NdasheneMbandu
JF-Expert Member
- Jan 2, 2012
- 940
- 308
Wadau wanaJF,
Dalili zipo wazi na kama kuna Mtanzania asiyeziona basi ana matatizo yake kwamba sasa ccm inaelekea kuzimu. Kwa mwenendo wa kisiasa ulivyo, sasa ni dhahiri kabisa kwamba miaka michache ijayo ccm itajiunga na kambi ya upinzani. Jana kwenye taarifa ya habari ya saa mbili usiku kupitia kituo cha ITV tulihabarishwa kwamba mbunge wa Geita aliahirisha mkutano na wananchi baada ya zomeazomea kutoka kwa wananchi wachache waliohudhuria mkutano huo. Lilikuwa ni tukio la aibu ambalo siku za nyuma lisingeweza kutokea. Nimeambiwa na mdau mmoja kwamba hali kama hiyo, ilijitokeza pia Shinyanga baada ya mbunge wa Shinyanga Mjini Mhe. Masele kukosa kabisa watu kwenye mkutano alioitisha. Matokeo yake, aliamua kuahirisha mkutano.
Kwa ujumla, ccm haina mvuto. Imechokwa na sasa inaishi kwa kupumulia mdomoni badala ya puani. Najua baadhi ya wadau watatofautiana nami katika hili lakini niseme tu kwamba uhai wa ccm unatoweka taratibu kama barafu inavyoyeyuka baada ya kutolewa kwenye freezer. Vijana wengi nchini ambao ndiyo nguvu ya chama wanaendelea mmoja baada ya mwingine kujiengua na kujiunga na cdm.
Hivi karibuni tumeshuhudia kupitia vyombo vya habari jinsi wanachama wa ccm maeneo ya Geita, Sengerema, Babati, n.k. wanavyorejesha kwa hasira kadi, kofia na TShirt za ccm na kujiunga na cdm. Kwa hali hiyo, kwa nini nipate shida kutabiri mwelekeo wa kisiasa hapa nchini!! Hakika kwa sasa hakuna ubishi kwamba ccm itakufa, itazikwa na itapotelea mbali. Itabaki kuwa historia kuwa hapo zamani kulikuwa na dude libaitwa ccm lilitamba na kutamalaki kwa muda wa nusu karne laini baadaye lilijisahau likapotea mwelekeo na kuangushwa na wapinzani wake. Ni nani asiyejua kwamba Engineer na Archtect wa yote hayo ni Mhe. Dr. Dr. Dr. (Heshima-UDOM) Kikwete? KWA MANTIKI HIYO, KWA NINI NISIMKUMBUKE KIKWETE KUWA MIONGONI MWA VIONGOZI MASHUJAA WA UKOMBOZI WA NCHI HII?
Dalili zipo wazi na kama kuna Mtanzania asiyeziona basi ana matatizo yake kwamba sasa ccm inaelekea kuzimu. Kwa mwenendo wa kisiasa ulivyo, sasa ni dhahiri kabisa kwamba miaka michache ijayo ccm itajiunga na kambi ya upinzani. Jana kwenye taarifa ya habari ya saa mbili usiku kupitia kituo cha ITV tulihabarishwa kwamba mbunge wa Geita aliahirisha mkutano na wananchi baada ya zomeazomea kutoka kwa wananchi wachache waliohudhuria mkutano huo. Lilikuwa ni tukio la aibu ambalo siku za nyuma lisingeweza kutokea. Nimeambiwa na mdau mmoja kwamba hali kama hiyo, ilijitokeza pia Shinyanga baada ya mbunge wa Shinyanga Mjini Mhe. Masele kukosa kabisa watu kwenye mkutano alioitisha. Matokeo yake, aliamua kuahirisha mkutano.
Kwa ujumla, ccm haina mvuto. Imechokwa na sasa inaishi kwa kupumulia mdomoni badala ya puani. Najua baadhi ya wadau watatofautiana nami katika hili lakini niseme tu kwamba uhai wa ccm unatoweka taratibu kama barafu inavyoyeyuka baada ya kutolewa kwenye freezer. Vijana wengi nchini ambao ndiyo nguvu ya chama wanaendelea mmoja baada ya mwingine kujiengua na kujiunga na cdm.
Hivi karibuni tumeshuhudia kupitia vyombo vya habari jinsi wanachama wa ccm maeneo ya Geita, Sengerema, Babati, n.k. wanavyorejesha kwa hasira kadi, kofia na TShirt za ccm na kujiunga na cdm. Kwa hali hiyo, kwa nini nipate shida kutabiri mwelekeo wa kisiasa hapa nchini!! Hakika kwa sasa hakuna ubishi kwamba ccm itakufa, itazikwa na itapotelea mbali. Itabaki kuwa historia kuwa hapo zamani kulikuwa na dude libaitwa ccm lilitamba na kutamalaki kwa muda wa nusu karne laini baadaye lilijisahau likapotea mwelekeo na kuangushwa na wapinzani wake. Ni nani asiyejua kwamba Engineer na Archtect wa yote hayo ni Mhe. Dr. Dr. Dr. (Heshima-UDOM) Kikwete? KWA MANTIKI HIYO, KWA NINI NISIMKUMBUKE KIKWETE KUWA MIONGONI MWA VIONGOZI MASHUJAA WA UKOMBOZI WA NCHI HII?