Ama kweli CCM ni chama kinachotegemea"Zidumu fikra za Mwenyekiti". Hivyo CCM wameshapima madhara ya baadae yatakayosababishwa na "ahadi zisizotekelezeka" zinazotolewa na Mwenyekiti wao katika jitihada zake za kuendelea madarakani?
Ahadi anazotowa JK zinataka kutekelezwa na Serikali na uzoefu umetuonyesha kuwa Serikali yetu haina uwezo na viongozi wenye utashi wa kutekeleza yale yatakayowanufaisha walio wengi. Naamini Kikwete angependa atekeleze yale alioyaahidi mwaka 2005 lakini factors mbili za juu zinamgomba. Angekuwa na uwezo wa kutekeleza ahadi zake asingerejea kutowa ahadi kwa mambo yale yale. Kila anapopita anatowa ahadi ya barabara, maji, elimu, afya na mengine ambayo yeye alishindwa kuyatafutia ufumbuzi na CCM ilishindwa kwa kipindi cha karibu miaka 50 iliyopita.
Inapaswa kujiuliza huu mwaka wa 2010 baada ya kupita miaka yote hiyo ndiyo umepatikana muarubaini wa kutatuwa matatizo yote hayo? Na kwanini kipindi chote hicho hawakuwa tayari kututatulia matatizo yanayotukabili isipokuwa sasa? JK amekuwa akitembea na kile kinachoitwa"kipete wa kipete" yaani anatembea na utatuzi wa kila shida hivi sasa.Amekuwa na jibu kwa kila tatizo, amekuwa msikivu na kukubali kila ombi la mgombea wa CCM, amekuwa na fedha lukuki katika Coffers za Serikali. WHY ONLY NOW? Mbona tungekwishapiga hatuwa ya maendeleo na watoto wasingekosa elimu , watu tungekuwa na maji safi, afya bora na miundombinu bora kama hiki kipete wa kipete cha JK kingefanyakazi mapema.
NI kweli kuwa Watanzania ni rahisi kudanganyika lakini tabu za maisha zinawafanya taratibu kujiuliza iwapo wanaowadanganya wanawaona wajinga au vipi? Ninahakika hakuna kitu kitachomzuia JK kurudi madarakani lakini nawatahadharisha CCM kuwa kwanza hawatapata msanii mwengine kama walienae sasa,pili harakati za upinzani mwaka2015 zitapata silaha ya kuimaliza CCM kwa kushindwa kutimiza ahadi zinazoahidiwa sasa kwani nina hakika kwa uongozi wa CCM (ule ule) serikali haiwezi kabisa kupata uwezo wa kutekeleza ahadi lukuki zinazoahidiwa sasa. Wapinzani watawaambia wapiga kura kiwapi mlichoahidiwa? Na tatu wapiga kura watakasirika kuchukuliwa kama watoto na ahadi bila utekelezaji.
Ole wake CCM na tabia ya zidumu fikra za mwenyekiti. Sijui harakati hizi za ahadi zina organization au ni fikra binafsi. Hongera CCM kwa ushindi wa 2010 utakaoleta kuporomoka mwa 2015!
Ahadi anazotowa JK zinataka kutekelezwa na Serikali na uzoefu umetuonyesha kuwa Serikali yetu haina uwezo na viongozi wenye utashi wa kutekeleza yale yatakayowanufaisha walio wengi. Naamini Kikwete angependa atekeleze yale alioyaahidi mwaka 2005 lakini factors mbili za juu zinamgomba. Angekuwa na uwezo wa kutekeleza ahadi zake asingerejea kutowa ahadi kwa mambo yale yale. Kila anapopita anatowa ahadi ya barabara, maji, elimu, afya na mengine ambayo yeye alishindwa kuyatafutia ufumbuzi na CCM ilishindwa kwa kipindi cha karibu miaka 50 iliyopita.
Inapaswa kujiuliza huu mwaka wa 2010 baada ya kupita miaka yote hiyo ndiyo umepatikana muarubaini wa kutatuwa matatizo yote hayo? Na kwanini kipindi chote hicho hawakuwa tayari kututatulia matatizo yanayotukabili isipokuwa sasa? JK amekuwa akitembea na kile kinachoitwa"kipete wa kipete" yaani anatembea na utatuzi wa kila shida hivi sasa.Amekuwa na jibu kwa kila tatizo, amekuwa msikivu na kukubali kila ombi la mgombea wa CCM, amekuwa na fedha lukuki katika Coffers za Serikali. WHY ONLY NOW? Mbona tungekwishapiga hatuwa ya maendeleo na watoto wasingekosa elimu , watu tungekuwa na maji safi, afya bora na miundombinu bora kama hiki kipete wa kipete cha JK kingefanyakazi mapema.
NI kweli kuwa Watanzania ni rahisi kudanganyika lakini tabu za maisha zinawafanya taratibu kujiuliza iwapo wanaowadanganya wanawaona wajinga au vipi? Ninahakika hakuna kitu kitachomzuia JK kurudi madarakani lakini nawatahadharisha CCM kuwa kwanza hawatapata msanii mwengine kama walienae sasa,pili harakati za upinzani mwaka2015 zitapata silaha ya kuimaliza CCM kwa kushindwa kutimiza ahadi zinazoahidiwa sasa kwani nina hakika kwa uongozi wa CCM (ule ule) serikali haiwezi kabisa kupata uwezo wa kutekeleza ahadi lukuki zinazoahidiwa sasa. Wapinzani watawaambia wapiga kura kiwapi mlichoahidiwa? Na tatu wapiga kura watakasirika kuchukuliwa kama watoto na ahadi bila utekelezaji.
Ole wake CCM na tabia ya zidumu fikra za mwenyekiti. Sijui harakati hizi za ahadi zina organization au ni fikra binafsi. Hongera CCM kwa ushindi wa 2010 utakaoleta kuporomoka mwa 2015!