Kikwete amkacha Rostam Afrika ya Kusini

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
233
Katika gazeti la MwanaHalisi la leo habri kuu ya ukurasa wa mbele ilikuwa na kichwa cha Habari "Rostam azimwa." Hii kutokana na ruling ya Mahakama y rufaa ya rufani ya gazeti hilo dhidi ya Rostam. Lakini Habari ya kusimumua zaidi kutokana na stori hiyo inatokana na kibwagizo "Kikwete ‘amkacha (Rostam) Afrika ya kusini", Habari ambayo iko mwishoni mwa stori hiyo na ninairudia hapa kuwarahisishia wana JF wenzangu:


…..Wachunguzi wa masuala ya vyombo vya Habari na haki ya uhuru wa kujileleza wanasema hukumu ya Mahakama Kuu ililenga kuzima uhuru wa Habari na kulinda mtu mmoja dhidi ya masilahi ya taifa.

Wamesema mahusiano ya kibiashara na kisiasa kati ya Rostam na wanasiasa na wafanyabiashara wengine, ambayo sharti yafahamike kwa kuwa yeye yuko katika nafasi ya kiongozi wa umma, yangezimwa moja kwa moja.

Kwa mfano, uhusiano wa Rostam na Rais Jakaya Kikwete, unaotajwa kutota hivi sasa, usingepata nafasi ya kuripotiwa katika chombo hiki na vingine.

Taarifa za kuaminika kutoka ndani ya serikali zinasema, Kikwete ameamua kujiweka kando na Rostam. Imefahamika kuwa kuna wakati amekataa kukutana naye ana kwa ana.

Tukio la karibuni linalosimuliwa na maofisa wengi serikalini ni lile la nchini Afrika ya Kusini ambako Rais amedaiwa kukataa kukutana na Rostam katika Hoteli ya Hilton mjini Pretoria.

Kikwete alikuwa nchini Afrika ya Kusini kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa rais wa nchi hiyo, Jacob Zuma.

Kwa mujibu wa kiongozi mmoja wa ngazi ya juu ndani ya CCM ambaye alikuwa nchini humo kuhudhuria sherehe hizo, Kikwete alikataa ombi la Rostam la kutaka kukutana naye lililowasilishwa kwake na wasaidizi wake.

"Ni kweli kwamba Rostam alifika katika Hoteli ya Hilton aliyofikia Kikwete kwa lengo la kutaka kumuona. Lakini hakufanikiwa kutokana na Kikwete kukataa kuonana naye," mtoa taarifa ameeleza.

Taarifa zinasema kuwa Rostam alikuwa amejifungia kwenye chumba kimoja hotelini humo akijaribu kusubiri jibu kutoka kwa wasaidizi wa Kikwete, lakini hakufaulu.

Aliamua kujaribu tena kuwasiliana na wasaidizi wa Rais Kikwete wakati wa sherehe fupi ya chakula cha usiku, lakini wasaidizi waliobeba ujumbe walianza kutupiana mpira wa kuwasilisha ombi la Rostam na ndiyo ikawa tamati ya juhudi za mbunge huyo wa Igunga, Tabora.

Haijaeleweka iwapo tangu hapo amefanya juhudi zozote tena za kukutana naye. Kama ada, simu ya Rostam ama haipatikani na ikiita haijibiwi.
 
Last edited by a moderator:
Niliwahi kuisoma habari hii humu JF -- kuna mwanaJF mmoja aliigusia wakati anachangia mada moja kuhusu thread moja kuhusu RA.

Lakini kama ni kweli tukio hilo inashangaza kuona security inayomzunguka JK imelala, -- yaani itakuwaje mtu asafiri hadi nchi za nje kumfuatilia Rais, akafikia hoteli hiyo hiyo aliyofikia -- na pengine floor hiyo hiyo. Je ingekuwa ni mtu tu mwenye nia ya kumdhuru?
 
Hizi ndio habari wanazozipenda wadanganyika!

Sijajua sababu ya JK kumkimbia kada wa CCM, king maker, family friend na shemeji wa siri!

Hii ndio style nyingine ya uandishi wa mwanahalisi ambao mra nyingi unahisiwa kumuinua JK.Na haya ni moja ya maswali na habari zinazoendelea chini chini kuwa hili gazeti l wenyewe! unajua kuhusu tindikali ilikuwa mambo yako ya mahusiano na sio ufisadi!

Hakuna mantiki ya JK kumkimbia RA, kwa nini kwa sababu fisadi? kwa nini yuko huru kama ameapa kuilinda katiba yetu?

Wa kunitukana mnitukane, kwa mara nyingine nawaambia fumbueni macho kuhusu mwnahalisi na uchaguzi ujao!

mpiganaji wa ufisadi haangalii usoni wala kuchagua wa kumpiga!

JK hana usafi wowote Kubenea, HANA!!!!!!!!!!
 
Kikwete is a cleanse person by heart, soul and ethics he is going to be the best presdent ever for thise nation . This is the oder from the higher power let every body funga domo lake juu ya mumkashifu muheshimiwa rais kama wakritu fuaata biblia waisilam fata msaafu wapagani fuata katiba, tumuombea rais we tu mbowe,zito slaa fungeni midomotaka yenu kuazia leo, end of cort prof dr ing rev tumaini geofrey temu
 
Last edited:
Niliwahi kuisoma habari hii humu JF -- kuna mwanaJF mmoja aliigusia wakati anachangia mada moja kuhusu thread moja kuhusu RA.

Lakini kama ni kweli tukio hilo inashangaza kuona security inayomzunguka JK imelala, -- yaani itakuwaje mtu asafiri hadi nchi za nje kumfuatilia Rais, akafikia hoteli hiyo hiyo aliyofikia -- na pengine floor hiyo hiyo. Je ingekuwa ni mtu tu mwenye nia ya kumdhuru?
Ni kweli security ya mkuu wa nchi ni kitu muhimu sana.Kuna sehemu inawezekana mambo hayako sawa upande wa security. Kwa mfano jamaa wa security walikuwa wapi Mzee Mwinyi alipopigwa kibao?Hiyo ni sign tu kuwa pengine nako kunatakiwa kuboreshwe.Times change.Tusije kujilaumu kuwa hatukujua.
 
Hizi ndio habari wanazozipenda wadanganyika!

Sijajua sababu ya JK kumkimbia kada wa CCM, king maker, family friend na shemeji wa siri!

Hii ndio style nyingine ya uandishi wa mwanahalisi ambao mra nyingi unahisiwa kumuinua JK.Na haya ni moja ya maswali na habari zinazoendelea chini chini kuwa hili gazeti l wenyewe! unajua kuhusu tindikali ilikuwa mambo yako ya mahusiano na sio ufisadi!

Hakuna mantiki ya JK kumkimbia RA, kwa nini kwa sababu fisadi? kwa nini yuko huru kama ameapa kuilinda katiba yetu?

Wa kunitukana mnitukane, kwa mara nyingine nawaambia fumbueni macho kuhusu mwnahalisi na uchaguzi ujao!

mpiganaji wa ufisadi haangalii usoni wala kuchagua wa kumpiga!

JK hana usafi wowote Kubenea, HANA!!!!!!!!!!

Mimi niliambiwa wiki kama tatu au maximum nne zilizopita kwamba RA alikuwa na appointment na JK. Tulikuwa tunaongelea mambo ya kawaida ya JF na ndio akasema tena leo RA ana appointment na JK. Hiyo ni baada ya rais Zuma kuapishwa.

Huyo jamaa namwamini na yuko kwenye nafasi ya kujua habari kama hizo kirahisi. Sikufuatilia tena lakini ninachotaka kusema huenda hii habari ya Mwanahalisi haina ukweli wowote.

Siku za karibuni nimesoma habari nyingi za Kubenea ambazo kama una uwezo wa kufikiri utagundua baadhi hazi make sense.

Hata kama ilitokea inaweza kuwa na maana tofauti kabisa na ambayo mwandishi anataka tuamini. Rais anaweza akawa alikuwa na ratiba yake. Pia kuonana na mtu kama RA ambaye ana scandals nyingi kwa TZ tena ugenini inaweza isiwe jambo jema kwa mwanasiasa yeyote. Tafsiri yake inaweza kuwa mbaya kuliko hata kukutana naye Dar.

Haya magazeti ya Tanzania yameshatekwa na watu binafsi na ni balaa kwa wasomaji maana tunaishia kulishwa sumu ambazo hata hatutaki kuzila.
 
Kikwete is a cleanse person by heart, soul and ethics he is going to be the best presdent ever for thise nation . This is the oder from the higher power let every body funga domo lake juu ya mumkashifu muheshimiwa rais kama wakritu fuaata biblia waisilam fata msaafu wapagani fuata katiba, tumuombea rais we tu mbowe,zito slaa fungeni midomotaka yenu kuazia leo, end of cort prof dr ing rev tumaini geofrey temu

I need a glass of milk to grasp this crappy!
 
Katika gazeti la MwanaHalisi la leo habri kuu ya ukurasa wa mbele ilikuwa na kichwa cha Habari "Rostam azimwa." Hii kutokana na ruling ya Mahakama y rufaa ya rufani ya gazeti hilo dhidi ya Rostam. Lakini Habari ya kusimumua zaidi kutokana na stori hiyo inatokana na kibwagizo "Kikwete ‘amkacha (Rostam) Afrika ya kusini", Habari ambayo iko mwishoni mwa stori hiyo na ninairudia hapa kuwarahisishia wana JF wenzangu:


…..Wachunguzi wa masuala ya vyombo vya Habari na haki ya uhuru wa kujileleza wanasema hukumu ya Mahakama Kuu ililenga kuzima uhuru wa Habari na kulinda mtu mmoja dhidi ya masilahi ya taifa.

Wamesema mahusiano ya kibiashara na kisiasa kati ya Rostam na wanasiasa na wafanyabiashara wengine, ambayo sharti yafahamike kwa kuwa yeye yuko katika nafasi ya kiongozi wa umma, yangezimwa moja kwa moja.

Kwa mfano, uhusiano wa Rostam na Rais Jakaya Kikwete, unaotajwa kutota hivi sasa, usingepata nafasi ya kuripotiwa katika chombo hiki na vingine.

Taarifa za kuaminika kutoka ndani ya serikali zinasema, Kikwete ameamua kujiweka kando na Rostam. Imefahamika kuwa kuna wakati amekataa kukutana naye ana kwa ana.

Tukio la karibuni linalosimuliwa na maofisa wengi serikalini ni lile la nchini Afrika ya Kusini ambako Rais amedaiwa kukataa kukutana na Rostam katika Hoteli ya Hilton mjini Pretoria.

Kikwete alikuwa nchini Afrika ya Kusini kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa rais wa nchi hiyo, Jacob Zuma.

Kwa mujibu wa kiongozi mmoja wa ngazi ya juu ndani ya CCM ambaye alikuwa nchini humo kuhudhuria sherehe hizo, Kikwete alikataa ombi la Rostam la kutaka kukutana naye lililowasilishwa kwake na wasaidizi wake.

"Ni kweli kwamba Rostam alifika katika Hoteli ya Hilton aliyofikia Kikwete kwa lengo la kutaka kumuona. Lakini hakufanikiwa kutokana na Kikwete kukataa kuonana naye," mtoa taarifa ameeleza.

Taarifa zinasema kuwa Rostam alikuwa amejifungia kwenye chumba kimoja hotelini humo akijaribu kusubiri jibu kutoka kwa wasaidizi wa Kikwete, lakini hakufaulu.

Aliamua kujaribu tena kuwasiliana na wasaidizi wa Rais Kikwete wakati wa sherehe fupi ya chakula cha usiku, lakini wasaidizi waliobeba ujumbe walianza kutupiana mpira wa kuwasilisha ombi la Rostam na ndiyo ikawa tamati ya juhudi za mbunge huyo wa Igunga, Tabora.

Haijaeleweka iwapo tangu hapo amefanya juhudi zozote tena za kukutana naye. Kama ada, simu ya Rostam ama haipatikani na ikiita haijibiwi.
Na hapa kazi ipo maana mnataka kuingiza makundi huku JF wengine upande wa JK wengine RA si muwaache tu muendelee na mengine
 
ROSTAM tena na JK wafikie Hivyo ??hiyo ndiyo sadiki ukipenda ni mazingaubwe mnafanyiwa kwa wale mlio lala usingizi mzito.
 
Kikwete is a cleanse person by heart, soul and ethics he is going to be the best presdent ever for thise nation . This is the oder from the higher power let every body funga domo lake juu ya mumkashifu muheshimiwa rais kama wakritu fuaata biblia waisilam fata msaafu wapagani fuata katiba, tumuombea rais we tu mbowe,zito slaa fungeni midomotaka yenu kuazia leo, end of cort prof dr ing rev tumaini geofrey temu


Aaghaaa, kumbe ni......

Limbukeni
user_online.gif
limbukeni TUMAINI GEOFREY
Banned

No need to answer.
 
Hii habari imekaa kimtego sana.
Rostam mbunge wa CCM,na mjumbe wa kamati kuu ya CCM yenye wajumbe 38 na mwenyekiti wake akiwa Jakaya Mrisho Kikwete.Idadi ya wajumbe hawa ni ndogo sana kufanya kuwa ngumu kwa mjumbe mmoja kushindwa kumwona mwenyekiti.

Safari za Kikwete nje haziwezi kumzuia Rostam asiweze kuonana na swahiba wake, kwani matukio mengi yanamfanya mtu yeyote kuweza kuwa karibu sana na Rais bila ya ulinzi mkali kama ilivyozoeleka hapa nyumbani, hivyo ni rahisi sana Rostam kumwona Jk na kuomba wakutane bila kumtumia mtu yeyote hasa ukizingatia Jk hawezi kukataa kuongea na Rostam akimkaribia.

Kusema kwamba Jk ni mtu safi huo ni uongo ulio kubuhu. Ni mara kazaa wakati Jk akiwa waziri amewahi kuagiza baadhi ya watu kupewa fedha na Rostam, je hizo fedha RA alikuwa anatengeneza au ulikuwa mgao wa bwana mkubwa. Na vilevile wakati Jk alipokwenda kuchukua form Dodoma alipelekwa na kamanda wake EL baada ya kuchangiwa fedha na akina Rostam.

Na kubwa zaidi kama kweli leo Jk anamwona RA ni mchafu angeanza kumtosa ndani ya chama kwa kumtoa kwenye ujumbe wa kamati kuu na kumwomba ajiuzulu ubunge halafu ifuate mahakamani. Siwezi kuamini kabisa kwamba eti Rostam kashindwa kuongea na Kikwete, Mbona Chenge wanachonga na Kikwete , Mbona Mkapa aliyekuwa mwenyekiti wa kutoa fedha za EPA walikuwa wote wakifungua maji juzi huko kanda ya ziwa. Mbona makamba bado ni katibu mkuu wakati inasadikika alikuwepo kwenye mkutano wa kuvunja BOT. Mbona kagoda bado ni kitendawili kikubwa. Mbona Sumari kamwambie Dr. Slaa awaachia Meremeta yao wanajua fedha zilikokwenda hakuna jeshi wala usalama wa taifa lao.

Kukaa hoteli moja na kiongozi hiyo sio ajabu, huwa wao wanalinda na kuangalia ni nani wapo hotelini na wanafanya nini, na inategemea na raisi gani yupo kwani kuna maraisi wasio na athari sana na kutafutwa. Na kazi ya ulinzi mara nyingi ni ya nchi host, walinzi wetu wanakuwa kama likizo vile na kuwasaidia wenyeji kwa mambo ya kimila ya raisi wenu.
 
Niliwahi kuisoma habari hii humu JF -- kuna mwanaJF mmoja aliigusia wakati anachangia mada moja kuhusu thread moja kuhusu RA.

Lakini kama ni kweli tukio hilo inashangaza kuona security inayomzunguka JK imelala, -- yaani itakuwaje mtu asafiri hadi nchi za nje kumfuatilia Rais, akafikia hoteli hiyo hiyo aliyofikia -- na pengine floor hiyo hiyo. Je ingekuwa ni mtu tu mwenye nia ya kumdhuru?

Hili la mafisadi kuwafuata viongozi nchi za nje kwenda kukutana nao nimeshalisikia sana maana wanaogopa kukutana nao nyumbani ili wasiripotiwe na vyombo vya habari. Lakini ni inafiki tu wa Kikwete kukataa kukutana naye wakati huo huo ameshindwa kumchukulia hatua zozote zile kutokana na ufisadi mkubwa amabo papa fisadi Rostam anahusika nao ikiwemo ule wa Richmond/Dowans.
 
Pamoja na ukweli kwamba RA yumo katika CCM-NEC na kamati Kuu, inawezekana anashindwa kuonana na JK, kwani huenda JK ameamua kujiweka mbali na maswahiba wake. Inawezekana washauri wake JK na watu wengine wamemwambia ni vyema akafanya hivyo -- angalau kwa sasa ktk kipindi hiki kigumu kwake (na kwa RA pia).

Nadhani huwa inafikia mahala ambapo mtu anaweza kumtosa swahiba wake, iwapo ataona ni usalama kwake kufanya hivyo. After all JK is President, tusisahau hilo, na ana kila aina ya uwezo, akitaka, kuhakikisha hapati embarrassments kutoka kwa RA, au kwa kiumbe chochote kilicho chini ya himaya yake.

The bottom line, au ninachotaka kusema ni kwamba huenda JK kafikia mahali hapo, yaani mtu mmoja tu -- pamoja kwamba ni swahiba wake, aweze kumshikilia at ransom na kujaribu kum-blackmail kiasi hata cha kuharibu urais wake na kumfanya asiufurahie.

Lakini pia nakubaliana na mwana JF aliyesema inawezekana RA alifikiri ingekuwa rahisi kukutana na JK nje ya nchi, mbali na macho, masikio na midomo-midomo ya wana-Bongo -- mkutano ambao JK aligoma kwa sababu nilizotaja hapo juu.

Lakini inawezekana vilevile RA alitaka kumuona JK kuhusu tuhuma zake za ufisadi -- labda Kagoda -- kwani inasemekana ni mojawapo ya kesi ambazo Hosea alitangaza mwezi uliopita kuwa za kutetemesha nchi na kwamba zingetinga mahakamani mwezi huu (June).

Huenda RA alitaka hata nusu dakika tu ya kumwambia JK: "Swahiba, unajua tulikotoka na yote tuliyofanya -- hivyo iwapo utaamua kunifanyia unachotaka kufanya, basi uelewe nami nitajua la kufanya." Angalau JK aipate tu hiyo tahadhari.
 
King Maker ndio waliosaidia kushinda kwa CCM mwaka 2005 na hivyo bado ni mdau mkubwa sana wa kisiasa
 
King Maker ndio waliosaidia kushinda kwa CCM mwaka 2005 na hivyo bado ni mdau mkubwa sana wa kisiasa

Huo ndiyo ukweli na Kikwete anajua fika kwamba Rostam ana data zote za uchafu na ufisadi uliofanyiak ili kuhakikisha anaingia Ikulu 2005 na akimkorofisha RA tu basi anaweza kuanika uchafu wote hadharani hapo ndiyo nchi itawaka moto.
 
Huo ndiyo ukweli na Kikwete anajua fika kwamba Rostam ana data zote za uchafu na ufisadi uliofanyiak ili kuhakikisha anaingia Ikulu 2005 na akimkorofisha RA tu basi anaweza kuanika uchafu wote hadharani hapo ndiyo nchi itawaka moto.

Mkuu unampa RA prominence asiyistahili.Ubavu wa kufanya hivyo atautoa wapi?
 
Back
Top Bottom