we Kada we, unampinga Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Visiwa vyake, aliyechaguliwa na Mungu na kupakwa mafuta, ambaye ni Amiri jeshi wa Majeshi yote ya Ulinzi na Usalama (Polisi, JKT, Mgambo, Magereza, JWTZ, Sungusungu na Chipukizi)? Unathubutu vipi?
Mwanakijiji,
Rais JK kachaguliwa na Watanzania. Kama rais JK hatufai basi ni makosa ya Watanzania wengi waliomweka madarakani pamoja na kujua
katiba mbaya iliyotumika na mapungufu ya JK.
Kusema JK kawekwa na mungu naona ni SPIN na haina ukweli wowote.
Kinachotakiwa Tanzania ni kupigania mabadiliko ya katiba ili kiongozi yeyote atakayeingia madarakani asiwe na power kubwa kama ilivyo sasa.
Kikubwa zaidi ni kuwaelemisha Watanzania na hasa huko vijijini ili waelewe kwamba wana nguvu ya kuweza kuleta mabadiliko Tanzania kama watatumia vizuri kura zao.