Kikwete amwambia Magufuli aache Ubabe kwenye bomoa bomoa; Magufuli ataaminika tena?

Rais Jakaya Kikwete leo amemgeukia mbogo waziri Magufuli kwa kumwambia waziwazi kuwa aache ubabe na mpango wake wa Bomoa Bomoa wakati wa ziara ya Rais alipotembelea wizara ya Ujenzi leo hii.

Huu unaonekana ni msumari mwingine kwa mpiganaji Magufuli, kufuatia msumari wa kwanza uliogongelewa na Pinda wakati akiwa Bukoba hivi karibuni.

Hapo awali magufuli aliwataka 'Wajenga Hovyo" kando kando ya hifadhi za barabara kuwa wanabomoa wenyewe kwa kipindi kifupi. Now Mheshimiwa JK amemuagiza kuwapa "Hata miaka miwili" na kuwalipa na fidia.

Kazi inaendelea.... Je, Magufuli kuamua kujiuzuru kama tetesi zilivyosambaa hapo awali?

Binafsi, sikubaliani na utaratibu huu wa kuendesha vikao na kufanya maamuzi hadharani. Masuala haya ya Pinda, JK na hata Magufuli mwenyewe wangeweza kuyafanya na kukubaiana katika vikao vya baraza la mawaziri badala ya kutengeneza sinema hadharani.

I striongly believe they are trying to create "storyboard" for winning public attention kwenye masuala yasiyo ya msingi na kusahau yanayogusa maisha yao moja kwa moja.



Kama kiranja mkuu ametenda hivyo unavyotulipotia,napata swali la kujiuuliza kwamba,hivi magufuli huwa anafanya kazi zake kwa kutumia ubabe au kwa kufuata sheria na taratibu za nchi? au ukisimamia sheria unakuwa mbabe? kama hili la pili ni ndio, namshauri jeyikkeyi nae awe mbabe kama magufuli ili ainusuru nchi hii toka mikononi mwa wakoloni weusi(mafisadi) Wanaoi -xploit nchi hii.ASIWAHADAE wananchi waaliokiuka sheria,akumbuke siku zote ukweli UTASIMAMA DAIMA!
 
Nimeshaona hii picha ilivyotengenezwa; Magufuli akijiuzulu tu anaweza kushtakiwa kwa kutumia madaraka vibaya na kuisababishia serikali hasara! Na kesi itakuwa prolonged hadi 2015 na kumuondoa kwenye kinyang'anyiro cha urais kabisa.

Mbona Gwiji la Mafisadi Lowassa halijafunguliwa kesi? mimi naona hapa pombe anatafutiwa kisa, kuna kitu aidha pombe amegundua ufisadi kwenye hiyo wizara au amekataa kutenga 10% cha Fisadi Kikwete ndio maana wanataka ajifukuze mwenyewe halafu wamuue kisiasa
 
Mbabe kweli awe huyu Mzee wa Chato kweli??

Nadhani Mhe Kikwete atakua amekosea kidogo hapa, siku zote sheria huwa ni mbabe na Dr Maghufuli huwa anatumia sana sheria to the letter bila kutazama mtu sura. Kama Kweli John Maghufuli ni MBABE YEYE TU NA WA SI SHERIA anazozitumia basi majaji wetu hamjamtendea haki waziri huyu kupumzika kule jela Ukonga ambapo wababe wasiotii sheria wanakopoa siku zote.

Sasa hapo mwenye ubabe ni John Pombe Maghufuli au sheria za nci?? Naona kazi safari hii itakua ngumu sana kwa mazingira haya kwa John Magufuli kuweza kufanikiwa kiutendaji.
 
Watu wengine utadhani walizaliwa na CCM, na watakufa nayo!!!!!!!!!! Kama Pombe angekuwa yuko serious hii ni sababu tosha kujua kwamba CCM haimtaki-aondoke!!!!!!!!!!!. Tusishangae mkwere leo hii jioni akatangaza kuiidhinisha resignation ya pombe makufuli!!!!!!!!!!!! WanaJF tumkaribishe CDM kwenye chama cha watu waliomaanisha kumwondoa mkwere kwa nguvu ya umma, kama ile iliyomshghulikia na kumwondoa mubaraka wa misri!!!!!!!!!!!

We mtu wa mungu nimekukubali unapeo na umepevuka kifkra mkwere kwa namna yoyote ile ataondoka na chama chake!! People power magufuli,mwakyembe sita karibu sana
 
Had it been that I'm JPombeM, this would've been my exite - without looking back.
Enough would've been enough with having my personality being politically tainted just because there's political naivity within the ruling elites - including the boss.
I would instead exert my political ambition to have the constitutional changes, changes that will erode the presidents' mighty powers that'll put him under the law.
ILA SIWEZI KUANZISHA CHAMA KIPYA AU KUJIUNGA NA CUF!
 
Haya yote yanatokea kwa sababu serikali ya CCM haina mipango. Kila mmoja anatoka kivyake. Watanzania tuna matatizo kibao, kuyatatua hawawezi kwasababu upeo wao umefika mwisho. Wanaishia kulialia tu, mara ghaddaffi mara soko la dunia, mvua haikunyesha. Watanzania tunatakiwa kujiokomboa wenyewe kabla hili genge la wahuni halijatumaliza
 
MwanaFalsafa1 said:
Magufuli asipo jiuzulu naye ana yataka. Maana ukidhalilishwa hivi na bado ukabaki inaonyesha ume kubali kutukanwa.

MwanaFalsafa1,

..huenda ana madudu ameyafanya hivyo hana ujasiri wa kuwakabili hao "wanaomnyanyasa."

..hivi unafikiri lile suala la kuuza nyumba za serikali kwa bei ya kutupa limeiingizia serikali na wananchi hasara kiasi gani?
 
ushaona wapi Tanzania kiongozi akijiuzulu?labda awe na kashfa ya kubaka ,Tanzanian leaders =Gaddafi
 
Wadau,
Nimemsikiliza rais Kikwete kwenye ITV jioni hii. Alilosema nakubaliana naye. Amelaumu uzembe wa kuacha mtu achimbe msingi, ajenge, na hakuna hatua zinazochukuliwa, na hatimaye baada ya nyumba kumalizika ndipo bomoabomoa inafuata. Ametaka kuwepo taratibu zitakazosaidia kuhakikisha kuwa bomoa bomoa inakuwa last resort (uelewa wangu.) Lakini hakusema kuwa bomoa bomoa isitishwe.
 
Sasa ni ruksa kuvunja sheria yoyote utapewa miaka miwili wa kujifikiria kama kweli umevunja sheria au la pia ruksa kudai kuwa maisha magumu yamekusukuma kuvunja sheria na unaweza ukaachwa uendelee kuvunka sheria.
 
Kikwete anajaribu ku win political situation kwa sasa bila kuangalia sheria inasemaje. That is not rule of law kwamba eti sheria inasema A halafu yeye anasema B. Kwani nani yuko juu ya sheria? Hii inaonesha kwamba there is no rule of law in Tanzania.
 
mbona habari ninazozipata zinaonekana kuchanganya! wengine wanadokeza kuwa kasema aendelee na shughuli zake bila ya kuogopa

Nimesikiliza habari yote na hakuna 'ubabe' wowote, he was just adviced not to issue 48hrs notice but in principal the exercise has his blessing,

He was also questioning modality, I sincerely hope a day will come when we separate facts and obsessions..
 
Hayo ni matokeo ya ubabe wa wabunge wa ccm, wakati sheria inapitishwa laijadili walishangilia sana, sasa magufuli ndio anaisimamia utekelezaji
 
Magufuli aelewe wenzake mambo ya maendeleo ya nchi sio kivile, wao siasa na kuchakachua tu. Sasa yeye akileta mambo ya kupiga kazi kiukweli kweli atawaumbua ndio maana wanamwambia kanyaga polepole
 
Hayo ni matokeo ya ubabe wa wabunge wa ccm, wakati sheria inapitishwa laijadili walishangilia sana, sasa magufuli ndio anaisimamia utekelezaji

Hiyo sheria imepitishwa kabla hata TANU haijazaliwa seuse CCM.
 
Inawezekana pia kuwa baada ya kumbembeleza kikubwa akaringa sasa tunatumia njia ya sizitaki mbichi hizi ili kama itakuwa basi ijulikane na sisi tulikuwa tumemchoka na hatumhitaji.
 
This is hilarious! In fact i didn't expect more than that from JK.Mnadhani JK angemwambia nini Magufuli zaidi ya hilo?Huu urais wa 2015?kazi ipo
 
Wakati wa kampeni alisema anataka flyover pale Ubungo....sasa magufulki anaanza kazi wanamzuia hiyo fyover itapita wapi? Huu msongamano utaisha kweli?

Kwa hakika, kwa stail hii flyovers zitaendelea kuwa ndoto za mchana kwa sababu bila kuziacha free hifadhi zote za barabara hasa ndani ya jiji la Dar, hizi fly overs alizoahidi JK zitabakia kuwa ndoto tu?

Magufulu anatakiwa kutathmini kimkakati nafasi yake katika serikali hii ya Mchakachuaji JK!
 
Haya yote yanatokea kwa sababu serikali ya CCM haina mipango. Kila mmoja anatoka jinsi anavyojua yeye. Watanzania tuna matatizo kibao, kuyatatua wameshindwa kwasababu upeo wao wa kufikiri umefika mwisho. Wanaishia kulialia tu, mara ghaddaffi mara soko la dunia, mvua haikunyesha, chadema wachochezi. Hapa hatuna serikali hili ni genge la wahuni :angry:
 
Back
Top Bottom