FDR.Jr
JF-Expert Member
- Jun 17, 2008
- 1,358
- 349
Umetenda jambo jema kama mkuu wa nchi kwa kutungozea majaji; nathubutu kusema hadharani kuwa ni uteuzi makini kwa waliostahiki.
Nimefurahishwa na ujasiri wako wa kutambua kada hii ya mahakama kama moja wa nguzo ya kuifanya legacy yako kujipambanua mapema mkuu.
** umewapa changamoto judiciary kuwa wajitahidi kutenda kazi na jicho lako litawaona pasipo kinyongo**
this time 90% ni wa judiciary wenyewe.
Songa mbele mkuu.
Hongereni majaji wapya, kwa niaba yenu wote ninapitisha pongezi via mh.jaji mteule ferdinand wambari, mh.jaji mteule kalombora na jaji mteule prof....
Habari yenyewe hii toka kwenye gazeti la Mwananchi:
Na Leon Bahati
RAIS Jakaya Kikwete ameteua majaji wengine wapya 10 wa Mahakama Kuu ya Tanzania katika jitihada zinazoonekana kuwa ni za kutatua upungufu wa watendaji wa idara ya mahakama ambao umesababisha kesi nyingi kuchukua muda mrefu kutolewa uamuzi.
Huu ni uteuzi wa tatu mkubwa tangu Rais Kikwete aingie madarakani mwaka 2005 baada ya kuteua kundi la kwanza la majaji 20 mwezi Desemba, 2006 na baadaye kuteua majaji 11 Mei mwaka 2008, huku akiongeza idadi ya wanawake hasa katika uteuzi wa mwaka jana alipoteua majaji saba wanawake.
Katika ya majaji walioteuliwa, sita ni wanawake na hivyo kufanya majaji wanawake walioteuliwa tangu Rais Kikwete aingie madarakani kuwa zaidi ya 10 kati ya majaji wapatao 41 walioteuliwa na kiongozi huyo wa serikali ya awamu ya nne.
Uteuzi huo umefanyika wakati tayari Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe akiwa ametangaza kuwa katika mwaka wa fedha 2009/10 serikali itaiimarisha idara ya mahakama kwa kuiwezesha kutumia vifaa vya kurekodi sauti ili kuharakisha usikilizaji wa kesi Mahakama Kuu.
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, ilimnukuu Katibu Mkuu Kiongozi Philemon Luhanjo akisema kuwa uteuzi huo ulianza tangu mwezi uliopita.
Taarifa hiyo inawataja walioteuliwa kuwa ni Ferdinand Wambali, aliyekuwa Msajili wa Mahakama ya Rufani, Eliamnani Mbise, aliyekuwa Msajili Mahakama Kuu na Sekela Moshi, ambaye awali alikuwa mkurugenzi wa mahakama za wilaya hadi rufani.
Wengine ni aliyekuwa mkurugenzi wa mahakama za mwanzo, Fatuma Hamisi Masengi, naibu msajili mwandamizi Mahakama ya Rufani, Sivangilwa Mwangesi, Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani, Pellagia Khaday na msajili wilaya wa Mahakama Kuu Iringa, Moses Mzuna.
Katika orodha hiyo ya majaji wapya, wapo pia msajili wa wilaya wa Mahakama Kuu Mbeya, Hamisa Kalombola, msajili wilaya wa Mahakama Kuu-Mwanza Fredrica Mgaya na mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria, Profesa Ibrahim Juma.
Katika maadhimisho ya Siku ya Sheria Februari mwaka jana, Jaji Mkuu Augustino Ramadhan alitoa ombi kwa Rais Kikwete kushughulikia idadi ndogo ya majaji akisema kuwa ucheleweshwaji wa kesi utaendelea iwapo mahakama haitakuwa na watendaji wa kutosha.
Kesi nyingi, hasa za mauaji, zimekuwa zikilalamikiwa kuwa zinachukua muda mrefu kabla ya kutolewa maamuzi na kusababisha baadhi ya watuhumiwa kukaa mahabusu kwa zaidi ya miaka mitano.
Katika bajeti ya mwaka 2009/10 ya Wizara ya Sheria na Katiba, Waziri Mathias Chikawe aliahidi kuongeza idadi ya watendaji kwenye idara hiyo kwa lengo la kuharakisha utoaji wa haki.
Nimefurahishwa na ujasiri wako wa kutambua kada hii ya mahakama kama moja wa nguzo ya kuifanya legacy yako kujipambanua mapema mkuu.
** umewapa changamoto judiciary kuwa wajitahidi kutenda kazi na jicho lako litawaona pasipo kinyongo**
this time 90% ni wa judiciary wenyewe.
Songa mbele mkuu.
Hongereni majaji wapya, kwa niaba yenu wote ninapitisha pongezi via mh.jaji mteule ferdinand wambari, mh.jaji mteule kalombora na jaji mteule prof....
Habari yenyewe hii toka kwenye gazeti la Mwananchi:
Rais Kikwete ateua majaji wengine 10 Mahakama Kuu
Na Leon Bahati
RAIS Jakaya Kikwete ameteua majaji wengine wapya 10 wa Mahakama Kuu ya Tanzania katika jitihada zinazoonekana kuwa ni za kutatua upungufu wa watendaji wa idara ya mahakama ambao umesababisha kesi nyingi kuchukua muda mrefu kutolewa uamuzi.
Huu ni uteuzi wa tatu mkubwa tangu Rais Kikwete aingie madarakani mwaka 2005 baada ya kuteua kundi la kwanza la majaji 20 mwezi Desemba, 2006 na baadaye kuteua majaji 11 Mei mwaka 2008, huku akiongeza idadi ya wanawake hasa katika uteuzi wa mwaka jana alipoteua majaji saba wanawake.
Katika ya majaji walioteuliwa, sita ni wanawake na hivyo kufanya majaji wanawake walioteuliwa tangu Rais Kikwete aingie madarakani kuwa zaidi ya 10 kati ya majaji wapatao 41 walioteuliwa na kiongozi huyo wa serikali ya awamu ya nne.
Uteuzi huo umefanyika wakati tayari Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe akiwa ametangaza kuwa katika mwaka wa fedha 2009/10 serikali itaiimarisha idara ya mahakama kwa kuiwezesha kutumia vifaa vya kurekodi sauti ili kuharakisha usikilizaji wa kesi Mahakama Kuu.
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, ilimnukuu Katibu Mkuu Kiongozi Philemon Luhanjo akisema kuwa uteuzi huo ulianza tangu mwezi uliopita.
Taarifa hiyo inawataja walioteuliwa kuwa ni Ferdinand Wambali, aliyekuwa Msajili wa Mahakama ya Rufani, Eliamnani Mbise, aliyekuwa Msajili Mahakama Kuu na Sekela Moshi, ambaye awali alikuwa mkurugenzi wa mahakama za wilaya hadi rufani.
Wengine ni aliyekuwa mkurugenzi wa mahakama za mwanzo, Fatuma Hamisi Masengi, naibu msajili mwandamizi Mahakama ya Rufani, Sivangilwa Mwangesi, Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani, Pellagia Khaday na msajili wilaya wa Mahakama Kuu Iringa, Moses Mzuna.
Katika orodha hiyo ya majaji wapya, wapo pia msajili wa wilaya wa Mahakama Kuu Mbeya, Hamisa Kalombola, msajili wilaya wa Mahakama Kuu-Mwanza Fredrica Mgaya na mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria, Profesa Ibrahim Juma.
Katika maadhimisho ya Siku ya Sheria Februari mwaka jana, Jaji Mkuu Augustino Ramadhan alitoa ombi kwa Rais Kikwete kushughulikia idadi ndogo ya majaji akisema kuwa ucheleweshwaji wa kesi utaendelea iwapo mahakama haitakuwa na watendaji wa kutosha.
Kesi nyingi, hasa za mauaji, zimekuwa zikilalamikiwa kuwa zinachukua muda mrefu kabla ya kutolewa maamuzi na kusababisha baadhi ya watuhumiwa kukaa mahabusu kwa zaidi ya miaka mitano.
Katika bajeti ya mwaka 2009/10 ya Wizara ya Sheria na Katiba, Waziri Mathias Chikawe aliahidi kuongeza idadi ya watendaji kwenye idara hiyo kwa lengo la kuharakisha utoaji wa haki.
Last edited by a moderator: