Kikwete aipasua zaidi CCM kwa upendeleo wa tuzo

Baba yake Mbowe (Mbowe Senior) ni mtu ambaye pia alistahili hiyo tuzo sema tu JK kaibadilisha imekuwa ya kichama zaidi na kuifanya ya Mawaziri Wakuu na Marais Wastaafu utadhani ndio wachapa kazi peke yao. Kama mtakumbuka Mzee Mbowe ndiye aliyekuwa anafadhili harakati zote za Mwalimu Nyerere. Ni kama Sobodo na CDM leo hii.

Mzee Edwin Mtei nae alipaswa apewe hiyo tuzo kwa mchango wake wa kusimamia sera yake ya Ubepari ambayo ilipingwa vikali na Nyerere hatimae akajiuzuru. Lakini baadae miaka ya 1990 serikali ikaanza kufanyia kazi mawazo ya Mtei. Na ndiyo inayoyatekeleza hadi leo.
Subiri FF akija hapa utasikia mambo yake, ni wazee wa gerezani tuu!
 
Hizo tile ni mbaya zinafanana na zile za chooni maryland full harufu ukiingia once hutoenda tena..

jk inaelekea amepachoka hapo, tiles Nyeupe huwekwa Chooni tu. Mzee Mwinyi bado anapiga Four Angle tu Dah!

Kweli mkuu pia angalia hizo gap zilivyo kubwa pia kunakuaga na mikanda inazunguka kwenye hizo line na angles,its very dangerous kwa mheshimia kwa jinsi nanyoangukaga,
 
Sasa mtoa mada ungepewa nafasi ya kutoa tuzo bado ungewapa hao unaowaona wanastahili na JK angekulaumu kuwa umewaacha wale aliowaona yeye wanastahili... tatizo litabaki palepale vinginenyo ni kujirekebisha mitazamo ya nafsi zetu, tusiwe wa kulaumu saana... kila kitu tunalaumu!!!!!!!!
 
HIvyo viatu vya hawa Marais khaaaaaaaaaaaaaaaa km mitumbwi duh

Tafadhali kuwa na fikira pevu, hii mada haihusiani na viatu au mavazi ya hao jamaa. Kama huna hoja sio lazima uandike, pamoja na uhuru wa maoni kuwepo, jamvi hili litumike kibusara sio kiholela.
 
Kumbe na Adam Sapi Mkwawa hakupewa!!!!!!!

Hayati Adam Sapi Mkwawa ni mmoja wa viongozi ambao walikuwa makini mno, alikuwa mnyenyekevu, mtendaji na mwenye nidhamu ya hali ya juu sana.

Nilibahatika kuonana naye kabla hajafa katika awamu yake ya mwisho kuwa speaker wa bunge karibu anastaafu kwenye sherehe fulani ya kusimikwa Mhashamu fulani. Mimi nilikuwa bado kijana mno ila hulka ya kupenda kuwa karibu na wazee na kuwauliza mawili matatu kulinipa fulsa nyingi za kuongea na watu hawa.

Katika maongezi yangu na Chief Adam Sapi Mkwawa akiwa speaker nilishangaa kuwahi mno kwenye tukio hilo kwa vile yeye kama mkuu wa mmoja wa mhimili wa nchi yetu angesubiri kwanza hadi muda unapokaribia. Akanijibu kuwa katika utumishi wake hajawahi kuchelewa kazini au kwenye wajibu wake hata siku moja labda kuwa na kikwazo kinachoshindikana. Tulikuwa tumemzunguka watu kama watano hivi kijana nikiwa pekee, nilishika tama na kumwangalia usoni, nikamsoma alivyo na kuelewa anachokiongea ndicho anachokifanya. Adam Sapi naye aliniangalia vizuri usoni na kunishika mkono, kisha akaniambia tunataka ninyi vijana mjifunze kuwajibika hivyo. Kilichonishangaza zaidi alivyokuwa very simple, hana makuu, hatafuti nafasi za viti vya mbele, wala kujitia kimbelembele mpaka wamkaribishe.

Binafsi nimeshangazwa sana na kusahauliwa kwa hayati Adam Sapi kutokana na mchango wake mkubwa kwa taifa hili pamoja na uadilifu katika utumishi wake uliotukuka. Kikwete ana lake.
 
Hizo tile ni mbaya zinafanana na zile za chooni maryland full harufu ukiingia once hutoenda tena..

jk inaelekea amepachoka hapo, tiles Nyeupe huwekwa Chooni tu. Mzee Mwinyi bado anapiga Four Angle tu Dah!-
Jk Pia anaonekana Bado mwanajeshi sababu viatu alivyovivaa ni vya maafisa wa Jeshi.

Kuvaa Vizuri unahitaji upate Mtaalam Kama anatizama Movie Namshauri amuulize jamaa yule kwenye Movie ya Pointman. Mtaalam wa Kuvaa mavazi yanayo fit na kumatch

ivo nyie hapo ndo ikulu ehh?
Au ni choo kipi?
 
Ile timu ya viongizi wa cdm walioenda ikulu kuhusu katiba mpya nayo ingetakiwa kukumbukwa kupewa nishani
 
Nishani imetolewa kwa wale tu wanaoiunga mkono mgombea wa JK mwaka 2015. Wasiokubaliana na mgombea wa JK au wanaotaka kugombea wenyewe hawana nafasi ktk nishani hii. That is my conclusion ktk nishani hii yenye utata mtupu.
 
Ruksa- kwa kumjenga Kikwete kisiasa mpaka kufikia ngazi aliyonayo kwa sasa.
Mkapa-kwa kuruhusu kupitishwa kikwete kuwa mgombea wa SISIEM pamoja na kuwa kulitokea kashfa wakati wa kikao cha ndani cha SISIEM kule Zanzibar, na pia kumuokoa kikwete katika kikao cha SISIEM kilicho isha hivi karibuni.
 
b4.jpg



Hivi huyu jamaa wa katikati ataacha lini kukenua kenua? Anakera sana huyu.
 
hizi tuzo JK AMEJICHONGEA

Yes, utoaji wa tunu hizo kama alivyosema John Malecela waulizwe ikulu ndio wanajua vigezo walivyotumia kuwapa wahusika. Kwani utoaji wa tunu hizo Kikwete ameonyesha wazi nani adui zake na nani rafiki zake. Halikadhalika ni uthibitisho kuhusu lile kundi ndani ya CCM linalopigania hazi za msingi, uaminifu, uwajibikaji wametengwa na Kikwete. Kikwete anawaenzi wezi wa mali ya umma na kuwatukunu tunu wasizostahili.
 
b4.jpg


Tuzo za viongozi mbalimbali hai na waliotutangulia zilizotolewa na Kikwete pale Ikulu siku ya jubilei ya miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika kwa mtazamo wa wengi ni kanyagaboya ambayo Kikwete atakuja kujutia siku yake. Bora angeacha kutoa tuzo hizo kabisa. Kwani kilichotokea ni kuonekana kwa tafsiri nyingi zambazo ndani ya CCM kuna wanaoshangaa baadhi kutopewa tuzo hizo wakati wanastahili. Baadhi ya walioachwa kama Adam Sapi ambaye ndiye speaker pekee aliyetumikia ofisi hiyo kwa miaka mingi, hali kadhalika Samweli Sitta ambaye alilijengea sifa kubwa bunge lililopita na kuwa bunge la kwanza kuibua madudu ya ovyo ndani ya serikali, na wengi wetu wanajua hilo. Gharama za tuzo alizotoa Rais juzi pale Ikulu kishindo chake tutakisikia siku zijazo ndani ya kambi za CCM.
Wala hujakosea tusubiri tuone sijui kama walioachwa watanyamaza!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom