Kikwete amuita Lowassa kwa mazungumzo ya siri!

The Informer

Senior Member
Jun 14, 2010
119
29
Mimi ni miongoni mwa waandishi tulio hapa Dodoma. Nimepata hii taarifa kwa watu waliokuwa karibu na Ikulu sasa hivi usiku huu.

Rais Jakaya Kikwete amemuita swahiba wake wa siku nyingi, Edward Lowassa, Ikulu ya Dodoma kwa mazungumzo ya faragha. Haijulikani watazungumza nini ila ni Kikwete ambaye ame initiate hayo mazungumzo. Inasemekana hata Lowassa amepigwa butwaa na hajui Kikwete amemuitia nini.

JK kufanya mazungumzo ya siri na Lowassa kunakuja baada ya baadhi ya wajumbe wa NEC leo hii kutoa matamshi makali dhidi ya Lowassa, Rostam Aziz na Andrew Chenge na kutaka vigogo hawa wenye tuhuma lukuki za ufisadi watimuliwe kwenye chama.

Kuna tetesi kuwa JK anataka kufanya Cabinet reshuffle baada ya CCM kujivua gamba. Huenda anataka kumpooza kwa kumrejesha swahiba wake kwenye Baraza la Mawaziri ili ajiandae vyema kumrithi 2015 baada ya kujeruhiwa kwenye NEC ya CCM.
 
inawezekana, lakini pia kuna mambo mawili.
i] anamuomba apunguze kasi ya kujiandaa na 2015 ili kulinda mshikamano wa chama.
au
ii] anamuomba ajiuzulu mwenyewe kwa sababu wajumbe wamechachamaa.
 
nchii hii haitakwisha sanaa milele...atashangaaje kuitwa na swahiba wake wakati kutwa wanashinda wanachat kwa sms
 
Tusubirie tuone itakuwaaje maana ndio anaanzaga hivi hivi.......
 
Ccm sasa inataka kumwaga sumu baada ya utoaji wa gamba la juu kutokuleta tija
 
Haijulikani watazungumza nini ila ni Kikwete ambaye ame initiate hayo mazungumzo.

. Huenda anataka kumpooza kwa kumrejesha swahiba wake kwenye Baraza la Mawaziri .

Tanzania na vioja, guilty conscious
 
As you said "shaiba wake" Haiwezekani JK kumuita EL na kutokujua anamuitia nini.! Imposble mkuu, he knows what goes on, wasanii tu hao hakuna lolote. Zen great thinker it can be eti Ngoayi apokunywe uanachama? Back to 1995 come 2005, they are very close! Shortly Jk hakohoi kwa EL n RA
 
Mimi ni miongoni mwa waandishi tulio hapa Dodoma. Nimepata hii taarifa kwa watu waliokuwa karibu na Ikulu sasa hivi usiku huu.

Rais Jakaya Kikwete amemuita swahiba wake wa siku nyingi, Edward Lowassa, Ikulu ya Dodoma kwa mazungumzo ya faragha. Haijulikani watazungumza nini ila ni Kikwete ambaye ame initiate hayo mazungumzo. Inasemekana hata Lowassa amepigwa butwaa na hajui Kikwete amemuitia nini.

JK kufanya mazungumzo ya siri na Lowassa kunakuja baada ya baadhi ya wajumbe wa NEC leo hii kutoa matamshi makali dhidi ya Lowassa, Rostam Aziz na Andrew Chenge na kutaka vigogo hawa wenye tuhuma lukuki za ufisadi watimuliwe kwenye chama.

Kuna tetesi kuwa JK anataka kufanya Cabinet reshuffle baada ya CCM kujivua gamba. Huenda anataka kumpooza kwa kumrejesha swahiba wake kwenye Baraza la Mawaziri ili ajiandae vyema kumrithi 2015 baada ya kujeruhiwa kwenye NEC ya CCM.

Anaweza kuwa anataka kumtisha -- yeye na RA kwamba wasithubutu kufanya chochote kama malipizo ama sivyo nguvu za dola.....?
 
nchi yetu wenyewe wanagawana kama ice cream za azam,kibaya zaidi tunawaangalia tu,Jwtz,polisi,uwt,umma wooote tupo tu!
 
Mimi ni miongoni mwa waandishi tulio hapa Dodoma. Nimepata hii taarifa kwa watu waliokuwa karibu na Ikulu sasa hivi usiku huu.

Rais Jakaya Kikwete amemuita swahiba wake wa siku nyingi, Edward Lowassa, Ikulu ya Dodoma kwa mazungumzo ya faragha. Haijulikani watazungumza nini ila ni Kikwete ambaye ame initiate hayo mazungumzo. Inasemekana hata Lowassa amepigwa butwaa na hajui Kikwete amemuitia nini.

JK kufanya mazungumzo ya siri na Lowassa kunakuja baada ya baadhi ya wajumbe wa NEC leo hii kutoa matamshi makali dhidi ya Lowassa, Rostam Aziz na Andrew Chenge na kutaka vigogo hawa wenye tuhuma lukuki za ufisadi watimuliwe kwenye chama.

Kuna tetesi kuwa JK anataka kufanya Cabinet reshuffle baada ya CCM kujivua gamba. Huenda anataka kumpooza kwa kumrejesha swahiba wake kwenye Baraza la Mawaziri ili ajiandae vyema kumrithi 2015 baada ya kujeruhiwa kwenye NEC ya CCM.
huu unafiki unanikera sana
 
Back
Top Bottom