Kamanda
Senior Member
- Dec 5, 2007
- 150
- 176
Rais Jakaya Kikwete leo amepatwa tena maswaibu yaliyomkuta Mwanza wakati wa kampeni 2005 akiwania kura za Watanzania huko Mwanza, safari hii siyo kwa kukabwa na Msukuma, bali afya kutetereka.
Afya ya Rais Kikwete ilitetereka akiwa jukwaani akihutubia waumini wa Kanisa la AICT na wananchi katika Kiwanja cha Kirumba ambapo iijisikia vibaya na kubebwa na watu wa usalama kutoka jukwani hadi chumba cha watu maarufu katika uwanja huo kwa mapumziko.
Rais Kikwete baada ya kuwa huko kwa mapumziko mafupi alirejea na kuendelea na hotuba yake.
Inawezeana ni uchovu wa safari kama alivyosema na safari hii amesema hatarudia 'mchezo' wa kuunganisha safari ili apate muda wa kupumzika.
Pole Rais Kikwete
Afya ya Rais Kikwete ilitetereka akiwa jukwaani akihutubia waumini wa Kanisa la AICT na wananchi katika Kiwanja cha Kirumba ambapo iijisikia vibaya na kubebwa na watu wa usalama kutoka jukwani hadi chumba cha watu maarufu katika uwanja huo kwa mapumziko.
Rais Kikwete baada ya kuwa huko kwa mapumziko mafupi alirejea na kuendelea na hotuba yake.
Inawezeana ni uchovu wa safari kama alivyosema na safari hii amesema hatarudia 'mchezo' wa kuunganisha safari ili apate muda wa kupumzika.
Pole Rais Kikwete