Malyamungu
JF-Expert Member
- Jul 5, 2009
- 363
- 12
sawaKwanini unogopa kukubali kuwa GDP ya TANZANIA IMEKUA? N a kama huamini takwimu za CIA, basi tupe kile chanzo unachokiamini. Kwa sababu hatuwezi kuishi bila takwimu kama tupo makini. Ni lazima tujue juzi tulikuwa wapi, jana, leo na ndipo tutaweza kupanga mipango ya kesho. Sasa tuambie mwenzetu unapotaka kujua uchumi wa nchi kama unapanda au kushuka unaangalia wapi?
HIV/AIDS inakula sana uchumi wa Taifa kuliko hilo punguo la watu.
1) Mgonjwa ambaye huugua zaidi ya miaka mitano anakosa nguvu na morali ya kufanya kazi.
2. Ndugu na jamaa huacha kazi kwa ajili ya kumuuguza mgonjwa.
3. Gharama kubwa kwa serikali katika kutoa elimu, matangazo, madawa na wataalam.
Kupungua kwa Annual growth rate kumetokana na azma ya Kikwete kushirikisha wananchi wa kawaida katika uchumi. Kitu ambacho mimi ninamuunga mkono, kwani Mkapa hakukifanya na hata kudharau kabisa kile tuitacho uti wa mgongo wa Uchumi "Kilimo". Kumbuka: Muundo wowote wa uchumi usiowashirikisha wananchi, utafeli.
Hatuwezi kujenga uchumi kama India. India ni moja kati ya nchi ambazo zinatafsiriwa kama Tajiri na masikini kwa wakati mmoja. Kwa sababu uchumi wa nchi umeshikwa na 20% ya wananchi, na wengine wamesahauliwa kabisa. Ninaposema kusahauliwa, ninamaanisha kuwa hawapo kabisa katika program ya taifa hata kwa siku zijazo. Hivyo japo India inaviwanda vikubwa (TATA, Vifaru, computa, matrekta n.k) lakini huwezi kuamini kuwa 60% ya wananchi wake wanaishi kwa kipato cha chini ya $1 kwa siku. China na India zina idadi ya watu karibu sawa, lakini tofauti ya nchi hizo ni mipango kwa wananchi wao. Wakati China ina mpango kwa wanachi wake (Elimu, afya, kilimo, malazi n.k), India haiwekezi hata senti tano kwenye hayo maeneo.
Ukifanya hivyo kama India, annual growth rate itakua. Mahesabu hapo ni madogo, chukulia unafamilia ya watoto 5 sawa na kaka yako. Wote mnafanya biashara ya Duka,, itoayo faida ya milioni 2 kwa mwezi. Watoto wako wakifika darasa la saba ndio mwisho, hakuna sekondari. Aidha waolewe au waoe na kujiendeshea maisha yao wenyewe. Na kaka yako akaamua kuwaendeleza na kulipa takriban 1milioni kwa mwaka kwa kila mtoto. Kimahesabu kaka yako yuko chini kwa 5milion (-5milion), kwa mwaka, nawe utakuwa na +5milion. Kama unadhani nchi iendeshwe hivyo kama mdogo wako +5M)basi Msifu Mkapa, Vinginevyo (-5M) msifu Kikwete.
Ni Zimbabe tu ndio iliyoshuka GDP yake, nyingine zote zimepanda lakini si kama Tanzania.
Kifupi unanikumbusha msemo niliousoma humu humu JF, Mwana JF aliandika " If you think that education is expensive, try ignorance"
[/QUkwani Mkapa hakukifanya na hata kudharau kabisa kile tuitacho uti wa mgongo wa Uchumi "Kilimo". Kumbuka: Muundo wowote wa uchumi usiowashirikisha wananchi, utafeli.
Hicho kisehemu kwamba kama wananchi hawatashirikishwa katka mambo ya uchumi wao na state security basi malengo yataanguka. Hii inafanana na hoja moja walioibuka nayo tribal leaders in Afghanistan na kuwaambia waandishi wa habari ; America will fail war in Afghanistan if will not involve tribes and communities in the removal of Taliban regime. Power and task force needed to be coordinated through particiaption na pia to maintain strong network.