Kikwete amka au unakwenda na maji
TATIZO la rais wetu mpendwa ni kujisahau na kuwaachia maofisa wa Ikulu kuendesha nchi.
Inaeleweka tena sana kuwa ni aina ya watu gani tuliokuwa nao pale Ikulu. Sio watu wanaona mbali wala wenye kuaminika kwa maana baadhi yao walikwishawauza wenzao katika biashara walizokuwa wakifanya pamoja.
Maamuzi ndio uongozi
Inavyoelekea sasa ni kwamba kuna 'paralysis' ya serikali katika masuala mbalimbali ambayo wananchi wamesubiri mpaka wamechoka kuona kama kuna maamuzi ya maana yatafanyika. Lakini hadi wa leo hayajafanyika.
Wakati Evo Morales katika kipindi cha chini ya miaka mitatu amefanya maajabu makubwa huko Bolivia bila kugwaya mahakama au nchi kubwa sivyo alivyo kiongozi wetu. Anaota matende hadi pale ambapo kila kitu kiko wazi kwamba lazima yeye abaki au sheria fulani iende.
Tukio la hivi karibuni la silaha kuuzwa kwa waasi Kongo ni kielelezo tosha kuwa katika serikali kuna serikali nyingine ambayo Kikwete haijui na hana mamlaka nayo kabisa. Na haya ni matokeo ya kuwashirikisha maswahiba wa Muairishi Nolan na wale Maburushi waliokubuhu kwa uroho wa fedha na maisha ya anasa kwa kutumia wajinga waliomo serikalini mwetu. Ninasema wajinga kwa makusudi kwa kuwa ni ukweli usiofichika kwamba Wanasiasa hawajui kabisa kutengeneza fedha ila wanajua kuzitumia. Na pale wanapoishiwa kabisa watu kama hao hapo juu huwatumia jinsi wapendavyo. Maaana wanasiasa wetu au viongozi wetu huweza kuwapa dili la bilioni moja wao wakatengneza bilioni 10 na bado wakakiachia chama hako kabilioni tu. Bilioni 9 wanaziswaga wao wenyewe.
Mfumo huu wa kutumia NJIA ZA PANYA katika kupata fedha kwa ajili ya chama na uchaguzi ndio uliotufikisha hapa. Tukitaka tutoke huko lazima kila kitu kifanyike juu ya meza.
Jamaa wa Ikulu na watumishi kadhaa katika wizara wameamua kujichukulia mamlaka wao wenyewe ama kwa kuamua au kutoamua juu ya chochote.
Inavyoelekea kuna mtu hapo Ikulu keshatangaza vita dhidi ya mtu yeyote anayeamua na kutekeleza jambo bila idhini yao na sio ya rais. Na rais inavyoelekea hajui kinachoendelea.
Kwa maneno mengine rais hana udhibiti wowote wa wale walio chini yake achilia mbali serikali yake katika mikoa 26 ya Tanzania.
Nchi inajiendesha yenyewe au inaendeshwa na wajanja wachache. Na hili linatutia wasiwasi kwamba njama za wasiomtaka Kikwete zinaweza kufanikiwa. Njama hizo ni zile za kuhonga wajumbe wote wa mkutano mkuu Tanzania nzima kumpigia kura mtu mwingine zaidi ya Kikwete. Na hivi sasa makundi ndani ya Vijana, Wazazi, wajumbe wa mkutano mkuu na wazee wa chama yameanza kujiuza kwa wenye bahasha kubwa tayari kuifanya kazi hiyo ambayo hatima yake ni ile ya jina la Kikwete kutorudi kati ya wagombea tano watarajiwa kwa tiketi ya CCM hapo mwakani.
Huyu Katibu Mkuu anayeropoka ovyo naye ni tatizo kwa chama. Hivi kweli kuna kiongozi anayeweza kusema kuwa kuna mtu fulani ni mkubwa zaidi kuliko chama au serikali ? Akili zake huyu ni sawa. Labda kwa kiongozi ambaye hataugua wala hatakufa. Lakini sio kwa viumbe hawa tunaowajua.
Makamba ni Liability kwa CCM. Na jinsi wanavyochelewa kumtosa ndivyo atakavyosababisha hasara kubwa zaidi kwa chama.
Rais anahitaji kuvuta hatua moja nyuma na kutafuta watu wasio karibu naye lakini wanaojua kinachoendelea katika nchi hii na wenye uchungu wa hasara uongozi mbovu unaosababishia nchi na mapenzi ya kuwaona Watanzania hawaendelei kubeba misalaba isiyo ya lazima ili kunufaisha mafisadi na viongozi walioiuza nchi huko nyuma.
Kubwa zaidi ni kwamba rais muoga wa mwamuzi, kilio kitamuumbua. Rais kuonekana kweli rais budi afanye maamuzi ambayo kila mtu anategemea yafanyike. Huu si wakati wa kujificha nyuma ya utawala wa sheria au ushahidi uliokamilika -maana kama ndivyo basi hiyo itakuwa kama sheria ya Kiislamu ambapo watu zaidi ya wawili wanahitajika kuona kabisa tendo la kuzini likifanyika ili mkeo au mmeo asemekane ana kosa la kuzini nje ya ndoa. Sahau kabisa hilo kutokea.
Aidha, staili ya uongozi wa Kikwete ni mbaya, mbaya kabisa. Huwezi kufanya kazi zote. Pengine hii inachangia kushikwa kisunzi na kuzirai majukwaani. Gawa madaraka mzee. Na hakikisha unaowagawia madaraka wanawajibika ipasavyo. Si wanakula kodi ya wananchi. Anayeshindwa atakuwa kashindwa na kujifukuzisha kazi mwenyewe. Sasa mzee masuala ya barabara na miundo mbinu ikiwe ni wewe, michezo ikiwa ni wewe, shule ikiwa ni wewe, albino ikiwa ni wewe, trafiki na ubabaishaji barabarani ikiwa ni wewe, nje ikiwa ni wewe, mikoani ikiwa ni wewe basi kweli kuna kitu kitafanyiaka hapo au ni kurashiarashia tu?
Kuna wizara au sio. Miundo mbinu tupate habari za barabara na tujue kinachoendelea. Afya nako tupate taarifa na tuone kazi inayofanyika. Tumsikie Waziri anayehusika na michezo na programu yake ya kuhakikisha kila kata ina stadium Tanzania au hilo ananyimwa kufanya. Tusikie Madini na nIshati wanavyowawezesha wachimba migodi wazawa kuwekeza katika uchimbaji madini na kadhalika.
Katika miaka hii ya TEKNOHAMA ni rahisi kabisa kujua kila kinachoendelea katika kila mkoa na wilaya, kila wizara na idara na kila ubalozi na wakala wa Kimataifa Mtanzania alioko. Na kwa utawala wa Management by Exception wawakilishi husika watakupa kile unachohitaji tu na sio cha kukusumbua kichwa. Waoneni wataalamu muwatumie, lakini sio kwa tamaa yenu ya fedha za wananchi na ukubwa wa ofisi ya ikulu na mawizara kula na kunywa tu halafu kutuharibia maisha yetu Watanzania ndio iwe asante yenu.
Haya nalo hilo Kongamano la Nyerere -limefanyiak kwa ajili ya kumsuta na kumuaibisha Kikwete au kumshauri na kumsaidia ili ajue kile kinachotakikakana kufanyika. Pengine masikini aliutaka urais kwa mteremko lakini kakuta sasa ni kupanda jilima hasa jilima zaidi ya Eversts niini Kilimanjaro!! Pole mjomba ushauri wangu ni huu. Lazima udhibiti serikali yako. Huwezi kuwa na usalama wa Taifa wanaowapelekea taarifa marais na mawaziri wakuu wa zamani na wewe ukasema kweli uko kwenye kiti cha udereva wa nchi hii.
TATIZO la rais wetu mpendwa ni kujisahau na kuwaachia maofisa wa Ikulu kuendesha nchi.
Inaeleweka tena sana kuwa ni aina ya watu gani tuliokuwa nao pale Ikulu. Sio watu wanaona mbali wala wenye kuaminika kwa maana baadhi yao walikwishawauza wenzao katika biashara walizokuwa wakifanya pamoja.
Maamuzi ndio uongozi
Inavyoelekea sasa ni kwamba kuna 'paralysis' ya serikali katika masuala mbalimbali ambayo wananchi wamesubiri mpaka wamechoka kuona kama kuna maamuzi ya maana yatafanyika. Lakini hadi wa leo hayajafanyika.
Wakati Evo Morales katika kipindi cha chini ya miaka mitatu amefanya maajabu makubwa huko Bolivia bila kugwaya mahakama au nchi kubwa sivyo alivyo kiongozi wetu. Anaota matende hadi pale ambapo kila kitu kiko wazi kwamba lazima yeye abaki au sheria fulani iende.
Tukio la hivi karibuni la silaha kuuzwa kwa waasi Kongo ni kielelezo tosha kuwa katika serikali kuna serikali nyingine ambayo Kikwete haijui na hana mamlaka nayo kabisa. Na haya ni matokeo ya kuwashirikisha maswahiba wa Muairishi Nolan na wale Maburushi waliokubuhu kwa uroho wa fedha na maisha ya anasa kwa kutumia wajinga waliomo serikalini mwetu. Ninasema wajinga kwa makusudi kwa kuwa ni ukweli usiofichika kwamba Wanasiasa hawajui kabisa kutengeneza fedha ila wanajua kuzitumia. Na pale wanapoishiwa kabisa watu kama hao hapo juu huwatumia jinsi wapendavyo. Maaana wanasiasa wetu au viongozi wetu huweza kuwapa dili la bilioni moja wao wakatengneza bilioni 10 na bado wakakiachia chama hako kabilioni tu. Bilioni 9 wanaziswaga wao wenyewe.
Mfumo huu wa kutumia NJIA ZA PANYA katika kupata fedha kwa ajili ya chama na uchaguzi ndio uliotufikisha hapa. Tukitaka tutoke huko lazima kila kitu kifanyike juu ya meza.
Jamaa wa Ikulu na watumishi kadhaa katika wizara wameamua kujichukulia mamlaka wao wenyewe ama kwa kuamua au kutoamua juu ya chochote.
Inavyoelekea kuna mtu hapo Ikulu keshatangaza vita dhidi ya mtu yeyote anayeamua na kutekeleza jambo bila idhini yao na sio ya rais. Na rais inavyoelekea hajui kinachoendelea.
Kwa maneno mengine rais hana udhibiti wowote wa wale walio chini yake achilia mbali serikali yake katika mikoa 26 ya Tanzania.
Nchi inajiendesha yenyewe au inaendeshwa na wajanja wachache. Na hili linatutia wasiwasi kwamba njama za wasiomtaka Kikwete zinaweza kufanikiwa. Njama hizo ni zile za kuhonga wajumbe wote wa mkutano mkuu Tanzania nzima kumpigia kura mtu mwingine zaidi ya Kikwete. Na hivi sasa makundi ndani ya Vijana, Wazazi, wajumbe wa mkutano mkuu na wazee wa chama yameanza kujiuza kwa wenye bahasha kubwa tayari kuifanya kazi hiyo ambayo hatima yake ni ile ya jina la Kikwete kutorudi kati ya wagombea tano watarajiwa kwa tiketi ya CCM hapo mwakani.
Huyu Katibu Mkuu anayeropoka ovyo naye ni tatizo kwa chama. Hivi kweli kuna kiongozi anayeweza kusema kuwa kuna mtu fulani ni mkubwa zaidi kuliko chama au serikali ? Akili zake huyu ni sawa. Labda kwa kiongozi ambaye hataugua wala hatakufa. Lakini sio kwa viumbe hawa tunaowajua.
Makamba ni Liability kwa CCM. Na jinsi wanavyochelewa kumtosa ndivyo atakavyosababisha hasara kubwa zaidi kwa chama.
Rais anahitaji kuvuta hatua moja nyuma na kutafuta watu wasio karibu naye lakini wanaojua kinachoendelea katika nchi hii na wenye uchungu wa hasara uongozi mbovu unaosababishia nchi na mapenzi ya kuwaona Watanzania hawaendelei kubeba misalaba isiyo ya lazima ili kunufaisha mafisadi na viongozi walioiuza nchi huko nyuma.
Kubwa zaidi ni kwamba rais muoga wa mwamuzi, kilio kitamuumbua. Rais kuonekana kweli rais budi afanye maamuzi ambayo kila mtu anategemea yafanyike. Huu si wakati wa kujificha nyuma ya utawala wa sheria au ushahidi uliokamilika -maana kama ndivyo basi hiyo itakuwa kama sheria ya Kiislamu ambapo watu zaidi ya wawili wanahitajika kuona kabisa tendo la kuzini likifanyika ili mkeo au mmeo asemekane ana kosa la kuzini nje ya ndoa. Sahau kabisa hilo kutokea.
Aidha, staili ya uongozi wa Kikwete ni mbaya, mbaya kabisa. Huwezi kufanya kazi zote. Pengine hii inachangia kushikwa kisunzi na kuzirai majukwaani. Gawa madaraka mzee. Na hakikisha unaowagawia madaraka wanawajibika ipasavyo. Si wanakula kodi ya wananchi. Anayeshindwa atakuwa kashindwa na kujifukuzisha kazi mwenyewe. Sasa mzee masuala ya barabara na miundo mbinu ikiwe ni wewe, michezo ikiwa ni wewe, shule ikiwa ni wewe, albino ikiwa ni wewe, trafiki na ubabaishaji barabarani ikiwa ni wewe, nje ikiwa ni wewe, mikoani ikiwa ni wewe basi kweli kuna kitu kitafanyiaka hapo au ni kurashiarashia tu?
Kuna wizara au sio. Miundo mbinu tupate habari za barabara na tujue kinachoendelea. Afya nako tupate taarifa na tuone kazi inayofanyika. Tumsikie Waziri anayehusika na michezo na programu yake ya kuhakikisha kila kata ina stadium Tanzania au hilo ananyimwa kufanya. Tusikie Madini na nIshati wanavyowawezesha wachimba migodi wazawa kuwekeza katika uchimbaji madini na kadhalika.
Katika miaka hii ya TEKNOHAMA ni rahisi kabisa kujua kila kinachoendelea katika kila mkoa na wilaya, kila wizara na idara na kila ubalozi na wakala wa Kimataifa Mtanzania alioko. Na kwa utawala wa Management by Exception wawakilishi husika watakupa kile unachohitaji tu na sio cha kukusumbua kichwa. Waoneni wataalamu muwatumie, lakini sio kwa tamaa yenu ya fedha za wananchi na ukubwa wa ofisi ya ikulu na mawizara kula na kunywa tu halafu kutuharibia maisha yetu Watanzania ndio iwe asante yenu.
Haya nalo hilo Kongamano la Nyerere -limefanyiak kwa ajili ya kumsuta na kumuaibisha Kikwete au kumshauri na kumsaidia ili ajue kile kinachotakikakana kufanyika. Pengine masikini aliutaka urais kwa mteremko lakini kakuta sasa ni kupanda jilima hasa jilima zaidi ya Eversts niini Kilimanjaro!! Pole mjomba ushauri wangu ni huu. Lazima udhibiti serikali yako. Huwezi kuwa na usalama wa Taifa wanaowapelekea taarifa marais na mawaziri wakuu wa zamani na wewe ukasema kweli uko kwenye kiti cha udereva wa nchi hii.