Elections 2010 Kikwete apendekezwa na CCM kugombea urais 2010

Aspirin wee acha tu.........

Acha nisepe mpaka mgombea mwenza atapotangazwa!
 
Nafikiri mwenyekiti alitakiwa kuwaomba radhi ukumbini wawakilishi wa vyama vya upinzani ili kuset stage kwa makasuku walio chini wanaojua kuwa kushambulia upinzani ndiyo kupata ushindi na kujikomba zaidi kwa viongozi wa juu CCM ili baadae wapatiwe posts.
Mkuu ni mpaka busara ya hivyo iwepo!

Kuna watu wanapumbazwa na makelele ya wanachama (wakishangilia) na wanashindwa kugundua kasoro hizi ambazo kwakweli kama wazalendo inabidi tuzipigie kelele sana.

Aidha, hili si kwa CCM tu; vyama vyote lazima vitambue kuwa havitakiwi kutugawa sisi kama watanzania. Kauli za kipuuzi za namna hii zinapotolewa bungeni na wapinzani wapo wanachekelea ni ishara tosha kuwa nao wamesahau wajibu wao kwetu wananchi.

Namwomba Mungu anipe nguvu za kuvumilia kutoporomosha tusi kwa viongozi wetu hawa... Wananiudhi SANA. Much respect kwa Slaa na Zitto; michango yenu naiona pamoja na Kiongozi wa Upinzani... Msinyamazie trend hii, ipigie kelele iachwe mara moja, itafikia kampeni mtaanza kutukanana hadharani na 'mtachukulia poa' ilhali mnazidi kuwafanya wanetu na wajukuu zetu waamini SIASA ndivyo ilivyo.

Ipo siku...!
 
Mkuu Lady N,

Hapo ndipo nilipokasirika SANA na kusema TUJALI MASLAHI YA NCHI na tuache ushabiki wa kipumbavu ambao uko waziwazi. Huwezi kudai vyama vya upinzani ni mavuvuzela ilhali umewaalika; ni ukosefu wa busara mkubwa kwa viongozi wa CCM na kwa hili wanatakiwa kuwaomba radhi.

Inaudhi sana; kama siasa ni matusi namna hii basi mimi sitarajii kushiriki siasa za namna hii! Nchi inaangamia kwa mfumuko wa bei watu wanakaa kuitana mavuvuzela...

Swali tu ni kwamba hii ni kauli ya Chama au ya mtu binafsi... huwa ndio maana vyama vingi vinakataa kufanya vitu live... maana mnabeba na yale ambayo yasingestahili kubebwa...

I'm sure walioalika hawawezi kusema hivyo... na hata wakisema hivyo ni kwa utani... it can be... lets be realistic
 
Wanafunzi wa vyuo vikuu wanaimba "CCM kiboko yao, na wapinzani wanajua". Wanasisitiza CUF wanajua...! Hahaha na TLP wanajua! Aibu kwa Mrema na Lipumba....

ha ha ha nimeipenda hio nyimbo yao mbele ya kina Lipumba na Mrema.mkuu ulitakiwa kuangalia reaction zao usoni ha ha ha.
 
Sikujua kama dokii ni mwimabaji mzuri hivyo. Ila navyomwona jakaya lazima aombe namba hapo maana mtoto si mchezo
 
Maina Owino bwana...ha ha ha...anaangaika kweli kweli...ila ndo zake toka enzi zake UDSM....alikuwa DARUSO huyo...!Watu kwenye DIASPORA wanataka kurudi kuwa wanasiasa tu...hakuna kitu kipya...

Hawa Albino inakuwaje?Mwenyekiti aliyeongea ni wa-chama cha ma-albino wana-CCM ama?

Kuna tetesi zinasema kwamba huyu "MAINA OWINO" ni MKENYA na amekulia na kusoma TANZANIA, na anajishughulisha na SIASA za USISIEMU na alishawahi kugombea huko RORYA na kutupwa chini na SARUNGI, Wakuu mnaomjua hii imekaaje?
 
Sikujua kama dokii ni mwimabaji mzuri hivyo. Ila navyomwona jakaya lazima aombe namba hapo maana mtoto si mchezo
Mwimbaji mzuri ndio lakini..nashangaa badala ya kumuimbia Mungu, anamuimba Kikwete kwamba no one like him in this world.

She is hopeless, anajaribu kuchumia tumbo. Hamna lolote. Nimemdharau sana na sintampenda kwa ujinga wake huu. Ukimuona mtu anajipendekeza kwa kikwete kwamba hakuna rais duniani mzuri kama kikwete ujue hamnazo. Nimuite libwege.

Well kwa kuwa ni mwana mama nisishangae sana maana huku kwetu kuna kamsemo kuwa mwanamke usifia kila mwanamme aliye naye kitandani kwamba yeye ndiye yeye hajawahi kukutana na mwingine kama yeye. Kumbe ulaghai.
 
Hawa wapinzani walioalikwa hapa kwa kweli wanatia RAHA.

Ningelikuwa mie ningelipanda na kuwatukana na wao vilevile.

Mtatualikaje na kutuita mavuvuzela? Halafu akina Mrema wanachekelea tu, heheheeee....

Ovyo kabisa.

Sijui miaka ya Nyerere, watu walikuwa wanakaa kishabiki na kinafikiri namna hii.

Mijitu ndani inashangilia utafikiri iko kwenye mechi. Kumbe hapa wanaamua maswala ya TAIFA na future yake.

Mungu IBARIKI TANZANIA. Kama kitabu cha KULI (Mwiba upo hapo), yule kule RASHID alisema "YANAMWISHO".
 
Mrema anakwambia wanaosema kuwa yeye ni mwanaccm wakome kabisa na ametangaza nia ya kugombea ubunge huko rorya na hataki kumwona mwanaccm yeyota kugombea......... wamwache naye coz biashara ya kugombea urais inakula kwake kila mwaka!!!!!!
anasema biashara ya jumla ikikushinda unafanya ht rejareja............
 
SIoni ajabu yeyote ile kwa wapinzani kuhudhuria mkutano wa CCM ,Mboni CCM ilihudhuria mkutano wa CCM ,hainishughulishi nani anahudhuria kutokana na cheo chake ,kwani hata akihudhuria mwanachama wa kawaida inatosha kabisa, kuhudhuria kwa Lipumba au mwengine kutoka chama pinzani huo ni kuonyesha ukomavu wa kisiasa,mpiganaji hodari ni yule alie tayari kuhudhuria kwenye uwanja wowote ule wa vita.

Maana kuhudhuria kwenye mkutano wa ccm kunataka ujasiri na huo ndio ulioonyeshwa na akina Lipumba na wenzake,
 
Kishatumbuiza Vick Kamata kisha wakatumbuiza wasanii wa TMK wakiongozwa na Juma Nature, wametinga mavazi ya CCM kwa raha zao.

Sasa anatumbuiza Flora Mbasha, anaimba "Kikwete Kiongozi bora, Ushindi ni LAZIMA".

Violeth Mzindakaya ndiye MC wa shughuli hii.

Wamehudhuria Lipumba, Mrema na viongozi wa Demokrasia Makini

Kuna vitu vidogo sana upinzani hufanya ambavyo huwa haribia sifa na wao hawa jui. Ingekua shughuli ya kitaifa sawa ila uongozi wa upinzani kwenda kwenye sherehe ya CCM wakati wa kuchagua wagomea wao wakuu? Au ni kusema upinzani ume kubali kushindwa na wana fuata falsafa ya "If you can't beat them then join them". Ningekua kiongozi wa upinzani hamna muakilishi yeyote wa chama changu angeenda kwenye shughuli ya chama kingine. Haya sasa kuna imbwa nyimbo za kuwa ponda wao wenyewe. Sometime nasema bora hata hiyo CCM iendelee kushinda tu maana hata hao wapinzani hamnazo.
 
Mwimbaji mzuri ndio lakini..nashangaa badala ya kumuimbia Mungu, anamuimba Kikwete kwamba no one like him in this world.

She is hopeless, anajaribu kuchumia tumbo. Hamna lolote. Nimemdharau sana na sintampenda kwa ujinga wake huu. Ukimuona mtu anajipendekeza kwa kikwete kwamba hakuna rais duniani mzuri kama kikwete ujue hamnazo. Nimuite libwege.

Well kwa kuwa ni mwana mama nisishangae sana maana huku kwetu kuna kamsemo kuwa mwanamke usifia kila mwanamme aliye naye kitandani kwamba yeye ndiye yeye hajawahi kukutana na mwingine kama yeye. Kumbe ulaghai.

Mkuu ukiona msanii anaingia kwenye nyimbo za siasa ujue huyo yupo kwenye "senescence stage" ya career yake ya muziki, kwani baada ya uchaguzi huo ndiyo utakuwa mwisho wa watu kununua kanda zake na atajikuta ama aendelee kwenye siasa ambako atakuwa kama kapi maana hawamuhitaji tena mpaka baada ya miaka mitano, au aachane na music kabisa na kurudi kijijini. Amuulize Bushoke yupo wapi?, Viki Kamata yeye alihiadhiwa pale BOT lakini kiujumla wamejimaliza kimuziki wenyewe.
 
Sasa kwani walilazimishwa kuja hapo?

Kwenye siasa unahitaji ngozi ngumu mkuu! Sasa hawa mafala sijui wameenda hapo kufanya nini? Wewe umeshaona Obama anahudhuria mikutano ya Republican kwa madai kuwa kakaribishwa? Mimi hata nashindwa kuelewa wamekaribishwa kufanya nini! Huu ni mkutano wa CCM na hivyo CCM ina haki ya kufanya itakavyo!

Wapinzani wakiamua wanaweza kutumia hizo kashfa za CCM kuonyesha ujinga wa CCM.
Chapakazi

Umesema vizuri ila hilo neno kwenye red limetumika ndivyo sivyo hata kama ukiliondoa sentesi italeta maana ile ile.
 
Back
Top Bottom