mafisadi mkome hii sinema ya hivi sasa juu ya dowans laasivyo
tukaporomoshe 'mi-wikileaks' zake hapa mpaka mjisikie kufakufa hivi!!!
hawa wamiliki wa dowans wa kukodi wala hatudanganyiki!! Lowassa na rostam azizi, kaundeni mpango mwingine; huu hapa tayari umeanguka kwa pua.
Na mkijaribu kubisha basi tutaporomosha ushahidi kama mvua hapa kuliko hata ya wikileaks mpaka mshangae wenyewe. Naona bora mkasimamishe hii sinema ya huyo msaudia aliyeletwa nchini na ridhiwani kikwete tayari na makabrasha yote bandia, kabla hamjapata kuabika zaidi!!!!
Ile pichaniloiona hapa jf nimehisi ni tofauti na nikoiona kupitia google images!
</p>HII HAPA YA UKWELI KABISA..........</p>
<p> </p>
<p><img src="http://www.oeronline.com/php/2008_may/in_news1.jpg" border="0" alt="" />
me wala huya al nani cjui hajanichosha kama hawa wahariri wetu..!! Mtu aitishe press conference afu agome kupigwa picha na wao bado wanaendelea kumsikiliza...!! Au alikua anagawa hela nini kiukweli me sipati picha hapa..!! Na kama ye ni mmiliki halali why agome kupigwa picha?? Im sure hata osama akija bongo hawezi kataa kupigwa picha why this fashist agome?? :blah:
Changa la macho mtakuja fumbua macho jamaa kesha chukua chake kasepa.
Inasemekana amefuata cheki yake ya mabilioni ya dola za kimarekani.
maana inabidi aisaini kbla ya kuitumbukiza benki, tehteh
Swali> Mr. prezidenti is it true?
Jibu> teh teh teh don't listen to radio mbao teh teh
Kwa mdadisi yeyote ziara ya anayejihita mmiliki wa Dowans Brig.Gen.Al Adawi inazua maswali mengi kuliko majibu; kwanza kwanini hakutaka kupigwa picha?
Pili katika hali ya kawaida R.A kama mwakilishi wake ndiye mwenyeji wake, hivyo alitakiwa awepo katika mkutano wake na wahandishi wa habari kwaajili ya kumtambulisha, inaonekana hilo halikufanyika.
Tatu ameingia tu na mtambo mmoja wa Dowans ukawashwa. Haiwezekanikuwashwa huko kwa mtambo huo ukatokana na mashauriano ya siku moja.
Inavyoelekea mipango yote tayari ilikwisha andaliwa, haya yanayotendeka sasa ni kiini macho, ndiyo maana kuna tetesi ya kwamba hata huyo anayejihita Brig. Gen. Al-Adawi uenda hasiwe mwenyewe bali kivuli chake.
.Sio mhusika kabisa huo ni mchoro JK, EL, RA, Ngereja na ridhiwani walikuwa wanaratafuta njia namna ya kuuwasha Ridhiwani amemfuata Dubai na kumleta, hao wahariri ni mataahira na wao watakaaje kwenye press conference na mmliki ambaye anakataa kupigwa picha siwangeondoka.
Hii serikali ya kikwete imeshatupima nakutuona watanzania hatujitambui hatuna mbele wala nyuma wanaweza wakasema na kufanya lolote na umma usifanye kitu ndio maana Raisi wa nchi anaweza akashirikiana na mamafia kuangamiza nchi
Haijulikani ndugu yangu na ndiyo sababu akachagua kundi la waandishi wa habari wachache ili wamuulize maswali. Huyu mtu haishi Tanzania kawafahamu vipi waandishi wa habari wa kuwaita katika hiyo news conference yake ili wamuulize maswali? Ni mchoro mtupu huu lakini Watanzania tumeshaushtukia.....na ni lazima tuhakikishe hapati hata senti moja.