Mnyakatari
JF-Expert Member
- Oct 25, 2010
- 2,027
- 1,791
Hotuba ya raisi Kikwete imeacha maswali mengi.Anasema chadema wanaandamana kushinikiza mambo yaleyale walioyashupalia kipindi cha kampeni na watanzania hawajaridhika nao nandomana wamewanyima uongozi.Malipo ya dowans ni suala jipya,halikuwemo kwenye kamapeni!Kupanda kwa gharama za maisha hakujakoma baada ya ccm kushinda,kwa nini liachwe?Gharama za umeme pamoja na kupigiwa kelele lakini wameonekana wanahitaji nguvu zaidi ya shinikizo la maandamano.Anakwenda mbali zaidi na kuwaita chadema wapenda vurugu na machafuko na kwamba wanataka kumpokönya madaraka ambayo watanzania hawakuwapa!Hii nayo ni propaganda nyingine.Kazi za chadema kama chama cha siasa sio kushiriki uchaguzi pekee balh ni kuwapa elimu wananchi na kuwafumbua macho jinsi watawala waliowaamini wanavyoliangamiza taifa.Sasa chadema wanafanya kosa gani?Kama wanaenda kinyume na katiba kwa nini asiwafungulie mashtaka mbona yeye ndo amiri jeshi mkuu?Raisi anawambia watz wawapuuze chadema na mambo yao!Chadema ni akina nani?Ni wabunge na viongozi wote wa chadema au na ule umati unaofurika kwenye maandamano?Chadema sio watanzania?Anawaambia watanzania au anawambia CCM?Raisi anapoanza kuexclude kundi mojawapo kwakuwa tu eti linasema ukweli unaomuuma,anakaribisha machafuko.Raisi anatakiwa awe informed kuwa chadema si kundi dogo la watu bali ni kundi kubwa la watanzania.Yeye anaongea na watanzania gani?