Kikwete akubali kukutana na CHADEMA

Hakika usemi huu umetimia "mtoto akikunyea mkono hautakiwi kuukata na badala yake unausafisha na maji". Si kitu cha ajabu kuona mtoto wako uliyemzaa anajaribu kujitutumua huku akijua fika kuwa wewe ndiye Baba yake, CHADEMA ni kama mtoto aliyepotoka na Sasa ametambua ya kwamba alifanya makosa na sasa anarudi nyumbani ili kuanza maisha mapya. Kwa maana hii Baba hana sababu ya kukataa kumkaribisha nyumbani kwa kuwa si yule tena aliyepotoka bali ni mtoto mwingine.

Umuhimu wa Baba kukubali kumpokea mtoto wake aliyeshindikana unatokana na mambo mengi, Mtoto huweza kubadilika tabia kutokana na makundi yanayomzunguka na hivyo kujikuta akifanya vitu visivyotarajiwa na hususani kile kipindi cha "Barehe" au anapopevuka na hivyo kuanza kujiona yeye ndiye yeye au inawezekana alikwisha pevuka lakini kwa bahati mbaya mawazo ya maisha yake ni ya utegemezi toka kwa wengine na hivyo siku zote ataendelea kuwa na mawazo tegemezi, hii ni sawa na kusema "TUMEAMBIWA NA MBOWE TOTOKE NJE YA BUNGE " lakini mtoto hapati nafasi ya kujiuliza na hata kama akipata nafasi hana uwezo wa kujua la kutenda au kutafakari kwa kina, Kwa hatua hii mtoto anahitaji maombi pekee toka ndugu zetu wakristu au dua kwa ndugu zetu wa kiislamu.

Nimatumani yangu maombi kwa njia ya sala au dua limeanza kufanya kazi au kipindi cha "Barehe" cha kujifanya mjuaji kimepita na sasa mtoto ametambua makosa aliyoyafanya na sasa anasema "BABA NARUDI NYUMBANI".

HONGERA MWENYEKITI WA CCM TAIFA.
Sio tatizo sana. Umeandika kwanza halafu baadae utafikiri ulichokiandika
 
Let us think positively. Tuamini kuwa ana nia njema mpaka hapo itakapodhihirika vinginevyo. Tukumbuke kuwa Rais JK amekuwa na mtazamo tofauti na viongozi wenzake ndani ya serikali na CCM kuhusiana na katiba toka mwanzo. Sijawahi kuwa shabiki wa JK, na ninaamini amefanya makosa mengi katika utawala wake LAKINI kwa uamuzi huu nampongeza kwa moyo wangu wa dhati. Tusimchukie JK kwa vile tumeamua kumchukia au kwa kufikiria kuwa hawezi kufanya jambo jema, tumlaumu alipokosea na tumpongeze na kumpa nguvu pale anapofanya vema. Pale anapofanya vema, naomba tumpongeza, la sivyo tutamkatisha tamaa na kuona kuwa hakuna chochote anachoweza kufanya hata kama ni kwa matakwa yetu, tukakikubali.


KWENYE HILI NAMPONGEZA JK. Akifanikiwa kusimamia mchakato wa katiba, ukaenda vizuri, tukapata katiba nzuri, hakika hiyo itatosha kufuta makosa yake yote. Matatizo mengi ambayo nchi hii imepitia chanzo chake ni katiba tuliyo nayo, na hakika tuna bahati kwa kutokupigana kutokana na katiba hii.

Wachangiaji amabao wameonyesha wasiwasi sio kwamba wana prejudiced mind na JK bali wanakumbuka jinsi alivyokuwa mwepesi wa kusema hili leo na kesho akasema jingine linalopingana na alilosema jana na hivyo dhana ya rais ni taasisi inakosa maaana. Nikukumbushe matukio machache ambayo yanatia shaka kauli na maamuzi yake. Ukwapuaji wa pesa ya EPA ulipodhihili akalitangazia Taifa kuunda tume na baadae akaenda kuutubia bunge akitumia maneno niliagiza kama mara mia moja kidogo. Badala ya kuwashtaki watuumiwa na pesa kurudishwa pamoja na riba akaagiza watu warudishe hiyo pesa. Mpaka leo hizo pesa zimekuwa kitendawili.

Kashifa ya Richmond/Dowans na Symbion. Ushiriki wa rais na kauli zake kinzani vinawafanya watanzania wawe na shaka na jk. Kwanza nafikiri inapokuja sifa anataka apewe kama JK na sio kama rais na linapokuja swala la lawama anataka watu watambue taasisi.Angekuwa anatanguliza taasisi mbele ktk kauli na maamuzi yake watu wasingekuwa na shaka. Na watanzania wengi wameangukia hapo hivi leo urais umekuwa ni hulka na haiba kuliko taasisi.

Si hilo tu safari za rais nje ya nchi zimepigiwa sana kelele kulinganisha na kile tunachopata. Ni jk yuleyule anayamua kuwakejeli watanzania kuwa asiposafiri tutkula mchicha. Hivi linganisha ukuaji wa uchumi na usimamizi wa raslimali tuzokuwanazo na uchangiaji wa uwekezaji ktk pato la taifa ukilinganisha na nchi jirani. Sisi tuko nyuma na tunazidi kurudi nyuma
 
Unaweza kuwa Rais wa wote kwa kutumia mabavu,udikteta na ubabe kama anavyofanya Rais Kiwete!

Ni lazima Kiwete akubali kukutana na CHADEMA maana wana mambo ya msingi wanayoyasimamia na yanakubalika kwa Watanzania walio wengi. Lazima ajue kuwa HATUKO KUUNDA KATIBA YA CCM BAALI YA WATANZANIA WOTE. Nafikiri Kiwete sasa ameanza kuona kuwa MAJI YANAANZA KUZIDI UNGA na lazima akae meza moja na upinzani ili asikie NGUVU ZA HOJA ZA CHADEMA na si HOJA ZA NGUVU za wabunge wa CCM wanaotaka kuwaburuza Watz.

Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana unaonyesha kuwa Kiwete alipata kura 5.2m kati ya Watanzania takribani milioni 45. Sasa wasemaje ni Rais wa wote?Ndani ya CCM yenyewe Kiwete kwa sasa hatakiwi halafu wewe unadanganya watu kuwa ni Rais wa wote,acha hizo mama.

Kiwete wako anatakiwa akubaliane na CHADEMA vile wanavyoona inafaa kuhusu mchakato wa Katiba Mpya. Si CHADEMA tu baali hata makundi mengi ya wanaharakati na Watanzania wasio na vyama hawajakubaliana na namna Bunge la CCM linavyotaka KUWABURUZA Watanzania kuhusiana na mchakato wa upatikanaji wa Katiba Mpya.

Kiwete na CCM yake lazima wasome alama za nyakati. Wasifikiri Tanzania ya sasa ni ile ya enzi za Mwalimu Nyerere ya CHAMA KIMOJA kwenye miaka ya 1960s. Huo jinga na upuuzi hauna nafasi kwa Tanzania na Dunia ya sasa.
Kila mtu anafahamu kwamba CCM na Kiwete wao wanataka kulazimisha mchakato uendelee kama wanavyotaka wao ILI WAENDELEE KUBAKIA MADARAKANI NA KUITAWALA TANZANIA MILELE KWA KUTUMIA KATIBA MBOVU ILIYOPO AMBAYO INAYOWALINDA.

Kiwete lazima akubali ili yaishe. Vinginevyo yeye na CCM yake watapambana na NGUVU YA UMMA WA WATANZANIA na siyo CDM.

Wewe kuna mtu atakuwa ameshikilia remote ya kichwa chako!! Unaongea pumba tupu. Kuna CUF, NCCR-MAGEUZI, CCM, SAU na vingine vingi, sasa nguvu ya umma iko chadema pekee yake? Je vyama vingine vinakubaliana na anayotaka Chadema?
 
Wachangiaji amabao wameonyesha wasiwasi sio kwamba wana prejudiced mind na JK bali wanakumbuka jinsi alivyokuwa mwepesi wa kusema hili leo na kesho akasema jingine linalopingana na alilosema jana na hivyo dhana ya rais ni taasisi inakosa maaana. Nikukumbushe matukio machache ambayo yanatia shaka kauli na maamuzi yake. Ukwapuaji wa pesa ya EPA ulipodhihili akalitangazia Taifa kuunda tume na baadae akaenda kuutubia bunge akitumia maneno niliagiza kama mara mia moja kidogo. Badala ya kuwashtaki watuumiwa na pesa kurudishwa pamoja na riba akaagiza watu warudishe hiyo pesa. Mpaka leo hizo pesa zimekuwa kitendawili.

Kashifa ya Richmond/Dowans na Symbion. Ushiriki wa rais na kauli zake kinzani vinawafanya watanzania wawe na shaka na jk. Kwanza nafikiri inapokuja sifa anataka apewe kama JK na sio kama rais na linapokuja swala la lawama anataka watu watambue taasisi.Angekuwa anatanguliza taasisi mbele ktk kauli na maamuzi yake watu wasingekuwa na shaka. Na watanzania wengi wameangukia hapo hivi leo urais umekuwa ni hulka na haiba kuliko taasisi.

Si hilo tu safari za rais nje ya nchi zimepigiwa sana kelele kulinganisha na kile tunachopata. Ni jk yuleyule anayamua kuwakejeli watanzania kuwa asiposafiri tutkula mchicha. Hivi linganisha ukuaji wa uchumi na usimamizi wa raslimali tuzokuwanazo na uchangiaji wa uwekezaji ktk pato la taifa ukilinganisha na nchi jirani. Sisi tuko nyuma na tunazidi kurudi nyuma

Baba wa Taifa hili,Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alikuwa na hekima na kipawa cha ajabu sana cha uongozi. Sina hakika kama Tanzania itakuja pata kiongozi mahiri kama huyo aliyekuwa na upeo wa kuona mbali na kusoma alama za nyakati.

Tangu aage dunia Baba wa Taifa,CCM kimebakia magamba tu! Napenda nirejee KAULI YA MWALIMU ALIPOKUWA AKIONGEA NA WAZEE WA DSM na akasema maneno yafuatayo: ''HATUTAKI TUCHAGUE RAIS AENDE IKULU AMBAYE ATAKUWA AKISHAURIWA NA MKEWE,HATUTAJUA KESHO ATASEMA NINI''.

Rais Kiwete amedhihirisha kuwa ni moja ya Marais waliowahi kuiongoza Tanzania wanaofuata USHAURI WA WAKE ZAO. Hili liko wazi kabisa kwa Watu wenye akili zinazofikiri kwa kutumia BONGO na siyo MASABURI. Ni dhahiri kabisa Kiwete anaongoza Nchi hii kwa kufuata ushauri wa mkewe ndiyo maana ANAPWAYA SANA KWENYE OFISI YA URAIS! Matatizo yote tunayoyapata Watanzania kwa sasa yanatokana na USHAURI MBOVU ANAOPEWA KIWETE NA MAMA KIWETE WANAPOKUWA CHUMBANI USIKU NA NDIYO MAANA WATANZANIA TUNAKUWA HATUNA UHAKIKA NA KILE RAIS WETU ATATUAMBIA KESHO!!!!Hili liko wazi na kuna mifano ya matukio mengi tu ambayo yametokea chini ya utawala wa huyu Bwana yanayoonyesha kuwa anashauriwa na mkewe!

Hata kile kijembe cha Edward Lowassa cha kusema kuwa SERIKALI INAOGOPA KUCHUKUA MAAMUZI MAGUMU kilikuwa kinamlenga rafiki wake wa zamani J,Kiwete kuwa hawezi kuchukua maamuzi magumu kwa vile anapenda sana kusikiliza ushauri wa First Lady! Ukweli unauma lakini lazima tuuseme.
 
Wewe kuna mtu atakuwa ameshikilia remote ya kichwa chako!! Unaongea pumba tupu. Kuna CUF, NCCR-MAGEUZI, CCM, SAU na vingine vingi, sasa nguvu ya umma iko chadema pekee yake? Je vyama vingine vinakubaliana na anayotaka Chadema?

damper,

Try to think critically before you spit your garbages!

Sentensi yangu ya mwisho inasema hivi,''Kiwete lazima akubali ili yaishe. Vinginevyo yeye na CCM yake watapambana na NGUVU YA UMMA WA WATANZANIA na siyo CDM.''

Just for your info, NGUVU YA CHADEMA HAIKO CHADEMA IKO KWA WANANCHI WA TANZANIA. Swali lako kuwa ati nguvu ya Umma iko Chadema pekee ni la kijinga kabisa! Mijitu ya CCM itaijua tu namna inavyofikiri na kuzungumza. Ni uharo mtupu!Wewe inaonekana unafikiri kwa kutumia masaburi na hiyo remote unayodai inaonekana ya kwako ndo IMESHIKILIWA na Chama chako cha Magamba-CCM ndiyo maana unaongea upuuzi.

Kumbuka kuwa NCCR-Mageuzi waliungana na CHADEMA kutoka Bungeni katika kupinga upitishwaji wa mswada fake wa Katiba mpya yenye kutaka kukidhi matakwa ya CCM.Tunajua CUF wana NDOA na CCM na waliunga mkono hoja kwa 100pc. Naona umetaja SAU,sijui na vyama vingine. Je SAU na hao wengine wana mbunge wapi katika nchi hii???? CHADEMA ndiyo chama kiongozi wa upinzania Bungeni hili hata Rais wako Kiwete analijua ndiyo maana kakubali kukutana na wanaume wa shoka!Nyambaf.
 
Jukwaa la katiba gani?! Lilelile linaloamua kufanya maigizo au lingine?! Eti wanaiomba Brass Band ya polisi isindikize maandamano yao; kama sio maigizo niite nini wakati wanajuwa wanalolihitaji haliwezekani?! Sana sana tusubirie kusikia wameetangaza kuahirisha maandamano hadi wapate feedback ya kukutana kwa CDM na mkulu!!

jamani wanafiki chadema wanakwenda ikulu kupiga picha na mhe rais na yote njaa ya kula ugali na rais kumbe vurugu zote wanataka tu ilimladi wakale makombo nakukanyaga ikulu hii kali si ndo hawa walimkataa raisi leo amekuwa rais tena. Mh kazi kweli. Hawahawa wanajitia kuzila nakutoka bungeni huku wakizitamani pesa za bunge wazile kabisa kama wenzao Cuf nakupelekea kura za maruhani hawa hawa kuonesha unafika hawa kuingia bungeni kabisa cdm wananjaa huku wakitaka kuonesha wao wanaweza wanafiki hawa
 
Hivi Rais kukubali kukutana ni kuvyata..mm! nafikiri ni muungwana na ana busara

Hivi Rais awaogope chadema kwa lipi hasa?? JK haogopi hoja mkuu??

Kama kukutana na cdm ni uoga I beg to differ siyo kila kitu mnatafuta umaarufu.
Hivi kuna Rais TZ!!?? sidhani TZ kama pori la somalia. Afadhali somalia Alshabab hawatakubali ukavuna raslimali ka shamba la bibi TZ. OMBWE la uongozi limeanzia toka 2005.
 
From deep inside I have a feeling kuwa CDM wanajimaliza wenyewe kwa jiengage na JK aliyewananga vya kutosha siku ya mkutano wake na wazee. CCM itatumia ombi hili la CDM kuwafunga mikono.
 
nampongeza raisi JK kwa kukubali kukutana na viongozi wa cdm,ni kitu kizuri sana,rai yangu kwake atumie hekima na busara kusikiliza kilio cha wana chadema na watanzania kwa ujumla ili tupate mswaada wenye kuakisi mawazo na matakwa ya Tanzania swala la katiba sim la chama cha siasa ni la watanzania,hivyo tulifanye kwa umoja na mshikamano.pamoja tulijenge taifa letu
 
damper,

Try to think critically before you spit your garbages!

Sentensi yangu ya mwisho inasema hivi,''Kiwete lazima akubali ili yaishe. Vinginevyo yeye na CCM yake watapambana na NGUVU YA UMMA WA WATANZANIA na siyo CDM.''

Just for your info, NGUVU YA CHADEMA HAIKO CHADEMA IKO KWA WANANCHI WA TANZANIA. Swali lako kuwa ati nguvu ya Umma iko Chadema pekee ni la kijinga kabisa! Mijitu ya CCM itaijua tu namna inavyofikiri na kuzungumza. Ni uharo mtupu!Wewe inaonekana unafikiri kwa kutumia masaburi na hiyo remote unayodai inaonekana ya kwako ndo IMESHIKILIWA na Chama chako cha Magamba-CCM ndiyo maana unaongea upuuzi.

Kumbuka kuwa NCCR-Mageuzi waliungana na CHADEMA kutoka Bungeni katika kupinga upitishwaji wa mswada fake wa Katiba mpya yenye kutaka kukidhi matakwa ya CCM.Tunajua CUF wana NDOA na CCM na waliunga mkono hoja kwa 100pc. Naona umetaja SAU,sijui na vyama vingine. Je SAU na hao wengine wana mbunge wapi katika nchi hii???? CHADEMA ndiyo chama kiongozi wa upinzania Bungeni hili hata Rais wako Kiwete analijua ndiyo maana kakubali kukutana na wanaume wa shoka!Nyambaf.
Badooooo!! una kaarufu ka u chadema kama uamini jinuse
 
Chadema kukutana na CCM ni sawa na usiku kukutana na mchana, au Mungu kukatana na shetani. ccm haina mpango mwema na nchi yetu hata siku moja. Ni sawa kwenda kukutana na majambazi na kuwaomba watunge sheria ya kuzuia wizi...IMPOSSIBLE!
 
headline_bullet.jpg
Aagiza matayarisho mkutano yaanze



Mbowe(38).jpg

Mwenyekiti Taifa CHADEMA, Freeman Mbowe


Siku moja tu baada ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuunda kamati ya watu saba ili kukutana na Rais Jakaya Kikwete kuzungumzia Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011, ombi hilo limekubaliwa.

Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais kwa vyombo vya habari jana, ilisema kuwa Rais amelipokea ombi hilo kwa furaha kwa sababu ni jambo jema.

“Mheshimiwa Rais Kikwete amelipokea ombi hilo kwa furaha kwa sababu ni jambo jema,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo fupi yenye aya tatu na kuongeza:

“Kufuatia kukubali kwake ombi hilo, Mheshimiwa Rais ameagiza mawasiliano yafanyike ili kupanga tarehe mwafaka ya kukutana na viongozi hao wa Chadema na kuzungumzia suala hilo.”

Mwishoni mwa wiki Kamati Kuu ya Chadema iliyokutana jijini Dar es Salaam iliunda kamati ndogo ya watu saba, wakiongozwa na Mwenyekiti Taifa, Freeman Mbowe, kwa ajili ya kwenda kuzungumza na Rais Kikwete, kuhusiana na msimamo wa chama hicho juu ya kuboresha mchakato wa kupata Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Wajumbe wengine wanaounda kamati hiyo, ni Katibu Mkuu, Dk. Willibrod Slaa; Makamu Mwenyekiti Tanzania Bara, Said Amour Arfi; Makamu Mwenyekiti Zanzibar, Said Issa Mohammed; Profesa Mwesiga Baregu, Profesa Abdallah Safari na Tundu Lissu, ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki na Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.

Hatua ya kuundwa kwa kamati hiyo, ni miongoni mwa maazimio tisa yaliyofikiwa na Kamati Kuu ya chama hicho katika kikao chake maalum, kilichofanyika baada ya kususia mjadala wa muswada wa katiba mpya ulipotishwa na bunge wiki iliyopita mjini Dodoma.
Pamoja na mambo mengine, kikao hicho kilipokea na kujadili kwa kina taarifa ya majadiliano na kupitishwa kwa muswada huo na hatua za kuchukua.

Maazimio hayo yalisomwa na Mbowe alipozungumza na waandishi wa habari makao makuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam juzi.
Akisoma maazimio hayo, Mbowe, ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, alisema mazungumzo kati ya kamati hiyo

na Rais Kikwete, yanalenga kutaka kumpa msimamo, mawazo na ushauri wao namna ya kuuboresha mchakato huo.
“(Rais Kikwete) akisikiliza mawazo yetu, tutashiriki mchakato (wa kuandika Katiba mpya), akikataa tutakwenda kwa wananchi,” alisema

Mbowe, ambaye pia ni Mbunge wa Hai.
Alisema Kamati Kuu inaamini kuwa pamoja na sheria hiyo kupitishwa, bado kuna fursa za kisiasa na kijamii katika kujenga mwafaka wa kitaifa juu ya haja, nia, mchakato na misingi ya Katiba mpya.

Hata hivyo, alisema Kamati Kuu imeshangazwa na kusikitishwa na uamuzi wa Rais Kikwete wa kutozitumia fursa hizo na badala yake kujiingiza katika kile alichokiita “Jalala la taka za upotoshaji” uliofanywa na wabunge wa CCM juu ya misingi na maudhui ya sheria hiyo.
Alisema Kamati Kuu inaamini kwamba, badala ya kuwaunganisha Watanzania na kujenga mwafaka unaohitajika katika mchakato wa Katiba

mpya, hotuba ya Rais Kikwete kwa wazee wa CCM wa Mkoa wa Dar es Salaam ya Ijumaa wiki iliyopita, imezidi kuwagawa Watanzania kwa misingi ya ushabiki wa vyama badala ya kuwaunganisha kwa misingi ya utaifa.
Hata hivyo, Mbowe alisema Chadema itaendelea kutoa elimu kwa wananchi na wadau wote juu ya haja ya kuwa na sheria itakayoweka

utaratibu bora zaidi wa kuunda Tume Shirikishi ya Katiba kwa lengo la kukusanya maoni ya wananchi, kuandaa ripoti na rasimu ya Katiba mpya, Bunge Maalum la Katiba na usimamizi wa kura ya maoni itakayowezesha wananchi kufanya maamuzi kwa uhuru na kwa haki.
Alisema ushiriki wa Chadema katika mchakato wa kupata katiba mpya uliowekwa na sheria hiyo, utategemea utayari wa serikali kufanya mabadiliko makubwa na ya kimsingi katika sheria hiyo kwa lengo la kujenga muafaka wa kitaifa juu ya mchakato huo.



CHANZO: NIPASHE

 
Naomba kwa kuanza kwamba mi siyo mshabiki wa chama chochote.

Nilisikiliza kwa makini sana hotuba ya Kiongozi wa kambi ya upinzania bungeni Mr Freeman Mbowe
Alisema kwamba " Wameandaa kamati ndogo kwa ajili ya kwenda kumwona JK kama raisi wa Tanzania na si mwenyekiti wa chama tawala"
Maono yangu.
Ni lini walifuta zile kejeli zao za kusema kua kura zilichakachuliwa?
Wawe na tabia za kuwapa wananchi majibu ya migomo yao ili wananchi wajue kinachoendelea kwa maana hawajawahi kuja public na kutoa majibu ya ni lini walikubali kua JK ni raisi halali na sababu zilikua zipi? Hii itasaidia kujenga heshima na mshikamano ndani ya nchi na pia wananchi kupigania maendeleo zaidi ya migomo yao wanayohamasisha kila mara.
 
Naomba kwa kuanza kwamba mi siyo mshabiki wa chama chochote.

Nilisikiliza kwa makini sana hotuba ya Kiongozi wa kambi ya upinzania bungeni Mr Freeman Mbowe
Alisema kwamba " Wameandaa kamati ndogo kwa ajili ya kwenda kumwona JK kama raisi wa Tanzania na si mwenyekiti wa chama tawala"
Maono yangu.
Ni lini walifuta zile kejeli zao za kusema kua kura zilichakachuliwa?
Wawe na tabia za kuwapa wananchi majibu ya migomo yao ili wananchi wajue kinachoendelea kwa maana hawajawahi kuja public na kutoa majibu ya ni lini walikubali kua JK ni raisi halali na sababu zilikua zipi? Hii itasaidia kujenga heshima na mshikamano ndani ya nchi na pia wananchi kupigania maendeleo zaidi ya migomo yao wanayohamasisha kila mara.

Unachokisema hapa hakilingani na status yako kama senior expert member wa Jf unless umefoji kama mlivyozoea. Gambas
 
Unachokisema hapa hakilingani na status yako kama senior expert member wa Jf unless umefoji kama mlivyozoea. Gambas

Hili ndo tatizo kubwa la humu JF watu hawaji na point zaidi ya kushabikia vyama fulani.
Mkuu mi ningependa sana kama ungenielewesha kwa pointi zaidi ya kunikashifu....Asante
 
Chadema wameomba kukutana na kikwete kuongelea mchakato wa katiba mpya,je wakikufikia muafaka na kikwete nakukubaliana itakua jambo jema kwa kila mpenda amani wa nchi hii,je wasipokubaliana je chadema watachukua hatua gani?watakubali yaishe au ndio hapatakalika kama kauli mbiu ya cdm?
 
Kwanza CDM pamoja na nia njema na mapenzi mema waliyo kwa amani ya tz, bahati mbaya ni kwamba wanaenda kukutana na mtu ambaye ana macho lakini haoni. Sina uhakika kama kuna lolote la maana litakalopatikana kutokana na mazungumzo hayo.
 
CHADEMA Wasipokuwa Makini, Namaanisha kwamba wakipumbazwa na kuwa kwao
mbele ya Utukufu wa Rais Mazungumzo yao yatakuwa kama apo chini.

Lakini wakienda full prepared kukabiliana na characteristics (zingine kupambana nazo
na zingine kuzitumia kama opportunity) zote za Kikwete as a Person Hiki kikao
kitakuwa ndio kikao pekee profitable ambacho Kikwete atakuwa amekifanya na
Watanzania kwa Ujumla wetu tukafaidika nacho katika viwango visivyohesabika.

Mazungumzo ya kamati ya CHADEMA na Jakaya kwa ufupi
Kikwete: Kwanza napenda kuwashukuru kwa kuonesha njia njema kabisa ya Kuzungumzia Mustakabali wa
Katiba ya nchi yetu. Kwa kweli nimefarijika sana na ninawapongeza sana kwa moyo wa kizarendo
Mliouonyesha.

Kikwete: Pili naomba tusahau yote yaliyopita hasa ukizingatia ukweli kwamba hata Glass Kabatini ugongana
Sembuse sisi binaadamu bwana, au siyo Bwana Mbowe.

Mbowe: Ni Kweli Muheshimiwa, lakini kwa Maslahi ya Taifa Letu, Kuna mambo ya Msingi ambayo si busara
Kuyasahu badala yake ni nyema kuendelea kuyakumbuka na kuyakumbusha mpaka pale yatakapopatiwa
Majibu ya uhakika.

Kikwete: Ni kweli, lakini ninachomaanisha ni kwamba kwa sababu tuko hapa kujadili mchakato wa kuandaa katiba
Mpya ni vyema tukasahau yote yaliyotokea apo nyuma kama Maswala ya CHADEMA kutoka nje ya Bunge,
Maswala ya Muswada ama kusomwa mara ya Kwanza ama Mara ya Pili Bungeni na hata Upitishwaji wake Bungeni
Ukizingatia kwamba Bado sijausign kuwa sheria nikitambua kwamba Mazungumzo yetu leo yanaweza kuboresha
zaidi mchakato huu kwa Maslahi ya Taifa.

LISSU: Samahani Mheshimiwa Rais, Kwani wewe binafsi umeuonaje mchakato mzima ulivyokwenda mpaka kufikia
Mswada huo kufikishwa kwako ili usainiwe kuwa sheria.

Kikwete: Tehe tehe tehe, LISSU bwana, tehe tehe tehe, aaaahaaaa. Unajua, haya mambo bwana, ndio maana
mimi nimesema hapa kwamba ni vyema tukasahau yaliyopita ama sivyo mazungumzo yetu yatakuwa mareefu
sana na mwisho wa siku watanzania watatushangaa wote.
Mimi, mimi, mimi dhamira yangu ni kuhakikisha kwamba, Katika mchakato wetu huu, hatufikii kwenye hatua
mbaya kama majirani zetu, sababu haya mambo ukianza kuyawekea maandamano na mihadhara mwisho wake
kwa kweli kabisa hauwezi kuwa mzuri.

Anakunywa Maji kidogo, kisha anaendelea
Pale Kenya pale, wakati wa mchakato wao damu imemwagika pale, sasa mimi siko tayari kuona hili linatokea hapa,
na ndio maana hata kwenye swala la madiwani wa arusha, mimi niliwaelekeza Waziri Mkuu na Katibu wangu Mkama
kuhakikisha Mnakaa, mnazungumza na kulimaliza hili, lakini kinachoendelea pale mi hata sikielewi nikiuliza naambiwa
tatizo ni Lema, vyombo vya habari kwanza vilikuwa vinasema tatizo ni Chitanda, sasa Chitanda simsikii tena
naambiwa tatizo ni Kamanda wa Polisi Zuberi na Mkuu wa Mkoa, mimi sielewi kabisa nini kinaendelea Pale, na hali
hii inachafua kabisa picha ya nchi yetu uko nje.

Anakunywa Maji tena.alafu
Pale Arusha Pale, kile ni kitovu cha Utalii nchini Mwetu, sasa Arusha tukiichezea itatualibia kabisa kabisa, ndio maana
mi nasema swala la Arusha tunatakiwa tukae kama hapa tuzungumze na kulipatia Muafaka. Hii nyumba tunajenga
wote kwa nini tugombee fito Jamani.

Mimi, mimi nasema, wakati tuko Kwenye kikao cha Kamati kuu Dodoma Pale, kuna watu walitaka kukataa nisionane
na CHADEMA, mi nikasema hapana, Lazima nionane nao hawa, kwa sababu hata mimi hili swala la Katiba mpya bado sijalielewa
vizuri.

Kwa hiyo mi nawashukuru sana kwa Moyo wa Uzalendo mliouonyesha, na niko tayari kuonana na nyie na kuzungumza
hata kwenye mambo mengine, sina tatizo hata kidogo na nyie, si unaona bwana, tumezungumza na hakuna mtu
ametoka damu, hii ndio watanzania wanataka kuona.

Mimi kwa kweli niwashukuru sana, na hizi ndio siasa za kizalendo kwelikweli, asanteni sana na karibu tena.​
 
Script imekaa vema tusubiri actor watapita humo au plot itachange kabisa na kulazimu kuandika script nyingine!
 
“…. serikali ni ya watanzania wote. Hata wale ambao hawakutuchagua CCM bado hawana serikali nyingine, ni hii hii. Watakwenda, watarudi. Hawana mwingine wakumlilia kwa yao ,hawana mwingine wakuomba yao yatimie isipokuwa serikali ya chama cha mapinduzi, ambayo mie ndo rais wake. Dr Mohamed Gharib Bilal ndo makamu wake wa rais.Serikali ambayo Dr Alli Mohamed shein ndo rais wa Zanzibar na Maalim seif sharif hamad makamu wa kwanza na balozi seif Alli idd makamu wa pili…..”
Ni sehemu ya hotuba ya rais Jakaya Kikwete wakati anafungua bunge tarehe 18-11-2010,ambapo wabunge wa chadema walitoka bungeni kususia hotuba yake kwa madai ya kutomtambua kama rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania,wakiongozwa na mwenyekiti wao freeman mbowe.
Ni mwaka mmoja na siku kama mbili tatu hivi,hatimaye maneno ya rais Jakaya kikwete yametimia,mnamo tarehe 21-11-2011,Mwenyekiti wa chadema freeman Mbowe atangaza kwa vyombo vya habari na kwa umma wa watanzania azma yao ya kutaka kuonana na Jakaya kikwete,sisi kama mwenyekiti wa CCM bali kama Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Kwanza wamemtabua kama JK ni rais,pili wamekimbilia kwake kutaka msaada wa mapendekezo yao juu ya sheria ya muundo wa kuunda tume ya kuratibu maoni ya wananchi juu ya katiba mpya.Kwa moyo wa furaha rais amekubali kukutana nao.
Nawapongeza chadema kwa uzalendo na mapenzi yao makubwa waliyoonesha kwa rais JK mbele ya umma wa watanzania,kwa kuithibitisha kauli yake kwa vitendo kwamba “….Watakwenda, watarudi. Hawana mwingine wakumlilia kwa yao ,hawana mwingine wakuomba yao yatimie isipokuwa serikali ya chama cha mapinduzi, ambayo mie ndo rais wake…”
 
Back
Top Bottom