Kikwete: I may be having a smiling face but am firm on issues

Kaka hufuatilii mambo? DOWANS kuvunjiwa mkataba (pamoja na madai ya wananchi wengi kudai uvunjwe) ulivunjwa kwa kuwa kulishaonekana mwanya wa kupata fedha zaidi kuliko ungesubiri kumalizika time. TANESCO walipokata rufaa swala la ufake wa Richmond halikuwasilishwa mahakamani ili DOWANS wapate mwanya wa kushinda na ikawa. Mwanasheria wa TANESCO alikuwa mwajiriwa wa Rostam (Voda) hadi miezi kadhaa iliyopita sawa na Waziri wa Wizara hiyo kabla ya kuingia Bungeni. Ndiyo maana Ngeleja alikuwa wa kwanza kushangilia malipo mapya ya DOWANS na sasa inadaiwa bado TANESCO wanaweza kukata rufaa kupinga kufanya malipo hayo jambo ambalo litawaongezea ulaji watakaposhinda mwishoni. Hujui serikali yetu kwa maana ya wakubwa wanapata zaidi DOWANS ikishinda kesi kuliko ikishindwa?

Very interesting riwaya..

Basi mzembe ni Wilson (CEO) wa Tanesco ambaye anashindwa kutoa ushauri wa kitaalamu wa ku-solve hilo tatizo..

Tuanze kuchunguza uzalendo wake kwa wananchi na Taifa..au unasemaje?
 
katika tanzania hii ni serikali ya kikwete pekee ndio imeonyesha kwa vitendo jinsi inavyopambana na mafisadi wakubwa mf.mramba,yona,liyumba nk
Hapa umeonyesha mrengo wako. Kumbe katika lile suala la Butiku na Kitine unanishambulia bure kwa sababu kwa mtazamo wako unaona Kikwete amefanya maajabu katika kupambana na ufisadi? For your information Kikwete ni janga la taifa. Rudi kule kwenye mada tuendelee na mjadala.
 
Hapa umeonyesha mrengo wako. Kumbe katika lile suala la Butiku na Kitine unanishambulia bure kwa sababu kwa mtazamo wako unaona Kikwete amefanya maajabu katika kupambana na ufisadi? For your information Kikwete ni janga la taifa. Rudi kule kwenye mada tuendelee na mjadala.

Hivi ni JK ndio janga la Taifa au CCM?

Kwa hiyo tukimuweka kesho 2015 (wale wenzenu) mambo poa au siyo?
 
Very interesting riwaya..

Basi mzembe ni Wilson (CEO) wa Tanesco ambaye anashindwa kutoa ushauri wa kitaalamu wa ku-solve hilo tatizo..

Tuanze kuchunguza uzalendo wake kwa wananchi na Taifa..au unasemaje?
Topical! Topical! Topical! Unajua kwa nini wafanyakazi wengi wa taasisi na mashirika ya umma ni walaji kupindukia? Inadaiwa hata pale wadogo wanapojaribu kufanya kazi kwa uadilifu fedha zinaishia kuliwa maksudi na wakubwa zaidi kupitia mikataba ya ajabu ajabu. So everyone tries to kwapua whatever within reach.
 
Topical! Topical! Topical! Unajua kwa nini wafanyakazi wengi wa taasisi na mashirika ya umma ni walaji kupindukia? Inadaiwa hata pale wadogo wanapojaribu kufanya kazi kwa uadilifu fedha zinaishiwa kuliwa maksudi na wakubwa zaidi kupitia mikataba ya ajabu ajabu. So everyone tries to kwapua whatever within reach.

Good na hiyo nalo tatizo la JK mkuu?

Inaonyesha ni tatizo la taifa na watu wake wote...tufanyeje?

JK peke yake hawezi ku-solve ulaji wa kila mwananchi ambaye anajiita MSOMI..

Nchi hii inaliwa na wanaojiita wasomi..sisi watu informal sector..mmmh
 
The Analyst.....
unatakiwa uandike kitabu kuhusu utawala wa JK.......
sijui title utaaiitaje....lol
Tatizo letu hakuna msafi miongoni mwetu! Kama ukiwa msafi kwa kutofanya uchafu basi utakuwa mchafu kwa kumwagiwa uchafu gizani na ghafla taa kuwashwa! Waaah! kila mtu atauona uchafu na utaishia magereza. Niandike kitabu halafu asipokipenda Mh. Dkt. Rais itakuwaje wakati naishi katika himaya yake? ... No Sir....! Nitaendelea kurisk hapa hapa JF.
 
Tatizo letu hakuna msafi miongoni mwetu! Kama ukiwa msafi kwa kutofanya uchafu basi utakuwa mchafu kwa kumwagiwa uchafu gizani na ghafla taa kuwashwa! Waaah! kila mtu atauona uchafu na utaishia magereza. Niandike kitabu halafu asipokipenda Mh. Dkt. Rais itakuwaje wakati naishi katika himaya yake? ... No Sir....! Nitaendelea kurisk hapa hapa JF.

Unaona sasa hii ndio tatizo la wasomi wetu yaani unafikir JK anaogopa wewe ukiandika kitabu? NAY

JK ukichukua data za kweli serikalini na mambo aliyoyafanya kwa wananchi wake..(anza kuandika) utaona tofauti kubwa kati ya unachosema na ukweli wa mambo
 
Good na hiyo nalo tatizo la JK mkuu?

Inaonyesha ni tatizo la taifa na watu wake wote...tufanyeje?

JK peke yake hawezi ku-solve ulaji wa kila mwananchi ambaye anajiita MSOMI..

Nchi hii inaliwa na wanaojiita wasomi..sisi watu informal sector..mmmh
Hata mimi sipendi Mh. Dkt. JK alaumiwe kwa kila kitu lakini tuwe wakweli pia kwamba kwa jamii iliyokomaa kwa rushwa na ufisadi kama Tanzania namna pekee ya kupambana na ufisadi ni kuanzia juu. Imagine Constable wa polisi aliyehonga mishahara yake mitano ili apangiwe usalama barabarani kupata maendeleo fasta ataacha vipi kupokea rushwa endapo atafuatilia kwa makini issues za Richmond, Dowans, EPA (Kagoda), na mengineyo ambayo kwa namna kibao ofisi kubwa zimehusika na kufumbia macho?
Rais akiwa mkali na kuwabana Mawaziri na Makatibu wakuu kwa juhudi zote ni wazi kwamba rushwa itakwenda inapungua kwa kuadabishana kunakowezekana na si hizi za sasa mara ooh..! Hosea mwache huyo, tuna mpango wa kumkataza kupokea rushwa....nk
 
Tatizo letu hakuna msafi miongoni mwetu! Kama ukiwa
msafi kwa kutofanya uchafu basi utakuwa mchafu kwa kumwagiwa uchafu
gizani na ghafla taa kuwashwa! Waaah! kila mtu atauona uchafu na
utaishia magereza. Niandike kitabu halafu asipokipenda Mh. Dkt. Rais
itakuwaje wakati naishi katika himaya yake? ... No Sir....! Nitaendelea
kurisk hapa hapa JF.

kwani umemtukana?
 
Unaona sasa hii ndio tatizo la wasomi wetu yaani unafikir JK anaogopa wewe ukiandika kitabu? NAY

JK ukichukua data za kweli serikalini na mambo aliyoyafanya kwa wananchi wake..(anza kuandika) utaona tofauti kubwa kati ya unachosema na ukweli wa mambo
Inawezekana haogopi kweli lakini vipi asipopenda au jamaa zake wenye nguvu wasipopenda? Umesahau issue ya kubenea mara hii? Who knows aliyefanya mambo hayo si mtu wa karibu na watawala ambao yeye amekuwa too critical about? Bro unadhani Kagoda na Dowans hawajulikani kweli?
 
Hata mimi sipendi Mh. Dkt. JK alaumiwe kwa kila kitu lakini tuwe wakweli pia kwamba kwa jamii iliyokomaa kwa rushwa na ufisadi kama Tanzania namna pekee ya kupambana na ufisadi ni kuanzia juu. Imagine Constable wa polisi aliyehonga mishahara yake mitano ili apangiwe usalama barabarani kupata maendeleo fasta ataacha vipi kupokea rushwa endapo atafuatilia kwa makini issues za Richmond, Dowans, EPA (Kagoda), na mengineyo ambayo kwa namna kibao ofisi kubwa zimehusika na kufumbia macho?
Rais akiwa mkali na kuwabana Mawaziri na Makatibu wakuu kwa juhudi zote ni wazi kwamba rushwa itakwenda inapungua kwa kuadabishana kunakowezekana na si hizi za sasa mara ooh..! Hosea mwache huyo, tuna mpango wa kumkataza kupokea rushwa....nk

Rais mkali kama nani? wewe au yule? na si kati yetu sisi?
Je si katika sisi ambao tunajiita wasomi, tunaongoza kufoji, kuandika proposal za uwizi, na kushauri viongozi wetu kwa mslahi yetu..

Tatizo si JK tatizo ni sisi, wasomi..tunashauri nini? kwa ajili yetu au kwa ajili ya watu na nchi yetu...

Bado hamjajua tatizo ndio maana mnarusha mawe kwa JK, JK anawasaidia sana kujitambua lakini wapi?
 
Inawezekana haogopi kweli lakini vipi asipopenda au jamaa zake wenye nguvu wasipopenda? Umesahau issue ya kubenea mara hii? Who knows aliyefanya mambo hayo si mtu wa karibu na watawala ambao yeye amekuwa too critical about? Bro unadhani Kagoda na Dowans hawajulikani kweli?

Nani aliyewaruhusu doawans? nani aliyeshauri dowans wapewe tender? bila shaka ni wanasheria wasomi wenzako..tunawaita techn..experts au siyo? don't tell walimuogopa Lowassa kwasababu huko ni kukosa uzalendo..
 
Very interesting riwaya..

Basi mzembe ni Wilson (CEO) wa Tanesco ambaye anashindwa kutoa ushauri wa kitaalamu wa ku-solve hilo tatizo..

Tuanze kuchunguza uzalendo wake kwa wananchi na Taifa..au unasemaje?
Hapo Mkuu naunga mkono. Ikibidi tuchunguze uzalendo wa MA CEO wote wa taasisi za umma.
 
Nani aliyewaruhusu doawans? nani aliyeshauri dowans wapewe tender? bila shaka ni wanasheria wasomi wenzako..tunawaita techn..experts au siyo? don't tell walimuogopa Lowassa kwasababu huko ni kukosa uzalendo..
Kuna stori za wanasheria wengi wanaofanyakazi chini ya Makatibu, Mawaziri kushinikizwa kukubaliana na mambo ili kuendelea kuwa kazini. Inapofikia mwanasheria akajua udhaifu wa bosi wake anachoanza kufanya ni kumwelekeza namna ambavyo wanaweza kunufaika pasipo kutiwa hatiani.
 
Vipi kuhusu mgogoro wa kisiasa Zanzibar mfupa uliowashinda wengi

Vipi kuhusu kuwapeleka Mahakamani Mawaziri na Katibu wakuu mfupa uliowashinda wengi..

Vipi kuhusu .....
hali ni ileile huko fiji......... hadi leo hauna solution zaidi ya kumrudisha mamluki (SS hamad nyumbani) na kuuwa kafu ambao raia wao waliuwawa kama mbung'o
 
Nani aliyewaruhusu doawans? nani aliyeshauri dowans wapewe tender? bila shaka ni wanasheria wasomi wenzako..tunawaita techn..experts au siyo? don't tell walimuogopa Lowassa kwasababu huko ni kukosa uzalendo..
rais alisema siwajui, sijui chochote mimi sijui hata kama ni waduwanzi pia siwajui.............. need we say more?? wakati alikunywa nao chai?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom