Kikwete awasha moto...

Jamani wanabodi,
Bila kuona haya napenda kusema kwamba Jakaya hana la maana alilosema na pia hakuna ukweli aliosema. Ametia aibu na kuchekesha. Wakati naangalia TV nilikuwa nacheka kwani hana tofauti na ze comedy original.

Ni jambo la aibu mno kwa Raisi wa nchi kukubali na kujisifia kwamba Tanzania ni omba omba. Bila haya anatueleza jinsi alivyopanga mikakati ya kuzunguka duniani na kuomba omba misaada. Nilitegemea atueleze ni jinsi gani amekuja na mikakati ya kuzalisha ili kuondokana na kuwa omba omba.

Hivi kweli Raisi wa nchi na wapambe wake anapanda ndege mpaka USA kwenda kuomba msaada wa vyandarua milioni 14?. Vitu kama hivi ni kujitia aibu kwani viko ndani ya uwezo wetu. Siwezi kukubali na wala sintakubali kwamba safari za Jakaya zinafaida zaidi kwa Taifa kuliko hasara.

Watanzania wenzangu ukweli tumeula wachuya. JK ni mtupu na wala si utani. Ni uswahili na ujanja ujanja tu wa lugha.

Waalimu wa shule za msingi hawajalipwa mpaka leo, Raisi bila haya anatuambia waalimu wamelipwa. Tumuelewe vipi?.

Kufanya kosa si kosa, bali kurudia kosa ni kosa. 2010 tusifanye makosa ya kuchagua sura. Ni bora kumpata mtu mwenye sura kama Remmy Ongala akawa Raisi, la maana ni kichwa kilichokamilika.
 
Kwanza inaonyesha huna data za elimu ilivyopanda za kutosha, wanafunzi wa vyuo vikuu wapenda kwa asili mia mia moja au zaidi kulinganisha na waliokuwepo mwaka 2005. Shule za Sekondari, wanafunzi walioanza form 1 ni zaidi ya wote waliokuwepo mwaka 2005 yaani zaidi ya waliokuwa form 1 mpaka 6, Shule za Sekondari kwa kipindi hicho hicho zimezidi kwa zaidi ya shule elfu 3 ambazo ni zaidi ya shule zote zilizokuwepo kuanzia tulipokabidhiwa nchi hii na Umoja wa Mataifa (tusijidanganye kuwa ulikuwa ukoloni), ukichanganya awamu zote zilizopita hawajajenga hata robo ya shule alizojenga JMK katika muda mfupi aliopo madarakani.

Jee, ni nani alieacha Taifa la wajinga?

Huo ufisadi unaousema, ni awamu gani unaongeleka na unachukuliwa hatua? hakuna jibu ila ni awamu hii ya JMK. Huo ufisadi ulianzia wapi? jibu unalo!

Sema usemayo, ukweli utabaki ukweli na takwimu ndio zenye kuthibitisha ukweli.

Unajua nini maana ya elimu?. Tanzania hakuna elimu na wala haijawahi kuwepo. Hivyo vyuo vikuu unavyovitaja ni vipi?. Kwa kifupi Tanzania hakuna vyuo vikuu. Vyuo vikuu vinatakiwa kutambulika kwa utafiti unaofanyika na chuo husika, na ndiyo njia kubwa ya vyuo kujipatia mapato. Nieleze ni utafiti gani umefanyika katika vyuo vikuu vya Tanzania. Tanzania hakuna vyuo vikuu bali kuna madarasa ya kufundisha watoto wetu mambo yaliyovumbuliwa ama yaliyofanyiwa utafiti na watu wengine wa nchi za nje. Na kukuhakikishia hilo ndiyo maana mpaka maprofesa wanaacha kazi na kuingia kwenye siasa.
 
Unajua nini maana ya elimu?. Tanzania hakuna elimu na wala haijawahi kuwepo. Hivyo vyuo vikuu unavyovitaja ni vipi?. Kwa kifupi Tanzania hakuna vyuo vikuu. Vyuo vikuu vinatakiwa kutambulika kwa utafiti unaofanyika na chuo husika, na ndiyo njia kubwa ya vyuo kujipatia mapato. Nieleze ni utafiti gani umefanyika katika vyuo vikuu vya Tanzania. Tanzania hakuna vyuo vikuu bali kuna madarasa ya kufundisha watoto wetu mambo yaliyovumbuliwa ama yaliyofanyiwa utafiti na watu wengine wa nchi za nje. Na kukuhakikishia hilo ndiyo maana mpaka maprofesa wanaacha kazi na kuingia kwenye siasa.
Vyuo vipo ila watu wa siku hizi hawana haja ya kusoma vitabu zaidi ya copy and paste tu ni hatari sana kwa taifa hili
 
Kwa watanzania waliokaa kungalia kipindi kile tulipoteza muda kweli! Amini usimini rais wetu anashangaza. Ninamshauri kuwa wakati mwingine akitaka kujibu maswali asituletee aibu. If he couldn't transcend beyond the people asking qestions, why did he subject himself to so strong questions while he was weak? Tuna kazi ndg zangu. Alisema alipochaguliwa kuwa " I may be wearing a smilie, but....very strong? or weak?
 
Sasa wakati ule wagombea wa urais walikuwa wanaomba sana midahalo na mgombea wa CCM maana alikuwa anakimbia sasa
 
Ukisoma magazeti jinsi yalivyoripoti haya mahojiano utagundua kwa nini Tanzania itaendelea kuwa masikini. Nilisikiliza hii kitu live, thankx to Radio Maria, and I was more than disgusted with majibu ya Kikwete.
 
Ukisoma magazeti jinsi yalivyoripoti haya mahojiano utagundua kwa nini Tanzania itaendelea kuwa masikini. Nilisikiliza hii kitu live, thankx to Radio Maria, and I was more than disgusted with majibu ya Kikwete.
Ni kweli kabisa ila Sisi Watanzania tuna ugonjwa wa kusahau mambo muhimu sana katika Jamii yetu na ndio maana tumeweza kufika hapa tulipo
 
Back
Top Bottom