QUALITY
JF-Expert Member
- Sep 27, 2010
- 853
- 115
Ndugu zangu, jana ilikuwa siku yangu ya nne nikiwangalia JK katika mikutano yake ya hadhara "ya kampeni" lakini ukimsikiliza haongei kama mgombea bali Rais. Kwa mfano jana katika ITV alisema "wanaoiba hati punguzo za pembejeo watashughulikiwa kama wahujumu uchumi"!! Hii si kauli ya mgombea bali ya yule aliyeishapewa madaraka.
Akasema, tutajenga barabara ya rami kupitia mbuga za wanyama, Serengeti. Hizi zote ni orders. Mbaya zaidi, wandishi wa habari humnukuu "Serikali imesema...." Siyo JK amesema akipewa ridhaa tena ata....
Je hii ni kusema kuwa Hakuna haja ya kufanya uchaguzi sababu anayetaka kushinda ameishajitangazia ushindi? Je hapo kutakuwa na uchaguzi huru na haki? wale wenye maoni ya mtizamo wa kidini kama Ami wasichangie hapa.
Karibuni kuchangia.
Akasema, tutajenga barabara ya rami kupitia mbuga za wanyama, Serengeti. Hizi zote ni orders. Mbaya zaidi, wandishi wa habari humnukuu "Serikali imesema...." Siyo JK amesema akipewa ridhaa tena ata....
Je hii ni kusema kuwa Hakuna haja ya kufanya uchaguzi sababu anayetaka kushinda ameishajitangazia ushindi? Je hapo kutakuwa na uchaguzi huru na haki? wale wenye maoni ya mtizamo wa kidini kama Ami wasichangie hapa.
Karibuni kuchangia.