JAYJAY
JF-Expert Member
- Oct 31, 2008
- 7,510
- 7,534
nilitegemea JK kampeni zake za kipindi hiki kuwa za utulivu zaidi ya zile za 2005 kwa sababu tayari ameshakuwa madarakani na ametekeleza yale aliyoahidi. kwamba hana sababu ya kuwa na hofu kwa sababu waTZ ni waelewa na hawawezi kumlipa ubaya(kutomchagua) kwa wema wake aliowatendea(kutimiza ahadi) kwa sababu inafahamika mtenda wema hulipwa kwa wema(sidhani kama hili limabadilika) au waTZ ni wabaya kiasi hicho kwenda kinyume na hoja hiyo.lakini hali haiko hivyo gharama inayotumiwa ni kubwa zaidi( angalia wingi wa mabango, kama yanalipiwa lakini!),helcopter (kuna wakati mpaka tatu, imeripotiwa hii), machapisho ya fulana na vipeperushi vingine.kwa kweli naamini hii gharama itavunja rekodi ya matumizi katika kampeni za CCM.hoja yangu ni, je JK anahofu ya nini wakati yeye tayari ana mtaji wa utendaji wake kufahamika na wananchi? au wananchi hawa ni mbumbumbu kiasi kwamba wanasahau haraka sana mema waliyotendewa yaani wanadanganyika kirahisi zaidi?. mimi nadhani ambao wanastahili kufanya kampeni kwa nguvu zaidi ni wagombea ambao hawajawahi kuendesha nchi kwa sababu wao ndio wanastahili kuwashawishi wananchi zaidi ili wawaamini na sio ndugu JK. napata mashaka na hili.