Kikwete agoma kutoa misaada ya Ambulances; Ikulu yaboronga!

Kitu kingine nimekisoma hapo ni kuwa hao madereva walishakuwepo hapo kwa muda na kupata tayari mafunzo ya magari hayo..
 
Kitu kingine nimekisoma hapo ni kuwa hao madereva walishakuwepo hapo kwa muda na kupata tayari mafunzo ya magari hayo..

Mwanakijiji ongezea hapo na wameshakula per diem zao wako poaa kabisa na wale wengine nao inabidia wapite tena mafunzo wale per diem ili mradi mtafaruku wa fikra na tu
 
Hivi maafisa wote Ikulu hawakugundua tofauti kati ya Longido na Loliondo hadi Rais mwenyewe!? Mnajua huko aliko mwenyewe anajipongeza kuwa amesevu na gazeti la Daily News na mengine ya serikali yatatoa pongezi kubwa kwa Rais huku yakilaumu watendaji wake.

Hapo RC alishacheza 'dili' lakini bahati mbaya limebumbuluka. Inawezekana magazeti ya serikali na baadhi ya viongozi kulaumu watendaji wa Rais, lakini mwisho wa siku anayebeba lawama ni Rais mwenyewe kwani ana uwezo wa kuwawajibisha wazembe katika suala hili. Kung'aka tu ni sawa na mbwa anayeishia kubweka tu bila kumtafuna mwizi!
 
Yah niliona kwenye habari ya jana mkuu,muungwana alionekana kuchukia,lakini mpaka sasa sielewi kuwa mpaka rais anatoka ofisini hakujua anaenda kumpa nani gari?,je huyo mkurugenzi aliyenyimwa hilo gari halihitaji(na maana kwake hakuna uhaba wa magari ya kubeba wagonjwa?).Anyway tuwaachie wenyewe bwana na protocal zao


Mkuu Hassan, swali lako ni zuri sana. Kwa hali tunayoijua nchi yetu wilaya nyingi zina upungufu mkubwa wa magari ya kubebea Wagonjwa. Sasa sijui ni utaratibu gani uliotumika na Ikulu kuamua hizo wilaya tatu ndizo zipewe hizo ambulance tatu na pia wapewe Longido na siyo Loliondo. Inawezekana kabisa kwamba CMC ambao ndiyo watoaji wa msaada huo kwa masharti kwamba yapelekwe katika Wilaya hizo tatu na si wilaya nyingine vinginevyo Ikulu inahitaji kutoa maelezo zaidi kuhusu criteria waliyotumia kuzichagua hizo wilaya tatu na kwanini wapewe Longido na siyo Loliondo.
 
Nimesikiliza Clouds FM asubuhi hii wakimhoji DED wa Longido. Anyway,kuhojiwa kwake sio hoja ila nilishangazwa na jinsi Clouds walivyoamua kumfagilia JK kwamba ni Rais mwenye kumbukumbu nzuri sana kutokana na utendaji mzuri. Aibu kwa Clouds! wametengeneza mpaka katangazo kwamba Rais si mchezo hadanganyiki.
Upotoshaji na kujikomba tupu.
 
Nimesikiliza Clouds FM asubuhi hii wakimhoji DED wa Longido. Anyway,kuhojiwa kwake sio hoja ila nilishangazwa na jinsi Clouds walivyoamua kumfagilia JK kwamba ni Rais mwenye kumbukumbu nzuri sana kutokana na utendaji mzuri. Aibu kwa Clouds! wametengeneza mpaka katangazo kwamba Rais si mchezo hadanganyiki.
Upotoshaji na kujikomba tupu.

Mimi nakubaliana na clouds FM, hao wahusika wa Ikulu wajiuzulu kabisa maana kama dogo hivi hawawezi je kubwa wataliwezea wapi? Inaonekana walikuwa na njama zao za kutaka gari iende sehemu nyingine na ndio maana hawakumwambia JK, mtu ameingia mpaka Ikulu and I am sure alisachiwa pia kama ana chochote cha kudhuru, saa zote hizi hawakuweza kugundua kweli? Si bure walikula njama hawa na Jk akawashtukia...
 
Mimi nakubaliana na clouds FM, hao wahusika wa Ikulu wajiuzulu kabisa maana kama dogo hivi hawawezi je kubwa wataliwezea wapi? Inaonekana walikuwa na njama zao za kutaka gari iende sehemu nyingine na ndio maana hawakumwambia JK, mtu ameingia mpaka Ikulu and I am sure alisachiwa pia kama ana chochote cha kudhuru, saa zote hizi hawakuweza kugundua kweli? Si bure walikula njama hawa na Jk akawashtukia...
Kwani hao wasaidizi wake alishushiwa toka Mbinguni? Team ya kutenda nayo kazi kaiandaa mwenyewe, na kubambikizwa mambo hakukuanza leo na bado anao tuu. Kikombe hicho lazima akinywe mwenyewe.
 
Hivi hicho kitengo cha habari Ikulu kina tatizo gani? Ni professionalism ndogo au ni mzaha? Kwa nini huyo mkurugenzi wake asijiuzulu tu? Mara nyingi migongano kibao ya habari na bado Mh. Rais anamvumilia tu. Hayo ndiyo matatizo ya kubeba vibaraka wa maswahiba huku uwezo hawana. Itabidi habari maelezo wachukue jukumu la kusemea habari za nchi maana hicho kitengo cha habari Ikulu bomu la nuclear kabisa.

Thubutu! Rais atamfanya nini Salva? Pale Ikulu kapelekwa na Rostam. JK hawezi kumgusa.
 
Tatizo la JK anaaibisha Ikulu yetu. Kutaka publicity sana kuna mgharimu. Tumechoshwa kusikia failures zinazoihusu ikulu hata kwa masuala madodo madogo kama haya.

vitu vingine vidogo vidogo kama hivi angelikuwa anawaachia wasaidizi wake wahusike navyo. Anajaribu kujiaibisha na intelligence yake/yetu bureeee!!. Wakati fulani, hata kama kuna udhaifu kwenye nyumba, mama au baba hujaribu kujistiri kidogo!

JK hajifunzi tu? Juzi juzi tu hapa katuacha hoi na ile hotel ya Arusha, hatujakaa sawa mkenge na CMC.

Uozo wa CMC tunaufahamu. Wahindi hawa, wanadhurumu mali ya wa TZ kwa kukwepa kodi, halafu wanatumia pesa walizokwepa kodi nk, kujifanya wanatoa misaada. Huu ni uhuni!

Kwa JK
Mh Rais unatuaibisha. Kwa nini kujihusisha husisha na uzinduzi wa vitu vidogo vidogo ambavyo hata havijawekwa sawa??. Kama, ndiyo njia ya kutaka mass support, poa! Ngoja nimalizie kajumba kangu, nami nianze kuwasiliana na wakuu wa itofaki; wakulete uje ukazindue. Huku utashangiliwa sana!

Ila ujapo uje na majibu ya swali hili: Wewe hauoni unatuaibisha kwa kujihusisha husisha na uzinduzi wa shughuli ndogo ndogo ambazo zingefanywa na wasaidizi wako wakiwemo wakuu wa wilaya?????
Umesema ukweli kabisa na hii yote ni Kampeni na kuona kuwa jinsi gani wapo makini,. sasa kama umakini kwa mambo madogo kama haya haupo basi mengine ni hatari kabisa
 
Sakata la gari la wagonjwa : DC wa Ngorongoro adai Ikulu waliboronga
gariikulu.jpg
Katibu wa Rais Prosper Mbenna, akimkabidhi funguo za gari la kubebea wagonjwa (ambulance), Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido, Mkoani Arusha ChristianLaiser kwa niaba ya Rais Jakaya Kikwete, kwa ajili ya kituo cha afya cha Engarenaibor wilayani humo, hafla iliyofanyika Ikulu Dar es Salaam jana.Juzi rais Kikwete aligoma kukabidhi gari hilo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ngorongoro baada ya kubaini kuwa si mlengwa*WASOMI, WANASIASA WAMTAKA RAIS KIKWETE WAWAJIBISHE KWA UZEMBE

Boniface Meena na Freddy Azzah

MKUU wa Wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali amesema kuwa, alimtuma mkurugenzi wake kwenda Ikulu jijini Dar es Salaam kupokea gari la kubebea wagonjwa kutokana na maelezo aliyopewa na ofisi hiyo ya Rais.

Lali alisema hayo jana baada ya juzi Rais Jakaya Kikwete kugeuka mbogo na kumtimua Mkurugenzi wa Wilaya ya Ngorongoro, Kayange Jacob ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, baada ya kubaini kuwa wasaidizi wake wamemdanganya.

Mbali na kumtimua mkurugenzi huyo, Rais Kikwete ambaye alitakiwa kukabidhi magari ya wagonjwa kwa halmashauri za wilaya za Mbozi na Longido, aliondoka katika hafla hiyo kwa hasira bila kugawa magari hayo.

Lali alitoa ufafanuzi huo kwa kueleza kuwa yeye alipigiwa simu na Ikulu na kutakiwa kumtaarifu mkurugenzi wake kufika Ikulu kwaajili ya kukabidhiwa gari.

"Mimi nilipigiwa simu na Ikulu ikinitaka kumtaarifu mkurugenzi wangu afike Ikulu kukabidhiwa gari, lakini sikujua ni gari la nini hivyo mimi nilimuagiza kama nilivyoagizwa," alisema Lali.

Alisema kuwa baada ya kutakiwa kufanya hivyo alimtaarifu mkurugenzi wake ambaye alifika Ikulu kwa ajili ya makabidhiano hayo.

Wakati Lali akitoa ufafanuzi huo, wanasiasa na wasomi wamesema kitendo hicho cha kumdanganya Rais ni chakufedhesha na kuwa kilikusudiwa huku CUF kikimtaka Rais kuwawajibisha waliohusika.

Akizungumza na Mwananchi jana, Katibu wa NCCR Mageuzi Samuel Ruhuza alisema, wasaidizi wa rais walijua kutoka mwanzo kuwa mtu aliyekuja kuchukua gari hilo ni Mkurugenzi wa Wilaya ya Ngorongoro na siyo wa Longido na hivyo kitendo hicho cha kudanganya kilikusudiwa.

"Huyu jamaa alishatuma madereva wawili kwa ajili ya training (mafunzo) na lazima walikuwa wa Ngorongoro na siyo Longido, kwa hiyo waliamua kumdanganya rais kwa makusudi. Halafu toka ametoka huko akaja mpaka Ikulu akajitambulisha na akaingia mpaka ndani lazima hawa wasaidizi walijua," alisema Ruhuza.

Hata hivyo, Ruhuza alisema uongozi kwa ujumla kutoka katika Wilaya aliyotoka ya Ngorongoro aliyotoka Mkurugenzi huyo kulikuwa na uzembe.

"Kweli inawezekana kuwa Ngorongoro kuna shida ya ambulance (gari la kubeba wagonjwa) kuliko Longodo, lakini bado hiyo siyo sababu, na uongozi wa wilaya hiyo ndiyo iliyompa huyu jamaa access (kumwezesha) mpaka akafika Ikulu, kwa hiyo wote walidhamiria kudanganya Rais," alisema Ruhuza.

Naye Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Profesa Mwesiga Baregu alisema kitendo hicho ni ishara ya ukosefu wa nidhamu ya kazi na mmomonyoko wa maadili kwa viongozi.

"Mimi nadhani ni tukio linaloonyesha dalili kubwa ya vurugu zilizopo serikalini, siyo mara moja yametokea matukio kama haya, kwa hiyo hali hii inaonyesha mmomonyoko wa maadili kwa viongozi na utovu wa nidhamu ya kazi kwasababu maadili ni pamoja na kuhakikisha shughuli zinaenda kama zilivyopangwa," alisema Profesa Baregu.

Msomi huyu alisema lawama zisielekezwe kwa wasaidizi wa rais pekee bali hata kwa Wizara ya Utumishi pamoja na Rais mwenyewe kwa kuteua watu wasiokuwa makini na kazi zao.

"Siyo wasaidizi wake pekee waliomwangusha Rais, kuna utumishi hawa ambao walinisimamisha mimi kazi wakisema kuwa sisitahili kufundisha chuo kikuu, hawa wote wanausika," alisisitiza Profesa Baregu.

Naye mwanasheria mkogwe nchini, Bob Makani alisema kuwa kitendo hicho ni kidogo sana na kuwa kimetokana na mkanganyiko mdogo tu.

"Kama nimesoma vizuri habari hii, suala hili ni dogo sana, rais alikuwa ameahidi mahali pengine na akaja mtu mwingine, kwa hiyo mimi naona ni kitu kidogo sana," alisema Bob Makani.

Katika hatua nyingine, CUF kimeelezwa kusikitishwa na tukio hilo huku kikimtaka Rais Kikwete kuchukua hatua kuwawajibisha maofisa waliohusika.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Naibu Mkurugenzi, Uenezi na Mahusiano ya Umma wa CUF, Ashura Mustapha chama hicho kinaelezea kitendo hicho kuwa ni cha makusudi.

"Kitendo hiki si cha bahati mbaya kwa kuwa viongozi wengi wa serikali ya CCM wapo madarakani kwa maslahi yao binafsi na kujineemesha kwa kutumia rasilimali za umma ndio maana wasaidizi wa Rais walifanya udanganyifu huo kutaka kupinda ahadi ya Rais Kikwete," ilisema sehenu ya taarifa ya CUF. Chama hicho kilimtaka Rais Kikwete kuchukua hatua za haraka za kuwawajibisha wote waliohusika na kashfa hii ya kuidanganya Ikulu.

My Take:
Creating mountains out of mole hills?!

Issue hii sasa imekuwa 'dili' ya kisiasa. Baregu naye kapata mwanya wa kupenyeza dukuduku lake kuhusu uozo wa Idara ya Utumishi!

Kama taarifa hii ni sahihi moja kwa moja Afisa wa Ikulu aliyepiga simu Loliondo ndiye mwenye makosa. Bila shaka ulikuwa ni mkanganyiko wa majina ya Longodi na Loliondo ambayo kidogo yanafanana na yanaweza kumchanganya mtu ambaye hayuko makini. Na kwa afisa wa Ikulu kosa hilo halina mjadala ni uzembe mkubwa.

Bado swali lipo, kwa nini Rais aliteremka kwenda kwenye tukio la kugawa magari hali akijua kuna makosa yaliyotendeka?

Kingine ninachokiona hapa ni dalili za 'fitna' miongoni mwa watendaji wa Ikulu. Huyo aliyekwenda kumwambia ama kumnong'oneza Rais dakika za mwisho kwamba aliyekuja kuchukua gari hatoki Longido bali Loliondo bila kwanza kupeleleza imekuwaje, kujua ukweli na kuweka mambo sawa, naye hafai kuwa karibu na Rais wa nchi!
 
2010-01-20 09:17:00
New twist in State House vehicle presentation sagaBy Zephania Ubwani, Arusha and Alex Bitekeye, Dar
THE CITIZEN

It has emerged that President Jakaya Kikwete's aides caused Monday's confusion that prompted him to furiously call off the presentation at State House of two ambulances donated to Mbozi and Longido districts.

The Citizen has established that State House officials contacted Ngorongoro and Longido district officials, and asked them to attend the presentation ceremony, which degenerated into a public relations fiasco.

It was not immediately clear why different calls were made to Ngorongoro and Longido district commissioners on the presentation of one of the ambulances, but State House press secretary Premi Kibanga said yesterday that steps were being taken to establish what caused the embarrassing mix-up.

She said in a telephone interview that all heads of department at State House witnessed the unfolding drama, and would have by now established what went wrong.

A visibly angry President Kikwete sparked panic among his aides when he called off the ceremony and walked away after giving them a public tongue-lashing.

Longido District Commissioner James ole Millya confirmed yesterday that he received a call from State House a few hours before the ceremony, and immediately dispatched the district executive director (DED), who arrived late.

He was still in Dar es Salaam yesterday waiting to take the ambulance to Longido.

His Ngorongoro counterpart, Mr Elias Wawa Lali, said he also directed the DED to travel to Dar es Salaam to collect the vehicle after receiving a call from State House a week ago.

Interestingly, drivers from both Ngorongoro and Loliondo had been receiving training from CMC Automobiles Ltd, which donated the $108,000 (Sh140 million) vehicles.

Mr Wawa Lali said he had not been in contact with the DED, Mr Jacob Kayange, who was at the centre of the protocol fiasco when the Head of State turned him away, saying he could not collect the ambulance meant for Longido.

The DC defended Mr Kayange, saying he could not have known that the vehicle was actually supposed to have been presented to Longido.

According to a State House statement released on Monday evening, even though the Mbozi DED, Mr Levison Jeremiah Chilewa, also arrived late, the ambulance donated to the district was later released to him.

The State House protocol department came under intense scrutiny after Monday's incident, which was a reminder of other embarrassing blunders involving the Head of State in recent months.

Last December, the Tanzania Roads Agency (Tanroads) demolished the perimeter fence of a tourist hotel in Arusha only three days after President Kikwete had presided at its colourful opening.

The fence was knocked down on the grounds that it had been built on a road reserve.

Questions were raised as to why the President was invited to open a facility whose owners were involved in a dispute with Tanroads, whose officials insisted that they were merely doing their job.

State House spokesperson Salva Rweyemamu said the President's named should not be dragged into the controversy.

In November 2008, President Kikwete shared a bench with mourners in a church in Mbezi, Dar es Salaam, during the funeral service for former Mbeya Rural MP Richard Nyaulawa.

Organisers apparently had no prior knowledge of his arrival. Matters were not helped when the President insisted on staying after declining to use the chair reserved for the priest, which was hastily offered to him by his aides.

In October 2008, the President's aides were involved in another embarrassing blunder when they failed to provide a car for the wife of former Madagascar President Marc Ravalomanana, when he arrived in the country for a state visit.

In yet another incident, President Kikwete declined to hand over motorcycles to ruling party officials in Arusha after it was claimed in the last minute that the donation had a hidden political agenda. The President left the function and ordered his aides to explain why he had been misled.

Yesterday, Arusha Regional Commissioner Isidori Shirima could not be contacted to comment on the blunder that involved two districts under his watch.

A senior official of the regional secretariat refused to comment, saying only the State House could clarify on the matter.

But a long-serving government official, who asked not to be identified, absolved the regional secretariat, noting that new powers bestowed on local authorities, ministries and other government institutions allowed direct communication with the district councils on issues such as donations.

Confusion on district names was also blamed, with Mr Wawa Lali saying many officials in Dar es Salaam failed to distinguish Longido from Loliondo.

The latter is the Ngorongoro District headquarters, while Longido is the newest district in Arusha Region, having been curved out of Monduli District last year.

"Loliondo is more well known than Longido because of the publicity it is getting due to the never-ending conflicts there. Confusion on the names of localities is not confined to Arusha, but is also prevalent in neighbouring Manyara Region," added another government official.

Many senior government officials often wrongly think that Karatu was in Manyara Region, Hanang in Mbulu District and Simanjiro in Arusha Region, said a retired public servant.

A recent meeting in Arusha suggested that the names of the local authorities be revisited to end confusion.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom