Kwa kazi kubwa waliyomfanyia kuiba kura na kuchakachua matokeo ya uchaguzi 2010.
Ama kweli kuna kazi kuitoa CCM madarakani kama mambo ndo haya.
soc: ITV news bullet
duh! Kama ndiyo hivyo basi mkweree ni noma! Yaani anawashukuru live kwa kazi kubwa ya kuiba kura na kuchakachua matokeo, kweli magamba wana kazi kubwa!!
****** anatia aibu sawa aliiba kura lakini sasa nayeye mpaka awashukuru waziwazi,kweli JK noma,basi na RITH yeye ashukuru,au mkuu wa kaya alishukuru kwa niaba ya familia
Ulitegemea nini? Bado kutoa shukurani kwa Lipumba, Mrema, Mbatia na APPT maendeleo kwa kumsaidia kupunguza kura za dk wa kweli? Hongera Kikwete, lakini miaka mitano inakaribia kuisha utaingia katika mahakama ya umma kwa kuvuruga taifa.
Nilimwona anachekacheka kinafiki huku kama anaona aibu.
Eti akaahidi kufanya marekebisho kuondoa kasoro!! Jk inakiwa tume huru wewe usitie mkono hapo!
Kwa mwendo tutarajie mgogoro mkubwa na uvunjifu wa amani kwenye uchaguzi mkuu ujao! Jk nae kumbe ni kama kia Mugabe, Gaddafi!
Lazima awashukuru wanatume, ila kawasahau wanajeshi,usalama wa taifa waliopita kituo kwa kituo cha kupigia au kuhesabia kura na kuzichakachua kura. Au hao atawashukuru siku nyingine? au alishawashukuru?
Nawashukuru baadhi ya polisi waliotutonya tulipokuwa tunalinda kura kwamba tusiruhusu magari ya jeshi kusogea vituoni. Maeneo mengi ambayo wananchi wapenda haki walikojulishwa njama hizi za jeshi na usalama wa taifa na wananchi wakawa makini angalau uchakachuaji haukufanyika.
Kwa kazi kubwa waliyomfanyia kuiba kura na kuchakachua matokeo ya uchaguzi 2010.
Ama kweli kuna kazi kuitoa CCM madarakani kama mambo ndo haya.
soc: ITV news bullet
Watanzania hatuna aibu, hivi kwa madudu yale ya Makame na wenzake JK anawashukuru, najua ni sababu ya kumfanya arejee madarakani maana kamba tayari ilikuwa imeshakatika.
Tunasubiri waitoe hadharani tuone uongo wao. Chakusitaajabisha jamaa wamekaa wakaona kazi kubwa walioifanya ya kuchakachua matekeo hadi JK karudi madarakani, hivyo wameona wapewe cha juu bilioni 2.5 kwani JK hataweza kukataa, lazima azitoe kama shukurani. Lakini NEC wakumbuke kwamba huo mchezo wao ulitaka kuleta umwagikaji mkubwa wa damu hapa nchini kama Rwanda!. Wao wanachojali ni hayo mabilioni wayaweke mifukoni mwao. Mungu hapeni jambo - NEC watubu wamurudie muumba wao.
pole sana km kuna wana cdm wanaohisi nchi haitatawalika me nawaonea huruma mana wanawaza pua na mdomo.ccm inazidi kuwa pigia ngoma na wachezaji ndo nyie cdm ila hamjatambua mchezo.msisahau kucheza kiduku basi.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.