 5 ijayo na Djibout ya sasa? nchi ambayo hao hao CIA wanasema ni nchi yenye ukame na inaimport sehemu kubwa ya chakula na ina mali asili chache, ukosefu wa ajira karibu 60% nk nk…

Kama GDP imepanda maradufu toka 600 hadi 1300 ina maana na maisha ya watanzania walio wengi kule vijijini yangekuwa na ahueni sana tu…lakini mbona mambo hayako hivyo?
sawa Kikwete ana mazuri na mapungufu yake lakini leo hii sidhani kama anaweza kusimama kifua juu mbele ya watanzania na kuwaambia ameukuza uchumi..
 
DAR-ES SALAAM KASEMA
Ahsante JMK, toka umeingia madarakani, takwimu zote zinaonyesha ukuaji, mashule ya sekondari zaidi ya asilimia 100 juu, vyuo vikuu zaidi ya asili mia 100, mazahanati zaidi ya asilimia 100, kazi mpya zaidi ya asilimia mia moja, uchumi ndio kama hiyo report hapo juu inavyojieleza, kesi zinazosikilizwa na kumalizwa mahakamani zaidi ya asilimia 200, na, na, na, Yote hiyo kwa muda mchache wa kuanzia 2005.

Ni Rais gani mwingine wa Tanzania aliyeweka rekodi inayokaribia hii? = HAKUNA!

JE NI SHULE GANI MPYA YENYE HADHI YA ILBORU AU MZUMBE!SHULE SI IDADI BALI KIWANGO. ni bora ujenge shule tatu kama Ilboru ya Arusha kuliko kujenga shule 20 zenye hadhi ya chini na hazina walimu. Kwanini wasikuze shule zilizopo!
Unajua, ndugu Kamundu nikwambie kitu kimoja ambacho bado hujakifahamu. Ikitokea vita, utafunzwa kuendesha gari masaa 5, na kukabidhiwa Scania kupeleka chakula kwenye uwanja wa mapambano. Askari atafundishwa silaha na ujanja wa porini kwa siku 5, na kukabidhiwa bnduki na kwenda mapambanoni. Hivyo ndivyo ilivyo popote duniani.

Sasa kitu usichokifahamu ni kuwa Tanzania tupo katika VITA. Vita ya kumuondoa adui ujinga. Hii ni vita kubwa kuliko ya kumtoa Idd Amin. Maana si vita utayoimaliza kwa mwaka au miaka10, bali ni vita endelevu. Tunawasiliana mimi na wewe kwa sabau tulikwenda shule. Lakini kwa mtindo ule, kati ya wanafunzi darasa la saba 100 eti wanafaulu 2 tu, ni aibu kubwa sana. Katika hilo hakukua na jinsi ila kutangaza vita.

Ikiwa vijana hawajui kusoma na kuandika, hata kama ukaweka matangazo ya kukomesha ukimwi lakini vijana hawajui kusoma unapoteza pesa yako tu. Lakini kwa sasa hivi, angalia hata magazeti wanunuaji ni walala hoi ambao zamani walikuwa hawajui kusoma. Hii itaturahisishia hata katika ukuaji wa Demokrasia nchini. Hivyo tuunge mkono hali iliyopo, angalau moja tumetatua, hili la madarasa. Kuwa hatutaonyeshwa tena kwenye CNN vijana wetu wkisomea kwenye miti. Sasa tuje kwenye hili la walimu. Ninahakika kabisa kuwa linawezekana. Tumuunge mkono Rais wetu Kikwete.
 
Zawadi,

Kwa nini Deni la Taifa limeongezeka marudufu?

Ikiwa Deni hili ni 33% ya GDP kwa mwaka wa pesa 2008, si kweli kuwa true GDP basi si $1300 bali ni $910?

Je kwa nini Matumizi ya Serikali kuu yameongezeka na ile Surplus aliyotuachia MKapa imepotea kabisa?

Je kukua huku kwa uchumi kuna factor rushwa katika Baeti ya nchi ambapo kwa kauli yake mwenyeke Kikwete ni kuwa mwaka jana wa fedha, rushwa, ubadhirifu, hujuma na matumizi mabaya ya fedha kwenye bajeti ilikuwa ni 30% ya Bajeti ya 2008 ikiwa ni ongezeko la 10% kutoka kiwando cha rushwa cha 20% kwenye bajeti ya 2007?

Je ikiwa kila sarafu ya Dunia ilipata nguvu dhidi ya Dola ya Marekani kutokana na Uchumi wa Marekani kuporomoka, ni kwa nini sisi bado tunachechemea na hatukuona ahueni?
Nchi zote hizo toka 1.Zimbabwe..........21.Uganda....24.Mali......28.Tanzania. zimechukua mikopo kama hiyo ya Tanzania, na bado hawakutupiku. Mfano Deni la Tanzania ni Takriban $5bilioni, naa Kenya ni $6bilion. Hivyo hiyo sio ajenda.

Matumizi ya serikali kuu yameongezeka kwa sababu, Serikali kuu imeongezeka kutokana na kuongezeka kwa kazi husika. Kuhusu Surplus, hiyo sina uhakika kama imepotea. Na kama imepotea ni kwa kiasi gani, au yote. Jaribu kuthibitisha maneno yako kwa kutumia vyanzo vinavyoaminika.

Si kweli kuwa kila sarafu ya dunia ilipata nguvu dhidi ya Dola, Mfano rahisa Zimbabwe.
 
no social mobility

poor programmes to reach the poor

no encouragement to grow internal bussinessess

no self help programmes to increase the government income

still looking for doners on his budget

begging investors to rob us (by the way this is where the GDP inakuongopea)

lastly poor kilimo, kilimo strategy looh! ebu nendeni mka waulize wa-russia, romania etc kilimo kiliwapeleka wapi zaidi ya kuishia kuwacha vyakula vinaoza kwenye ma-warehouse. You need all you can get to advance. Na si kuangalia projection or facts ambazo zina base na government income through foreign investment.

$1,300 GDP hiyo ni kusema bongo over 1.5mil (lowest estimate) bongo shillings, monthly ni karibu laki 140,000 uoni hadithi tupu on what transactions tumetengeneza hiyo GDP. It does not reflect the income of 36million people nor the government revenue for that period year so how did you come up with those figure pleeease.

Na education in terms of literacy nyerere katuacha na almost ninety percent the decline ni walio fuatia hana shughuli JK.

Even the society ina msuta with the amount of poverty watu walionayo. Aende badilisha sheria na kujipunguzia madaraka kwanza kama kweli ana nia na maendeleo.

Na si kuja kuwacha watu waendelee na ignorance sijui za kuja na project nini wala nini ambazo ni malumbano yasiokuwa na muelekeo ni yeye kipenzi chako ndio anaweza kuleta mabadiliko. Kwa kuanza na kuimarisha sheria zifanye kazi yake na kuangalia uchumi ulivyo vinginevyo mta corrupt jamii nzima iseme miafrica ndivyo ilivyo.

na watu wengine waje hapa kutuhamasisha na project zao zisizo kua na vichwa wala miguu sijui project Y sijui nini pumba tupu. wengine atuko intrest na politics but social mobility na kuweza kuleta changamoto nyumbani na sheria za Tanzania zina kwamisha na ufisadi wa chini pia unakwamisha sort that mess.

na wenye personal vendetta na serikali sijui baadhi ya watu serikalini waendelee but sort the mess and open the economy channels sisi wengine ndio tunachokitaka.
Umeandika mengi sana, lakini ya muhimu ni matatu.
1. kwa mwenzi ni sh 140000 kwa kili mtanzania, kutokana na mahesabu ya GDP.
2. Jamii inamsuta kwa umasikini
3. Fungua milango ya uchumi

Nikianza na hili la GDP. Kwa lugha nyepesi ni kwamba, GDP ni kiwango cha pesa ilichonacho Nchi gawanya kwa idadi ya wananchi wake. Mfano, kama Zawadi nina sh 1000 na mwenzaqngu Juma contena una 10,000, kama sisi ndio tunafanya nchi basi GDP = (1000+10000)/2 =5500 sh. Huu ndio utaratibu unaotumika. Kama unaona utaratibu huu unamakosa basi lazima uje na ule mpya unaodhani uafaa. Lakini mpaka leo huu ndio utaratibu unaotumika.

Pengine nikusaidie kitu usichokijua kimoja na kikubwa sana. Ni vipi mgawanyo wa pesa hiyo iliyomkononi mwa matajiri itawafikia walala hoi? SWALI HILI NDIO LA KUTATULIWA NA NDIO SUALA LA WANASIASA. Na hapa ndio hutofautiana kati ya komunisti, wasocialist, liberal, mabepari wenye mlengo mkali kama Republican au wale waingereza maconservative. CHA MSINGI NA CHA AWALI NI KUWA PESA YENYEWE IPO NCHINI, MGAWANYO NI NYINYI KATIKA UCHAGUZI NDIO MNAAMUA.

Ufunguzi wa milango ya uchumi, hilo halina mjadala. Si kitu cha kuomb li nni wajibu wakee kufanya hivyo. Ameanza, lakini mwendokasi ni mdogo mo. Mfano, ukinunua kiwanja Mbezi toka kwa Zawadi, unaweza kubadili jina moja kwa moja. Sio kama zamani mpaka ujene kwanza.

Kifupi nawez kuseaa kuwa eneo hili la kutoa sheia za kirasimu katika biashara a maswala mengine ni lazim lishughulikiwe. Na litasaidia sana kwenye kuondoa rushwa na kuongeza uchumi.
 
Back
Top Bottom