Ndachuwa
JF-Expert Member
- Mar 8, 2006
- 6,269
- 4,569
Hii ina maana hawa wateulewa watakuwa mawaziri katika serikali ya Muungano. Nilishangaa sana Shein alipomuacha Nahodha bila kumpa uwaziri kule Zanzibar kumbe walikuwa wameshafanya mawasiliona na Kikwete kwamba Nahodha atakuwa waziri kwenye serikali ya muungano. Mama Zakia yeye alipigwa chini baada ya EL kujuuzulu. Huyu mama alikuwa waziri wa fedha wakati wa sakata la EPA. Alishindwa kutoa taarifa sahihi kwa wananchi wakati ule kueleza jinsi hii kashfa ilitokea. Pia alichemsha sana kupandisha kodi ya petroli huku alikujua kwamba kufanya hivyo ni kupandisha bei ya kila kitu nchi na gharama ya maisha kwa ujumla. Sasa anarudi kufanya nini wakati aliprove failure?
Huyu Prof Makame mimi binafsi sina CV yake. Ila nadhani atakuwa ni mtu wa Dr Balal (makamu wa Rais). Hapa Jamaa anampa rafiki yake ulaji tu hakuna cha maana zaidi.
Matatizo ya EPA yalitokea mwishoni mwa mwaka 2005, aliyekuwa Waziri wa Fedha si Zakhia, ila ukaguzi wa Benki uliogundua upotevu wa EPA ulifanyika yeye akiwa Waziri wa Fedha na ni yeye aliyeajiri kampuni ya kuchunguza sasa anahusikaje? Matatizo ya kodi si uamuzi wa mtu mmoja hivyo huwezi mlaumu waziri wa fedha labda uilaumu serikali yote