Kikwete asoma mwelekeo wa upepo, aruhusu mjadala wa Muungano kiaina.

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,883
6,884
jk2_448_280.jpg

Rais Kikwete katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi, katika kuongelea tukio la machafuko huko Zanzibar, licha ya kusikitikia uchomwaji makanisa na kwamba wanauamsho wanafanya kinyume cha malengo ya kusajiliwa, amesema pia uwanja uko wazi kujadili Muungano kwa kupeleka mapendekezo kwa Tume ya Katiba.

kikwete.jpg


Ikumbukwe wakati anatangaza kuanza mchakacho wa Katiba na pale alipotangaza Tume ya Katiba alitamka wazi kwamba Muungano usiongelewe. Rasimu ya awali ya sheria ya kupitiaji upya Katiba iliyopelekwa bungeni ilitoa tishio la adhabu kali kwa atakayekiuka maagizo na sheria ya marekebisho ya Katiba.
 
"The hand writing on the wall" (or "the handwriting on the wall" or "the writing is on the wall" or "Mene Mene"), an idiom, is a portent of doom or misfortune. It originates from the Biblical book of Daniel chapter 5 in which the fingers of a supernatural hand write a mysterious message in the presence ofBelshazzar, king of Babylon, who is meanwhile drinking at a major feast. It is revealed by Daniel that the writing foretells the demise of the Babylonian Empire and the story concludes with the Persians capturing Babylon. The phrase "the writing is on the wall" is now a popular idiom for "something bad is about to happen.
 
wazo zuri muheshmiwa wapeleke mapendekezo yao katika tume ya katiba kila kitu kina taratibu zake,tusizikeuke
 
Politics as usual, hajaruhusu Muungano kujadiliwa ila anataka kuwahadaa wazenji ambao hawataki Muungano. Mkuu hotuba ya Rais ya mwisho wa mwezi sio hadidu rejea za tume. kwenye hadidu rejea za tume moja ya maneno aliyoyasema wazi ni kuwa hii si tume ya masuala ya Muungano kwa hiyo hotuba hii haibadilishi zile hadidu rejea, vingine mtuambie kuwa tume imepokea maelekezo mapya but kama ni kutegemea hii hotuba is just politics as usual
 
Politics as usual, hajaruhusu Muungano kujadiliwa ila anataka kuwahadaa wazenji ambao hawataki Muungano. Mkuu hotuba ya Rais ya mwisho wa mwezi sio hadidu rejea za tume. kwenye hadidu rejea za tume moja ya maneno aliyoyasema wazi ni kuwa hii si tume ya masuala ya Muungano kwa hiyo hotuba hii haibadilishi zile hadidu rejea, vingine mtuambie kuwa tume imepokea maelekezo mapya but kama ni kutegemea hii hotuba is just politics as usual

Kwa vile alisema mabadiliko ya sheria ya kuratibu kanuni itatokea mara kwa mara, ni mapema mno kwangu kukubaliana na wazo lako kwa vile bado ana nafasi ya kuwasilisha bungeni mabadiliko ya sheria kadiri ya kuhitajika.
 
Sawa mkuu tusubiri tuone hayo mabadiliko kama yatapelekwa kwa wakati na kama kweli yatapekekwa, suala la Muungano wamelifanya kuwa kitu kishichoguswa mkuu ingawa wakati umefika lazima muungano uzungumzwe lakini pia kukubali kwamba rais amekubali muungano ujadiliwe kwa sasa tunajua sio
Kwa vile alisema mabadiliko ya sheria ya kuratibu kanuni itatokea mara kwa mara, ni mapema mno kwangu kukubaliana na wazo lako kwa vile bado ana nafasi ya kuwasilisha bungeni mabadiliko ya sheria kadiri ya kuhitajika.
 
Sawa mkuu tusubiri tuone hayo mabadiliko kama yatapelekwa kwa wakati na kama kweli yatapekekwa, suala la Muungano wamelifanya kuwa kitu kishichoguswa mkuu ingawa wakati umefika lazima muungano uzungumzwe lakini pia kukubali kwamba rais amekubali muungano ujadiliwe kwa sasa tunajua sio

Kama umegundua sijasema moja kwa moja kwamba Rais amekubali kujadili Muungano, bali nimesema amekubali kiaina. Hii ni kutokana na kusema suala la kujadili Muungano halikutakiwa kuiingiza Zenj katika matatizo kama ilivyotokea, kama ni suala la muungano wana nafasi ya kuongelea kwenye kamati ya kuratibu mapendekezo ya Katiba. Hii ni kauli ambayo haijawai kuzungumzwa na Kikwete na mara zote amekuwa kinyume cha kugusia Muungano katika mapendekezo ya katiba.
 
Kinachonishangaza kila siku lazima kushinikizwa ndipo ulegeze moyo, naona washauri wake wanamshauri vibaya au hashauriki.

Moyoni wanasema jamani hata sisi tunashangaa tunamshauri vizuri tu lakini akienda home akirudi utasikia anatamka vinginevyo sasa sijui makusudi au home anapata ushauri mwingine au labda anakuwa usingizini bila kujijua wakati anaongea basi hakuna jibu kamili
 
Back
Top Bottom