Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
umetoa point nzuri sana na ambayo inahitaji kuangalia kwa karibu.
a. Je, yawezekana kuna wanajeshi wengi wa vyeo vya chini ambao walicheleweshwa kupanda vyao kwa wakati katika miaka hii sita? Au walirukwa vyeo?
b. Je, kuna wastaafu wengi wanakuja katika vyeo hivyo ndani ya miezi michache ijayo?
Jambo moja kubwa na la msingi ni kuwa hili si jambo dogo. Misri chini ya Morsi imewastaafisha baadhi ya majenerali kwa mkupuo na ikawa habari ya kimataifa; ilitokea pia Uturuki baada ya Chama cha Kiislamu kushika madaraka. Kwa Tanzania inabidi hili liangaliwe kwa karibu kwani ama ni udhaifu wa hali ya juu vinginevyo naliangalia kwa yale yaliyotokea kati ya Malawi na Tanzania.
Lakini vile vile tumesikia kuwa Tanzania imeombwa na sasa imekubali kuongoza kikosi cha kimataifa cha Africa huko Congo. Na wanaokumbuka tayari Marekani iliiomba Tanzania kupeleka wanajeshi Somalia (TZ ilikataa na kukubali kutoa mafunzo tu).
Mabadiliko haya si ya kawaida na hayawezi kuchukuliwa kwa kawaida na majirani zetu na taasisi za kimataifa za kiinteligensia. Ni makubwa mno kutokea kwa wakati mmoja.
Note:
Ukiangalia majina ya waliopandishwa vyeo utaona kuwa hatujaambiwa wanapangiwa majukumu gani mapya au wanapewa kazi gani mpya (ukiondoa ya Chief of Staff na yule wa JKT).
Maswali yamebakia.
a. Je, yawezekana kuna wanajeshi wengi wa vyeo vya chini ambao walicheleweshwa kupanda vyao kwa wakati katika miaka hii sita? Au walirukwa vyeo?
b. Je, kuna wastaafu wengi wanakuja katika vyeo hivyo ndani ya miezi michache ijayo?
Jambo moja kubwa na la msingi ni kuwa hili si jambo dogo. Misri chini ya Morsi imewastaafisha baadhi ya majenerali kwa mkupuo na ikawa habari ya kimataifa; ilitokea pia Uturuki baada ya Chama cha Kiislamu kushika madaraka. Kwa Tanzania inabidi hili liangaliwe kwa karibu kwani ama ni udhaifu wa hali ya juu vinginevyo naliangalia kwa yale yaliyotokea kati ya Malawi na Tanzania.
Lakini vile vile tumesikia kuwa Tanzania imeombwa na sasa imekubali kuongoza kikosi cha kimataifa cha Africa huko Congo. Na wanaokumbuka tayari Marekani iliiomba Tanzania kupeleka wanajeshi Somalia (TZ ilikataa na kukubali kutoa mafunzo tu).
Mabadiliko haya si ya kawaida na hayawezi kuchukuliwa kwa kawaida na majirani zetu na taasisi za kimataifa za kiinteligensia. Ni makubwa mno kutokea kwa wakati mmoja.
Note:
Ukiangalia majina ya waliopandishwa vyeo utaona kuwa hatujaambiwa wanapangiwa majukumu gani mapya au wanapewa kazi gani mpya (ukiondoa ya Chief of Staff na yule wa JKT).
Maswali yamebakia.