Kikwete anapoteua mawaziri wake ...

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,011
Kikwete anapoteua mawaziri wake ...

2009-02-08 11:02:06
Na Simon Mhina​

Baadhi ya wasomi na wanasiasa wa kambi ya upinzani, wamemtaka Rais Jakaya Kikwete, kuwa makini anapoteua mawaziri, ili kuepuka kuteua watu wasio na sifa za uongozi.

Wametoa wito huo, kufuatia matukio kadhaa ya hivi karibuni ya baadhi ya mawaziri kutoa kauli zenye utata au kuchukuwa maamuzi yaliyo kinyume na sheria na taratibu na kusababisha mtafaruku katika jamii.

Wakizungumza na Nipashe Jumapili kwa nyakati tofauti, wasomi na wanasiasa hao, wamesema matukio ya viongozi kutoa kauli tata au kuchukua maamuzi yaliyo kinyume na sheria na taratibu ni ishara kuwa wapo viongozi waliopewa nafasi hizo kwa bahati mbaya kwani hawajui nini maana ya dhamana ya kuwa kiongozi.

Akizungumza na Nipashe Jumapili jana, Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Mwesiga Baregu, alisema matukio hayo yanatia shaka juu ya baadhi ya viongozi tulionao kama wanastahili kushika nafasi walizonazo.

``Inatia hofu kwa sababu tunategemea kwamba kiongozi wa kiwango hicho anaelewa dhamana ya vitendo na kauli yake kwa jamii``, alisema.

Akizungumzia tuhuma inayomkabili Waziri wa Mambo ya Ndani, Laurance Masha, ambaye anadaiwa kuingilia mchakato wa kumpata mzabuni wa kutengeneza vitambulisho vya taifa, Profesa Baregu, alisema tukio hilo linaonyesha tabia ya ubinafsi miongoni mwa viongozi kwa kuweka mbele maslahi binafsi kuliko ya umma.

Alisema hali hiyo pia inaonyesha kuanguka kwa maadili ya uongozi kwa kiwango cha juu na kuitaka serikali isimamie ipasavyo maadili ya viongozi wake kwani endapo baadhi ya viongozi wasipodhibitiwa kauli na vitendo vyao vinaweza kusababisha matatizo makubwa ndani ya nchi.


Pia alilitaka Bunge kusimamia ipasavyo utendaji wa serikali na viongozi wake kwa wabunge kuweka mbele maslahi ya umma kuliko ya vyama vyao vya siasa.

``Bunge liisimamie vyema serikali na viongozi wake ili kuhakikisha hawaendi nje ya mipaka na hii ifanywe bila ya wabunge kujali vyama vyao na rais naye aonyeshe njia akemee mawaziri wake wanaotenda kinyume na taratibu, kinachoonekana ni kama Baraza la Mawaziri limemgeuka hawazungumzi kwa sauti moja na kuyatetea maamuzi yao, kila mmoja anazungumza lake kwa maslahi yake``, alisema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Tanzania Labor Party (TLP), Augustine Mrema, amemtaka Rais Jakaya Kikwete, asibabaishwe na mawaziri wake wanaoboronga.
[/B]

Alimshambulia Waziri wa Mambo ya Ndani, Laurance Masha, kwa kujiingiza katika matendo aliyoyaita ya aibu kutokana na kutia mkono katika tenda ya kutafuta kampuni ya kutengeneza vitambulisho vya taifa.

Mrema aliyewahi kuongoza wizara hiyo, alisema amekuwa akishangazwa na matendo ya Waziri Masha.

``Kwanza Masha mwenyewe lazima aelewe kuwa yupo kwenye Baraza la Mawaziri kwa bahati ya mtende, hana sifa za kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani``, alisema na kuongeza mambo kama haya yamfanye Rais afikirie kuvunja baraza``
[/B]

Pia alikemea tabia iliyoibuka ya baadhi ya mawaziri wanaotoa kauli ama maamuzi yaliyo kinyume cha taratibu na sheria kuishia kuomba radhi bila ya kuchukua hatua ya kujiuzulu nafasi zao.

``Ni aibu waziri kuboronga halafu ngao yake inakuwa kuomba radhi Bungeni, Kikwete avunje baraza la mawaziri, ili mwakani aingie kwenye uchaguzi mkuu na baraza jipya, safi lisilo na watu wenye tuhuma za ufisadi,`` alisema na kuongeza, ``Haya mambo ya kuomba radhi kwa makosa ya wazi kabisa yanaashiria kukata tamaa na kushindwa kazi``, alisema Mrema.

Aliongeza kusema kuwa huu si wakati wa mawaziri komba radhi bungeni, bali wanatakiwa kueleza kwamba wamefanya nini muda wote walipokuwa madarakani.

Naye Mbunge wa Chama cha Wananchi (CUF), Ali Khamis Seif (Mkoani), alisema kilichotokea kwenye Wizara ya Maliasili na Utalii kuhusu vitalu vya uwindaji na ile ya Mambo ya Ndani kuhusu utengenezaji wa vitambulisho vya taifa, msingi wake ni ufisadi.

Aliwataka mawaziri wanaoboronga waachie ngazi kwa vile sio tu wanawatia hasara Watanzania, lakini wanamdhalilisha Rais aliyewateua.

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Sengodo Mvungi, yeye alisema hatua ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Waziri wa Maliasili na utalii kuliomba bunge radhi kwa nyakati tofauti kutokana na kutoa maamuzi yenye utata na yenye kukiuka katiba na maamuzi ya bunge, inaashiria kuwa wameingiwa na kiwewe.

Alisema kiwewe hicho kinatokana na ukweli kwamba mawaziri hao ambao ni wasaidizi wakuu wa rais, wamegundua kwamba mambo si shwari katika kutekeleza ilani ya CCM kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu mwakani.

``Wameingiwa na kiwewe na radhi wanazoomba ni geresha, wanajifanya wanyenyekevu kipindi hiki ambapo tunaelekea uchaguzi Mkuu,``alisema.


Dk. Mvungi, alidai kuwa kwa vile mawaziri wengi wameshindwa kutekeleza ahadi za serikali kwa kwa wananchi na hivi sasa wanataka wananchi wawaonee huruma kwa kujifanya wanyenyekevu.

``Huu ni unyenyekevu wa kutaka kuonewa huruma mwakani, huu unyenyekevu wa kuomba radhi umeanza lini? Wanachokifanya wanajenga uadilifu wa bandia wa kutaka waonewe huruma``, alisema.

SOURCE: Nipashe
 
Last edited:
Bubu mkuu, it is about time that the opposition start talking and playing hard ball, siyo danganya toto ya miaka ya nyuma. They have some good points but I feel that they shouldn't waste good advice on a president that is not ready to listen. JK will never change his cabinet, hata hii reshuffle ya juzi alilazimishwa, si kwamba alitaka. This prez has decided to be a one term president that is my current view. I stand to be corrected.
 
``Ni aibu waziri kuboronga halafu ngao yake inakuwa kuomba radhi Bungeni, Kikwete avunje baraza la mawaziri, ili mwakani aingie kwenye uchaguzi mkuu na baraza jipya, safi lisilo na watu wenye tuhuma za ufisadi,`` alisema na kuongeza, ``Haya mambo ya kuomba radhi kwa makosa ya wazi kabisa yanaashiria kukata tamaa na kushindwa kazi``, alisema Mrema.

- Hawa kina Mrema, wafike mahali wakubali tu kuwa hizi siasa zimewapita tayari, I mean Mkapa amebadili cabinet mara ngapi? Kikwete amebadili cabinet mara ngapi? Kilichobadilika ni kipi? Kila kukicha zinaibuka habari za ufisadi na mawaziri, yeye mwenyewe Mremna mpaka leo hajawahi kutueleza zile dhahabu zilienda wapi pale Airport, majuzi alikuwa Mbeya akiwashambulia Chadema, leo amegeuka na kushambulia mawaziri lakini sio rais,

nani atakayelisaidia hili taifa jamani?
 
- Hawa kina Mrema, wafike mahali wakubali tu kuwa hizi siasa zimewapita tayari, I mean Mkapa amebadili cabinet mara ngapi? Kikwete amebadili cabinet mara ngapi? Kilichobadilika ni kipi? Kila kukicha zinaibuka habari za ufisadi na mawaziri, yeye mwenyewe Mremna mpaka leo hajawahi kutueleza zile dhahabu zilienda wapi pale Airport, majuzi alikuwa Mbeya akiwashambulia Chadema, leo amegeuka na kushambulia mawaziri lakini sio rais,

nani atakayelisaidia hili taifa jamani?

Kubadili baraza la maziri peke yake hata mara 100 hakutoshi kama bado kuna mawaziri katika baraza hilo ambao ni mafisadi, hawawezi kazi na wameweka mbele maslahi yao wenyewe badala ya Taifa. KAma tungekuwa na Bunge ambalo limeweka mbele maslahi ya Watanzania basi Bunge hilo lingeshapiga kura siku nyingi kwamba halina imani na Rais na baraza lake la mawaziri hivyo kusababisha uchaguzi mwingine, lakini Bunge hilo ni Bunge la CCM ambalo siku zote limeweka mbele maslahi ya CCM badala ya yale ya Taifa. Watanyamazia lolote lile ambalo halina maslahi kwa Watanzania ali mradi tu wanahakikisha CCM inaendelea kubaki madarakani milele, sijui kubaki madarakani milele kea faida ya nani hasa!!!!?
 
Mimi nilisemaga tokea mwaka 2005 kule bcstimes.com kuwa Kikwete siyo makini na matokeo yake sasa ndio haya tunayoyaona, kuteu watu wasio makini kuongoza wizara muhimu (wizara karibu zote muhimu). Kwanza alianza vibaya kwa kuunda baraza kubwa mno la mawaziri. I mean, what the hell....baraza kubwa hivyo lilikuwa la nini?

Kwa hiyo siku zote mimi huwa nasema mtu asiye makini ni rahisi sana kwake yeye kuteua watu wasio makini pia. Na sasa ndio haya tunayoyaona....
 
Mimi nilisemaga tokea mwaka 2005 kule bcstimes.com kuwa Kikwete siyo makini na matokeo yake sasa ndio haya tunayoyaona, kuteu watu wasio makini kuongoza wizara muhimu (wizara karibu zote muhimu). Kwanza alianza vibaya kwa kuunda baraza kubwa mno la mawaziri. I mean, what the hell....baraza kubwa hivyo lilikuwa la nini?

Kwa hiyo siku zote mimi huwa nasema mtu asiye makini ni rahisi sana kwake yeye kuteua watu wasio makini pia. Na sasa ndio haya tunayoyaona....

Mkapa alikuwa makini? Akina Chenge, Mramba na Yona?
 
2010 ni wakati mzuri sana wa kuwapima watanzania kama wana akili timamu...Tusubiri tuone 2010 kama wabongo wasipoonyesha uelewa na ukomavu basi mafisadi watatawala milele.
 
Mkapa alikuwa makini? Akina Chenge, Mramba na Yona?

Kujaribu kumbomoa MKapa, haimjengi Kikwete, do you understand that? Sasa ni utetezi gani huu kusema hata Mkapa hakuwa makini? This is childish! Is Mkapa the standard, now? Kikwete hayuko makini, unakubali au hukubali?
 
Balaa linalomwandama Kikwete mtengenezaji wake ni Mkapa...ndiye muasisi wa siasa za wenye nacho watashinda na wasionacho wakae pembeni. Wabunge wamechaguliwa kwa takrima ambayo ni rushwa ktk jina tofauti....that does mean most of the politicians either walikopa au waliiba au walifadhiliwa ili kuingia bungeni na wanataka kurudisha hela hizo walizotumia.
Wanapata wapi kama sio kwenye ufisadi na tender za serikali?
Kwa vyovyote Kikwete ataunda baraza la mawaziri kutumia hao wanasiasa waliotoa takrima kuingia bungeni...tatizo bado lipo na binafsi namsifu Kikwete kwa kujua kusoma angalau alama chache za nyakati.
Hivi angekuwa Mkapa tungemweleza nini? Wote alituona wajinga na hatuna akili kasoro Sir Chande na majambazi wenzake masons ambao alikuwa anawaita watajiri tutao waonea wivu wa kike.Hawa ndo wameifaidi hii nchi mana wamegawana yote na Mkapa akiwa kimya.
Nina imani kikubwa ni kuendelea kumpa support na genuine challenges Kikwete. Nionavyo, hajaziba masikio kabisa...kuna anayosikia.Tuendelee kusema bila kuchoka!!
 
Mkapa alikuwa makini? Akina Chenge, Mramba na Yona?

Mkapa kumlinganisha na Kikwete? Ndio, alikuwa makini zaidi. Je, alikuwa na sifa za kuwa kiongozi? Hilo tunaweza kulijadili.

Kwa hiyo, pamoja na mtu (kiongozi) kuwa makini, tabia ya baadaye ya mtu haitabiriki. Sasa kiongozi (note nimesema kiongozi) yoyote yule aliye bora na makini, wateule wake wanapoboronga, hufanya kila awezalo kuwarudisha ndani ya mstari.
 
Mkapa ama JK ofisi ni ile ile na sera ni zile zile...JK yeye bado Zenji tu kuuwa,ufisadi the same nk. Hizi siasa zenu za kuanza kusema eti Mkpa this JK si more ni upuuzi tu....Chama ni kile kile na sera ni zile zile.. Wote ni kitu moja,wabongo wanadhani wanajuwa siasa kumbe bure, wanachezewa sana akili,no wonder rais wenu kasema mtaliwa sana..Tatizo mnaweza msile.
 
Balaa linalomwandama Kikwete mtengenezaji wake ni Mkapa...ndiye muasisi wa siasa za wenye nacho watashinda na wasionacho wakae pembeni. Wabunge wamechaguliwa kwa takrima ambayo ni rushwa ktk jina tofauti....that does mean most of the politicians either walikopa au waliiba au walifadhiliwa ili kuingia bungeni na wanataka kurudisha hela hizo walizotumia.
Wanapata wapi kama sio kwenye ufisadi na tender za serikali?
Kwa vyovyote Kikwete ataunda baraza la mawaziri kutumia hao wanasiasa waliotoa takrima kuingia bungeni...tatizo bado lipo na binafsi namsifu Kikwete kwa kujua kusoma angalau alama chache za nyakati.
Hivi angekuwa Mkapa tungemweleza nini? Wote alituona wajinga na hatuna akili kasoro Sir Chande na majambazi wenzake masons ambao alikuwa anawaita watajiri tutao waonea wivu wa kike.Hawa ndo wameifaidi hii nchi mana wamegawana yote na Mkapa akiwa kimya.
Nina imani kikubwa ni kuendelea kumpa support na genuine challenges Kikwete. Nionavyo, hajaziba masikio kabisa...kuna anayosikia.Tuendelee kusema bila kuchoka!!

Ndahani, I respect your views mkuu, lakini kumbuka Kikwete pia alikuwa mbunge na waziri chini ya Mkapa kwa hiyo naye aliingia kwa takrima na yote yale uliyoyataja hapo juu. Worse, yeye ni follower siyo leader, kwa maelezo yako. Hana busara ya kusema that he will lead and be different. Hivyo kumshikilia bango Mkapa bado si suluhisho, sisi tunam-judge JK kwa ufanisi wake kama yeye kama rais. And kama anaboronga basi anaboronga!
Pia nadhani you are a fan (which is absolutely your right!), lakini hata wewe ume-doubt kama kweli anasikiliza ushauri umesema KUNA ANAYOSIKIA, well that is not good enough. Either anasikiliza au la.
 
Mkapa kumlinganisha na Kikwete? Ndio, alikuwa makini zaidi. Je, alikuwa na sifa za kuwa kiongozi? Hilo tunaweza kulijadili.

Kwa hiyo, pamoja na mtu (kiongozi) kuwa makini, tabia ya baadaye ya mtu haitabiriki. Sasa kiongozi (note nimesema kiongozi) yoyote yule aliye bora na makini, wateule wake wanapoboronga, hufanya kila awezalo kuwarudisha ndani ya mstari.

Thank you Nyani Ngabu, halafu kuna watu walinirushia madongo kwa kukupongeza kwa mchango wako mkubwa hapa ukumbini na kufikisha jumbe 8,000!!! :)
 
Mkapa ama JK ofisi ni ile ile na sera ni zile zile...JK yeye bado Zenji tu kuuwa,ufisadi the same nk. Hizi siasa zenu za kuanza kusema eti Mkpa this JK si more ni upuuzi tu....Chama ni kile kile na sera ni zile zile.. Wote ni kitu moja,wabongo wanadhani wanajuwa siasa kumbe bure, wanachezewa sana akili,no wonder rais wenu kasema mtaliwa sana..Tatizo mnaweza msile.

JMushi that is my view as well, lakini what I disagree with is when we judge the leadership skills of a president, there should be no excuse. Siyo kusema eti na fulani naye hakuwa msafi... sasa huu si utetezi ni utoto.
 
2010 ni wakati mzuri sana wa kuwapima watanzania kama wana akili timamu...Tusubiri tuone 2010 kama wabongo wasipoonyesha uelewa na ukomavu basi mafisadi watatawala milele.

Mkuu, unachokisema ni sahihi lakini tunapaswa kuendelea kuwaelimisha watanzania. Zaidi ni kuwapa hamasa na kujitokeza kupiga kura, uzoefu unaonyesha wanaojua ukweli wa siasa na wachambuzi wazuri wa mambo ya kisiasa kama sisi huwa hatuendi kupiga kula kwa visingizio mbalimbali ikiwemo ubusy. Hii pia kwa kiasi fulani linachangia kushindwa. Pia kuhakikisha kura haziibiki maana hawa jama washasema upinzani hauwezi ingia IKULU kwa njia ya kura, kwa maana hiyo wameamua kutamka wazi wazi kama alivyo tamka MGABE ndio maana hakuna kiongozi wa Afrika anaye thubutu kukemea sera za MGABE kwa kuwa hata wao wanafanya yale yale. Tuhakikishe vjarida kama vya cheche za fikra vinawafikia wananchi na wanasoma ikiwa ni pamoja na kuvisoma kwa niaba yao ikibidi na kuwafafanulia ukweli na kuchambua feki report za mafanikio ya CCM kwa wananchi.
 
Mkuu, unachokisema ni sahihi lakini tunapaswa kuendelea kuwaelimisha watanzania. Zaidi ni kuwapa hamasa na kujitokeza kupiga kura, uzoefu unaonyesha wanaojua ukweli wa siasa na wachambuzi wazuri wa mambo ya kisiasa kama sisi huwa hatuendi kupiga kula kwa visingizio mbalimbali ikiwemo ubusy. Hii pia kwa kiasi fulani linachangia kushindwa. Pia kuhakikisha kura haziibiki maana hawa jama washasema upinzani hauwezi ingia IKULU kwa njia ya kura, kwa maana hiyo wameamua kutamka wazi wazi kama alivyo tamka MGABE ndio maana hakuna kiongozi wa Afrika anaye thubutu kukemea sera za MGABE kwa kuwa hata wao wanafanya yale yale. Tuhakikishe vjarida kama vya cheche za fikra vinawafikia wananchi na wanasoma ikiwa ni pamoja na kuvisoma kwa niaba yao ikibidi na kuwafafanulia ukweli na kuchambua feki report za mafanikio ya CCM kwa wananchi.

Wataondoka tu na kuachia madaraka wakiona hamna njia ya kuiba, ndo maana nasema inabidi tuwabane sana wasipate mwanya wa kuiba. Then utaona uzalendo utawashinda na mshahara wa kawaida!
 
wakuu haiwezekani haya yote mabaya yanayotokea serikali ya awamu ya nne kwa kipindi cha miaka mitatu,bali kinachofanyika na awamu ya nne ni kurekebisha makosa yaliyofanywa awamu zote tatu zilizopita kama mzee ruksa alivyosema jana.

Kilichokuwa kinatakiwa ni good intentions ya kila rais anayekuja kuchukulia yaliyote mabaya yaliyofanywa na seriali iliyomtangulia kama changamoto na kuyarekebisha kwa kufuata taratibu na sheria za nchi ilizojiwekea.

kama ingefanyika hivyo kwa kila awamu basi serikali ya awamu ya nne ingekuwa na vitu vichache kama changamoto kubwa lingekuwa kuleta maendeleo halisi kwa watanzania .

thx
 
wakuu haiwezekani haya yote mabaya yanayotokea serikali ya awamu ya nne kwa kipindi cha miaka mitatu,bali kinachofanyika na awamu ya nne ni kurekebisha makosa yaliyofanywa awamu zote tatu zilizopita kama mzee ruksa alivyosema jana.

Kilichokuwa kinatakiwa ni good intentions ya kila rais anayekuja kuchukulia yaliyote mabaya yaliyofanywa na seriali iliyomtangulia kama changamoto na kuyarekebisha kwa kufuata taratibu na sheria za nchi ilizojiwekea.

kama ingefanyika hivyo kwa kila awamu basi serikali ya awamu ya nne ingekuwa na vitu vichache kama changamoto kubwa lingekuwa kuleta maendeleo halisi kwa watanzania .

thx

Issue hapa ni kuwa wote walikuwa wanasimamia sera za chama cha mapinduzi na si vinginevyo. Watanzania wanaifanya siasa ionekane kama ni mazingaombwe,hao wote hawawezi kwenda nje ya sera na ilani za chama chao,lakini watanzania walivyo watu wa ajabu,utaona wanaanza kuongelea mtu mmoja mmoja na kwamba viongozi hao walikuwa wanatumia sera za chama gani wanasahahu...Wanafikiri ni rais mwenyewe binafsi ama kiongozi mwingine atakuja kuwakomboa,remember walivyokuwa wakimwita Mrema Mkombozi wa wanyonge nk? Na jinsi baba wa Taifa alivyoliliwa? No wonder wengi wetu wanaamini matatizo yetu someone else atayasolve..Ni kasumba na tabia mbaya sana kuwa wategemezi kwenye kila kitu,jamii ni lazima ibadilike kuanzia ngazi ya familia,ccm imo ndani ya familia zetu na ccm ni ufisadi,ufisadi ni kama ujiko flani,sasa hili ndiyo tatizo kubwa kupita yote.

Watanzania waeleweshwe kuwa ni chama kinachotakiwa kupigwa chini kwenye uchaguzi kwani ni sera zake ndizo zinafuatwa wakati wa uongozi,sasa humo kwenye hicho chama kuna JK,Mkapa,Mwinyi na wengineo,na si tuanze kuwazungumzia hao watu as if wakati wakiwa madarakani chama kilikuwa kimekufa...Wao hawaoni kama chama chao kina matatizo,wanadhani ni tujimakosa flani flani tu na watu wajiuzulu kwa heshma zao.

Wabongo mtumie akili na muache mawazo ya kukumbatia watu waliotufikisha hapa...Sisemi kwa ubaya lakini inabidi tuwe makini sana wakati wa upigaji kura na usimamizi uwe makini.

Ili upinzani uweze kushinda inabidi wananchi walio wengi waikatae ccm,kumkataa JK na kumkubali Mkapa si solution ya ushindi dhidi ya ccm.

Si unaona wananchi wanachezewa akili...Eti JK abadilishe baraza la mawaziri basi kutakuwa na utofauti, tunakuwa kama tumesahahu hata vikao vya huko Butiama nk,wote Mkapa na JK ndani ya nyumba na JK keshasema aachwe apumzike mzee wa watu, sasa wakina Mramba wanapowekwa ndani kiusanii basi na ccm nao eti wanapata nafasi ya kuongea,ni maajabu.

Wanaweza kuwa na mawazo tofauti ndani ya chama lakini ufisadi ndio nguzo kuu ya ccm kwa mtizamo wangu.Tulishawahi kuanzisha mada nyingi sana za kuisema ccm,ikaishia kupitisha ile bajeti ya kifisadi wakisaidiwa na Mzee Mapesa....Wananchi wameshasahau kwani nadhani ni wachache mno wanaojuwa bajeti ni nini let it alone kupata muda wa kufuatilia mambo hayo,wao huwa wanaona tu picha ya Mramba na briefcase anaingia bungeni huku akilpigwa mipicha lukuki.

Ilidaiwa kuwa issue zitajadiliwa kuhusu mikataba ya madini nk,lakini mara watu wakatishwa mara wengine wakafa kiutatanishi mara wengine wakabakia kulazwa hospital siku ya mjadala....Na huku unga wa mahindi ukinyunyizwa huko ndani ya bunge tukufu.

Mama Kilango naye kimya nadhani watakuwa wamemtisha nyau.

Mimi wana JF nasema kweli kama JK atakuwa anafanya usanii ifikapo 2010 kama wananchi wakiipigia kura ccm nitashangazwa sana siyo siri.
 
Mimi nilisemaga tokea mwaka 2005 kule bcstimes.com kuwa Kikwete siyo makini na matokeo yake sasa ndio haya tunayoyaona, kuteu watu wasio makini kuongoza wizara muhimu (wizara karibu zote muhimu). Kwanza alianza vibaya kwa kuunda baraza kubwa mno la mawaziri. I mean, what the hell....baraza kubwa hivyo lilikuwa la nini?

Kwa hiyo siku zote mimi huwa nasema mtu asiye makini ni rahisi sana kwake yeye kuteua watu wasio makini pia. Na sasa ndio haya tunayoyaona....
You couldnt be more right.

Mkapa alikuwa makini? Akina Chenge, Mramba na Yona?

Sasa ndugu Mzalendohalisi, mbona unachafua hewa - Mkapa anaingiaje hapa ? Mapenzi ni kikohozi, hayawezi kufichana ........Tunamwongelea JK, period.
 
Back
Top Bottom