BabuK
JF-Expert Member
- Jul 30, 2008
- 1,845
- 329
MFUKO wa Bill na Melinda Gates utaendelea kuisaidia Tanzania katika masuala mbalimbali ya Utafiti katika sekta za afya na kilimo.
Tuko tayari kuendelea kuisaidia Tanzania kama mtatupa vipaumbele vyenu, Mwenyekiti
mwenza wa Mfuko wa Bill na Melinda Gates, Bill Gates alimwambia Rais Kikwete jana
mchana alipofika Ikulu kumsalimia.
Rais Kikwete amemshukuru Gates na mkewe Melinda kwa msaada wao mkubwa wanaoupatia
Tanzania.
Gates, ambaye ni tajiri mkubwa duniani na mkewe Melinda, wapo nchini kwa ziara binafsi ya kifamilia na wametembelea mbuga za Serengeti na shughuli nyingine za kikazi, ikiwemo kukagua miradi ya Mfuko huo iliyopo nchini.
Tayari wametembelea Kituo cha Utafiti na Mafunzo katika Hospitali ya Bagamoyo mkoani Pwani, ambacho ni sehemu ya Kituo cha Utafiti cha Ifakara kilichoko Morogoro na Kituo cha Serikali cha Utafiti wa Kilimo cha Mikocheni (MARI) vinavyosaidiwa
na Mfuko huo.
Kituo cha Bagamoyo kinatafuta kinga ya malaria wakati kituo cha Mikocheni kinatafuta chanzo cha ugonjwa wa muhogo.
Wakati huo huo, Rais Kikwete anaondoka leo mchana kwenda Malabo, Equatorial Guinea kuhudhuria kikao cha kila mwaka cha wakuu wa nchi za Afrika, chini ya Uenyekiti wa Rais Teodoro Mbasogo.
Mada kuu ya kikao cha mwaka huu ni Uwezeshaji wa Vijana kwa ajili ya Maendeleo.
Rais Kikwete anatarajiwa kurejea nchini Julai 2, na Julai 3 atakuwa mgeni rasmi katika Siku ya Washirika wa Tumbaku mkoani Kagera.
Julai 4, Rais Kikwete ataongoza sherehe za ufunguzi rasmi wa barabara ya Mwandiga-Manyovu, uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Kidahwe-Uvinza na pia atazindua ujenzi wa daraja la Malagarasi.
Source: HABARILEO
Tuko tayari kuendelea kuisaidia Tanzania kama mtatupa vipaumbele vyenu, Mwenyekiti
mwenza wa Mfuko wa Bill na Melinda Gates, Bill Gates alimwambia Rais Kikwete jana
mchana alipofika Ikulu kumsalimia.
Rais Kikwete amemshukuru Gates na mkewe Melinda kwa msaada wao mkubwa wanaoupatia
Tanzania.
Gates, ambaye ni tajiri mkubwa duniani na mkewe Melinda, wapo nchini kwa ziara binafsi ya kifamilia na wametembelea mbuga za Serengeti na shughuli nyingine za kikazi, ikiwemo kukagua miradi ya Mfuko huo iliyopo nchini.
Tayari wametembelea Kituo cha Utafiti na Mafunzo katika Hospitali ya Bagamoyo mkoani Pwani, ambacho ni sehemu ya Kituo cha Utafiti cha Ifakara kilichoko Morogoro na Kituo cha Serikali cha Utafiti wa Kilimo cha Mikocheni (MARI) vinavyosaidiwa
na Mfuko huo.
Kituo cha Bagamoyo kinatafuta kinga ya malaria wakati kituo cha Mikocheni kinatafuta chanzo cha ugonjwa wa muhogo.
Wakati huo huo, Rais Kikwete anaondoka leo mchana kwenda Malabo, Equatorial Guinea kuhudhuria kikao cha kila mwaka cha wakuu wa nchi za Afrika, chini ya Uenyekiti wa Rais Teodoro Mbasogo.
Mada kuu ya kikao cha mwaka huu ni Uwezeshaji wa Vijana kwa ajili ya Maendeleo.
Rais Kikwete anatarajiwa kurejea nchini Julai 2, na Julai 3 atakuwa mgeni rasmi katika Siku ya Washirika wa Tumbaku mkoani Kagera.
Julai 4, Rais Kikwete ataongoza sherehe za ufunguzi rasmi wa barabara ya Mwandiga-Manyovu, uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Kidahwe-Uvinza na pia atazindua ujenzi wa daraja la Malagarasi.
Source: HABARILEO