Mwigulu Jisandu
Member
- Jul 1, 2010
- 32
- 2
Kwa kiasi fulani nimefuatilia ziara zinazoitwa za kampeni za Kikwete. Kinachonishangaza ni jinsi anavyotumia mamlaka yake kushawishi watanzania wampigie kura.
Akiwa Bukoba aliagiza ununuzi wa meli.
Kilosa ujenzi wa nyumba za waathirika wa mafuriko ambao alishawahi kwenda kuwaona lakini alisubiri wakati huu wa kampeni.
Kaenda Mtibwa katatua kero zao ikiwa ni pamoja na kumfukuza kazi meneja.
Na mengine mengi. Ni wazi kuwa wagombea wengine wa urais hawana mamlaka ya kufukuza mfanyakazi kwa kuwa hawako kwenye system. Kweli kwa staili hii kuna haja ya kufanya kampeni?
Hawa wengine wataonekana vipi wakati hawajafanya chochote?
Naomba wana JF mnisaidie inawezekana silielewi vizuri neno hili kampeni.
Nawasilisha hoja.
Akiwa Bukoba aliagiza ununuzi wa meli.
Kilosa ujenzi wa nyumba za waathirika wa mafuriko ambao alishawahi kwenda kuwaona lakini alisubiri wakati huu wa kampeni.
Kaenda Mtibwa katatua kero zao ikiwa ni pamoja na kumfukuza kazi meneja.
Na mengine mengi. Ni wazi kuwa wagombea wengine wa urais hawana mamlaka ya kufukuza mfanyakazi kwa kuwa hawako kwenye system. Kweli kwa staili hii kuna haja ya kufanya kampeni?
Hawa wengine wataonekana vipi wakati hawajafanya chochote?
Naomba wana JF mnisaidie inawezekana silielewi vizuri neno hili kampeni.
Nawasilisha hoja.