Lukansola
JF-Expert Member
- Sep 5, 2010
- 5,435
- 1,597
Jamani hizo kashfa mnazotoa kwa rais wetu ni ukosefu wa adabu.Yeye ni kiongozi wetu mkuu kwa mujibu wa sheria za nchi hivyo ni lazima tumheshimu hata kama ana mapungufu yake.
Yeye ni binadamu na si malaika.Amewazidi umri karibu member wote wa JF hivyo apewe heshima yake kama mkubwa wetu.Au mnataka kusema kuwa wazazi wenu wakifanya mambo ya ajabu huwa mnawadhalilisha kiasi hiki? Sio fair jamani,tuwe na staha kwa viongozi wetu kwani ndo wanaotoa picha halisi ya nchi yetu kwa nchi nyingine.
1. Hajakashfiwa anapewa ukweli
2. Sidhani kama yuko hapo kwa mujibu wa sheria (chakachua)
3. Mapungufu yake ni mengi kuliko kawaida.
4. Unajuaje kama katuzidi umri karibu member wote wa JF, basi na sisi tumemzidi busara.
5. Kama anatoa picha halisi ya nchi yetu kwa nchi zingine, basi wenzetu wanatushangaa huko.
6. Ukitaka kuheshimiwa jiheshimu.