Elections 2010 Kikwete awateua Meghji na Nahodha ubunge

Hii ina maana hawa wateulewa watakuwa mawaziri katika serikali ya Muungano. Nilishangaa sana Shein alipomuacha Nahodha bila kumpa uwaziri kule Zanzibar kumbe walikuwa wameshafanya mawasiliona na Kikwete kwamba Nahodha atakuwa waziri kwenye serikali ya muungano. Mama Zakia yeye alipigwa chini baada ya EL kujuuzulu. Huyu mama alikuwa waziri wa fedha wakati wa sakata la EPA. Alishindwa kutoa taarifa sahihi kwa wananchi wakati ule kueleza jinsi hii kashfa ilitokea. Pia alichemsha sana kupandisha kodi ya petroli huku alikujua kwamba kufanya hivyo ni kupandisha bei ya kila kitu nchi na gharama ya maisha kwa ujumla. Sasa anarudi kufanya nini wakati aliprove failure?

Huyu Prof Makame mimi binafsi sina CV yake. Ila nadhani atakuwa ni mtu wa Dr Balal (makamu wa Rais). Hapa Jamaa anampa rafiki yake ulaji tu hakuna cha maana zaidi.

Matatizo ya EPA yalitokea mwishoni mwa mwaka 2005, aliyekuwa Waziri wa Fedha si Zakhia, ila ukaguzi wa Benki uliogundua upotevu wa EPA ulifanyika yeye akiwa Waziri wa Fedha na ni yeye aliyeajiri kampuni ya kuchunguza sasa anahusikaje? Matatizo ya kodi si uamuzi wa mtu mmoja hivyo huwezi mlaumu waziri wa fedha labda uilaumu serikali yote
 
Hii kwangu si habari wala cha kushangaza!! Ukweli ni kuwa JK anauwezo wa kufanya lolote na ukashangaa!!
 
Prof Makame Mbarawa, Associate Professor at the Department of Mechanical Engineering, Faculty of Engineering and the Built Environment, recently returned to home soil after spending five months on sabbatical leave at the Combustion and Laser Diagnostic Laboratory of the Seoul National University in Korea. In the course of his visit to Korea, he also spent time working at the Combustion Laboratory of the Donkook University, also in Seoul.

Prof Mbarawa's main focus was to examine the effects of various gaseous additives on soot formation in laminar diffusion flames, using a laser light scattering/extinction technique. During his visit, he also read three papers at various international conferences.


Prof Mbarawa said he would like to use the knowledge he gained during the trip and compare it to the current teaching approaches in the Department, and identify and apply best practices. He added that he would also apply the quality of good supervision principles that he observed on postgraduate students.


The Seoul University's Mechanical and Aerospace Department comprises 1 300 students, 600 of whom are involved in postgraduate studies.


He explained that the research group he worked with had consisted of one post- doctorate, six doctorate and five master's students. The group met every week for two hours to discuss problems, find solutions and give feedback on the previous meeting's problems. This "buddy" approach between the students made a lasting impression on him, Prof Mbarawa added.


"I was amazed by the Korean people's dedication, culture and way of work. A typical workday during the week starts between 09:00 and 10:00 and lasts until 22:00. On Saturdays, the workday is up to 14:00.


He admitted that it was tricky to become accustomed to the chopsticks and highly spiced Korean dishes, but once he had adapted, he even enjoyed kimchi, a traditional Korean dish of fermented vegetables (mainly cabbage) seasoned with chili peppers and salt.

Sasa huyu kumtoa kwenye taaluma ya ufundishaji na kumleta kwenye SIASA ni matumizi mazuri kweli ya Rasilimali watu?
 
Matatizo ya EPA yalitokea mwishoni mwa mwaka 2005, aliyekuwa Waziri wa Fedha si Zakhia, ila ukaguzi wa Benki uliogundua upotevu wa EPA ulifanyika yeye akiwa Waziri wa Fedha na ni yeye aliyeajiri kampuni ya kuchunguza sasa anahusikaje? Matatizo ya kodi si uamuzi wa mtu mmoja hivyo huwezi mlaumu waziri wa fedha labda uilaumu serikali yote
Kama unapinga hayo yote, unaweza kutueleza kwa nini Kikwete aliona hafai baada ya EL kujiuzulu alipotaja baraza jipya la mawaziri alimuacha. Leo hii anaona Meghji anafaa!!!
Acha hizo, haya ni mambo yaleyale ya kuturudisha nyuma. Hatutakuwa na mawazo mapya ya kwenda mbele namna hii.
 
..I hope hatateua Wabunge, kama alivyofanya kwa Jussa,na Janet Mbene, kikiwa kimebakia kikao kimoja kabla Bunge halijavunjwa.
 
Nasikia JK anamtayarisha Zakia kuwa Waziri wa Utalii na Maliasili -- aliyokuwa nayo hapo zamani ambapo alifungulia milango kwa mafisadi kubaka mali asili za msituni.

Lakini JK na Zakia wajue -- hatujasahau kamwe ile Kashfa ya Kagoda ambayo Mama huyo 'alijikwaa' kidogo kwa kutoa tamko la kutaka kuficha ukweli -- baadaye akaja na barua ya kughushi ya kusema 'afanaleik!! kumbe nilipotoshwa na Katibu Mkuu wangu -- Mgonja' -- ambaye sasa ana kesi -- ingawa haihusiani na Kagoda.!!

Akimpa tu uwaziri -- tunaye mama huyu, hatumuachilii hadi ayabwage manyanga.
 
Kama unapinga hayo yote, unaweza kutueleza kwa nini Kikwete aliona hafai baada ya EL kujiuzulu alipotaja baraza jipya la mawaziri alimuacha. Leo hii anaona Meghji anafaa!!!
Acha hizo, haya ni mambo yaleyale ya kuturudisha nyuma. Hatutakuwa na mawazo mapya ya kwenda mbele namna hii.

Mbona walioachwa ni wengi tuu - Antonny Diallo, Mramba, Mungai...wote hao walikomba EPA au kupandisha bei ya mafuta?
 
Mbona walioachwa ni wengi tuu - Antonny Diallo, Mramba, Mungai...wote hao walikomba EPA au kupandisha bei ya mafuta?

Unaboa wewe mtoto! Kwanini Zakhia asiende kupambana kwenye majimbo kila wakati anasubiria mbereko ya kuteuliwa? Amekuwa serikalini miaka mingi mno akiteuliwa katika nyadhifa mbali mbali. This is stiffly stinking. Nadhani unaelewa
 
Unaboa wewe mtoto! Kwanini Zakhia asiende kupambana kwenye majimbo kila wakati anasubiria mbereko ya kuteuliwa? this is stiffly stinking. Nadhani unaelewa

Tunalingana tuu kiumri na sura yako usiniite mtoto. Zakhia alijaribu Moshi hakuvuka kura za maoni kwenye Chama Chake na hata aliyemshinda Shemeji yake na Mkapa hakuweza kupeta kwa sababu kule Moshi maswala ya Beijing bado hayajafika na wala hayahitajiki ili kudumisha nidhamu katika jamii
 
Huu ni mwanzo wa kuwafahamu mawaziri wake wateule, ishu hapa ni kujua watapelekwa wizara gani, Mama mkwe wizara ya mali asili na Utalii.

mama mkwe kivipi? tujuze mkuu inawezekana wengine tupo nyuma ya wakati
 
Rais has that prerogative power under the current constitution nan haina ubaya kabisa.

I have a feeling that Nahodha may come to constest for the presidency under CCM ticket come 2015.

Congrats to the wateule.
 
Yaani pamoja na kashfa zote zilizomkabili huyo Zakia bado anampa nafasi katika serikali yake! Jamani jamani! Mimi siangalii hayo mengine, maana sio lazima amefikiri kwa misingi ya udini, lakini naona anaendekeza taabu alizokuwa tayari anaziweka kando. Zakia kule Mali Asili Zakia kule Wizara ya Fedha - madudu yale!!!!!!

Kungekuwa na thermometer ya kupima kichefuchefu nimsikiapo huyu mama lazima watu wangenilazimisha nilazwe hospitali. Hivi Wa Tz milioni 40 hakuna mama wa kufanya kazi anazotaka Jk mpaka huyu ??? ahhhhkrrrr
 
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116539
E-mail: press@ikulu.go.tz
Website: www.mawasilianoikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425



PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, amefanya uteuzi wa Wabunge watatu (3) kwa mujibu wa Ibara ya 66 (1) (e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977, kama ilivyorekebishwa na kupewa mamlaka ya kuteua Wabunge 10.

Wabunge walioteuliwa ni Ndugu Shamsi Vuai Nahodha, Prof. Makame Mnyaa Mbarawa na Ndugu Zakia Hamdan Meghji.

Rais atateua wengine waliosalia siku zijazo.

Rais Kikwete ameshawasilisha majina ya wateule hao kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Anne Semamba Makinda (Mb) kwa ajili ya hatua zipasazo.

MWISHO
Imetolewa na Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi,
Ikulu.
Dodoma
17 Novemba, 2010

Nangojea baraza la mawaziri litangazwe. Yawezekana kukawa na staili ile ya THREE MINISTRIES WITHOUT PORTFOLIO KAMA ZENJ.
 
JK na Uozo wake wa siku zote!!
Hoyo mama since 1980s yupo serikalini, amekuwa Waziri miaka mingi...sijui Afya, Maliasili, Fedha n.k, hana jipya na wala hakuwa na utendaji mzuri kama watu wanavyodhani! Ni kwamba jamaa ameishiwa, anaogopa kuteua mawaziri wapya kutoka miongoni mwa wabunge wake....anataka kurejesha walewale waliowahi kushika nyadhifa kadhaa..kwa ku-shake kidogo tu majina na Wizara husika....!! Mwaka huu, na miaka mitano inyokuja TUTAONA MADUDU AMBAYO HAYAJAWAHI KUTOKEA TANGU NCHI IPATE UHURU
 
Jamani sitaki niongelee kuwa walioteuliwa hawa watatu hawafai au laa,ila kitu kimoja wana jf tusaidiane ni how Shamsi Nahodha atatumikia bunge la muungangano na zanzibar, wakati mwingine session zinakuwa kipindi kimoja now kutumikia mabwana hawa wawili itakuwaje? Nawakilisha
 
Back
Top Bottom